Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 19.11
Bible en Swahili de l’est


Ministère de Jésus en Judée

Divorce et célibat

1 Ikawa Yesu alipomaliza maneno hayo, akatoka Galilaya akafika mipaka ya Uyahudi, ng’ambo ya Yordani.
Jean 10.40 Marc 10.1-10.12 Matthieu 7.28 Matthieu 19.1-19.9
2 Makutano mengi wakamfuata, akawaponya huko.
Matthieu 12.15 Marc 6.55-6.56 Matthieu 15.30-15.31 Matthieu 14.35-14.36 Matthieu 9.35-9.36
3 Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamjaribu, wakimwambia, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe kwa kila sababu?
Marc 10.2 Hébreux 3.9 Marc 12.13 Matthieu 22.35 Luc 11.53-11.54
4 Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,
Genèse 5.2 Genèse 1.27 Genèse 2.18 Luc 10.26 Genèse 2.23
5 akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?
1 Corinthiens 6.16 Ephésiens 5.31 Genèse 2.21-2.24 1 Rois 11.2 Deutéronome 4.4
6 Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.
Romains 7.2 Marc 10.9 1 Corinthiens 7.10-7.14 Malachie 2.14 Hébreux 13.4
7 Wakamwambia, Jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha?
Deutéronome 24.1-24.4 Matthieu 5.31 Jérémie 3.8 Marc 10.4 Esaïe 50.1
8 Akawaambia, Musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi.
Malachie 2.13-2.14 Matthieu 3.15 Genèse 2.24 Marc 10.5 Psaumes 95.8
9 Nami nawaambia ninyi, Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini.
Matthieu 5.32 1 Corinthiens 7.39 Luc 16.18 1 Corinthiens 7.10-7.13 Jérémie 3.8
10 Wanafunzi wake wakamwambia, Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa.
1 Corinthiens 7.32-7.35 Proverbes 5.15-5.19 1 Timothée 5.11-5.15 Proverbes 18.22 Proverbes 19.13-19.14
11 Lakini yeye akawaambia, Si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa.
1 Corinthiens 7.17 1 Corinthiens 7.35 1 Corinthiens 7.2 Matthieu 13.11 1 Corinthiens 7.7-7.9
12 Maana wako matowashi waliozaliwa hali hiyo toka matumboni mwa mama zao; tena wako matowashi waliofanywa na watu kuwa matowashi; tena wako matowashi waliojifanya kuwa matowashi kwa ajili ya ufalme wa mbinguni. Awezaye kulipokea neno hili, na alipokee.
Esaïe 56.3-56.4 1 Corinthiens 9.5 1 Corinthiens 9.15 1 Corinthiens 7.32-7.38 Esaïe 39.7

Les premiers et les derniers

13 Ndipo akaletewa watoto wadogo ili aweke mikono yake juu yao na kuwaombea; wanafunzi wake wakawakemea.
Jérémie 32.39 Genèse 48.9-48.20 Matthieu 18.2-18.5 Genèse 48.1 Matthieu 16.22
14 Lakini Yesu akasema, Waacheni watoto wadogo waje kwangu; wala msiwazuie; kwa maana walio mfano wa hao, ufalme wa mbinguni ni wao.
Matthieu 18.3 Luc 18.16-18.17 1 Corinthiens 14.20 1 Samuel 1.24 1 Samuel 1.22
15 Akaweka mikono yake juu yao, akatoka huko.
1 Corinthiens 7.14 Esaïe 40.11 2 Timothée 3.15 Marc 10.16
16 Na tazama, mtu mmoja akamwendea akamwambia, Mwalimu, nitende jambo gani jema, ili nipate uzima wa milele?
Matthieu 25.46 Jean 3.15 Jude 1.21 1 Jean 1.2 Marc 10.17-10.30
17 Akamwambia Kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja. Lakini ukitaka kuingia katika uzima, zishike amri.
Lévitique 18.5 1 Jean 4.16 Romains 10.5 1 Samuel 2.2 Ezéchiel 20.11-20.12
18 Akamwambia, Zipi? Yesu akasema, Ni hizi, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo,
Jacques 2.10-2.11 Deutéronome 5.16-5.21 Galates 3.10 Romains 13.8-13.10 Marc 10.19
19 Waheshimu baba yako na mama yako, na, Mpende jirani yako kama nafsi yako.
Lévitique 19.18 Matthieu 22.39 Jacques 2.8 Luc 10.27 Galates 5.14
20 Yule kijana akamwambia, Haya yote nimeyashika; nimepungukiwa na nini tena?
Philippiens 3.6 Luc 18.11-18.12 Luc 15.29 Galates 3.24 Jean 8.7
21 Yesu akamwambia, Ukitaka kuwa mkamilifu, enenda ukauze ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate.
Marc 10.21 Actes 2.45 Luc 12.33 Luc 16.9 Matthieu 5.48
22 Yule kijana alipolisikia neno lile, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
Ezéchiel 33.31 Matthieu 13.22 Marc 10.22 Matthieu 6.24 Luc 18.23
23 Yesu akawaambia wanafunzi wake, Amin, nawaambieni, ya kwamba itakuwa shida tajiri kuingia katika ufalme wa mbinguni.
Matthieu 13.22 1 Timothée 6.9-6.10 Luc 18.24 Marc 10.23 1 Corinthiens 1.26
24 Nawaambia tena, Ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu ya sindano, kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.
Jérémie 13.23 Luc 18.25 Matthieu 19.26 Marc 10.24-10.25 Jean 5.44
25 Wanafunzi waliposikia, walishangaa mno, wakisema, Ni nani basi awezaye kuokoka?
Romains 11.5-11.7 Matthieu 24.22 Luc 13.23-13.24 Marc 13.20 Romains 10.13
26 Yesu akawakazia macho, akawaambia, Kwa wanadamu hilo haliwezekani; bali kwa Mungu yote yawezekana.
Job 42.2 Jérémie 32.27 Luc 18.27 Luc 1.37 Zacharie 8.6
27 Ndipo Petro akajibu, akamwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata; tutapata nini basi?
Philippiens 3.8 Luc 15.29 Luc 5.27-5.28 Marc 1.17-1.20 1 Corinthiens 1.29
28 Yesu akawaambia, Amin, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli.
Apocalypse 3.21 Matthieu 25.31 Luc 22.28-22.30 Matthieu 16.27 Apocalypse 21.5
29 Na kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu wa kiume au wa kike, au baba, au mama, au watoto, au mashamba, kwa ajili ya jina langu, atapokea mara mia, na kuurithi uzima wa milele.
Luc 18.29-18.30 Philippiens 3.8 Luc 14.26 Matthieu 16.25 Marc 10.29-10.30
30 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.
Luc 13.30 Matthieu 20.16 Marc 10.31 Matthieu 21.31-21.32 Luc 18.13-18.14

Cette Bible est dans le domaine public.