Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jean 14.29
Bible en Swahili de l’est


Jésus encourage les siens

1 Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi.
Jean 16.22-16.23 Jean 14.27-14.28 Esaïe 12.2-12.3 Esaïe 26.3 Ephésiens 1.12-1.13
2 Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali.
Jean 13.36 Hébreux 13.14 2 Corinthiens 5.1 Apocalypse 21.2 Apocalypse 3.12
3 Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo.
Jean 12.26 Jean 14.18-14.23 Jean 14.28 Actes 1.11 1 Thessaloniciens 4.16-4.17
4 Nami niendako mwaijua njia.
Jean 10.9 Jean 14.2 Jean 14.28 Jean 3.16-3.17 Jean 6.68-6.69
5 Tomaso akamwambia, Bwana, sisi hatujui uendako; nasi twaijuaje njia?
Jean 11.16 Marc 9.19 Marc 8.17-8.18 Luc 24.25 Jean 15.12
6 Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
Jean 10.9 Actes 4.12 Ephésiens 2.18 Jean 1.4 Jean 1.14
7 Kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba; tangu sasa mnamjua, tena mmemwona.
Jean 8.19 Luc 10.22 Colossiens 1.15-1.17 Jean 14.9-14.10 Jean 17.8
8 Filipo akamwambia, Bwana, utuonyeshe Baba, yatutosha.
Exode 33.18-33.23 Jean 1.43-1.46 Job 33.26 Apocalypse 22.3-22.5 Psaumes 17.15
9 Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba?
Hébreux 1.3 Colossiens 1.15 Jean 12.45 Philippiens 2.6 Jean 10.30
10 Husadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu? Hayo maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa shauri langu; lakini Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake.
Jean 5.19 Jean 10.38 Actes 10.38 Colossiens 2.9 Jean 8.28
11 Mnisadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu; la! Hamsadiki hivyo, sadikini kwa sababu ya kazi zenyewe.
Jean 5.36 Jean 10.38 Jean 10.25 Hébreux 2.4 Actes 2.22
12 Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba.
Matthieu 21.21 Marc 16.17 Luc 10.17-10.19 Actes 3.6-3.8 Actes 19.12
13 Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana.
Matthieu 7.7 Jean 15.7 Marc 11.24 Matthieu 21.22 1 Jean 5.14
14 Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya.

Promesse de l’envoi du Saint-Esprit

15 Mkinipenda, mtazishika amri zangu.
1 Jean 2.3-2.5 1 Jean 5.2-5.3 1 Jean 4.19-4.20 2 Jean 1.6 Jean 14.21-14.24
16 Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele;
Jean 15.26 Jean 14.26 1 Jean 2.1 Jean 16.7-16.15 Matthieu 28.20
17 ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu.
1 Jean 2.27 Jean 16.13 1 Corinthiens 2.14 Jean 15.26 1 Jean 4.6
18 Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu.
Jean 14.3 Matthieu 18.20 Matthieu 28.20 Jean 14.27-14.28 Psaumes 23.4
19 Bado kitambo kidogo na ulimwengu haunioni tena; bali ninyi mnaniona. Na kwa sababu mimi ni hai, ninyi nanyi mtakuwa hai.
Jean 16.16 Jean 7.33 Hébreux 7.25 Romains 5.10 Jean 6.56-6.58
20 Siku ile ninyi mtatambua ya kuwa mimi ni ndani ya Baba yangu, nanyi ndani yangu, nami ndani yenu.
Jean 15.5-15.7 Galates 2.20 Jean 17.26 Jean 10.38 Jean 14.10
21 Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye; naye anipendaye atapendwa na Baba yangu; nami nitampenda na kujidhihirisha kwake.
Jean 14.15 1 Jean 2.5 1 Jean 5.3 2 Jean 1.6 1 Jean 3.18-3.24
22 Yuda (siye Iskariote), akamwambia, Bwana, imekuwaje ya kwamba wataka kujidhihirisha kwetu, wala si kwa ulimwengu?
Luc 6.16 Actes 1.13 Jean 16.17-16.18 Jean 6.52 Matthieu 10.3
23 Yesu akajibu, akamwambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake.
Jean 14.21 Jean 14.15 Psaumes 91.1 1 Jean 4.15-4.16 1 Jean 2.24
24 Mtu asiyenipenda, yeye hayashiki maneno yangu; nalo neno mnalolisikia silo langu, ila ni lake Baba aliyenipeleka.
Jean 7.16 Matthieu 25.41-25.46 Jean 14.10 Jean 8.42 1 Jean 3.16-3.20
25 Hayo ndiyo niliyowaambia wakati nilipokuwa nikikaa kwenu.
Jean 15.11 Jean 14.29 Jean 17.6-17.8 Jean 13.19 Jean 16.1-16.4
26 Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.
Jean 15.26 Jean 14.16 Jean 16.7 Jean 2.22 1 Jean 2.20
27 Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga.
Philippiens 4.7 Jean 16.33 Esaïe 41.10 Colossiens 3.15 2 Timothée 1.7
28 Mlisikia ya kwamba mimi naliwaambia, Naenda zangu, tena naja kwenu. Kama mngalinipenda, mngalifurahi kwa sababu naenda kwa Baba, kwa maana Baba ni mkuu kuliko mimi.
Jean 14.18 Jean 5.18 Jean 14.12 Psaumes 47.5-47.7 Jean 14.2-14.4
29 Na sasa nimewaambia kabla halijatokea, kusudi litakapotokea mpate kuamini.
Jean 13.19 Matthieu 24.24-24.25 Jean 16.4-16.31
30 Mimi sitasema nanyi maneno mengi tena, kwa maana yuaja mkuu wa ulimwengu huu, wala hana kitu kwangu.
Apocalypse 12.9 1 Jean 5.19 Jean 12.31 Hébreux 4.15 Ephésiens 6.12
31 Lakini ulimwengu ujue ya kuwa nampenda Baba; na kama vile Baba alivyoniamuru; ndivyo nifanyavyo. Ondokeni, twendeni zetu.
Jean 10.18 Philippiens 2.8 Jean 12.49 Hébreux 5.7-5.8 Matthieu 26.39

Cette Bible est dans le domaine public.