Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 12.13
Bible en Swahili de l’est


Arrestation et libération de Pierre

1 Panapo majira yale yale Herode mfalme akanyosha mikono yake kuwatenda mabaya baadhi ya watu wa kanisa.
Matthieu 24.9 Matthieu 10.17-10.18 Luc 22.53 Jean 16.2 Jean 15.20
2 Akamwua Yakobo, ndugu yake Yohana, kwa upanga.
Matthieu 20.23 Hébreux 11.37 Marc 10.35 Marc 10.38 Matthieu 4.21-4.22
3 Na akiona ya kuwa imewapendeza Wayahudi akaendelea akamshika na Petro. Siku hizo zilikuwa siku za mikate isiyochachwa.
Actes 24.27 Exode 23.15 Actes 25.9 Exode 12.14-12.20 Jean 21.18
4 Alipokwisha kumkamata, akamweka gerezani akamtia mikononi mwa vikosi vinne vya askari wanne wanne, wamlinde, akitaka baada ya Pasaka kumtoa na kumweka mbele ya watu.
Luc 21.12 Proverbes 19.21 Luc 22.33 Proverbes 27.1 Actes 4.28
5 Basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake.
Matthieu 18.19 2 Corinthiens 1.11 Actes 12.12 1 Thessaloniciens 5.17 Jacques 5.16
6 Hata wakati Herode alipotaka kumtoa, usiku ule ule Petro alikuwa analala katikati ya askari wawili, amefungwa minyororo miwili; walinzi mbele ya mlango wakailinda gereza.
Actes 21.33 Matthieu 28.4 Jérémie 40.4 1 Samuel 23.26-23.27 Deutéronome 32.26
7 Mara malaika wa Bwana akasimama karibu naye, nuru ikamulika mle chumbani, akampiga Petro ubavuni, akamwamsha, akisema, Ondoka upesi. Minyororo yake ikamwanguka mikononi.
Actes 16.26 Actes 5.19 1 Rois 19.7 Psaumes 142.6-142.7 Habakuk 3.11
8 Malaika akamwambia, Jifunge, kavae viatu vyako. Akafanya hivyo. Kisha akamwambia, Jivike nguo yako, ukanifuate.
9 Akatoka nje, akamfuata; wala hakujua ya kuwa ni kweli yaliyofanywa na malaika; bali alidhani kwamba anaona maono.
Psaumes 126.1 Actes 9.10 2 Corinthiens 12.1-12.3 Jean 2.5 Hébreux 11.8
10 Na walipopita lindo la kwanza na la pili, wakaja hata mlango wa chuma wa kuingilia mjini, ukawafungukia wenyewe. Wakatoka nje, wakapita katika njia moja; mara malaika akamwacha.
Actes 5.19 Actes 16.26 Esaïe 45.1-45.2 Apocalypse 3.7 Esaïe 21.8
11 Hata Petro alipopata fahamu akasema, Sasa nimejua yakini ya kuwa Bwana amempeleka malaika wake na kunitoa katika mkono wa Herode na katika kutazamia kote kwa taifa la Wayahudi.
Luc 15.17 Daniel 6.22 Daniel 3.28 Psaumes 34.7 Psaumes 33.18
12 Na alipokuwa akifikiri haya akafika nyumbani kwa Mariamu, mamaye Yohana, ambaye jina lake la pili ni Marko; na watu wengi walikuwa wamekutana humo wakiomba.
Actes 12.5 Actes 12.25 Philémon 1.24 Colossiens 4.10 Actes 13.5
13 Naye alipobisha kilango cha lango, kijakazi, jina lake Roda, akaja kusikiliza.
Luc 13.25 Actes 12.16 Jean 18.16-18.17
14 Alipoitambua sauti ya Petro, hakukifungua lango, kwa ajili ya furaha, bali alipiga mbio, akaingia ndani akawaambia kwamba Petro anasimama mbele ya lango.
Luc 24.41 Matthieu 28.8
15 Wakamwambia, Una wazimu. Lakini yeye akakaza sana, akasema ya kwamba ndivyo hivyo. Wakanena, Ni malaika wake.
Matthieu 18.10 Genèse 48.16 Luc 24.37-24.38 Marc 16.11 Marc 16.14
16 Petro akafuliza kugonga, hata walipokwisha kumfungulia wakamwona, wakastaajabu.
17 Naye akawapungia mkono wanyamaze, akawaeleza jinsi Bwana alivyomtoa katika gereza. Akasema, Kampasheni Yakobo na wale ndugu habari hizi. Akaondoka, akaenda mahali pengine.
Actes 21.40 Actes 13.16 Actes 19.33 Actes 15.13 Galates 2.12
18 Hata kulipopambauka askari wakaingiwa na fadhaa nyingi, amekuwaje Petro.
Actes 5.22-5.25 Actes 19.23 Actes 16.27
19 Na Herode alipomtafuta, asimwone, aliwauliza-uliza wale walinzi, akaamuru wauawe. Kisha akatelemkia kutoka Uyahudi kwenda Kaisaria, akakaa huko.
Actes 16.27 Jean 12.10-12.11 Esther 6.12 Actes 27.42 Matthieu 2.16
20 Naye Herode alikuwa amewakasirikia sana watu wa Tiro na Sidoni; wakamwendea kwa nia moja, na wakiisha kufanya urafiki na Blasto, mwenye kukitunza chumba cha mfalme cha kulalia, wakataka amani; kwa maana nchi yao ilipata riziki kwa nchi ya mfalme.
Ezéchiel 27.17 Esdras 3.7 Genèse 10.15 Esaïe 27.4-27.5 Luc 16.8
21 Basi siku moja iliyoazimiwa, Herode akajivika mavazi ya kifalme, akaketi katika kiti cha enzi, akatoa hotuba mbele yao.
22 Watu wakapiga kelele, wakisema, Ni sauti ya Mungu, si sauti ya mwanadamu.
Daniel 6.7 Psaumes 12.2 Jude 1.16 Apocalypse 13.4 Actes 14.10-14.13
23 Mara malaika wa Bwana akampiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na chango, akatokwa na roho.
1 Samuel 25.38 2 Samuel 24.16-24.17 Psaumes 115.1 Esaïe 51.8 Ezéchiel 28.2
24 Neno la Bwana likazidi na kuenea.
Actes 6.7 Actes 19.20 Actes 5.39 2 Thessaloniciens 3.1 Daniel 2.44
25 Na Barnaba na Sauli, walipokwisha kutimiza huduma yao, wakarejea kutoka Yerusalemu, wakamchukua pamoja nao Yohana aitwaye Marko.
Actes 12.12 Actes 15.37 Actes 4.36 Actes 11.29-11.30 1 Pierre 5.13

Cette Bible est dans le domaine public.