Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 11.19
Bible en Swahili de l’est


1 Ikawa Yesu alipokwisha kuwaagiza wanafunzi wake kumi na wawili, alitoka huko kwenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao.
2 Thessaloniciens 3.6 Matthieu 7.28 Luc 8.1 Matthieu 28.20 Actes 10.38

Jean-Baptiste vu par Jésus

2 Naye Yohana aliposikia huko gerezani matendo yake Kristo, alituma wanafunzi wake, kumwuliza,
Matthieu 14.3 Matthieu 9.14 Marc 6.17 Matthieu 4.12 Actes 19.1-19.3
3 Wewe ndiwe yule ajaye, au tumtazamie mwingine?
Hébreux 10.37 Jean 11.27 Deutéronome 18.15-18.18 Malachie 3.1 Genèse 3.15
4 Yesu akajibu akawaambia, Nendeni mkamweleze Yohana mnayoyasikia na kuyaona;
5 vipofu wanapata kuona, viwete wanakwenda, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema.
Esaïe 35.4-35.6 Luc 4.18 Esaïe 61.1-61.3 Jacques 2.5 Luc 7.21-7.22
6 Naye heri awaye yote asiyechukizwa nami.
Esaïe 8.14-8.15 1 Corinthiens 2.14 Luc 4.23-4.29 Matthieu 26.31 Matthieu 24.10
7 Na hao walipokwenda zao, Yesu alianza kuwaambia makutano habari za Yohana, Mlitoka kwenda nyikani kutazama nini? Unyasi ukitikiswa na upepo?
Jacques 1.6 Ephésiens 4.14 2 Corinthiens 1.17-1.18 Luc 3.3-3.7 Luc 8.18
8 Lakini mlitoka kwenda kuona nini? Mtu aliyevikwa mavazi mororo? Tazama, watu wavaao mavazi mororo wamo katika nyumba za wafalme.
Apocalypse 11.3 Esaïe 20.2 2 Corinthiens 11.27 Matthieu 3.4 1 Corinthiens 4.11
9 Lakini kwa nini mlitoka? Ni kuona nabii? Naam, nawaambia, na aliye mkuu zaidi ya nabii.
Luc 1.76 Matthieu 14.5 Matthieu 21.24-21.26 Matthieu 11.13-11.14 Luc 1.15-1.17
10 Huyo ndiye aliyeandikiwa haya, Tazama, mimi namtuma mjumbe wangu Mbele ya uso wako, Atakayeitengeneza njia yako mbele yako.
Malachie 3.1 Esaïe 40.3 Marc 1.2 Malachie 4.5 Jean 1.23
11 Amin, nawaambieni, Hajaondokea mtu katika wazao wa wanawake aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji; walakini aliye mdogo katika ufalme wa mbinguni ni mkuu kuliko yeye.
Ephésiens 3.8 Romains 16.25-16.26 1 Corinthiens 15.9 Luc 1.15 Hébreux 11.40
12 Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka.
Luc 16.16 Luc 13.24 Philippiens 2.12 Jean 6.27 Ephésiens 6.11-6.13
13 Kwa maana manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana.
Jean 5.46-5.47 Actes 13.27 Romains 3.21 Luc 24.27 Luc 24.44
14 Na ikiwa mnataka kukubali, yeye ndiye Eliya atakayekuja.
Malachie 4.5 Marc 9.11-9.13 Matthieu 17.10-17.13 Luc 1.17 Ezéchiel 3.10-3.11
15 Mwenye masikio, na asikie.
Marc 4.23 Matthieu 13.9 Matthieu 13.43 Luc 8.8 Apocalypse 2.7
16 Lakini nitakifananisha na nini kizazi hiki? Kimefanana na watoto wanaokaa sokoni, wanaowaita wenzao, wakisema,
Luc 7.31-7.35 Marc 4.30 Lamentations 2.13 Matthieu 23.36 Luc 13.18
17 Tuliwapigia filimbi, wala hamkucheza; tuliomboleza, wala hamkulia.
Esaïe 28.9-28.13 Esaïe 30.29 Jérémie 9.17-9.20 Jérémie 31.4 Matthieu 9.15
18 Maana Yohana alikuja, hali wala hanywi, wakasema, Yuna pepo.
Matthieu 3.4 Luc 1.15 Jean 10.20 Jean 8.48 Jean 7.20
19 Mwana wa Adamu alikuja, akila na kunywa, wakasema, Mlafi huyu, na mlevi, rafiki yao watoza ushuru na wenye dhambi! Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa kazi zake.
Luc 5.29-5.30 Luc 19.7 Luc 14.1 Matthieu 9.10-9.11 Romains 15.2
20 Ndipo akaanza kuikemea miji ile ambamo ndani yake ilifanyika miujiza yake iliyo mingi, kwa sababu haikutubu.
Psaumes 81.11-81.13 Esaïe 1.2-1.5 Luc 10.13-10.15 Michée 6.1-6.5 2 Timothée 2.25-2.26
21 Ole wako, Korazini! Ole wako, Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika katika Tiro na Sidoni, wangalitubu zamani kwa kuvaa magunia na majivu.
Matthieu 15.21 Luc 9.10 Jean 12.21 Marc 6.45 Matthieu 11.22
22 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi Tiro na Sidoni kustahimili adhabu zao siku ya hukumu kuliko ninyi.
Matthieu 10.15 Matthieu 11.24 Luc 12.47-12.48 Matthieu 12.36 Jérémie 25.22
23 Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa mpaka mbinguni? Utashushwa mpaka kuzimu; kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwako ingalifanyika katika Sodoma, ungalikuwapo mji huo hata leo.
Matthieu 4.13 Esaïe 14.13-14.15 Luc 16.23 Genèse 13.13 Matthieu 16.18
24 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma kustahimili adhabu yake siku ya hukumu kuliko wewe.
Matthieu 10.15 Matthieu 11.22 Lamentations 4.6 Luc 10.12 Marc 6.11
25 Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga.
Psaumes 8.2 Matthieu 16.17 Matthieu 21.16 Jean 11.41 Jean 9.39-9.41
26 Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako.
Luc 10.21 Ephésiens 3.11 Job 33.13 Esaïe 46.10 2 Timothée 1.9
27 Akasema, Nimekabidhiwa vyote na baba yangu; wala hakuna amjuaye Mwana, ila Baba; wala hakuna amjuaye Baba, ila Mwana, na ye yote ambaye Mwana apenda kumfunulia.
Jean 14.6-14.9 Matthieu 28.18 Jean 10.15 2 Jean 1.9 Jean 17.25-17.26
28 Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
Matthieu 11.29 Jean 7.37 Galates 5.1 Esaïe 55.1-55.3 Jean 6.37
29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;
1 Jean 2.6 Philippiens 2.7-2.8 Jérémie 6.16 Jean 13.15 Philippiens 2.5
30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.
1 Jean 5.3 Jean 16.33 Proverbes 3.17 Philippiens 4.13 2 Corinthiens 12.9-12.10

Cette Bible est dans le domaine public.