Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Galates 3.6
Bible en Swahili de l’est


Justifiés par la foi, non par la loi

1 Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya macho yenu ya kuwa amesulibiwa?
Hébreux 5.9 Romains 6.17 Matthieu 7.26 1 Corinthiens 1.23-1.24 Luc 24.25
2 Nataka kujifunza neno hili moja kwenu. Je! Mlipokea Roho kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani?
Actes 15.8 Actes 19.2-19.6 Galates 3.14 Actes 2.38 Actes 11.15-11.18
3 Je! Mmekuwa wajinga namna hii? Baada ya kuanza katika Roho, mnataka kukamilishwa sasa katika mwili?
Galates 5.4-5.8 Galates 4.7-4.10 Hébreux 9.9-9.10 Galates 6.12-6.14 Hébreux 7.16-7.19
4 Mmepatikana na mateso makubwa namna hii bure? Ikiwa ni bure kweli.
2 Jean 1.8 Hébreux 10.32-10.39 2 Pierre 2.20-2.22 Hébreux 6.4-6.6 Ezéchiel 18.24
5 Basi, yeye awapaye Roho na kufanya miujiza kati yenu, je! Afanya hayo kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani?
1 Corinthiens 1.4-1.5 Galates 3.2 Actes 19.11-19.12 Actes 14.3 Actes 14.9-14.10
6 Kama vile Ibrahimu alivyomwamini Mungu akahesabiwa haki.
Genèse 15.6 Romains 4.3-4.6 Romains 4.24 Romains 4.21-4.22 Jacques 2.23
7 Fahamuni basi, ya kuwa wale walio wa imani, hao ndio wana wa Ibrahimu.
Galates 3.9 Psaumes 100.3 Romains 4.24 Romains 9.7-9.8 Galates 3.26-3.29
8 Na andiko, kwa vile lilivyoona tangu zamani kwamba Mungu atawahesabia haki Mataifa kwa imani, lilimhubiri Ibrahimu habari njema zamani, kusema, Katika wewe Mataifa yote watabarikiwa.
Genèse 12.3 Hébreux 4.2 Genèse 22.18 Apocalypse 11.15 Genèse 49.10
9 Basi hao walio wa imani hubarikiwa pamoja na Ibrahimu aliyekuwa mwenye imani.
Romains 4.11 Romains 4.16 Galates 3.29 Galates 3.7-3.8 Romains 4.24
10 Kwa maana wale wote walio wa matendo ya sheria, wako chini ya laana; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu asiyedumu katika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha torati, ayafanye.
Deutéronome 27.26 Jérémie 11.3 Luc 18.9-18.13 Deutéronome 11.26-11.28 Ezéchiel 18.4
11 Ni dhahiri ya kwamba hakuna mtu ahesabiwaye haki mbele za Mungu katika sheria; kwa sababu Mwenye haki ataishi kwa imani.
Hébreux 10.38 Habakuk 2.4 Romains 1.17 Galates 2.16 Esaïe 53.6
12 Na torati haikuja kwa imani, bali, Ayatendaye hayo ataishi katika hayo.
Lévitique 18.5 Romains 10.5-10.6 Néhémie 9.29 Romains 4.14 Romains 11.6
13 Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti;
Deutéronome 21.23 1 Pierre 2.24 Galates 4.5 1 Pierre 1.18-1.21 1 Jean 4.10
14 ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani.
Actes 2.33 Galates 3.2 Jean 7.39 Esaïe 32.15 Ezéchiel 39.29

Le rôle de la loi et le statut des croyants

15 Ndugu zangu, nanena kwa jinsi ya kibinadamu. Lijapokuwa ni agano la mwanadamu, hata hivyo likiisha kuthibitika, hakuna mtu alibatilishaye, wala kuliongeza neno.
Hébreux 9.17 1 Corinthiens 15.32 Romains 3.5 Romains 6.19
16 Basi ahadi zilinenwa kwa Ibrahimu na kwa mzao wake. Hasemi, Kwa wazao, kana kwamba ni wengi, bali kana kwamba ni mmoja, Kwa mzao wako, yaani, Kristo.
Genèse 12.7 Genèse 49.10 Romains 4.16 Romains 4.13 Luc 1.55
17 Nisemalo ni hili; agano lililothibitishwa kwanza na Mungu, torati iliyotokea miaka mia nne na thelathini baadaye hailitangui, hata kuibatilisha ile ahadi.
Genèse 15.13 Luc 1.68-1.79 1 Corinthiens 1.17 Hébreux 7.18 1 Corinthiens 10.19
18 Kwa maana urithi ukiwa kwa sheria, hauwi tena kwa ahadi; lakini Mungu alimkirimia Ibrahimu kwa njia ya ahadi.
Romains 4.13-4.16 Hébreux 6.12-6.15 Psaumes 105.42 Galates 3.10 Romains 8.17
19 Torati ni nini basi? Iliingizwa kwa sababu ya makosa, hata aje huyo mzao aliyepewa ile ahadi; iliamriwa kwa utumishi wa malaika kwa mkono wa mjumbe.
Actes 7.53 Galates 3.16 Hébreux 2.2 Deutéronome 5.5 Romains 7.7-7.13
20 Basi aliye mjumbe si mjumbe wa mmoja; bali Mungu ni mmoja.
1 Timothée 2.5 Hébreux 12.24 Hébreux 9.15 Deutéronome 6.4 Hébreux 8.6
21 Basi je! Torati haipatani na ahadi za Mungu? Hasha! Kwa kuwa, kama ingalitolewa sheria iwezayo kuhuisha, yakini haki ingalipatikana kwa sheria.
Galates 2.21 Romains 9.31 Galates 2.17 Romains 7.7-7.13 Romains 10.3-10.6
22 Lakini andiko limeyafunga yote chini ya nguvu ya dhambi, makusudi hao waaminio wapewe ile ahadi kwa imani ya Yesu Kristo.
Romains 11.32 Hébreux 9.15 1 Jean 2.25 Romains 3.9-3.20 Galates 3.23
23 Lakini kabla ya kuja ile imani tulikuwa tumewekwa chini ya sheria, tumefungwa mpaka ije ile imani itakayofunuliwa.
Galates 4.21 Hébreux 11.13 1 Pierre 1.11-1.12 Galates 3.19 Galates 4.1-4.5
24 Hivyo torati imekuwa kiongozi kutuleta kwa Kristo, ili tuhesabiwe haki kwa imani.
Galates 2.16 Romains 10.4 Colossiens 2.17 1 Corinthiens 4.15 Hébreux 9.8-9.16
25 Lakini, iwapo imani imekuja, hatupo tena chini ya kiongozi.
Romains 7.4 Hébreux 10.15-10.18 Romains 6.14 Hébreux 8.3-8.13 Galates 4.1-4.6
26 Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu.
2 Corinthiens 6.18 1 Jean 3.1-3.2 Ephésiens 1.5 Romains 8.14-8.17 Jean 1.12-1.13
27 Maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo mmemvaa Kristo.
Romains 13.14 Actes 2.38 1 Pierre 3.21 Romains 6.3-6.4 1 Corinthiens 12.13
28 Hapana Myahudi wala Myunani. Hapana mtumwa wala huru. Hapana mtu mume wala mtu mke. Maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu.
Colossiens 3.11 1 Corinthiens 12.12-12.13 Galates 5.6 Jean 10.16 Romains 3.29-3.30
29 Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi.
Romains 9.7-9.8 Ephésiens 3.6 Galates 4.22-4.31 Romains 8.17 2 Corinthiens 10.7

Cette Bible est dans le domaine public.