Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 11.27
Bible en Swahili de l’est


1 Ikawa Yesu alipokwisha kuwaagiza wanafunzi wake kumi na wawili, alitoka huko kwenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao.
Actes 10.42 Jean 15.10 Matthieu 4.23 Luc 4.15-4.21 1 Thessaloniciens 4.2

Jean-Baptiste vu par Jésus

2 Naye Yohana aliposikia huko gerezani matendo yake Kristo, alituma wanafunzi wake, kumwuliza,
Matthieu 14.3 Matthieu 4.12 Matthieu 9.14 Marc 6.17 Actes 19.1-19.3
3 Wewe ndiwe yule ajaye, au tumtazamie mwingine?
Jean 11.27 Hébreux 10.37 Jean 7.31 Deutéronome 18.15-18.18 Malachie 3.1
4 Yesu akajibu akawaambia, Nendeni mkamweleze Yohana mnayoyasikia na kuyaona;
5 vipofu wanapata kuona, viwete wanakwenda, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema.
Esaïe 35.4-35.6 Esaïe 61.1-61.3 Luc 4.18 Luc 7.21-7.22 Jacques 2.5
6 Naye heri awaye yote asiyechukizwa nami.
Esaïe 8.14-8.15 Matthieu 24.10 1 Corinthiens 2.14 Luc 4.23-4.29 Matthieu 26.31
7 Na hao walipokwenda zao, Yesu alianza kuwaambia makutano habari za Yohana, Mlitoka kwenda nyikani kutazama nini? Unyasi ukitikiswa na upepo?
Ephésiens 4.14 Jacques 1.6 Jean 5.35 Matthieu 21.25 Genèse 49.4
8 Lakini mlitoka kwenda kuona nini? Mtu aliyevikwa mavazi mororo? Tazama, watu wavaao mavazi mororo wamo katika nyumba za wafalme.
1 Corinthiens 4.11 Zacharie 13.4 2 Rois 1.8 Apocalypse 11.3 Esaïe 20.2
9 Lakini kwa nini mlitoka? Ni kuona nabii? Naam, nawaambia, na aliye mkuu zaidi ya nabii.
Luc 1.76 Matthieu 14.5 Matthieu 17.12-17.13 Matthieu 21.24-21.26 Matthieu 11.13-11.14
10 Huyo ndiye aliyeandikiwa haya, Tazama, mimi namtuma mjumbe wangu Mbele ya uso wako, Atakayeitengeneza njia yako mbele yako.
Malachie 3.1 Esaïe 40.3 Marc 1.2 Jean 1.23 Malachie 4.5
11 Amin, nawaambieni, Hajaondokea mtu katika wazao wa wanawake aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji; walakini aliye mdogo katika ufalme wa mbinguni ni mkuu kuliko yeye.
1 Corinthiens 15.9 Ephésiens 3.8 Romains 16.25-16.26 Jean 1.15 Jean 1.27
12 Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka.
Luc 16.16 Luc 13.24 Philippiens 2.12 Ephésiens 6.11-6.13 Jean 6.27
13 Kwa maana manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana.
Matthieu 5.17-5.18 Malachie 4.6 Actes 3.22-3.24 Jean 5.46-5.47 Actes 13.27
14 Na ikiwa mnataka kukubali, yeye ndiye Eliya atakayekuja.
Matthieu 17.10-17.13 Malachie 4.5 Marc 9.11-9.13 Luc 1.17 Ezéchiel 2.5
15 Mwenye masikio, na asikie.
Matthieu 13.9 Matthieu 13.43 Marc 4.23 Luc 8.8 Apocalypse 2.7
16 Lakini nitakifananisha na nini kizazi hiki? Kimefanana na watoto wanaokaa sokoni, wanaowaita wenzao, wakisema,
Luc 7.31-7.35 Luc 13.18 Matthieu 24.34 Matthieu 12.34 Marc 4.30
17 Tuliwapigia filimbi, wala hamkucheza; tuliomboleza, wala hamkulia.
Esaïe 28.9-28.13 Matthieu 9.23 1 Corinthiens 9.19-9.23 Esaïe 30.29 Jérémie 9.17-9.20
18 Maana Yohana alikuja, hali wala hanywi, wakasema, Yuna pepo.
Matthieu 3.4 Luc 1.15 Jean 7.20 Jean 10.20 Jean 8.48
19 Mwana wa Adamu alikuja, akila na kunywa, wakasema, Mlafi huyu, na mlevi, rafiki yao watoza ushuru na wenye dhambi! Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa kazi zake.
Luc 19.7 Luc 14.1 Matthieu 9.10-9.11 Luc 5.29-5.30 Luc 15.1-15.2
20 Ndipo akaanza kuikemea miji ile ambamo ndani yake ilifanyika miujiza yake iliyo mingi, kwa sababu haikutubu.
Luc 10.13-10.15 Psaumes 81.11-81.13 Esaïe 1.2-1.5 Jacques 1.5 Matthieu 12.41
21 Ole wako, Korazini! Ole wako, Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika katika Tiro na Sidoni, wangalitubu zamani kwa kuvaa magunia na majivu.
Luc 9.10 Jean 12.21 Marc 6.45 Matthieu 15.21 Marc 8.22
22 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi Tiro na Sidoni kustahimili adhabu zao siku ya hukumu kuliko ninyi.
Matthieu 10.15 Matthieu 11.24 Luc 12.47-12.48 Matthieu 12.36 Jérémie 27.3
23 Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa mpaka mbinguni? Utashushwa mpaka kuzimu; kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwako ingalifanyika katika Sodoma, ungalikuwapo mji huo hata leo.
Esaïe 14.13-14.15 Matthieu 4.13 Lamentations 2.1 Matthieu 17.24 2 Pierre 2.4-2.9
24 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma kustahimili adhabu yake siku ya hukumu kuliko wewe.
Matthieu 10.15 Matthieu 11.22 Luc 10.12 Marc 6.11 Lamentations 4.6
25 Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga.
Psaumes 8.2 Matthieu 16.17 Matthieu 21.16 Jean 11.41 Luc 22.42
26 Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako.
Ephésiens 1.9 Romains 11.33-11.36 Ephésiens 1.11 Luc 10.21 Ephésiens 3.11
27 Akasema, Nimekabidhiwa vyote na baba yangu; wala hakuna amjuaye Mwana, ila Baba; wala hakuna amjuaye Baba, ila Mwana, na ye yote ambaye Mwana apenda kumfunulia.
Jean 14.6-14.9 Matthieu 28.18 2 Jean 1.9 Jean 10.15 Jean 17.25-17.26
28 Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
Matthieu 11.29 Jean 7.37 Galates 5.1 Esaïe 55.1-55.3 Jean 6.37
29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;
1 Jean 2.6 Philippiens 2.7-2.8 Jérémie 6.16 Jean 13.15 Philippiens 2.5
30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.
1 Jean 5.3 Jean 16.33 Proverbes 3.17 Philippiens 4.13 2 Corinthiens 12.9-12.10

Cette Bible est dans le domaine public.