Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Marc 4.32
Bible en Swahili de l’est


Le semeur et les terrains

1 Akaanza kufundisha tena kando ya bahari. Wakamkusanyikia mkutano mkubwa mno, hata yeye akapanda chomboni, akakaa baharini, mkutano wote ulikuwako juu ya nchi kavu kando ya bahari.
Marc 2.13 Luc 5.1-5.3 Luc 8.4-8.10 Matthieu 13.1-13.15 Marc 3.7
2 Akawafundisha mambo mengi kwa mifano, akawaambia katika mafundisho yake,
Marc 4.11 Matthieu 13.34-13.35 Marc 3.23 Matthieu 13.10 Matthieu 13.3
3 Sikilizeni; Tazama, mpanzi alitoka kwenda kupanda;
1 Corinthiens 3.6-3.9 Matthieu 13.26 Luc 8.5-8.8 Deutéronome 4.1 Jean 4.35-4.38
4 ikawa alipokuwa akipanda, mbegu nyingine ilianguka kando ya njia, wakaja ndege wakaila.
Matthieu 13.19 Genèse 15.11 Matthieu 13.4 Marc 4.15 Luc 8.5
5 Nyingine ikaanguka penye mwamba, pasipokuwa na udongo mwingi; mara ikaota kwa kuwa na udongo haba;
Amos 6.12 Ezéchiel 36.26 Matthieu 13.5-13.6 Matthieu 13.20 Luc 8.6
6 hata jua lilipozuka iliungua, na kwa kuwa haina mizizi ikanyauka.
Jacques 1.11 Colossiens 2.7 Cantique 1.6 2 Thessaloniciens 2.10 Esaïe 25.4
7 Nyingine ikaanguka penye miiba; ile miiba ikamea ikaisonga, isizae matunda.
Jérémie 4.3 Genèse 3.17-3.18 Matthieu 13.7 1 Jean 2.15-2.16 Luc 8.14
8 Nyingine zikaanguka penye udongo ulio mzuri, zikazaa matunda, zikimea na kukua, na kuzaa, moja thelathini, moja sitini, na moja mia.
Jean 15.5 Marc 4.20 Colossiens 1.6 Genèse 26.12 Matthieu 13.8
9 Akasema, Aliye na masikio ya kusikilia, na asikie.
Matthieu 11.15 Marc 4.23-4.24 Luc 8.18 Marc 7.14-7.15 Matthieu 15.10
10 Naye alipokuwa peke yake, wale watu waliomzunguka, na wale Thenashara, walimwuliza habari za ile mifano.
Matthieu 13.10-13.17 Marc 4.34 Marc 7.17 Proverbes 13.20 Matthieu 13.36
11 Akawaambia, Ninyi mmejaliwa kuijua siri ya ufalme wa Mungu, bali kwa wale walio nje yote hufanywa kwa mifano,
Matthieu 11.25 1 Timothée 3.7 Colossiens 4.5 1 Thessaloniciens 4.12 1 Corinthiens 5.12-5.13
12 ili wakitazama watazame, wasione; Na wakisikia wasikie, wasielewe; Wasije wakaongoka, na kusamehewa.
Esaïe 6.9-6.10 Jérémie 5.21 Esaïe 44.18 Deutéronome 29.4 Matthieu 13.14-13.15
13 Akawaambia, Hamjui mfano huu? Basi mifano yote mtaitambuaje?
Apocalypse 3.19 Matthieu 15.15-15.17 Luc 24.25 Luc 8.11-8.15 Matthieu 13.51-13.52
14 Mpanzi huyo hulipanda neno.
Matthieu 13.37 Marc 2.2 Colossiens 1.5-1.6 Marc 4.3 Matthieu 13.19
15 Hawa ndio walio kando ya njia lipandwapo neno; nao, wakiisha kusikia, mara huja Shetani, akaliondoa lile neno lililopandwa mioyoni mwao.
1 Pierre 5.8 Apocalypse 20.10 Apocalypse 20.7 Apocalypse 20.2-20.3 Actes 26.31-26.32
16 Kadhalika na hawa ndio wapandwao penye miamba, ambao kwamba wakiisha kulisikia lile neno, mara hulipokea kwa furaha;
Marc 6.20 Ezéchiel 33.31-33.32 Matthieu 13.20-13.21 Jean 5.35 Luc 8.13
17 ila hawana mizizi ndani yao, bali hudumu muda mchache; kisha ikitokea dhiki au udhia kwa ajili ya lile neno, mara hujikwaa.
Matthieu 12.31 Matthieu 11.6 1 Thessaloniciens 3.3-3.5 Job 19.28 2 Timothée 1.15
18 Na hawa ndio wale wapandwao penye miiba; ni watu walisikiao lile neno,
Marc 4.7 Luc 8.14 Jérémie 4.3 Matthieu 13.22
19 na shughuli za dunia, na udanganyifu wa mali, na tamaa za mambo mengine zikiingia, hulisonga lile neno, likawa halizai.
1 Timothée 6.17 1 Timothée 6.9-6.10 2 Timothée 4.10 1 Jean 2.15-2.17 1 Pierre 4.2-4.3
20 Na hawa ndio waliopandwa penye udongo ulio mzuri; ni watu walisikiao lile neno na kulipokea, na kuzaa matunda, mmoja thelathini, mmoja sitini, na mmoja mia.
Marc 4.8 Romains 7.4 Jean 15.4-15.5 Genèse 26.12 Philippiens 1.11
21 Akawaambia, Mwaonaje? Taa huja ili kuwekwa chini ya pishi, au mvunguni? Si kuwekwa juu ya kiango?
Matthieu 5.15 Luc 11.33 Luc 8.16 1 Corinthiens 12.7 Ephésiens 5.3-5.15
22 Kwa maana hakuna neno lililositirika, ila makusudi lije likadhihirika; wala hakuna lililofichwa, ila makusudi lije likatokea wazi.
Luc 8.17 Actes 4.20 1 Corinthiens 4.5 Psaumes 40.9-40.10 Ecclésiaste 12.14
23 Mtu akiwa na masikio ya kusikilia, na asikie.
Marc 4.9 Matthieu 11.15 Apocalypse 2.17 Apocalypse 2.29 Apocalypse 2.7
24 Akawaambia, Angalieni msikialo; kipimo kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa, na tena mtazidishiwa.
Matthieu 7.2 2 Pierre 2.1-2.3 Luc 8.18 1 Jean 4.1 Jean 10.16
25 Kwa maana mwenye kitu atapewa, naye asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang’anywa.
Matthieu 13.12 Luc 8.18 Jean 15.2 Luc 19.24-19.26 Luc 16.9-16.12

La semence et la graine de moutarde

26 Akasema, Ufalme wa Mungu, mfano wake ni kama mtu aliyemwaga mbegu juu ya nchi;
Matthieu 13.24 Jean 4.36-4.38 1 Pierre 1.23-1.25 Ecclésiaste 11.6 Luc 8.5
27 akawa akilala na kuondoka, usiku na mchana, nayo mbegu ikamea na kukua, asivyojua yeye.
Ecclésiaste 11.5 2 Thessaloniciens 1.3 2 Pierre 3.18 1 Corinthiens 15.37-15.38 Ecclésiaste 8.17
28 Maana nchi huzaa yenyewe; kwanza jani, tena suke, kisha ngano pevu katika suke.
Marc 4.31-4.32 Philippiens 1.6 Philippiens 1.9-1.11 Ecclésiaste 3.11 Psaumes 92.13-92.14
29 Hata matunda yakiiva, mara atapeleka mundu, kwa kuwa mavuno yamefika.
Joël 3.13 Matthieu 13.40-13.43 Apocalypse 14.13-14.17 2 Timothée 4.7-4.8 Matthieu 13.30
30 Akasema, Tuulinganishe na nini ufalme wa Mungu? Au tuutie katika mfano gani?
Matthieu 13.31-13.32 Matthieu 13.24 Matthieu 11.16 Luc 13.18-13.21 Lamentations 2.13
31 Ni kama punje ya haradali, ambayo ipandwapo katika nchi, ingawa ni ndogo kuliko mbegu zote zilizo katika nchi,
Amos 9.11-9.15 Malachie 1.11 Actes 19.20 Esaïe 60.22 Genèse 22.17-22.18
32 lakini ikiisha kupandwa hukua, ikawa kubwa kuliko miti yote ya mboga, ikafanya matawi makubwa; hata ndege wa angani waweza kukaa chini ya uvuli wake.
Lamentations 4.20 Cantique 2.3 Proverbes 4.18 Daniel 4.10-4.14 Psaumes 91.1
33 Kwa mifano mingi ya namna hii alikuwa akisema nao neno lake, kwa kadiri walivyoweza kulisikia;
Jean 16.12 Hébreux 5.11-5.14 Matthieu 13.34-13.35 1 Corinthiens 3.1-3.2
34 wala pasipo mfano hakusema nao; lakini akawaeleza wanafunzi wake mwenyewe mambo yote kwa faragha.
Jean 16.25 Matthieu 15.15-15.20 Matthieu 13.36-13.43 Luc 24.27 Marc 4.10

Jésus, plus fort que la nature et les démons

35 Siku ile kulipokuwa jioni, akawaambia, Na tuvuke mpaka ng’ambo.
Matthieu 8.18 Luc 8.22 Matthieu 8.23-8.27 Jean 6.1 Marc 6.45
36 Wakauacha mkutano, wakamchukua vile vile alivyo katika chombo. Na vyombo vingine vilikuwako pamoja naye.
Marc 3.9 Marc 4.1 Marc 5.2 Marc 5.21
37 Ikatokea dhoruba kuu ya upepo, mawimbi yakakipiga chombo hata kikaanza kujaa maji.
Job 1.19 Matthieu 8.23-8.24 Psaumes 107.23-107.31 Job 1.12 Luc 8.22-8.23
38 Naye mwenyewe alikuwapo katika shetri, amelala juu ya mto; wakamwamsha, wakamwambia, Mwalimu, si kitu kwako kuwa tunaangamia?
1 Pierre 5.7 Esaïe 54.6-54.8 Esaïe 64.12 1 Rois 18.27-18.29 Psaumes 77.7-77.10
39 Akaamka, akaukemea upepo, akaiambia bahari, Nyamaza, utulie. Upepo ukakoma, kukawa shwari kuu.
Psaumes 89.9 Psaumes 29.10 Psaumes 107.29 Psaumes 65.7 Job 38.11
40 Akawaambia, Mbona mmekuwa waoga? Hamna imani bado?
Esaïe 43.2 Matthieu 16.8 Matthieu 14.31 Luc 8.25 Esaïe 42.3
41 Wakaingiwa na hofu kuu, wakaambiana, Ni nani huyu, basi, hata upepo na bahari humtii?
Luc 8.25 Matthieu 14.32 Psaumes 89.7 1 Samuel 12.24 Matthieu 8.27

Cette Bible est dans le domaine public.