Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 3.5
Bible en Swahili de l’est


Ministère de Jean-Baptiste

1 Siku zile aliondokea Yohana Mbatizaji akihubiri katika nyika ya Uyahudi, na kusema,
Esaïe 40.3-40.6 Juges 1.16 Jean 1.6-1.8 Josué 14.10 Matthieu 16.14
2 Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia.
Matthieu 4.17 Matthieu 6.10 Daniel 2.44 Marc 1.15 Matthieu 10.7
3 Kwa sababu huyo ndiye aliyenenwa na nabii Isaya, akisema, Sauti ya mtu aliaye nyikani, Itengenezeni njia ya Bwana, Yanyosheni mapito yake.
Esaïe 40.3 Jean 1.23 Luc 1.76 Malachie 3.1 Luc 1.17
4 Naye Yohana mwenyewe alikuwa na vazi lake la singa za ngamia, na mshipi wa ngozi kiunoni mwake; na chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu.
2 Rois 1.8 Lévitique 11.22 Zacharie 13.4 Matthieu 11.8 Marc 1.6
5 Ndipo walipomwendea Yerusalemu, na Uyahudi wote, na nchi zote za kandokando ya Yordani;
Marc 1.5 Matthieu 4.25 Matthieu 11.7-11.12 Jean 5.35 Luc 3.7
6 naye akawabatiza katika mto wa Yordani, huku wakiziungama dhambi zao.
Actes 19.18 Actes 2.38-2.41 Marc 1.5 Actes 1.5 Matthieu 3.11
7 Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?
Matthieu 23.33 Matthieu 12.34 1 Thessaloniciens 1.10 Matthieu 22.23 Romains 5.9
8 Basi zaeni matunda yapasayo toba;
Actes 26.20 Ephésiens 5.9 Galates 5.22-5.23 Luc 3.8 Jérémie 36.3
9 wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba Mungu aweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto.
Actes 13.26 Romains 9.7-9.8 Jean 8.33 Romains 4.1 Jean 8.53
10 Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.
Jean 15.6 Jean 15.2 Matthieu 7.19 Luc 13.6-13.9 Luc 3.9
11 Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
Actes 1.5 Luc 3.16 Esaïe 4.4 Ephésiens 3.8 Marc 1.7-1.8
12 Ambaye pepeto lake li mkononi mwake, naye atausafisha sana uwanda wake; na kuikusanya ngano yake ghalani, bali makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.
Malachie 4.1 Luc 3.17 Matthieu 13.30 Jérémie 7.20 Esaïe 41.16
13 Wakati huo Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka Yordani kwa Yohana ili abatizwe.
Matthieu 2.22 Jean 1.32-1.34 Marc 1.9-1.11 Luc 3.21-3.22
14 Lakini Yohana alitaka kumzuia, akisema, Mimi nahitaji kubatizwa na wewe, nawe waja kwangu?
Jean 13.6-13.8 Galates 3.27-3.29 Jean 3.3-3.7 Luc 1.43 Galates 3.22
15 Yesu akajibu akamwambia, Kubali hivi sasa; kwa kuwa ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote. Basi akamkubali.
Jean 8.29 Jean 4.34 Esaïe 42.21 Jean 15.10 1 Pierre 2.21-2.24
16 Naye Yesu alipokwisha kubatizwa mara akapanda kutoka majini; na tazama, mbingu zikamfunukia, akamwona Roho wa Mungu akishuka kama hua, akija juu yake;
Marc 1.10 Luc 3.21-3.22 Esaïe 42.1 Esaïe 11.2 Jean 1.31-1.34
17 na tazama, sauti kutoka mbinguni ikisema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye.
Psaumes 2.7 Matthieu 17.5 Esaïe 42.1 Luc 9.35 2 Pierre 1.17

Cette Bible est dans le domaine public.