Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 13.13
Bible en Swahili de l’est


Paraboles du royaume des cieux

Le semeur et les terrains

1 Siku ile Yesu akatoka nyumbani, akaketi kando ya bahari.
Matthieu 13.1-13.15 Luc 8.4-8.10 Marc 2.13 Marc 4.1-4.12 Matthieu 13.36
2 Wakamkusanyikia makutano mengi, hata akapanda chomboni, akaketi; na ule mkutano wote wakasimama pwani.
Luc 5.3 Matthieu 4.25 Luc 8.4-8.8 Marc 4.1 Matthieu 15.30
3 Akawaambia mambo mengi kwa mifano, akisema, Tazama, mpanzi alitoka kwenda kupanda.
Marc 4.33 Matthieu 13.34-13.35 Matthieu 13.53 Marc 4.13 Marc 4.2-4.9
4 Hata alipokuwa akipanda, mbegu nyingine zilianguka karibu na njia, ndege wakaja wakazila;
Matthieu 13.18-13.19
5 nyingine zikaanguka penye miamba, pasipokuwa na udongo mwingi; mara zikaota, kwa udongo kukosa kina;
Ezéchiel 36.26 Zacharie 7.12 Ezéchiel 11.19 Matthieu 13.20 Amos 6.12
6 na jua lilipozuka ziliungua; na kwa kuwa hazina mizizi zikanyauka.
Matthieu 13.21 Jacques 1.11-1.12 Luc 8.13 Ephésiens 3.17 Apocalypse 7.16
7 Nyingine zikaanguka penye miiba; ile miiba ikamea, ikazisonga;
Jérémie 4.3-4.4 Genèse 3.18 Marc 4.18-4.19 Matthieu 13.22
8 nyingine zikaanguka penye udongo mzuri, zikazaa, moja mia, moja sitini, moja thelathini.
Matthieu 13.23 Genèse 26.12 Philippiens 1.11 Romains 7.18 Luc 8.15
9 Mwenye masikio na asikie.
Matthieu 11.15 Apocalypse 2.17 Apocalypse 3.22 Apocalypse 2.29 Apocalypse 2.7
10 Wakaja wanafunzi, wakamwambia, Kwa nini wasema nao kwa mifano?
Marc 4.33-4.34 Marc 4.10
11 Akajibu, akawaambia, Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za ufalme wa mbinguni, bali wao hawakujaliwa.
1 Corinthiens 2.9-2.10 1 Jean 2.27 1 Corinthiens 2.14 Matthieu 19.11 Matthieu 16.17
12 Kwa maana ye yote mwenye kitu atapewa, naye atazidishiwa tele; lakini ye yote asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang’anywa.
Matthieu 25.29 Luc 8.18 Apocalypse 2.5 Marc 12.9 Luc 16.2
13 Kwa sababu hii nasema nao kwa mifano; kwa kuwa wakitazama hawaoni, na wakisikia hawasikii, wala kuelewa.
Ezéchiel 12.2 Jérémie 5.21 Jean 9.39-9.41 Deutéronome 29.3-29.4 2 Corinthiens 4.3-4.4
14 Na neno la nabii Isaya linatimia kwao, likisema, Kusikia mtasikia, wala hamtaelewa; Kutazama mtatazama, wala hamtaona.
Esaïe 6.9-6.10 Luc 8.10 Actes 28.25-28.27 2 Corinthiens 3.14 Marc 4.12
15 Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito, Na kwa masikio yao hawasikii vema, Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia kwa masikio yao, Wakaelewa kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya.
Jean 8.43-8.44 Hébreux 5.11 Zacharie 7.11 Psaumes 119.70 2 Timothée 4.4
16 Lakini, heri macho yenu, kwa kuwa yanaona; na masikio yenu, kwa kuwa yanasikia.
Luc 10.23-10.24 Matthieu 16.17 Ephésiens 1.17-1.18 2 Corinthiens 4.6 Jean 20.29
17 Kwa maana, amin, nawaambia, Manabii wengi na wenye haki walitamani kuyaona mnayoyaona ninyi, wasiyaone; na kuyasikia mnayoyasikia ninyi, wasiyasikie.
1 Pierre 1.10-1.12 Hébreux 11.13 Jean 8.56 Luc 10.24 Ephésiens 3.5-3.6
18 Basi ninyi sikilizeni mfano wa mpanzi.
Luc 8.11-8.15 Matthieu 13.11-13.12 Marc 4.13-4.20
19 Kila mtu alisikiapo neno la ufalme asielewe nalo, huja yule mwovu, akalinyakua lililopandwa moyoni mwake. Huyo ndiye aliyepandwa karibu na njia.
Luc 8.11-8.15 Matthieu 13.38 Hébreux 2.1 Matthieu 4.23 Actes 24.25-24.26
20 Naye aliyepandwa penye miamba, huyo ndiye alisikiaye lile neno, akalipokea mara kwa furaha;
Psaumes 106.12-106.13 Esaïe 58.2 Marc 6.20 Jean 5.35 Ezéchiel 33.31-33.32
21 lakini hana mizizi ndani yake, bali hudumu kwa muda; ikitukia dhiki au udhia kwa ajili ya lile neno, mara huchukizwa.
Matthieu 11.6 Osée 6.4 Marc 4.17 Psaumes 36.3 Job 19.28
22 Naye aliyepandwa penye miiba, huyo ndiye alisikiaye lile neno; na shughuli za dunia, na udanganyifu wa mali hulisonga lile neno; likawa halizai.
1 Timothée 6.9-6.10 2 Timothée 4.10 1 Timothée 6.17 Luc 8.14 Psaumes 52.7
23 Naye aliyepandwa penye udongo mzuri, huyo ndiye alisikiaye lile neno, na kuelewa nalo; yeye ndiye azaaye matunda, huyu mia, na huyu sitini, na huyu thelathini.
Matthieu 13.8 Matthieu 12.33 Philippiens 1.11 Colossiens 1.6 Jean 15.16

La mauvaise herbe et le bon grain

24 Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;
Matthieu 13.47 Matthieu 25.1 Luc 13.20 Matthieu 20.1 Matthieu 13.33
25 lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
1 Pierre 5.8 Galates 2.4 2 Pierre 2.1 Actes 20.30-20.31 Hébreux 12.15
26 Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu.
Marc 4.26-4.29
27 Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu?
Romains 16.17 2 Corinthiens 5.18-5.20 Jacques 4.4 Jacques 3.15-3.16 1 Corinthiens 3.5-3.9
28 Akawaambia, Adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, Basi, wataka twende tukayakusanye?
1 Corinthiens 5.3-5.7 2 Corinthiens 2.6-2.11 Luc 9.49-9.54 Jude 1.22-1.23 1 Thessaloniciens 5.14
29 Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo.
30 Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu.
Matthieu 3.12 1 Corinthiens 4.5 Malachie 3.18-4.1 1 Timothée 5.24 Luc 3.17

La graine de moutarde et le levain

31 Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na punje ya haradali, aliyoitwaa mtu akaipanda katika shamba lake;
Marc 4.30-4.32 Luc 13.18-13.19 Matthieu 13.24 Matthieu 17.20 Luc 17.6
32 nayo ni ndogo kuliko mbegu zote; lakini ikiisha kumea, huwa kubwa kuliko mboga zote, ikawa mti, hata nyuni wa angani huja na kukaa katika matawi yake.
Daniel 4.12 Ezéchiel 31.6 Actes 21.20 Romains 15.18-15.19 Daniel 2.44-2.45
33 Akawaambia mfano mwingine; Ufalme wa mbinguni umefanana na chachu aliyoitwaa mwanamke, akaisitiri ndani ya pishi tatu za unga, hata ukachachwa wote pia.
Galates 5.9 Luc 13.21 Proverbes 4.18 Genèse 18.6 1 Corinthiens 5.6-5.7
34 Hayo yote Yesu aliwaambia makutano kwa mifano; wala pasipo mfano hakuwaambia neno;
Marc 4.33-4.34 Jean 16.25 Matthieu 13.13
35 ili litimie neno lililonenwa na nabii, akisema, Nitafumbua kinywa changu kwa mifano, Nitayatamka yaliyositirika tangu awali.
Psaumes 78.2 Ephésiens 3.9 1 Corinthiens 2.7 Romains 16.25-16.26 1 Pierre 1.20-1.21

Explication de la parabole de la mauvaise herbe

36 Kisha Yesu akawaaga makutano, akaingia nyumbani; wanafunzi wake wakamwendea, wakasema, Tufafanulie mfano wa magugu ya kondeni.
Matthieu 13.1 Matthieu 15.15-15.16 Marc 8.9 Marc 7.17 Marc 4.34
37 Akajibu, akasema, Azipandaye zile mbegu njema ni Mwana wa Adamu;
Actes 1.8 Hébreux 2.3 Matthieu 13.24 Luc 10.16 Matthieu 8.20
38 lile konde ni ulimwengu; zile mbegu njema ni wana wa ufalme; na yale magugu ni wana wa yule mwovu;
Jean 8.44 Actes 13.10 Matthieu 13.19 1 Jean 3.8-3.10 Romains 10.18
39 yule adui aliyeyapanda ni Ibilisi; mavuno ni mwisho wa dunia; na wale wavunao ni malaika.
Matthieu 24.3 Matthieu 13.49 Joël 3.13 2 Corinthiens 2.17 Apocalypse 14.15-14.19
40 Basi, kama vile magugu yakusanywavyo na kuchomwa motoni; ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia.
Matthieu 13.39
41 Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka katika ufalme wake machukizo yote, na hao watendao maasi,
Matthieu 24.31 Matthieu 18.7 Matthieu 8.20 Romains 2.16 Hébreux 1.6-1.7
42 na kuwatupa katika tanuru ya moto, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
Matthieu 13.50 Apocalypse 20.14-20.15 Matthieu 8.12 Apocalypse 20.10 Luc 16.23-16.24
43 Ndipo wenye haki watakapong’aa kama jua katika ufalme wa Baba yao. Mwenye masikio, na asikie.
Daniel 12.3 Luc 12.32 Matthieu 26.29 1 Corinthiens 15.41-15.54 Matthieu 25.34

Comparaisons diverses

44 Tena ufalme wa mbinguni umefanana na hazina iliyositirika katika shamba; ambayo mtu alipoiona, aliificha; na kwa furaha yake akaenda akauza alivyo navyo vyote, akalinunua shamba lile.
Colossiens 2.3 Proverbes 2.2-2.5 Proverbes 16.16 Hébreux 11.24-11.26 Philippiens 3.7-3.9
45 Tena ufalme wa mbinguni umefanana na mfanya biashara, mwenye kutafuta lulu nzuri;
Proverbes 8.18-8.20 Job 28.18 Matthieu 16.26 Psaumes 39.6-39.7 Psaumes 4.6-4.7
46 naye alipoona lulu moja ya thamani kubwa, alikwenda akauza alivyo navyo vyote, akainunua.
Colossiens 2.3 Marc 10.28-10.31 Proverbes 2.4 Ephésiens 3.8 Luc 18.28-18.30
47 Tena ufalme wa mbinguni umefanana na juya, lililotupwa baharini, likakusanya samaki wa kila namna;
Matthieu 4.19 1 Jean 4.1-4.6 Matthieu 25.1-25.4 Apocalypse 3.15-3.17 Marc 1.17
48 hata lilipojaa, walilivuta pwani; wakaketi, wakakusanya walio wema vyomboni, bali walio wabaya wakawatupa.
Matthieu 13.40-13.43 Matthieu 13.30 Matthieu 3.12
49 Ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia; malaika watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki,
Apocalypse 20.12-20.15 Matthieu 13.39 2 Thessaloniciens 1.7-1.10 Matthieu 25.19-25.33 Matthieu 22.12-22.14
50 na kuwatupa katika tanuru ya moto; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
Matthieu 13.42 Apocalypse 14.10-14.11 Matthieu 8.12 Apocalypse 16.10-16.11 Luc 13.27-13.28
51 Yesu aliwauliza, Mmeyafahamu hayo yote? Wakamwambia, Naam.
Matthieu 13.11 Marc 4.34 Marc 8.17-8.18 Matthieu 16.11 Matthieu 24.15
52 Akawaambia, Kwa sababu hiyo, kila mwandishi mwenye elimu ya ufalme wa mbinguni amefanana na mtu mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale.
Proverbes 15.7 1 Jean 2.7-2.8 Proverbes 18.4 Tite 1.9 Matthieu 23.34
53 Ikawa Yesu alipoimaliza mifano hiyo, alitoka akaenda zake.
Matthieu 7.28 Marc 4.33-4.35

Fin du ministère de Jésus en Galilée et au-delà

Jésus rejeté à Nazareth

54 Na alipofika nchi yake, akawafundisha katika sinagogi lao, hata wakashangaa, wakasema, Huyu amepata wapi hekima hii na miujiza hii?
Matthieu 4.23 Luc 4.16-4.30 Matthieu 2.23 Matthieu 7.28 Jean 1.11
55 Huyu si mwana wa seremala? Mamaye si yeye aitwaye Mariamu? Na nduguze si Yakobo, na Yusufu, na Simoni, na Yuda?
Jean 6.42 Luc 3.23 Marc 6.3 Marc 15.40 Jean 19.25
56 Na maumbu yake wote hawapo hapa petu? Basi huyu amepata wapi haya yote?
57 Wakachukizwa naye. Yesu akawaambia, Nabii hakosi kupata heshima, isipokuwa katika nchi yake, na nyumbani mwake mwenyewe.
Matthieu 11.6 Jean 4.44 Luc 4.24 Jean 6.61 Marc 6.3
58 Wala hakufanya miujiza mingi huko, kwa sababu ya kutokuamini kwao.
Marc 6.5-6.6 Romains 11.20 Hébreux 4.6-4.11 Luc 4.25-4.29 Hébreux 3.12-3.19

Cette Bible est dans le domaine public.