Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Luc 6.27
Bible en Swahili de l’est


Jésus et le sabbat

1 Ikawa siku ya sabato moja alikuwa akipita katika mashamba, wanafunzi wake wakawa wakivunja masuke na kuyala, wakiyapukusa-pukusa mikononi mwao.
Deutéronome 23.25 Matthieu 12.1-12.8 Marc 2.23-2.28 Lévitique 23.10-23.11 Lévitique 23.15
2 Basi baadhi ya Mafarisayo wakawaambia, Mbona mnafanya lisilo halali siku ya sabato?
Matthieu 12.2 Exode 22.10 Esaïe 58.13 Luc 5.33 Marc 2.24
3 Yesu akawajibu akawaambia, Hamkulisoma hata hilo alilolifanya Daudi, alipokuwa na njaa, yeye na wale aliokuwa nao?
1 Samuel 21.3-21.6 Matthieu 21.16 Marc 2.25-2.26 Marc 12.10 Matthieu 21.42
4 Jinsi alivyoingia katika nyumba ya Mungu, akaitwaa mikate ile ya Wonyesho, akaila akawapa na hao wenziwe, ambayo si halali kuila ila kwa makuhani peke yao.
Lévitique 24.5-24.9
5 Akawaambia, Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato.
Apocalypse 1.10 Marc 2.27 Marc 9.7
6 Ikawa siku ya sabato nyingine aliingia katika sinagogi akafundisha; na mlikuwamo mtu ambaye mkono wake wa kuume umepooza.
Marc 3.1-3.6 Matthieu 12.9-12.14 Matthieu 4.23 Jean 5.3 Luc 6.1
7 Na waandishi na Mafarisayo walikuwa wakimvizia, ili waone kwamba ataponya siku ya sabato; kusudi wapate neno la kumshitakia.
Luc 11.53-11.54 Luc 20.20 Marc 3.2 Jean 9.16 Luc 13.14
8 Lakini yeye akayatambua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, Ondoka, simama katikati; akaondoka akasimama.
Matthieu 9.4 Apocalypse 2.23 Hébreux 4.13 Job 42.2 Jean 9.4
9 Ndipo Yesu akawaambia, Nawauliza ninyi, Je! Ni halali siku ya sabato kutenda mema, au kutenda mabaya; kuponya roho au kuangamiza?
Luc 14.3 Marc 3.4 Matthieu 12.12-12.13 Jean 7.19-7.23 Luc 9.56
10 Akawakazia macho wote pande zote, akamwambia yule mtu, Nyosha mkono wako. Akaunyosha; mkono wake ukawa mzima tena.
Marc 3.5 Exode 4.6-4.7 1 Rois 13.6 Jean 5.8 Psaumes 107.20
11 Wakajawa na uchungu, wakashauriana wao kwa wao wamtendeje Yesu.
Actes 5.33 Jean 7.1 Matthieu 21.45 Actes 4.15 Actes 26.11

Choix des douze apôtres

12 Ikawa siku zile aliondoka akaenda mlimani ili kuomba, akakesha usiku kucha katika kumwomba Mungu.
Hébreux 5.7 Matthieu 14.23-14.25 Daniel 6.10 Genèse 32.24-32.26 Colossiens 4.2
13 Hata kulipokuwa mchana aliwaita wanafunzi wake; akachagua kumi na wawili miongoni mwao, ambao aliwaita Mitume;
Marc 6.7 Marc 6.30 Apocalypse 21.14 Marc 3.13-3.19 Matthieu 19.28
14 Simoni, aliyemwita jina la pili Petro, na Andrea nduguye, na Yakobo na Yohana, na Filipo na Bartolomayo,
Actes 1.13 Matthieu 4.21 Matthieu 4.18 Luc 5.8 Jean 21.15-21.24
15 na Mathayo na Tomaso, na Yakobo wa Alfayo, na Simoni aitwaye Zelote,
Matthieu 9.9 Marc 3.18 Actes 1.13 Jean 11.16 Actes 15.13
16 na Yuda wa Yakobo, na Yuda Iskariote, ndiye aliyekuwa msaliti.
Jean 14.22 Matthieu 26.14-26.16 Actes 1.25 Jean 6.70-6.71 Actes 1.16-1.20
17 Akashuka pamoja nao, akasimama mahali tambarare, pamoja na wanafunzi wake wengi, na makutano makubwa ya watu waliotoka Uyahudi wote na Yerusalemu, na pwani ya Tiro na Sidoni; waliokuja kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao;
Matthieu 11.21 Luc 5.15 Matthieu 15.21 Matthieu 12.15 Marc 7.24-7.31
18 na wale waliosumbuliwa na pepo wachafu; waliponywa.
Matthieu 17.15 Actes 5.16 Matthieu 15.22
19 Na makutano yote walikuwa wakitaka kumgusa, kwa sababu uweza ulikuwa ukimtoka ukiwaponya wote.
Matthieu 14.36 Matthieu 9.20-9.21 Marc 5.30 Marc 3.10 Luc 5.17

Le sermon sur la montagne

20 Akainua macho yake akawatazama wanafunzi wake, akasema, Heri ninyi mlio maskini, kwa sababu ufalme wa Mungu ni wenu.
Jacques 2.5 Jacques 1.9-1.10 Luc 12.32 2 Corinthiens 8.9 2 Corinthiens 6.10
21 Heri ninyi mlio na njaa sasa, kwa sababu mtashiba. Heri ninyi mliao sasa, kwa sababu mtacheka.
Jacques 1.12 Matthieu 5.4 Matthieu 5.6 1 Corinthiens 4.11 Esaïe 55.1-55.2
22 Heri ninyi watu watakapowachukia, na kuwatenga, na kuwashutumu, na kulitupa nje jina lenu kama neno ovu, kwa ajili ya Mwana wa Adamu.
Matthieu 10.22 Matthieu 5.10-5.12 Jean 16.2 1 Pierre 2.19-2.20 1 Pierre 4.12-4.16
23 Furahiwani siku ile na kuruka-ruka, kwa kuwa, tazama, thawabu yenu ni kubwa mbinguni, maana, baba zao waliwatenda manabii vivyo hivyo.
Matthieu 5.12 Apocalypse 2.7 Apocalypse 21.7 2 Chroniques 36.16 1 Pierre 4.13
24 Lakini, ole wenu ninyi mlio na mali, kwa kuwa faraja yenu mmekwisha kuipata.
Matthieu 6.2 Psaumes 49.6-49.7 Psaumes 49.16-49.19 Psaumes 73.3-73.12 Luc 16.19-16.25
25 Ole wenu ninyi ambao mmeshiba sasa, kwa kuwa mtaona njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka sasa, kwa kuwa mtaomboleza na kulia.
Esaïe 65.13 Proverbes 14.13 Jacques 4.9 Ecclésiaste 7.6 Ecclésiaste 2.2
26 Ole wenu ninyi watu wote watakapowasifu, kwa kuwa baba zao waliwatenda manabii wa uongo mambo kama hayo.
Matthieu 7.15 Michée 2.11 Jean 15.19 Jacques 4.4 Esaïe 30.10
27 Lakini nawaambia ninyi mnaosikia, Wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale ambao wawachukia ninyi,
Luc 6.35 1 Thessaloniciens 5.15 Galates 6.10 Romains 12.17-12.21 Matthieu 5.43-5.45
28 wabarikieni wale ambao wawalaani ninyi, waombeeni wale ambao wawaonea ninyi.
1 Pierre 3.9 Romains 12.14 Luc 23.34 1 Corinthiens 4.12 Jacques 3.10
29 Akupigaye shavu moja, mgeuzie la pili, naye akunyang’anyaye joho yako, usimzuilie na kanzu.
Hébreux 10.34 Esaïe 50.6 Luc 22.64 1 Corinthiens 6.7 Actes 23.2
30 Mpe kila akuombaye, na akunyang’anyaye vitu vyako, usitake akurudishie.
Deutéronome 15.7-15.10 Proverbes 21.26 2 Corinthiens 8.9 Matthieu 6.12 Matthieu 18.27-18.30
31 Na kama mnavyotaka watu wawatendee ninyi, watendeeni vivyo hivyo.
Matthieu 7.12 Matthieu 22.39 Galates 5.14 Jacques 2.8-2.16
32 Maana mkiwapenda wale wawapendao ninyi, mwaonyesha fadhili gani? Kwa kuwa hata wenye dhambi huwapenda wale wawapendao.
Matthieu 5.46-5.47 1 Pierre 2.19-2.20
33 Nanyi mkiwatendea mema wale wawatendeao mema, mwaonyesha fadhili gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo.
34 Na mkiwakopesha watu huku mkitumaini kupata kitu kwao, mwaonyesha fadhili gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi, ili warudishiwe vile vile.
Matthieu 5.42 Luc 14.12-14.14 Luc 6.35 Deutéronome 15.8-15.11
35 Bali wapendeni adui zenu, tendeni mema, na kukopesha msitumaini kupata malipo, na thawabu yenu itakuwa nyingi; nanyi mtakuwa wana wa Aliye juu, kwa kuwa yeye ni mwema kwa wasiomshukuru, na waovu.
Matthieu 5.44-5.45 Jean 13.35 Psaumes 112.5 Psaumes 145.9 Proverbes 22.9
36 Basi, iweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma.
Matthieu 5.48 Ephésiens 5.1-5.2 Ephésiens 4.31 1 Pierre 1.15-1.16
37 Msihukumu, nanyi hamtahukumiwa; msilaumu, nanyi hamtalaumiwa; achilieni, nanyi mtaachiliwa.
Colossiens 3.13 Marc 11.25 Romains 14.3-14.4 Ephésiens 4.32 1 Corinthiens 4.3-4.5
38 Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa.
Marc 4.24 2 Corinthiens 9.6-9.8 Matthieu 7.2 Proverbes 3.9-3.10 Deutéronome 15.10
39 Akawaambia mithali, Je! Aliye kipofu aweza kuongoza kipofu? Hawatatumbukia shimoni wote wawili?
Matthieu 15.14 2 Timothée 3.13 Jérémie 14.15-14.16 Matthieu 23.16-23.26 Esaïe 9.16
40 Mwanafunzi hawi mkuu kuliko mwalimu wake, lakini kila mtu ambaye amehitimu hulingana na mwalimu wake.
Jean 13.16 Jean 15.20 Matthieu 10.24-10.25 Matthieu 23.15
41 Basi, mbona wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe huiangalii?
Jean 8.7 Jacques 1.24 Ezéchiel 18.28 Romains 2.21-2.24 Jérémie 17.9
42 Au, utawezaje kumwambia ndugu yako, Ndugu yangu, niache nikitoe kibanzi kilicho ndani ya jicho lako, nawe huiangalii boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe, itoe kwanza ile boriti katika jicho lako mwenyewe, ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi kilichomo katika jicho la ndugu yako.
Actes 13.10 Romains 2.1 2 Timothée 2.21 Actes 2.38 Actes 8.21
43 Kwa maana hakuna mti mzuri uzaao matunda mabaya, wala mti mbaya uzaao matunda mazuri;
Jérémie 2.21 Matthieu 3.10 Matthieu 12.33 Esaïe 61.3 Matthieu 7.16-7.20
44 kwa kuwa kila mti hutambulikana kwa matunda yake; maana, katika miiba hawachumi tini, wala katika michongoma hawachumi zabibu.
Jacques 3.12 Matthieu 12.33 Jude 1.12 Galates 5.19-5.23 Tite 2.11-2.13
45 Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake.
Proverbes 4.23 Ephésiens 4.29 Matthieu 12.34-12.37 Colossiens 4.6 Jean 7.38
46 Na kwa nini mnaniita, Bwana, Bwana, walakini hamyatendi nisemayo?
Malachie 1.6 Matthieu 7.21-7.23 Luc 13.25-13.27 Galates 6.7 Jean 13.13-13.17
47 Kila mtu ajaye kwangu, na kuyasikia maneno yangu na kuyatenda, nitawaonyesha mfano wake.
Jacques 1.22-1.25 Luc 11.28 Jacques 4.17 Matthieu 7.24-7.27 Romains 2.7-2.10
48 Mfano wake ni mtu ajengaye nyumba, na kuchimba chini sana, na kuweka msingi juu ya mwamba; na kulipokuja gharika, mto uliishukia nyumba ile kwa nguvu, usiweze kuitikisa; kwa kuwa imejengwa vizuri.
Esaïe 28.16 1 Corinthiens 3.10-3.15 Psaumes 62.2 Jude 1.24 Apocalypse 6.14-6.17
49 Lakini yule aliyesikia ila hakutenda, mfano wake ni mtu aliyejenga nyumba juu ya ardhi pasipokuwa na msingi, mto ukaishukia kwa nguvu, ikaanguka mara; na maangamizi yake nyumba ile yakawa makubwa.
Proverbes 28.18 1 Thessaloniciens 3.5 Jean 15.2 Actes 20.29 1 Jean 2.19

Cette Bible est dans le domaine public.