Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Corinthiens 11.18
Bible en Swahili de l’est


1 Mnifuate mimi kama mimi ninavyomfuata Kristo.
1 Corinthiens 4.16 Philippiens 3.17 Ephésiens 5.1-5.2 Hébreux 6.12 1 Thessaloniciens 1.6

Attitudes dans l’Église

2 Basi nawasifu, kwa sababu mmenikumbuka katika mambo yote, nanyi mmeyashika yale mapokeo vile vile kama nilivyowatolea.
2 Thessaloniciens 2.15 1 Corinthiens 4.17 1 Corinthiens 11.17 2 Thessaloniciens 3.6 1 Corinthiens 11.22
3 Lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila mwanamume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha Kristo ni Mungu.
Genèse 3.16 Colossiens 1.18 1 Corinthiens 3.23 Ephésiens 4.15 Colossiens 2.19
4 Kila mwanamume, asalipo, au anapohutubu, naye amefunikwa kichwa, yuaaibisha kichwa chake.
2 Samuel 15.30 1 Corinthiens 12.28 1 Corinthiens 11.14 1 Corinthiens 12.10 1 Corinthiens 14.1-14.25
5 Bali kila mwanamke asalipo, au anapohutubu, bila kufunika kichwa, yuaaibisha kichwa chake; kwa maana ni sawasawa na yule aliyenyolewa.
Luc 2.36 Deutéronome 21.12 1 Corinthiens 14.34 Actes 21.9 Actes 2.17
6 Maana mwanamke asipofunikwa na akatwe nywele. Au ikiwa ni aibu mwanamke kukatwa nywele zake au kunyolewa, na afunikwe.
Deutéronome 22.5
7 Kwa maana kweli haimpasi mwanamume kufunikwa kichwa, kwa sababu yeye ni mfano na utukufu wa Mungu. Lakini mwanamke ni utukufu wa mwanamume.
1 Corinthiens 11.3 Genèse 5.1 Genèse 9.6 Jacques 3.9 Genèse 1.26-1.27
8 Maana mwanamume hakutoka katika mwanamke, bali mwanamke katika mwanamume.
1 Timothée 2.13 Genèse 2.21-2.23
9 Wala mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, bali mwanamke kwa ajili ya mwanamume.
Genèse 2.18 Genèse 2.20 Genèse 2.23-2.24
10 Kwa hiyo imempasa mwanamke awe na dalili ya kumilikiwa kichwani, kwa ajili ya malaika.
Genèse 24.64-24.65 Hébreux 1.14 Genèse 20.16 Matthieu 18.10
11 Walakini si mwanamke pasipo mwanamume, wala mwanamume pasipo mwanamke, katika Bwana.
Galates 3.28 1 Corinthiens 12.12-12.22 1 Corinthiens 7.10-7.14
12 Maana kama mwanamke alitoka katika mwanamume, vile vile mwanamume naye huzaliwa na mwanamke; na vitu vyote asili yake hutoka kwa Mungu. Hukumuni ninyi wenyewe katika nafsi zenu.
Romains 11.36 Hébreux 1.2-1.3 Proverbes 16.4 1 Corinthiens 8.6
13 Je! Inapendeza mwanamke amwombe Mungu asipofunikwa kichwa?
Luc 12.57 Jean 7.24 1 Corinthiens 10.15
14 Je! Hayo maumbile yenyewe hayawafundishi ya kwamba mwanamume akiwa na nywele ndefu ni aibu kwake?
1 Corinthiens 14.35 2 Samuel 14.26
15 Lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni fahari kwake. Kwa sababu amepewa zile nywele ndefu ili ziwe badala ya mavazi.
16 Lakini mtu ye yote akitaka kuleta fitina, sisi hatuna desturi kama hiyo, wala makanisa ya Mungu.
1 Corinthiens 7.17 1 Timothée 6.3-6.4 1 Thessaloniciens 2.14 Actes 21.24 1 Corinthiens 16.1
17 Lakini katika kuagiza haya, siwasifu, ya kwamba mnakusanyika, si kwa faida bali kwa hasara.
1 Corinthiens 11.22 1 Corinthiens 11.2 1 Pierre 2.14 1 Corinthiens 11.34 1 Corinthiens 14.23
18 Kwa maana kwanza mkutanikapo kanisani nasikia kuna faraka kwenu; nami nusu nasadiki;
1 Corinthiens 3.3 1 Corinthiens 1.10-1.12 1 Corinthiens 5.1 1 Corinthiens 6.1
19 kwa maana lazima kuwapo na uzushi kwenu, ili waliokubaliwa wawe dhahiri kwenu.
1 Jean 2.19 Deutéronome 13.3 Luc 17.1 Matthieu 18.7 Actes 20.30
20 Basi mkutanikapo pamoja haiwezekani kula chakula cha Bwana;
21 kwa maana kila mmoja hutangulia kutwaa chakula chake katika kule kula; hata huyu ana njaa, na huyu amelewa.
Jude 1.12 2 Pierre 2.13 1 Corinthiens 10.16-10.18 1 Corinthiens 11.23-11.25
22 Je! Hamna nyumba za kulia na kunywea? Au mnalidharau kanisa la Mungu, na kuwatahayarisha hao wasio na kitu? Niwaambieni? Niwasifu? La! Siwasifu kwa ajili ya hayo.
1 Corinthiens 10.32 Actes 20.28 Proverbes 17.5 1 Timothée 3.5 Jacques 2.5-2.6
23 Kwa maana mimi nalipokea kwa Bwana niliyowapa nanyi, ya kuwa Bwana Yesu usiku ule aliotolewa alitwaa mkate,
1 Corinthiens 15.3 Matthieu 26.26-26.28 Luc 22.19-22.20 Marc 14.22-14.24 Matthieu 26.17
24 naye akiisha kushukuru akaumega, akasema, Huu ndio mwili wangu ulio kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.
1 Corinthiens 10.3-10.4 Exode 12.14 Psaumes 22.29 Esaïe 55.1-55.3 Proverbes 9.5
25 Na vivi hivi baada ya kula akakitwaa kikombe, akisema, Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu; fanyeni hivi kila mnywapo, kwa ukumbusho wangu.
Luc 22.20 Hébreux 9.15-9.20 Hébreux 13.20 2 Corinthiens 3.6 2 Corinthiens 3.14
26 Maana kila mwulapo mkate huu na kukinywea kikombe hiki, mwaitangaza mauti ya Bwana hata ajapo.
Jean 21.22 1 Corinthiens 4.5 Jean 14.3 1 Jean 2.28 Actes 1.11
27 Basi kila aulaye mkate huo, au kukinywea kikombe hicho cha Bwana isivyostahili, atakuwa amejipatia hatia ya mwili na damu ya Bwana.
Jean 6.51 Nombres 9.10 Nombres 9.13 1 Corinthiens 10.21 Lévitique 10.1-10.3
28 Lakini mtu ajihoji mwenyewe, na hivyo aule mkate, na kukinywea kikombe.
2 Corinthiens 13.5 Galates 6.4 Lamentations 3.40 Psaumes 26.2-26.7 Matthieu 5.23-5.24
29 Maana alaye na kunywa, hula na kunywa hukumu ya nafsi yake, kwa kutokuupambanua ule mwili.
1 Corinthiens 11.27 1 Corinthiens 11.30 1 Corinthiens 11.24 Ecclésiaste 8.5 Romains 13.2
30 Kwa sababu hiyo wako wengi kwenu walio hawawezi na dhaifu, na watu kadha wa kadha wamelala.
1 Thessaloniciens 4.14 Nombres 21.6-21.9 Nombres 20.12 1 Corinthiens 11.32 Exode 15.26
31 Lakini kama tungejipambanua nafsi zetu, tusingehukumiwa.
1 Jean 1.9 Psaumes 32.3-32.5 Jérémie 31.18-31.20 Apocalypse 3.2-3.3 Luc 15.18-15.20
32 Ila tuhukumiwapo, twarudiwa na Bwana, isije ikatupasa adhabu pamoja na dunia.
Hébreux 12.5-12.11 Psaumes 118.18 Apocalypse 3.19 1 Corinthiens 11.30 Proverbes 3.11-3.12
33 Kwa hiyo, ndugu zangu, mkutanikapo mpate kula, mngojaneni;
34 mtu akiwa na njaa, na ale nyumbani kwake; msipate kukutanika kwa hukumu. Na hayo yaliyosalia nijapo nitayatengeneza.
1 Corinthiens 11.21-11.22 1 Corinthiens 4.19 1 Corinthiens 7.17 Tite 1.5 1 Corinthiens 16.5

Cette Bible est dans le domaine public.