Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 29.11
Bible en Swahili de l’est


Des attitudes opposées

1 Aonywaye mara nyingi akishupaza shingo, Atavunjika ghafula, wala hapati dawa.
Proverbes 6.15 1 Samuel 2.25 Jean 13.18 Proverbes 1.24-1.31 Jean 13.26
2 Wenye haki wakiwa na amri, watu hufurahi; Bali mwovu atawalapo, watu huugua.
Esther 8.15 Proverbes 28.12 Proverbes 11.10 Proverbes 28.28 Esther 3.15
3 Apendaye hekima humfurahisha babaye; Bali ashikamanaye na makahaba hutapanya mali.
Luc 15.30 Proverbes 10.1 Proverbes 28.7 Proverbes 27.11 Luc 15.13
4 Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu; Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.
Proverbes 29.14 Psaumes 89.14 2 Chroniques 9.8 2 Rois 15.18-15.20 Esaïe 49.8
5 Mwenye kujipendekeza kwa jirani yake, Hutandika wavu ili kuitega miguu yake.
Psaumes 5.9 Psaumes 12.2 Proverbes 7.5 Proverbes 7.21 Osée 5.1
6 Kuna mtego katika kosa la mtu mbaya; Bali mwenye haki huimba na kufurahi.
Job 18.7-18.10 Proverbes 11.5-11.6 Proverbes 5.22 Psaumes 97.11 Psaumes 11.6
7 Mwenye haki huyaangalia madai ya maskini; Bali mtu mbaya hana ufahamu hata ayajue.
Psaumes 41.1 Job 29.16 Proverbes 31.8-31.9 Proverbes 21.13 Ezéchiel 22.29-22.31
8 Watu wenye dharau huwasha mji moto; Bali wenye hekima hugeuzia mbali ghadhabu.
Proverbes 11.11 Nombres 25.11 Amos 7.2-7.6 Jean 11.47-11.50 Proverbes 16.14
9 Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu; Akikasirika au akicheka, pia hapana raha.
Ecclésiaste 10.13 Matthieu 11.17-11.19 Proverbes 26.4 Matthieu 7.6
10 Wamwagao damu humchukia mtu mkamilifu; Bali wenye haki humtunza nafsi yake.
Genèse 4.5-4.8 Marc 6.18-6.19 1 Samuel 20.31-20.33 1 Samuel 15.11 1 Jean 3.12-3.13
11 Mpumbavu hudhihirisha hasira yake yote; Bali mwenye hekima huizuia na kuituliza.
Proverbes 12.16 Proverbes 19.11 Juges 16.17 Proverbes 14.33 Proverbes 12.23
12 Mwenye kutawala akisikiliza uongo; Basi watumishi wake wote watakuwa waovu.
Psaumes 101.5-101.7 Proverbes 25.23 1 Samuel 22.8-22.23 2 Rois 10.6-10.7 2 Samuel 3.7-3.11
13 Maskini na mdhalimu hukutana pamoja; Bwana huwatia nuru macho yao wote wawili.
Proverbes 22.2 Matthieu 5.45 Psaumes 13.3 Néhémie 5.5-5.7 Ephésiens 2.1
14 Mfalme awahukumuye maskini kwa uaminifu; Kiti chake cha enzi kitathibitika milele.
Proverbes 16.12 Proverbes 25.5 Esaïe 11.4 Psaumes 72.2-72.4 Proverbes 29.4
15 Fimbo na maonyo hutia hekima; Bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye.
Proverbes 10.1 Proverbes 17.25 Proverbes 22.15 Proverbes 22.6 Proverbes 29.17
16 Waovu wakiongezeka, maasi huongezeka; Bali wenye haki watayatazama maanguko yao.
Psaumes 92.11 Psaumes 37.36 Psaumes 91.8 Psaumes 58.10 Psaumes 37.34
17 Mrudi mwanao naye atakustarehesha; Naam, atakufurahisha nafsi yako.
Proverbes 13.24 Proverbes 29.15 Proverbes 22.15 Proverbes 23.13-23.14 Proverbes 10.1
18 Pasipo maono, watu huacha kujizuia; Bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
Jacques 1.25 Luc 11.28 Matthieu 9.36 1 Samuel 3.1 Romains 10.13-10.15
19 Haitoshi mtumwa kuonywa kwa maneno; Maana ajapoyafahamu hataitika.
Proverbes 26.3 Proverbes 30.22 Job 19.16
20 Je! Umemwona mtu mwenye kuhamaki katika maneno? Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye.
Jacques 1.19 Proverbes 26.12 Proverbes 14.29 Proverbes 21.5 Ecclésiaste 5.2
21 Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto, Mwisho wake atakuwa ni mwanawe.
22 Mtu wa hasira huchochea ugomvi; Na mtu mwenye ghadhabu huasi sana.
Proverbes 15.18 Proverbes 17.19 Proverbes 26.21 Proverbes 14.17 Proverbes 10.12
23 Kiburi cha mtu kitamshusha; Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa.
Matthieu 23.12 Luc 14.11 Esaïe 66.2 Proverbes 11.2 1 Pierre 5.5
24 Mshiriki wa mwivi huichukia nafsi yake mwenyewe; Asikia maapizo, wala hana neno.
Lévitique 5.1 Proverbes 8.36 Proverbes 6.32 Proverbes 15.32 Marc 11.17
25 Kuwaogopa wanadamu huleta mtego; Bali amtumainiye Bwana atakuwa salama.
Luc 12.4 Psaumes 91.14 Psaumes 118.8 Proverbes 18.10 Proverbes 16.20
26 Watu wengi hutafuta upendeleo wa mkuu; Bali hukumu ya kila mtu hutoka kwa Bwana
Proverbes 19.6 Psaumes 20.9 Proverbes 21.1 Esdras 7.27-7.28 Proverbes 19.21
27 Mtu aliye dhalimu ni chukizo kwa wenye haki; Na mnyofu wa mwenendo ni chukizo kwa waovu.
Psaumes 139.21 1 Jean 3.13 Psaumes 119.115 Proverbes 24.9 Zacharie 11.8

Cette Bible est dans le domaine public.