Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 23.8
Bible en Swahili de l’est


1 Paulo akawakazia macho watu wa baraza, akasema, Ndugu zangu, mimi kwa dhamiri safi kabisa nimeishi mbele za Mungu hata leo hivi.
2 Timothée 1.3 Actes 24.16 2 Corinthiens 1.12 Hébreux 13.18 1 Corinthiens 4.4
2 Kuhani Mkuu Anania akawaamuru wale waliosimama karibu naye wampige kinywa chake.
Actes 24.1 Jean 18.22 1 Rois 22.24 Michée 5.1 Matthieu 26.67
3 Ndipo Paulo akamwambia, Mungu atakupiga wewe, ukuta uliopakwa chokaa. Wewe umeketi kunihukumu sawasawa na sheria, nawe unaamuru nipigwe kinyume cha sheria?
Jean 7.51 Deutéronome 25.1-25.2 Matthieu 23.27-23.28 Ecclésiaste 3.16 Lévitique 19.35
4 Wale waliosimama karibu wakasema, Je! Unamtukana Kuhani Mkuu wa Mungu?
5 Paulo akasema, Sikujua, ndugu zangu, ya kuwa yeye ni Kuhani Mkuu; maana imeandikwa, Usimnenee mabaya mkuu wa watu wako.
Exode 22.28 Ecclésiaste 10.20 2 Pierre 2.10 Jude 1.8-1.9
6 Paulo alipotambua ya kuwa sehemu moja ni Masadukayo, na sehemu ya pili ni Mafarisayo, akapaza sauti yake katika ile baraza, Ndugu zangu, mimi ni Farisayo mwana wa Farisayo; mimi ninahukumiwa kwa ajili ya tumaini la ufufuo wa wafu.
Actes 24.21 Actes 24.15 Actes 26.5-26.8 Philippiens 3.5 Actes 28.20
7 Alipokwisha kunena hayo palikuwa na mashindano baina ya Mafarisayo na Masadukayo, mkutano ukafarakana.
Matthieu 10.34 Psaumes 55.9 Jean 7.40-7.43 Actes 14.4
8 Kwa maana Masadukayo husema ya kwamba hakuna kiyama wala malaika wala roho; bali Mafarisayo hukiri yote.
Matthieu 22.23 Luc 20.27 Marc 12.18 Actes 4.1
9 Pakawa na makelele mengi. Waandishi wengine wa upande wa Mafarisayo wakasimama, wakateta, wakisema, Hatuoni uovu wo wote katika mtu huyu; bali ikiwa roho au malaika amesema naye, ni nini?
Actes 22.7 Actes 22.17-22.18 Jean 12.29 Actes 25.25 Actes 26.31
10 Ugomvi mkubwa ulipotokea, yule jemadari akachelea Paulo asije akararuliwa nao, akaamuru askari washuke na kumwondoa kwa nguvu mikononi mwao, na kumleta ndani ya ngome.
Actes 22.24 Psaumes 50.22 Actes 21.30-21.36 Michée 3.3 Actes 23.27

Transfert de Paul à Césarée

11 Usiku ule Bwana akasimama karibu naye, akasema, Uwe na moyo mkuu; kwa sababu, kama ulivyonishuhudia habari zangu Yerusalemu, imekupasa kunishuhudia vivyo hivyo Rumi nako.
Actes 18.9 Actes 19.21 Matthieu 9.2 2 Timothée 4.17 Jérémie 15.19-15.21
12 Kulipopambauka, Wayahudi wakafanya mapatano, wakajifunga kwa kiapo kwamba hawatakula wala hawatakunywa hata wamwue Paulo.
Actes 23.21 Actes 23.30 Actes 23.14 2 Rois 6.31 Esaïe 8.9-8.10
13 Na hao walioapiana hivyo walipata zaidi ya watu arobaini.
Jean 16.2 2 Samuel 15.31 2 Samuel 15.12
14 Nao wakaenda kwa wakuu wa makuhani na wazee, wakasema, Tumejifunga kwa kiapo tusionje kitu hata tumwue Paulo.
Jérémie 8.12 Actes 23.12 Esaïe 3.9 Michée 7.3 Psaumes 52.1-52.2
15 Basi sasa ninyi pamoja na wazee wa baraza mwambieni jemadari amlete chini kwenu, kana kwamba mnataka kujua habari zake vizuri zaidi; na sisi tu tayari kumwua kabla hajakaribia.
Psaumes 37.32-37.33 Esaïe 59.7 Proverbes 4.16 Actes 22.30-23.1 Romains 3.14-3.16
16 Mjomba wake Paulo akasikia habari za kuotea kwao, akaenda akaingia ndani ya ngome akampasha Paulo habari.
Actes 23.10 Actes 23.32 Actes 21.34 Proverbes 21.30 Lamentations 3.37
17 Paulo akamwita akida mmoja, akasema, Mchukue kijana huyu kwa jemadari; maana ana neno la kumwarifu.
Actes 22.26 Proverbes 22.3 Matthieu 10.16 Actes 23.23 Matthieu 8.8-8.9
18 Basi akamchukua, akampeleka kwa jemadari, akamwambia, Paulo, yule mfungwa, aliniita akataka nikuletee kijana huyu kwa kuwa ana neno la kukuambia.
Ephésiens 3.1 Genèse 40.14-40.15 Actes 28.17 Luc 7.40 Actes 27.1
19 Yule jemadari akamshika mkono akajitenga pamoja naye kando, akamwuliza kwa faragha, Una neno gani utakalo kuniarifu?
Marc 9.27 Néhémie 2.4 Marc 10.51 Esther 9.12 Esther 7.2
20 Akasema Wayahudi wamepatana kukuomba umlete Paulo chini kesho, ukamweke mbele ya baraza, kana kwamba wanataka kupata habari zake kwa usahihi zaidi.
Actes 23.14-23.15 Psaumes 12.2 Actes 23.1 Daniel 6.5-6.12
21 Basi wewe usikubali; kwa maana watu zaidi ya arobaini wanamwotea, wamejifunga kwa kiapo wasile wala wasinywe hata watakapomwua; nao sasa wako tayari, wakiitazamia ahadi kwako.
Actes 23.12-23.14 Exode 23.2 Actes 25.3 Romains 9.3 Actes 9.23-9.24
22 Basi yule jemadari akamwacha kijana aende zake, akimwagiza, Usimwambie mtu awaye yote ya kwamba umeniarifu haya.
Marc 1.44 Josué 2.14
23 Akawaita maakida wawili, akasema, Wekeni tayari askari mia mbili kwenda Kaisaria, na askari wapanda farasi sabini, na wenye mikuki mia mbili, kwa saa tatu ya usiku.
Actes 23.33 Actes 8.40 Luc 12.38 Matthieu 14.25
24 Akawaambia kuweka wanyama tayari wampandishe Paulo, na kumchukua salama kwa Feliki liwali.
Actes 23.26 Actes 25.14 Actes 24.10 Actes 23.33-24.3 Esther 8.12
25 Akaandika barua, kwa namna hii,
26 Klaudio Lisia kwa liwali mtukufu Feliki, Salamu!
Actes 15.23 Actes 26.25 Actes 24.3 Luc 1.3 3 Jean 1.14
27 Mtu huyu alikamatwa na Wayahudi, wakawa karibu kumwua, ndipo nikaenda pamoja na kikosi cha askari nikamwokoa, nilipopata habari ya kuwa yeye ni Mrumi.
Actes 22.25-22.29 Actes 21.31-21.33 Actes 23.10 Actes 24.6
28 Nami nikitaka kulijua lile neno walilomshitakia, nikamtelemsha nikamweka mbele ya baraza;
Actes 22.30
29 nikaona kwamba ameshitakiwa kwa ajili ya maswali ya sheria yao, wala hakushitakiwa neno lo lote la kustahili kuuawa wala kufungwa.
Actes 26.31 Actes 18.15 Actes 25.25 Actes 28.18 Actes 23.6-23.9
30 Hata nilipopewa habari kwamba patakuwa na vitimvi juu ya mtu huyu, mara nikampeleka kwako, nikawaagiza na wale waliomshitaki, wanene habari zake mbele yako. Wasalamu.
Actes 23.20 Actes 24.19 Actes 25.16 Actes 23.35 Actes 25.5-25.6
31 Basi, wale askari wakamchukua Paulo kama walivyoamriwa, wakampeleka hata Antipatri usiku;
Luc 7.8 Actes 23.23-23.24 2 Timothée 2.3-2.4
32 hata asubuhi wakawaacha wale wapanda farasi waende pamoja naye, nao wakarudi zao ngomeni.
Actes 23.23 Actes 23.10
33 Na wale walipofika Kaisaria, na kumpa liwali ile barua, wakamweka Paulo mbele yake.
Actes 23.26 Actes 8.40 Actes 23.23-23.24 Actes 28.16
34 Naye alipokwisha kuisoma, akawauliza, Mtu huyu ni wa jimbo gani? Alipoarifiwa ya kuwa ni mtu wa Kilikia,
Actes 21.39 Actes 25.1 Luc 23.6 Esther 8.9 Actes 6.9
35 akasema, Nitakusikia wewe watakapokuja wale waliokushitaki; akaamuru alindwe katika nyumba ya uliwali ya Herode.
Actes 23.30 Actes 25.16 Matthieu 27.27 Matthieu 2.1 Actes 24.22

Cette Bible est dans le domaine public.