Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jean 13.29
Bible en Swahili de l’est


Dernières instructions de Jésus à ses disciples

Jésus lave les pieds de ses disciples

1 Basi, kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu, hali akijua ya kuwa saa yake imefika, atakayotoka katika ulimwengu kwenda kwa Baba, naye ali amewapenda watu wake katika ulimwengu, aliwapenda upeo.
Jean 13.34 Jean 16.28 Jean 12.23 Jean 13.3 Jean 17.16
2 Hata wakati wa chakula cha jioni; naye Ibilisi amekwisha kumtia Yuda, mwana wa Simoni Iskariote, moyo wa kumsaliti;
Actes 5.3 Apocalypse 17.17 Jean 13.26-13.27 Esdras 7.27 Jacques 1.13-1.17
3 Yesu, hali akijua ya kuwa Baba amempa vyote mikononi mwake, na ya kuwa alitoka kwa Mungu naye anakwenda kwa Mungu,
Jean 8.42 Matthieu 28.18 Jean 3.35 Jean 17.2 Jean 16.27-16.28
4 aliondoka chakulani; akaweka kando mavazi yake, akatwaa kitambaa, akajifunga kiunoni.
Luc 22.27 Luc 12.37 2 Corinthiens 8.9 Luc 17.7 Philippiens 2.6-2.8
5 Kisha akatia maji katika bakuli, akaanza kuwatawadha wanafunzi miguu, na kuifuta kwa kile kitambaa alichojifunga.
Luc 7.44 2 Rois 3.11 Genèse 18.4 Genèse 19.2 1 Timothée 5.10
6 Hivyo yuaja kwa Simoni Petro. Huyo akamwambia, Bwana! Wewe wanitawadha miguu mimi?
Luc 5.8 Matthieu 3.11-3.14 Jean 1.27
7 Yesu akajibu, akamwambia, Nifanyalo wewe hujui sasa; lakini utalifahamu baadaye.
Jean 12.16 Daniel 12.12 Jean 13.36 Habakuk 2.1-2.3 Jérémie 32.24-32.25
8 Petro akamwambia, Wewe hutanitawadha miguu kamwe. Yesu akamwambia, Kama nisipokutawadha, huna shirika nami.
Tite 3.5 Hébreux 10.22 1 Corinthiens 6.11 Ephésiens 5.26 Actes 22.16
9 Simoni Petro akamwambia, Bwana, si miguu yangu tu, hata na mikono yangu na kichwa changu pia.
Psaumes 51.7 Psaumes 51.2 Psaumes 26.6 Hébreux 10.22 1 Pierre 3.21
10 Yesu akamwambia, Yeye aliyekwisha kuoga hana haja ila ya kutawadha miguu, bali yu safi mwili wote; nanyi mmekuwa safi, lakini si nyote.
Jean 15.3 2 Corinthiens 7.1 2 Corinthiens 5.17 Romains 7.20-7.23 Jérémie 50.20
11 Kwa maana alimjua yeye atakayemsaliti; ndiyo maana alisema, Si nyote mlio safi.
Jean 2.25 Matthieu 26.24-26.25 Jean 13.26 Jean 13.18 Jean 13.21
12 Basi alipokwisha kuwatawadha miguu, na kuyatwaa mavazi yake, na kuketi tena, akawaambia, Je! Mmeelewa na hayo niliyowatendea?
Jean 13.7 Jean 13.4 Matthieu 13.51 Ezéchiel 24.19 Marc 4.13
13 Ninyi mwaniita, Mwalimu, na, Bwana; nanyi mwanena vema, maana ndivyo nilivyo.
Philippiens 2.11 1 Corinthiens 12.3 Jean 11.28 Luc 6.46 1 Corinthiens 8.6
14 Basi ikiwa mimi, niliye Bwana na Mwalimu, nimewatawadha miguu, imewapasa vivyo kutawadhana miguu ninyi kwa ninyi.
1 Pierre 5.5 Luc 22.26-22.27 Romains 12.10 1 Corinthiens 9.19-9.22 Actes 20.35
15 Kwa kuwa nimewapa kielelezo; ili kama mimi nilivyowatendea, nanyi mtende vivyo.
Matthieu 11.29 Ephésiens 5.2 1 Pierre 2.21 Romains 15.5 1 Jean 2.6
16 Amin, amin, nawaambia ninyi, Mtumwa si mkuu kuliko bwana wake; wala mtume si mkuu kuliko yeye aliyempeleka.
Jean 15.20 Luc 6.40 Matthieu 10.24-10.25 Jean 3.5 Jean 3.3
17 Mkiyajua hayo, heri ninyi mkiyatenda.
Luc 11.28 Matthieu 7.24-7.25 Ezéchiel 36.27 Jacques 1.25 Galates 5.6
18 Sisemi habari za ninyi nyote; nawajua wale niliowachagua; lakini andiko lipate kutimizwa, Aliyekula chakula changu Ameniinulia kisigino chake.
Psaumes 41.9 Jean 17.12 Matthieu 26.23 Jean 13.26 Marc 14.20
19 Tangu sasa nawaambia kabla hayajatukia, ili yatakapotukia mpate kuamini ya kuwa mimi ndiye.
Jean 14.29 Jean 16.4 Jean 8.58 Apocalypse 1.17-1.18 Matthieu 11.3
20 Amin, amin, nawaambieni, Yeye ampokeaye mtu ye yote nimpelekaye, anipokea mimi; naye anipokeaye mimi; ampokea yeye aliyenipeleka.
Luc 10.16 Marc 9.37 Luc 9.48 Matthieu 25.40 Matthieu 10.40-10.42
21 Naye alipokwisha kusema hayo, Yesu alifadhaika rohoni, akashuhudia akisema, Amin, amin, nawaambieni, Mmoja wenu atanisaliti.
Matthieu 26.21 Jean 12.27 Marc 14.18 Jean 13.18 Jean 11.33
22 Wanafunzi wakatazamana, huku wakiona shaka ni nani amtajaye.
Luc 22.23 Matthieu 26.22 Marc 14.19 Genèse 42.1
23 Na palikuwapo mmoja wa wanafunzi wake, ameegama kifuani pa Yesu, ambaye Yesu alimpenda.
Jean 21.7 Jean 19.26 Jean 20.2 Jean 21.20 Jean 1.18
24 Basi Simoni Petro akampungia mkono, akamwambia, Uliza, ni nani amtajaye?
Luc 1.22 Actes 13.16 Actes 12.17 Luc 5.7 Actes 21.40
25 Basi yeye, hali akimwelekea Yesu kifua chake, akamwambia, Bwana, ni nani?
Jean 21.20 Esther 7.5 Genèse 44.4-44.12
26 Basi Yesu akajibu, Ndiye mtu yule nitakayemtowelea tonge na kumpa. Akatowelea tonge, akalitwaa akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskariote.
Matthieu 26.23 Luc 22.21 Marc 14.19-14.20 Jean 6.70-6.71 Jean 12.4-12.6
27 Na baada ya hilo tonge Shetani alimwingia. Basi Yesu akamwambia, Uyatendayo yatende upesi.
Luc 22.3 Jean 13.2 Daniel 2.15 Jacques 1.13-1.15 Psaumes 109.6
28 Wala hakuna mtu katika wale walioketi chakulani aliyeijua sababu ya kumwambia hivyo.
29 Kwa maana wengine walidhania, kwa kuwa Yuda huchukua mfuko, ya kwamba Yesu alimwambia kama, Nunua mnavyovihitaji kwa sikukuu; au kwamba awape maskini kitu.
Jean 12.5-12.6 Galates 2.10 Jean 13.1 Actes 20.34-20.35 Ephésiens 4.28
30 Basi huyo, akiisha kulipokea lile tonge, akatoka mara hiyo. Nako kulikuwa ni usiku.
Romains 3.15 Esaïe 59.7 Job 24.13-24.15 Proverbes 4.16 Luc 22.53
31 Basi huyo alipokwisha kutoka, Yesu alisema, Sasa ametukuzwa Mwana wa Adamu, naye Mungu ametukuzwa ndani yake.
1 Pierre 4.11 Jean 14.13 Jean 7.39 Jean 11.4 Colossiens 2.14-2.15
32 Mungu naye atamtukuza ndani ya nafsi yake; naye atamtukuza mara.
Jean 12.23 Jean 17.1 Apocalypse 22.1 Apocalypse 22.3 Apocalypse 21.22-21.23
33 Enyi watoto wadogo, bado kitambo kidogo nipo pamoja nanyi; mtanitafuta; na kama vile nilivyowaambia Wayahudi ya kwamba, Mimi niendako ninyi hamwezi kuja; kadhalika sasa nawaambia ninyi.
Jean 7.33-7.34 1 Jean 2.1 1 Jean 4.4 Jean 14.4-14.6 Galates 4.19
34 Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.
Lévitique 19.18 Ephésiens 5.2 1 Pierre 1.22 1 Corinthiens 12.26-12.27 Galates 6.2
35 Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.
1 Jean 4.20-4.21 1 Jean 3.10-3.14 Jean 17.21 1 Jean 2.5 1 Jean 2.10
36 Simoni Petro akamwambia, Bwana, unakwendapi? Yesu akamjibu, Niendako huwezi kunifuata sasa; lakini utanifuata baadaye.
2 Pierre 1.14 Jean 21.18-21.19 Jean 13.33 Jean 14.2 Jean 16.17
37 Petro akamwambia, Bwana, kwa nini mimi nisiweze kukufuata sasa? Mimi nitautoa uhai wangu kwa ajili yako.
Actes 20.24 Luc 22.31-22.34 Matthieu 26.31-26.35 Actes 21.13 Marc 14.27-14.31
38 Yesu akamjibu, Je! Wewe utautoa uhai wako kwa ajili yangu? Amin, amin, nakuambia, Jimbi hatawika hata wewe utakapokuwa umenikana mara tatu.
Proverbes 16.18 Marc 14.30 Marc 14.66-14.72 Matthieu 26.69-26.75 Jean 18.25-18.27

Cette Bible est dans le domaine public.