Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Marc 3
Bible en Swahili de l’est


1 Akaingia tena katika sinagogi; na palikuwako huko mtu mwenye mkono uliopooza;
Luc 6.6-6.11 Matthieu 12.9-12.14 Marc 1.21
2 wakamvizia ili kuona kama atamponya siku ya sabato; wapate kumshitaki.
Luc 14.1 Psaumes 37.32 Luc 20.20 Luc 6.7 Luc 11.53-11.54
3 Akamwambia yule mtu mwenye mkono uliopooza, Simama katikati.
Jean 9.4 Philippiens 1.28-1.30 Daniel 6.10 1 Pierre 4.1 Esaïe 42.4
4 Akawauliza, Ni halali siku ya sabato kutenda mema, au kutenda mabaya? Kuponya roho au kuiua? Wakanyamaza.
Luc 6.9 Matthieu 12.10-12.12 Luc 14.1-14.5 Marc 2.27-2.28 Osée 6.6
5 Akawakazia macho pande zote kwa hasira, akiona huzuni kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao, akamwambia yule mtu, Nyosha mkono wako. Naye akaunyosha; mkono wake ukawa mzima tena.
Luc 6.10 Ephésiens 4.26 Romains 11.25 Ephésiens 4.18 Matthieu 12.13
6 Mara wakatoka wale Mafarisayo, wakawa wakifanya shauri juu yake pamoja na Maherodi, jinsi ya kumwangamiza.
Matthieu 22.16 Marc 12.13 Matthieu 12.14 Marc 8.15 Luc 22.2
7 Naye Yesu akajitenga, yeye na wanafunzi wake, akaenda baharini. Mkutano mkuu ukamfuata, kutoka Galilaya, na Uyahudi,
Luc 6.17 Matthieu 4.25 Matthieu 12.15 Luc 6.12 Josué 20.7
8 na Yerusalemu, na Idumaya, na ng’ambo ya Yordani, na pande za Tiro na Sidoni, mkutano mkuu, waliposikia habari za mambo yote aliyokuwa akiyatenda, wakamwendea.
Ezéchiel 35.15 Esaïe 34.5 Ezéchiel 36.5 Matthieu 11.21 Josué 13.8-13.14
9 Akawaambia wanafunzi wake ya kwamba chombo kidogo kikae karibu naye, kwa sababu ya mkutano, wasije wakamsonga.
Marc 5.30 Jean 6.15
10 Maana aliponya wengi, hata wote waliokuwa na misiba wakamrukia wapate kumgusa.
Marc 6.56 Matthieu 14.36 Actes 19.11-19.12 Matthieu 4.23 Luc 7.2
11 Na pepo wachafu, kila walipomwona, walianguka mbele yake, wakalia wakisema, Wewe ndiwe Mwana wa Mungu.
Matthieu 4.3 Luc 4.41 Matthieu 8.29 Luc 8.28 Marc 1.23-1.24
12 Akawakataza sana, wasimdhihirishe.
Matthieu 12.16 Marc 1.34 Actes 16.18 Marc 1.25 Matthieu 8.4

Choix des douze apôtres

13 Akapanda mlimani, akawaita aliowataka mwenyewe; wakamwendea.
Luc 9.1 Matthieu 5.1 Marc 6.7 Matthieu 10.1-10.4 Luc 6.12-6.16
14 Akaweka watu kumi na wawili, wapate kuwa pamoja naye, na kwamba awatume kuhubiri,
Jean 15.16 Galates 1.1 Actes 1.8 Luc 9.1-9.6 Actes 1.24-1.25
15 tena wawe na amri ya kutoa pepo.
16 Akawaweka wale Thenashara; na Simoni akampa jina la Petro;
Jean 1.42 Actes 1.13 Marc 1.16 Luc 6.14-6.16 1 Corinthiens 1.12
17 na Yakobo, mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye Yakobo, akawapa jina la Boanerge, maana yake, wana wa ngurumo;
Marc 10.35 Marc 1.19-1.20 Marc 5.37 Hébreux 4.12 Esaïe 58.1
18 na Andrea, na Filipo, na Bartholomayo, na Mathayo, na Tomaso, na Yakobo wa Alfayo, na Thadayo, na Simoni Mkananayo,
Actes 1.13 Marc 2.14 Matthieu 9.9 Actes 21.18 1 Corinthiens 15.7
19 na Yuda Iskariote, ndiye aliyemsaliti. Kisha akaingia nyumbani.
Matthieu 27.3-27.5 Jean 6.64 Actes 1.16-1.25 Matthieu 26.14-26.16 Jean 13.2

Jésus contesté

20 Mkutano wakakusanyika tena, hata wao wenyewe wasiweze hata kula mkate.
Marc 6.31 Jean 4.31-4.34 Marc 9.28 Marc 7.17 Marc 3.9
21 Jamaa zake walipopata habari wakatoka kwenda kumkamata; maana walisema, Amerukwa na akili.
Actes 26.24 Jean 10.20 Marc 3.31 2 Corinthiens 5.13 Jean 7.3-7.10
22 Nao waandishi walioshuka kutoka Yerusalemu wakasema, Ana Beelzebuli, na, Kwa mkuu wa pepo huwatoa pepo.
Matthieu 9.34 Matthieu 10.25 Matthieu 15.1 Matthieu 12.24 Jean 7.20
23 Akawaita, akawaambia kwa mifano, Awezaje Shetani kumtoa Shetani?
Matthieu 13.34 Matthieu 12.25-12.30 Psaumes 49.4 Luc 11.17-11.23 Marc 4.2
24 Na ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, ufalme huo hauwezi kusimama;
1 Corinthiens 1.10-1.13 Esaïe 19.2-19.3 1 Rois 12.16-12.20 Ezéchiel 37.22 Esaïe 9.20-9.21
25 na nyumba ikifitinika juu ya nafsi yake, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
Genèse 37.4 Genèse 13.7-13.8 Jacques 3.16 Psaumes 133.1 Galates 5.15
26 Na kama Shetani ameondoka juu ya nafsi yake, akafitinika, hawezi kusimama, bali huwa na kikomo.
27 Hawezi mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu, na kuviteka vitu vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu; ndipo atakapoiteka nyumba yake.
Matthieu 12.29 Ephésiens 6.10-6.13 Hébreux 2.14 Esaïe 53.12 Luc 11.21-11.23
28 Amin, nawaambia, Dhambi zote watasamehewa wanadamu, na kufuru zao watakazokufuru zote;
Matthieu 12.31-12.32 Luc 12.10 1 Jean 5.16 Hébreux 6.4-6.8 Marc 3.28-3.30
29 bali mtu atakayemkufuru Roho Mtakatifu hana msamaha hata milele; ila atakuwa ana dhambi ya milele,
Luc 12.10 Matthieu 12.31-12.32 Matthieu 25.46 2 Thessaloniciens 1.9 Marc 12.40
30 kwa vile walivyosema, Ana pepo mchafu.
Marc 3.22 Jean 10.20
31 Wakaja mamaye na nduguze; wakasimama nje, wakatuma mtu kumwita.
Luc 8.19-8.21 Matthieu 12.46-12.50
32 Na makutano walikuwa wameketi, wakimzunguka, wakamwambia, Tazama, mama yako na ndugu zako wako nje, wanakutafuta.
33 Akawajibu, akisema, Mama yangu na ndugu zangu ni akina nani?
Marc 3.21 Marc 6.3 Jean 7.3-7.5 Deutéronome 33.9 Jean 2.4
34 Akawatazama wale walioketi wakimzunguka pande zote, akasema, Tazama, mama yangu na ndugu zangu!
Cantique 4.9-4.10 Romains 8.29 Matthieu 25.40-25.45 Cantique 5.1-5.2 Matthieu 12.49-12.50
35 Kwa maana mtu ye yote atakayeyafanya mapenzi ya Mungu, huyo ndiye ndugu yangu, na umbu langu, na mama yangu.
Matthieu 7.21 1 Jean 2.17 Jean 7.17 Jacques 1.25 1 Jean 3.22-3.23

Cette Bible est dans le domaine public.