Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 50.21
Bible en Swahili de l’est


Prophétie sur Babylone

1 Neno hili ndilo alilosema Bwana, katika habari za Babeli, na katika habari za Wakaldayo, kwa kinywa cha Yeremia, nabii.
Jérémie 25.26-25.27 Esaïe 13.1-13.3 Jérémie 51.1-51.14 Apocalypse 18.1-18.24 Jérémie 27.7
2 Tangazeni katika mataifa, Mkahubiri na kutweka bendera; Hubirini, msifiche, semeni, Babeli umetwaliwa! Beli amefedheheka; Merodaki amefadhaika; Sanamu zake zimeaibishwa, Vinyago vyake vimefadhaika.
Esaïe 46.1 Esaïe 21.9 Jérémie 51.44 Jérémie 51.47 Esaïe 12.4
3 Maana toka kaskazini taifa linakuja juu yake, litakaloifanya nchi yake kuwa ukiwa; wala hapana mtu atakayekaa humo; wamekimbia, wamekwenda zao, mwanadamu na mnyama pia.
Sophonie 1.3 Jérémie 50.9 Jérémie 51.11 Jérémie 51.62 Esaïe 14.22-14.24
4 Katika siku hizo, na wakati huo, asema Bwana, wana wa Israeli watakuja, wao na wana wa Yuda pamoja; Wataendelea njiani mwao wakilia, nao watamtafuta Bwana, Mungu wao.
Osée 3.5 Osée 1.11 Esaïe 11.12-11.13 Esdras 3.12-3.13 Jérémie 31.31
5 Watauliza habari za Sayuni, na nyuso zao zitaelekea huko, wakisema, Njoni ninyi, mjiunge na Bwana, kwa agano la milele ambalo halitasahauliwa.
Jérémie 32.40 Esaïe 55.3 Hébreux 8.6-8.10 Genèse 17.7 Esaïe 35.8
6 Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea, wachungaji wao wamewapoteza; wamewapotosha milimani; wamekwenda toka mlima hata kilima, wamesahau mahali pao pa kupumzika.
Esaïe 53.6 Matthieu 9.36 Matthieu 10.6 Jérémie 50.17 Ezéchiel 34.14
7 Watu wote waliowaona wamewala; na adui zao walisema, Sisi hatuna hatia, kwa kuwa hao wametenda dhambi juu ya Bwana, aliye kao la haki, yaani, Bwana, tumaini la baba zao.
Jérémie 14.8 Jérémie 2.3 Jérémie 31.23 Jérémie 40.2-40.3 Zacharie 11.5
8 Kimbieni kutoka kati ya Babeli, mkatoke katika nchi ya Wakaldayo, mkawe kama mabeberu mbele ya makundi.
Esaïe 48.20 Jérémie 51.6 Apocalypse 18.4 Jérémie 51.45 Zacharie 2.6-2.7
9 Kwa maana juu ya Babeli nitaamsha na kuleta kusanyiko la mataifa makubwa, toka nchi ya kaskazini; nao watajipanga juu yake; kutoka huko atatwaliwa; mishale yao itakuwa kama ya mtu shujaa aliye stadi; hapana hata mmoja utakaorudi bure.
Jérémie 51.27-51.28 Esdras 1.1-1.2 Esaïe 41.25 Jérémie 51.1-51.4 Jérémie 51.11
10 Nao Ukaldayo utakuwa mateka; wote wautekao watashiba, asema Bwana.
Jérémie 25.12 Esaïe 33.23 Apocalypse 17.16 Esaïe 45.3 Jérémie 27.7
11 Kwa sababu mnafurahi, kwa sababu mnashangilia, enyi mnaouteka urithi wangu, kwa sababu mmewanda kama mtamba akanyagaye nafaka, nanyi mnalia kama farasi wenye nguvu;
Esaïe 47.6 Psaumes 22.12 Lamentations 4.21-4.22 Jérémie 5.8 Jérémie 51.34-51.35
12 mama yenu atatahayarika sana; yeye aliyewazaa atafadhaika; tazama, atakuwa taifa lililo nyuma katika mataifa yote, atakuwa jangwa, nchi ya ukame, na nyika.
Jérémie 51.43 Apocalypse 18.21-18.23 Apocalypse 17.5 Galates 4.26 Jérémie 50.35-50.40
13 Kwa sababu ya ghadhabu ya Bwana haitakaliwa na mtu, bali itakuwa ukiwa mtupu; kila mtu apitaye karibu na Babeli atashangaa, atazomea kwa sababu ya mapigo yake yote.
Jérémie 18.16 Jérémie 49.17 Zacharie 1.15 Jérémie 19.8 Esaïe 14.4-14.17
14 Jipangeni juu ya Babeli pande zote, Ninyi nyote mpindao upinde; Mpigeni, msiuzuie hata mshale mmoja; Kwa maana amemtenda Bwana dhambi.
Jérémie 50.29 Jérémie 50.9 Habakuk 2.17 Jérémie 50.7 Jérémie 50.42
15 Mpigieni kelele pande zote; amejitoa; Maboma yake yameanguka, kuta zake zimebomolewa; Kwa maana ni kisasi cha Bwana; mlipizeni kisasi; Kama yeye alivyotenda, mtendeni yeye.
Jérémie 51.58 Jérémie 51.6 Apocalypse 18.6 Jérémie 46.10 Jérémie 51.14
16 Mpanzi mkatilie mbali na Babeli, Naye ashikaye mundu wakati wa mavuno; Kwa sababu ya kuuogopa upanga uoneao, Watageuka kila mtu kwa watu wake, Nao wataikimbilia kila mmoja nchi yake.
Esaïe 13.14 Jérémie 51.9 Jérémie 46.16 Joël 1.11 Amos 5.16
17 Israeli ni kondoo aliyetawanywa; simba wamemfukuzia mbali; kwanza mfalme wa Ashuru amemla, na mwisho Nebukadreza huyu, mfalme wa Babeli, amemvunja mifupa yake.
Jérémie 2.15 Jérémie 50.6 Joël 3.2 2 Rois 18.9-18.13 Jean 10.10-10.12
18 Basi, Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Tazama, mimi nitamwadhibu mfalme wa Babeli, na nchi yake, kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru.
Esaïe 10.12 Esaïe 37.36-37.38 Sophonie 2.13-2.15 Ezéchiel 31.3-31.17 Nahum 1.1-1.3
19 Nami nitamleta Israeli tena malishoni kwake, naye atalisha juu ya Karmeli, na Bashani, na nafsi yake itashiba juu ya milima ya Efraimu, na katika Gileadi.
Jérémie 31.6 Ezéchiel 34.13-34.14 Michée 7.14 Ezéchiel 36.33 Esaïe 35.2
20 Katika siku hizo na wakati huo, asema Bwana, uovu wa Israeli utatafutwa, wala uovu hapana; na dhambi za Yuda zitatafutwa, wala hazitaonekana; maana nitawasamehe wale niwaachao kuwa mabaki.
Michée 7.19 Jérémie 31.34 Esaïe 1.9 Esaïe 43.25 Jérémie 33.15
21 Panda juu ya nchi ya Merathaimu, naam, juu yake, na juu yao wakaao Pekodi; ua, ukaangamize nyuma yao, asema Bwana, ukatende kama nilivyokuagiza, yote pia.
Ezéchiel 23.23 Esaïe 48.14 2 Rois 18.25 Jérémie 50.3 1 Samuel 15.11-15.24
22 Pana mshindo wa vita katika nchi, Mshindo wa uharibifu mkuu.
Jérémie 4.19-4.21 Jérémie 51.54-51.56 Esaïe 21.2-21.4
23 Imekuwaje nyundo ya dunia yote Kukatiliwa mbali na kuvunjwa? Imekuwaje Babeli kuwa ukiwa Katikati ya mataifa?
Jérémie 51.20-51.24 Esaïe 14.12-14.17 Esaïe 14.4-14.6 Apocalypse 18.16
24 Nimekutegea mtego, Ee Babeli, nawe ukanaswa, nawe ulikuwa huna habari; umeonekana, ukakamatwa, kwa sababu ulishindana na Bwana.
Daniel 5.30-5.31 Job 9.4 Job 40.2 Job 40.9 Esaïe 45.9
25 Bwana amefungua akiba yake ya silaha, naye amezitoa silaha za ghadhabu yake; maana Bwana, Bwana wa majeshi, ana kazi atakayofanya katika nchi ya Wakaldayo.
Jérémie 51.25 Jérémie 51.55 Jérémie 50.15 Esaïe 21.7-21.9 Psaumes 45.3
26 Njoni juu yake toka mpaka ulio mbali; Zifungueni ghala zake; Mfanyeni kuwa magofu na kumharibu kabisa; Msimsazie kitu cho chote.
Esaïe 14.23 Esaïe 45.3 Jérémie 50.10 Esaïe 5.26 Apocalypse 18.21-18.24
27 Wachinjeni mafahali wake wote; Na watelemkie machinjoni; Ole wao! Maana siku yao imewadia, Wakati wa kujiliwa kwao.
Esaïe 34.7 Jérémie 46.21 Psaumes 22.12 Jérémie 48.44 Psaumes 37.13
28 Sauti yao wakimbiao na kuokoka, Kutoka katika nchi ya Babeli, Ili kutangaza Sayuni kisasi cha Bwana, Mungu wetu, Kisasi cha hekalu lake.
Jérémie 50.15 Lamentations 1.10 Esaïe 48.20 Daniel 5.23 Lamentations 2.6-2.7
29 Waiteni wapiga mishale juu ya Babeli, Naam, wote waupindao upinde; Pangeni hema kumzunguka pande zote; Ili asiokoke hata mtu mmoja wao; Mlipeni kwa kadiri ya kazi yake; Mtendeni sawasawa na yote aliyoyatenda; Kwa sababu amefanya kiburi juu ya Bwana, Juu yake aliye Mtakatifu wa Israeli.
Jérémie 51.56 Esaïe 47.10 Daniel 4.37 Apocalypse 18.6 Jérémie 50.14-50.15
30 Kwa sababu hiyo vijana wake wataanguka katika njia kuu zake, na watu wake wa vita, wote pia, watanyamazishwa katika siku hiyo, asema Bwana.
Jérémie 49.26 Jérémie 9.21 Jérémie 18.21 Jérémie 51.56-51.57 Esaïe 13.15-13.18
31 Tazama, mimi ni juu yako, Ewe mwenye kiburi, asema Bwana, Bwana wa majeshi; maana siku yako imewadia, wakati nitakapokujilia.
Jérémie 21.13 Nahum 2.13 Jérémie 50.29 Nahum 3.5 1 Pierre 5.5
32 Na mwenye kiburi atajikwaa, na kuanguka, wala hapana atakayemwinua; nami nitawasha moto katika miji yake, nao utawala wote wamzungukao pande zote.
Jérémie 21.14 Jérémie 49.27 Esaïe 10.12-10.15 Jérémie 51.64 Amos 1.7
33 Bwana wa majeshi asema hivi, Wana wa Israeli, na wana wa Yuda, wameonewa pamoja; na wote waliowachukua mateka wanawashika sana; wanakataa kuwaacha.
Esaïe 14.17 Esaïe 58.6 Zacharie 1.15-1.16 Esaïe 47.6 Jérémie 50.7
34 Mkombozi wao ni hodari; Bwana wa majeshi ndilo jina lake; yeye atawatetea kwa bidii, apate kuistarehesha nchi, na kuwasumbua wakaao katika Babeli.
Jérémie 51.36 Michée 7.9 Esaïe 43.14 Apocalypse 18.8 Esaïe 14.3-14.7
35 Upanga u juu ya Wakaldayo, asema Bwana, na juu yao wakaao Babeli, na juu ya wakuu wake, na juu ya watu wake wenye hekima.
Jérémie 47.6 Daniel 5.7-5.8 Jérémie 51.57 Daniel 5.1-5.2 Daniel 5.30
36 Upanga u juu ya hao wajisifuo, nao watapumbazika; upanga u juu ya mashujaa wake, nao watafadhaika.
Jérémie 49.22 Esaïe 44.25 Nahum 3.13 Jérémie 50.30 Nahum 2.8
37 Upanga u juu ya farasi zao, na juu ya magari yao ya vita; na juu ya watu wote waliochanganyika ndani yake, nao watakuwa kama wanawake; upanga u juu ya hazina zake, nazo zitaibwa.
Jérémie 51.30 Nahum 3.13 Jérémie 51.21 Jérémie 25.20 Jérémie 48.41
38 Ukosefu wa mvua u juu ya maji yake, nayo yatakaushwa; maana ni nchi ya sanamu za kuchongwa, nao wameingiwa na wazimu kwa ajili ya sanamu.
Jérémie 50.2 Esaïe 44.27 Jérémie 51.52 Apocalypse 16.12 Jérémie 51.47
39 Basi, wanyama wakali wa jangwani, pamoja na mbwa-mwitu, watakaa huko, na mbuni watakaa ndani yake; wala haitakaliwa na watu milele; wala hapana mtu atakayekaa huko tangu kizazi hata kizazi.
Esaïe 13.20-13.22 Apocalypse 18.2 Jérémie 25.12 Jérémie 51.26 Jérémie 51.37-51.38
40 Kama vile vilivyotokea Mungu alipoangusha Sodoma na Gomora, na miji iliyokuwa karibu nayo, asema Bwana; kadhalika hapana mtu atakayekaa huko, wala hapana mwanadamu atakayekaa huko kama wageni wakaavyo.
Genèse 19.24-19.25 Jude 1.7 2 Pierre 2.6 Jérémie 49.18 Luc 17.28-17.30
41 Angalia, watu wanakuja watokao kaskazini; na taifa kubwa, na wafalme wengi wataamshwa toka pande za mwisho za dunia.
Jérémie 51.27-51.28 Jérémie 6.22-6.23 Jérémie 50.9 Esaïe 13.2-13.5 Jérémie 50.2-50.3
42 Wanashika upinde na mkuki; Ni wakatili, hawana huruma; Sauti yao inanguruma kama bahari, Nao wamepanda farasi; Kila mmoja amejipanga kama aendaye vitani, Juu yako, Ee binti Babeli.
Esaïe 5.30 Jérémie 47.3 Esaïe 13.17-13.18 Esaïe 47.6 Jérémie 8.16
43 Mfalme wa Babeli amesikia habari zao, Na mikono yake imekuwa dhaifu; Dhiki imemshika, na maumivu, Kama ya mwanamke katika utungu wake.
Jérémie 51.31 Jérémie 49.24 Esaïe 13.6-13.8 Daniel 5.5-5.6 Esaïe 21.3-21.4
44 Angalia, atapanda kama simba toka kiburi cha Yordani juu ya malisho yasiyonyauka; lakini nitamkimbiza ghafula ayaache; na yeye aliye mteule nitamweka juu yake; maana ni nani aliye kama mimi? Tena ni nani atakayeniandikia muda? Tena ni mchungaji yupi atakayesimama mbele zangu?
Jérémie 49.19-49.21 Esaïe 40.25 Jérémie 25.38 Esaïe 46.11 Esaïe 40.18
45 Basi, lisikieni shauri la Bwana, Alilolifanya juu ya Babeli; Na makusudi yake aliyoyakusudia Juu ya nchi ya Wakaldayo. Hakika watawaburura, naam, wadogo wa kundi; Hakika malisho yao yatafadhaika kwa ajili yao.
Jérémie 49.20 Jérémie 51.10-51.11 Ephésiens 1.11 Apocalypse 17.16-17.17 Actes 4.28
46 Kwa mshindo wa kutwaliwa Babeli nchi yatetemeka, Na kilio chake chasikiwa katika mataifa.
Jérémie 49.21 Apocalypse 18.9-18.19 Ezéchiel 26.18 Ezéchiel 31.16 Esaïe 14.9-14.10

Cette Bible est dans le domaine public.