Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 1.11
Bible en Swahili de l’est


Jugement de Jérusalem

Vision de la gloire de l’Éternel

1 Ikawa katika mwaka wa thelathini, mwezi wa nne, siku ya tano ya mwezi, nilipokuwa pamoja na watu waliohamishwa, karibu na mto Kebari, mbingu zilifunuka, nikaona maono ya Mungu.
Ezéchiel 11.24 Actes 7.56 Matthieu 3.16 Actes 10.11 Ezéchiel 3.23
2 Siku ya tano ya mwezi, nao ulikuwa ni mwaka wa tano wa kuhamishwa kwake mfalme Yehoyakini,
Ezéchiel 40.1 2 Rois 24.12-24.15 Ezéchiel 8.1 Ezéchiel 20.1 Ezéchiel 29.17
3 neno la Bwana lilimjia Ezekielii, kuhani, mwana wa Buzi, kwa dhahiri, katika nchi ya Wakaldayo, karibu na mto Kebari; na mkono wa Bwana ulikuwa hapo juu yake.
2 Rois 3.15 Ezéchiel 3.14 Ezéchiel 3.22 1 Rois 18.46 Ezéchiel 8.1
4 Nikaona, na tazama, upepo wa dhoruba ulitoka upande wa kaskazini, wingu kubwa sana, pamoja na moto, ukifanya duara ya nuru, na mwangaza pande zote, na katikati yake kitu kama rangi ya kaharabu, katikati ya moto huo.
Ezéchiel 8.2 Ezéchiel 1.27 Jérémie 23.19 Jérémie 25.32 Esaïe 21.1
5 Kukatokea katikati yake mfano wa viumbe hai vinne. Kuonekana kwao kulikuwa hivi; walikuwa na sura ya mwanadamu.
Apocalypse 6.6 Apocalypse 4.6-4.8 Ezéchiel 1.26
6 Na kila mmoja alikuwa na nyuso nne, na kila mmoja alikuwa na mabawa manne.
Ezéchiel 10.14 Exode 25.20 Ezéchiel 10.21-10.22 Ezéchiel 1.8-1.11 Apocalypse 4.7-4.8
7 Na miguu yao ilikuwa miguu iliyonyoka; na nyayo za miguu yao zilikuwa kama nyayo za miguu ya ndama; zikimetameta kama rangi ya shaba iliyosuguliwa sana.
Apocalypse 1.15 Daniel 10.6 Ezéchiel 1.13 Lévitique 11.47 Psaumes 104.4
8 Nao walikuwa na mikono ya mwanadamu chini ya mabawa yao, pande zote nne; na wote wanne walikuwa na nyuso zao na mabawa yao hivi;
Ezéchiel 10.21 Ezéchiel 8.3 Ezéchiel 10.18 Ezéchiel 1.17 Ezéchiel 10.11
9 mabawa yao yaliungana, hili na hili; nao hawakugeuka walipokwenda, walikwenda kila mmoja kuelekea mbele.
Ezéchiel 10.22 2 Chroniques 3.11-3.12 Ezéchiel 1.11-1.12 Ezéchiel 10.11 1 Corinthiens 1.10
10 Kwa habari za mfano wa nyuso zao; walikuwa na uso wa mwanadamu; na hao wanne walikuwa na uso wa simba upande wa kuume; na hao wanne walikuwa na uso wa ng’ombe upande wa kushoto; na hao wanne walikuwa na uso wa tai pia.
Ezéchiel 10.14 Apocalypse 4.7 1 Corinthiens 14.20 Esaïe 40.31 Nombres 2.10
11 Na nyuso zao na mabawa yao yalikuwa yametengana kwa juu; mabawa mawili ya kila mmoja yaliungana, hili na hili, na mawili yalifunika miili yao.
Esaïe 6.2 Ezéchiel 1.23 Ezéchiel 10.16 Ezéchiel 10.19
12 Nao walikwenda kuelekea mbele, kila mmoja wao; roho ilikotaka kwenda ndiko walikokwenda; hawakugeuka walipokwenda.
Ezéchiel 1.9 Ezéchiel 1.20-1.21 Hébreux 1.14 Ezéchiel 1.17 Ezéchiel 10.22
13 Kwa habari za kuonekana kwao vile viumbe hai; kuonekana kwao kulikuwa kama makaa ya moto yawakayo, kama kuonekana kwa vinga vya moto; moto ule ulikuwa ukienda juu na kushuka chini, katikati ya vile viumbe hai; na ule moto ulikuwa na mwangaza mwingi, na katika ule moto ulitoka umeme.
Apocalypse 4.5 Psaumes 104.4 Apocalypse 10.1 Daniel 10.5-10.6 Genèse 15.17
14 Na vile viumbe hai walipiga mbio, kwenda na kurudi, kama kuonekana kwa kumulika kwa umeme.
Zacharie 4.10 Matthieu 24.27 Matthieu 24.31 Psaumes 147.15 Marc 13.27
15 Basi, nilipokuwa nikivitazama vile viumbe hai, tazama, gurudumu moja juu ya nchi, karibu na kila kimoja cha vile viumbe hai, pande zake zote nne.
Ezéchiel 10.9 Daniel 7.9 Ezéchiel 1.6 Ezéchiel 1.19-1.21 Ezéchiel 10.13-10.17
16 Kuonekana kwake magurudumu hayo na kazi yake kulikuwa kama rangi ya zabarajadi; nayo yote manne yalikuwa na mfano mmoja; na kuonekana kwake na kazi yake kulikuwa kana kwamba ni gurudumu ndani ya gurudumu lingine.
Daniel 10.6 Ephésiens 3.10 Ezéchiel 10.9-10.11 Psaumes 40.5 Romains 11.33
17 Yalipokwenda yalikwenda pande zote nne; hayakugeuka yalipokwenda.
Ezéchiel 1.9 Ezéchiel 1.12 Esaïe 55.11 Ezéchiel 10.1-10.11
18 Katika habari za vivimbe vyake; vilikuwa virefu, vya kutisha; nayo yote manne, vivimbe vyake vimejaa macho pande zote.
Ezéchiel 10.12 Apocalypse 4.6 Apocalypse 4.8 Psaumes 77.16-77.19 Psaumes 97.2-97.5
19 Na viumbe hao walipokwenda, magurudumu yalikwenda kandokando yao, na viumbe hao walipoinuliwa, magurudumu nayo yaliinuliwa.
Ezéchiel 10.16 Psaumes 103.20 Ezéchiel 10.19
20 Kila mahali ambako roho hiyo ilitaka kwenda, walikwenda; walikuwa na roho ya kwenda huko; nayo magurudumu yaliinuliwa karibu nao; kwa maana roho ya viumbe hai ilikuwa ndani ya magurudumu.
Ezéchiel 1.12 Ezéchiel 10.17 1 Corinthiens 14.32 Zacharie 6.1-6.8
21 Walipokwenda hao, yalikwenda hayo nayo; na waliposimama hao, yalisimama hayo nayo; na walipoinuliwa hao juu ya nchi, magurudumu yaliinuliwa karibu nao; maana roho ya viumbe hai ilikuwa ndani ya magurudumu.
Ezéchiel 10.17 Ezéchiel 1.19-1.20 Romains 8.2
22 Tena juu ya vichwa vya viumbe hai palikuwa na kitu mfano wa anga, kama rangi ya bilauri, lenye kutisha, limetandwa juu ya vichwa vyao.
Ezéchiel 10.1 Apocalypse 4.6 Ezéchiel 1.26 Exode 24.10 Job 37.22
23 Na chini ya anga mabawa yao yamenyoshwa, moja kulielekea la pili; kila mmoja alikuwa na mawili yaliyowafunika miili yao upande mmoja, na kila mmoja alikuwa na mawili yaliyowafunika miili yao upande wa pili.
Job 4.18 Luc 17.10 Ezéchiel 1.11-1.12 Psaumes 89.7 Ezéchiel 1.24
24 Nao walipokwenda nalisikia mshindo wa mabawa yao, kama mshindo wa maji makuu, kama sauti yake Mwenyezi, mshindo wa mvumo, kama mshindo wa jeshi; hapo waliposimama walishusha mabawa yao.
Daniel 10.6 Apocalypse 19.6 Ezéchiel 43.2 Apocalypse 1.15 2 Rois 7.6
25 Tena palikuwa na sauti juu ya anga lile, lililokuwa juu ya vichwa vyao; hapo waliposimama walishusha mabawa yao.
Ezéchiel 1.22
26 Na juu ya anga, lililokuwa juu ya vichwa vyao, palikuwa na mfano wa kiti cha enzi, kuonekana kwake kama yakuti samawi; na juu ya mfano huo wa kiti cha enzi, ulikuwako mfano kama kuonekana kwa mfano wa mwanadamu juu yake.
Ezéchiel 10.1 Exode 24.10 Apocalypse 1.13 Esaïe 6.1 Ezéchiel 1.22
27 Nikaona kana kwamba ni rangi ya kaharabu, kama kuonekana kwa moto ndani yake pande zote, tangu kuonekana kwa viuno vyake na juu; na tangu kuonekana kwa viuno vyake na chini, naliona kana kwamba ni kuonekana kwa moto; tena palikuwa na mwangaza pande zake zote.
Ezéchiel 1.4 Ezéchiel 8.2 Psaumes 97.2 Hébreux 12.29 Psaumes 50.3
28 Kama kuonekana kwa upinde wa mvua, ulio katika mawingu siku ya mvua, ndivyo kulivyokuwa kuonekana kwa mwangaza ule pande zote. Ndivyo kulivyokuwa kuonekana kwake mfano huo wa utukufu wa Bwana. Nami nilipoona nalianguka kifudifudi, nikasikia sauti ya mmoja anenaye.
Ezéchiel 3.23 Apocalypse 10.1 Daniel 8.17 Apocalypse 4.3 Ezéchiel 8.4

Cette Bible est dans le domaine public.