Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 15.11
Bible en Swahili de l’est


Paroles et attitudes

1 Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.
Proverbes 25.15 Proverbes 29.22 Proverbes 15.18 1 Samuel 25.21-25.33 1 Rois 12.13-12.16
2 Ulimi wa mwenye hekima hutamka maarifa vizuri; Bali vinywa vya wapumbavu humwaga upumbavu.
Proverbes 12.23 Proverbes 13.16 Proverbes 15.28 Esaïe 50.4 Proverbes 16.23
3 Macho ya Bwana yako kila mahali; Yakimchunguza mbaya na mwema.
Hébreux 4.13 2 Chroniques 16.9 Jérémie 16.17 Job 34.21-34.22 Jérémie 23.24
4 Ulimi safi ni mti wa uzima; Bali ukorofi wa ulimi huvunja moyo.
Proverbes 3.18 Proverbes 16.24 Proverbes 12.18 Genèse 3.22-3.24 Malachie 4.2
5 Mpumbavu hudharau kurudiwa na babaye; Bali yeye aangaliaye maonyo hupata busara.
Proverbes 13.18 Proverbes 13.1 Proverbes 15.31-15.32 Proverbes 10.1 1 Chroniques 22.11-22.13
6 Katika nyumba ya mwenye haki mna akiba nyingi; Bali mapato ya mtu mbaya huwa taabu tu.
Proverbes 8.21 Proverbes 21.20 Proverbes 10.22 Psaumes 112.3 Ecclésiaste 5.10-5.14
7 Midomo ya mwenye haki hueneza maarifa; Bali moyo wa mpumbavu haufanyi hivyo.
Matthieu 12.34 Romains 15.18-15.21 Matthieu 28.18-28.20 Psaumes 45.2 Marc 16.15
8 Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa Bwana; Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake.
Proverbes 15.29 Proverbes 21.27 1 Chroniques 29.17 Jérémie 6.20 Esaïe 1.10-1.15
9 Njia ya mtu mbaya ni chukizo kwa Bwana; Bali humpenda mtu afuatiaye wema.
1 Timothée 6.11 Proverbes 21.21 Esaïe 51.7 Matthieu 7.13 Proverbes 4.19
10 Adhabu kali ina yeye aiachaye njia; Naye achukiaye kukemewa atakufa.
Proverbes 12.1 Proverbes 5.12 Jean 7.7 Proverbes 1.30 1 Rois 21.20
11 Kuzimu na Uharibifu vi wazi mbele za Bwana; Si zaidi basi, mioyo ya wanadamu?
Psaumes 44.21 2 Chroniques 6.30 Job 26.6 Psaumes 139.8 Jean 21.17
12 Mwenye mzaha hapendi kukaripiwa; Wala yeye hawaendei wenye hekima.
Amos 5.10 Job 21.14 Proverbes 9.7-9.8 2 Chroniques 18.7 2 Timothée 4.3
13 Moyo wa furaha huchangamsha uso; Bali kwa huzuni ya moyo roho hupondeka.
Proverbes 17.22 Proverbes 18.14 Proverbes 12.25 Proverbes 15.15 2 Corinthiens 2.7
14 Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa; Bali kinywa cha wapumbavu hula upumbavu.
Esaïe 30.10 Psaumes 119.97 Proverbes 18.15 Proverbes 9.9 1 Rois 3.6-3.12
15 Siku zote za mtu ateswaye ni mbaya; Bali ukunjufu wa moyo ni karamu ya daima.
Proverbes 15.13 Proverbes 17.22 2 Corinthiens 6.10 Romains 5.2-5.3 Romains 12.12
16 Kuwa na mali chache pamoja na kumcha Bwana; Ni bora kuliko mali nyingi pamoja na taabu.
1 Timothée 6.6 Proverbes 16.8 Psaumes 37.16 Ecclésiaste 5.10-5.12 Ecclésiaste 2.10-2.11
17 Chakula cha mboga penye mapendano; Ni bora kuliko ng’ombe aliyenona pamoja na kuchukiana.
Proverbes 17.1 Proverbes 21.19 Luc 15.23 Matthieu 22.4 1 Jean 4.16
18 Mtu wa hasira huchochea ugomvi; Bali asiye mwepesi wa hasira hutuliza mashindano.
Proverbes 26.21 Proverbes 29.22 Proverbes 14.29 Proverbes 28.25 Ecclésiaste 10.4
19 Njia ya mtu mvivu ni kama boma la miiba; Bali mapito yao wenye unyofu hufanyika njia kuu.
Proverbes 22.5 Proverbes 26.13 Proverbes 22.13 Proverbes 8.9 Nombres 14.7-14.9
20 Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye; Bali mpumbavu humdharau mamaye.
Proverbes 29.3 Proverbes 10.1 Proverbes 30.17 Proverbes 23.15-23.16 Exode 20.12
21 Upumbavu ni furaha kwake aliyepungukiwa na akili; Bali mwenye ufahamu huunyosha mwenendo wake.
Ephésiens 5.15 Proverbes 10.23 Proverbes 26.18-26.19 Psaumes 111.10 Proverbes 14.9
22 Pasipo mashauri makusudi hubatilika; Bali kwa wingi wa washauri huthibithika.
Proverbes 11.14 Proverbes 20.18 Ecclésiaste 8.6
23 Mtu hulifurahia jibu la kinywa chake; Na neno linenwalo wakati wa kufaa ni jema kama nini!
Esaïe 50.4 Proverbes 12.14 Proverbes 16.13 Proverbes 25.11-25.12 Ephésiens 4.29
24 Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu; Ili atoke katika kuzimu chini.
Philippiens 3.20 Proverbes 2.18 Colossiens 3.1-3.2 Psaumes 16.11 Proverbes 23.14
25 Bwana ataing’oa nyumba ya mwenye kiburi; Bali atauthibitisha mpaka wa mjane.
Psaumes 146.9 Proverbes 23.10 Proverbes 12.7 Psaumes 68.5-68.6 Proverbes 14.11
26 Mashauri mabaya ni chukizo kwa Bwana; Bali maneno yapendezayo ni safi.
Proverbes 6.16-6.19 Matthieu 15.19 Psaumes 37.30-37.31 Jérémie 4.14 Psaumes 19.14
27 Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe; Bali achukiaye zawadi ataishi.
Exode 23.8 Proverbes 1.19 Jérémie 17.11 2 Rois 5.27 Deutéronome 16.19
28 Moyo wa mwenye haki hufikiri jinsi atakavyojibu; Bali kinywa cha wasio haki humwaga mabaya.
1 Pierre 3.15 Proverbes 15.2 Proverbes 29.11 Proverbes 29.20 Jacques 3.6-3.8
29 Bwana yu mbali na wasio haki; Bali huisikia sala ya mwenye haki.
Jean 9.31 Proverbes 15.8 Psaumes 145.18-145.19 1 Pierre 3.12 Jacques 5.16-5.18
30 Mng’ao wa macho huufurahisha moyo; Habari njema huinenepesha mifupa.
Proverbes 25.25 Esdras 9.8 Psaumes 89.15 Apocalypse 21.23 Ecclésiaste 11.7
31 Sikio lisikilizalo lawama yenye uhai Litakaa kati yao wenye hekima.
Proverbes 15.5 Proverbes 25.12 Esaïe 55.3 Jean 15.3-15.4 Proverbes 19.20
32 Akataaye maonyo huidharau nafsi yake mwenyewe; Bali yeye asikilizaye lawama hujipatia ufahamu.
Proverbes 1.24-1.33 Proverbes 1.7 Matthieu 7.24-7.27 Jacques 1.22 Apocalypse 3.19
33 Kumcha Bwana ni maonyo ya hekima; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.
Proverbes 18.12 Proverbes 1.7 1 Pierre 5.5 Jacques 4.10 Proverbes 29.23

Cette Bible est dans le domaine public.