Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nombres 33.45
Bible en Swahili de l’est


Étapes des Israélites pendant leur voyage

1 Hizi ndizo safari za wana wa Israeli, hapo walipotoka nchi ya Misri kwa jeshi zao chini ya mkono wa Musa na Haruni.
Michée 6.4 Psaumes 77.20 Exode 12.37 Exode 12.51 Josué 24.5
2 Musa akaandika jinsi walivyotoka katika safari zao, kwa amri ya Bwana; na hizi ndizo safari zao kama kutoka kwao kulivyokuwa.
Nombres 9.17-9.23 Deutéronome 10.11 Deutéronome 1.2 Nombres 10.13 Nombres 10.6
3 Wakasafiri kutoka Ramesesi mwezi wa kwanza, siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza; siku ya pili baada ya Pasaka, wana wa Israeli wakatoka kwa mkono wa nguvu mbele ya macho ya Wamisri wote,
Exode 14.8 Exode 12.37 Exode 13.4 Exode 12.2 Michée 2.13
4 hapo Wamisri walipokuwa wanazika wazaliwa wa kwanza wao wote, Bwana aliokuwa amewapiga kati yao; Bwana akafanya hukumu juu ya miungu yao nayo.
Exode 12.12 Esaïe 19.1 Apocalypse 12.7-12.9 Exode 18.11 Exode 12.29-12.30
5 Wana wa Israeli wakasafiri kutoka Ramesesi, wakapanga katika Sukothi.
Exode 12.37
6 Kisha wakasafiri kutoka Sukothi, wakapanga Ethamu, palipo katika mwisho wa nyika.
Exode 13.20
7 Wakasafiri kutoka Ethamu, na kurudi nyuma hata Pi-hahirothi palipokabili Baal-sefoni; wakapanga mbele ya Migdoli.
Exode 14.2 Exode 14.9 Nombres 33.8
8 Wakasafiri kutoka hapo mbele ya Hahirothi, wakapita katikati ya bahari na kuingia jangwani; kisha wakaenda safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu, wakapanga Mara.
Exode 15.22-15.26 Exode 14.21-14.31
9 Wakasafiri kutoka Mara, wakafikilia Elimu; huko Elimu palikuwa na chemchemi za maji kumi na mbili, na mitende sabini; nao wakapanga hapo.
Exode 15.27
10 Wakasafiri kutoka Elimu wakapanga karibu na Bahari ya Shamu.
Exode 17.1 Exode 16.1
11 Wakasafiri kutoka Bahari ya Shamu, wakapanga katika nyika ya Sini.
Exode 16.1
12 Wakasafiri kutoka nyika ya Sini, wakapanga Dofka.
13 Wakasafiri kutoka Dofka, wakapanga Alushi.
14 Wakasafiri kutoka Alushi, wakapanga Refidimu, ambapo hapakuwa na maji ya watu kunywa.
Exode 17.1-17.8 Exode 19.2
15 Wakasafiri kutoka Refidimu, wakapanga katika nyika ya Sinai.
Exode 19.1-19.2 Exode 16.1
16 Wakasafiri kutoka nyika ya Sinai, wakapanga Kibroth-hataava.
Nombres 11.34 Nombres 11.4 Nombres 10.33 Nombres 10.11-10.13 Deutéronome 1.6
17 Wakasafiri kutoka Kibroth-hataava, wakapanga Haserothi.
Nombres 11.35
18 Wakasafiri kutoka Haserothi, wakapanga Rithma.
Nombres 12.16
19 Wakasafiri kutoka Rithma, wakapanga Rimon-peresi.
20 Wakasafiri kutoka Rimon-peresi, wakapanga Libna.
21 Wakasafiri kutoka Libna, wakapanga Risa.
Deutéronome 1.1
22 Wakasafiri kutoka Risa, wakapanga Keheletha.
23 Wakasafiri kutoka Keheletha, wakapanga katika mlima wa Sheferi
24 Wakasafiri kutoka huo mlima wa Sheferi, wakapanga Harada.
25 Wakasafiri kutoka Harada, wakapanga Makelothi.
26 Wakasafiri kutoka Makelothi, wakapanga Tahathi.
27 Wakasafiri kutoka Tahathi wakapanga Tera.
28 Wakasafiri kutoka Tera, wakapanga Mithka.
29 Wakasafiri kutoka Mithka, wakapanga Hashmona.
30 Wakasafiri kutoka Hashmona, wakapanga Moserothi.
Deutéronome 10.5-10.6
31 Wakasafiri kutoka Moserothi, wakapanga Bene-yakani.
Deutéronome 10.6 Genèse 36.27 1 Chroniques 1.43
32 Wakasafiri kutoka Bene-yakani, wakapanga Hor-hagidgadi.
Deutéronome 10.7
33 Wakasafiri kutoka Hor-hagidgadi, wakapanga Yotbatha.
Deutéronome 10.7
34 Wakasafiri kutoka Yotbatha, wakapanga Abrona.
35 Wakasafiri kutoka Abrona, wakapanga Esion-geberi.
Deutéronome 2.8 1 Rois 9.26 1 Rois 22.48 2 Chroniques 20.36 Nombres 14.25
36 Wakasafiri kutoka Esion-geberi, wakapanga katika nyika ya Sini (ni Kadeshi).
Nombres 20.1 Nombres 27.14 Nombres 13.21 Deutéronome 32.51
37 Wakasafiri kutoka Kadeshi wakapanga katika mlima wa Hori, katika mpaka wa nchi ya Edomu,
Nombres 21.4 Nombres 20.22-20.23 Nombres 20.16
38 Haruni akakwea mlima wa Hori, kwa amri ya Bwana, akafa hapo, katika mwaka wa arobaini baada ya wana wa Israeli kutoka katika nchi ya Misri, mwezi wa tano, siku ya kwanza ya mwezi.
Deutéronome 10.6 Deutéronome 32.50 Nombres 20.24-20.28
39 Naye Haruni alikuwa mtu wa umri wa miaka mia na ishirini na mitatu hapo alipokufa katika mlima wa Hori.
40 Ndipo Mkanaani, mfalme wa Aradi, aliyekaa pande za Negebu katika nchi ya Kanaani akasikia habari za kuja kwao wana wa Israeli.
Nombres 21.1-21.9
41 Nao wakasafiri kutoka mlima wa Hori, wakapanga Salmona.
Nombres 21.4
42 Wakasafiri kutoka Salmona, wakapanga Punoni.
43 Wakasafiri kutoka Punoni, wakapanga Obothi.
Nombres 21.10
44 Wakasafiri kutoka Obothi, wakapanga Iye-abarimu, katika mpaka wa Moabu.
Nombres 21.11
45 Wakasafiri kutoka Iye-abarimu, wakapanga Dibon-gadi.
46 Wakasafiri kutoka Dibon-gadi, wakapanga Almon-diblathaimu.
Jérémie 48.22 Jérémie 48.18 Nombres 32.34 Ezéchiel 6.14 Esaïe 15.2
47 Wakasafiri kutoka Almon-diblathaimu, wakapanga katika milima ya Abarimu, kukabili Nebo.
Deutéronome 32.49 Nombres 21.20 Deutéronome 34.1 Nombres 27.12
48 Wakasafiri kutoka hiyo milima ya Abarimu, wakapanga katika nchi tambarare za Moabu, karibu na mto wa Yordani, hapo Yeriko.
Nombres 22.1
49 Wakapanga karibu na Yordani, tangu Beth-yeshimothi hata kufikilia Abel-shitimu katika nchi tambarare za Moabu.
Exode 25.5 Josué 13.20 Exode 25.23 Exode 25.10 Ezéchiel 25.9

Loi pour la conquête de Canaan

50 Kisha Bwana akanena na Musa hapo katika nchi tambarare za Moabu, karibu na Yordani, hapo Yeriko, na kumwambia,
Nombres 33.48-33.49
51 Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Mtakapovuka mto wa Yordani na kuingia nchi ya Kanaani,
Josué 3.17 Deutéronome 9.1 Deutéronome 7.1
52 ndipo mtakapowafukuza wenyeji wote wa hiyo nchi mbele yenu, nanyi mtayaharibu mawe yao yote yenye kuchorwa sanamu, na kuziharibu sanamu zao zote za kusubu, kuvunja-vunja mahali pao pote palipoinuka;
Exode 23.24 Lévitique 26.1 Exode 23.31-23.33 Josué 11.11-11.12 Deutéronome 7.25-7.26
53 nanyi mtaishika hiyo nchi kuimiliki na kuketi humo; kwa kuwa mimi nimewapa ninyi hiyo nchi ili mwimiliki.
Psaumes 115.16 Deutéronome 32.8 Psaumes 24.1-24.2 Josué 21.43 Matthieu 20.15
54 Nanyi mtairithi nchi kwa kufanya kura, kama jamaa zenu zilivyo; hao walio wengi mtawapa urithi zaidi, na hao waliopunguka utawapa kama kupunguka kwao; mahali po pote kura itakapomwangukia mtu ye yote, mahali hapo ni pake; mtarithi kama kabila za baba zenu zilivyo.
Nombres 26.53-26.56 Josué 17.1-17.13 Josué 18.11-19.48 Josué 15.1-15.12 Josué 16.1-16.4
55 Lakini kama hamtaki kuwafukuza wenyeji wa nchi watoke mbele yenu; ndipo hao ambao mtakaowasaza watakuwa kama sindano machoni mwenu, na kama miiba ubavuni mwenu, nao watawasumbua katika hiyo nchi ambayo mwakaa.
Juges 2.3 Psaumes 106.34-106.36 Deutéronome 7.16 Juges 1.21-1.36 Exode 23.33
56 Kisha itakuwa, kama nilivyoazimia kuwatenda wao, ndivyo nitakavyowatenda ninyi.
Deutéronome 28.63 Lévitique 18.28 Josué 23.15-23.16 Deutéronome 29.28 Luc 21.23-21.24

Cette Bible est dans le domaine public.