Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 14.5
Bible en Swahili de l’est


1 Bwana akasema na Musa, akamwambia,
Exode 13.1 Exode 12.1
2 Waambie wana wa Israeli, kwamba warudi na kupiga kambi yao mbele ya Pi-hahirothi, kati ya Migdoli na bahari, kukabili Baal-sefoni; mtapanga mbele yake karibu na bahari.
Jérémie 44.1 Nombres 33.7-33.8 Jérémie 46.14 Exode 13.17-13.18 Exode 14.9
3 Naye Farao atasema katika habari za wana wa Israeli, Wametatanishwa katika nchi, ile jangwa imewazuia wasitoke.
1 Samuel 23.7 Deutéronome 31.21 Psaumes 71.11 Actes 4.28 1 Samuel 23.23
4 Nami nitaufanya uwe mgumu moyo wa Farao, naye atafuata nyuma yao; nami nitajipatia utukufu kwa Farao, na kwa jeshi lake lote; na Wamisri watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana. Basi wakafanya hivyo.
Romains 9.22-9.23 Exode 7.5 Romains 9.17 Exode 7.3 Exode 9.16
5 Mfalme wa Misri aliambiwa ya kuwa wale watu wamekwisha kimbia; na moyo wa Farao, na mioyo ya watumishi wake, iligeuzwa iwe kinyume cha hao watu, nao wakasema, Ni nini jambo hili tulilotenda, kwa kuwaacha Waisraeli waende zao wasitutumikie tena?
Psaumes 105.25 Exode 12.33 Luc 11.24-11.26 Jérémie 34.10-34.17 2 Pierre 2.20-2.22
6 Akaandalia gari lake, akawachukua watu wake pamoja naye;
7 tena akatwaa magari mia sita yaliyochaguliwa, na magari yote ya Wamisri, na maakida juu ya magari hayo yote.
Exode 15.4 Juges 4.15 Esaïe 37.24 Psaumes 68.17 Juges 4.3
8 Na Bwana akaufanya moyo wake Farao mfalme wa Misri kuwa mgumu, naye akawafuata wana wa Israeli; kwa sababu wana wa Israeli walitoka kwa ujeuri.
Actes 13.17 Nombres 33.3 Exode 6.1 Exode 14.4 Exode 13.16
9 Wamisri wakafuata nyuma yao, farasi zote na magari yote ya Farao, na askari zake wenye kupanda farasi, na jeshi lake, nao wakawapata hali wamepanga pale karibu na bahari, karibu na Pi-hahirothi, kukabili Baal-sefoni.
Exode 15.9 Josué 24.6 Exode 14.2
10 Hata Farao alipokaribia, wana wa Israeli wakainua macho yao, na tazama, Wamisri wanakuja nyuma yao; wakaogopa sana; wana wa Israeli wakamlilia Bwana.
Néhémie 9.9 Josué 24.7 Psaumes 34.17 Psaumes 107.6 Matthieu 14.30-14.31
11 Wakamwambia Musa, Je! Kwa sababu hapakuwa na makaburi katika Misri umetutoa huko ili tufe jangwani? Mbona umetutendea haya, kututoa katika nchi ya Misri?
Psaumes 106.7-106.8 Nombres 14.1-14.4 Genèse 43.6 Exode 16.2-16.3 Exode 15.23-15.24
12 Neno hili silo tulilokuambia huko Misri, tukisema, Tuache tuwatumikie Wamisri? Maana ni afadhali kuwatumikia Wamisri kuliko kufa jangwani.
Exode 5.21 Marc 5.7 Jonas 4.3 Osée 4.17 Jonas 4.8
13 Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa Bwana atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele.
Exode 14.30 2 Chroniques 20.17 Lamentations 3.26 Genèse 49.18 2 Chroniques 20.15
14 Bwana atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya.
Deutéronome 3.22 Deutéronome 20.4 Josué 23.3 Deutéronome 1.30 Esaïe 30.15
15 Bwana akamwambia Musa, Mbona unanililia mimi? Waambie wana wa Israeli waendelee mbele.
Esdras 10.4-10.5 Josué 7.10 Exode 17.4 Néhémie 9.9
16 Nawe inua fimbo yako, ukanyoshe mkono wako juu ya bahari, na kuigawanya; nao wana wa Israeli watapita kati ya bahari katika nchi kavu.
Exode 4.17 Exode 7.19 Exode 14.26 Exode 4.20 Exode 4.2
17 Nami, tazama, nitaifanya mioyo ya Wamisri kuwa migumu, nao wataingia na kuwafuatia, nami nitajipatia utukufu kwa Farao, na kwa jeshi lake lote, kwa magari yake na kwa wapanda farasi wake.
Exode 14.8 Exode 14.4 Esaïe 51.12 Deutéronome 32.39 Osée 5.14
18 Na Wamisri watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, nitakapokwisha kujipatia utukufu kwa Farao, na magari yake, na farasi zake.
Exode 7.5 Exode 7.17 Exode 14.4
19 Kisha malaika wa Mungu, aliyetangulia mbele ya jeshi la Israeli, akaondoka akaenda nyuma yao; na ile nguzo ya wingu ikaondoka hapo mbele yao, ikasimama nyuma yao;
Exode 13.21-13.22 Esaïe 63.9 Exode 32.34 Nombres 20.16 Exode 14.24
20 ikafika kati ya jeshi la Misri na jeshi la Israeli; napo palikuwa na lile wingu na lile giza, lakini lilitoa nuru wakati wa usiku; na hawa hawakuwakaribia hawa usiku kucha.
Proverbes 4.18-4.19 2 Corinthiens 2.15-2.16 Psaumes 18.11 Esaïe 8.14
21 Musa; akanyosha mkono wake juu ya bahari; Bwana akaifanya bahari irudi nyuma kwa upepo wa nguvu utokao mashariki, usiku kucha, akaifanya bahari kuwa nchi kavu, maji yakagawanyika.
Exode 15.8 Esaïe 63.12 Psaumes 66.6 Psaumes 78.13 Josué 4.23
22 Wana wa Israeli wakaenda ndani kati ya bahari katika nchi kavu; nayo maji yalikuwa ukuta kwao mkono wa kuume, na mkono wa kushoto.
Psaumes 66.6 Hébreux 11.29 Exode 15.19 Psaumes 78.13 Exode 14.29
23 Na wale Wamisri wakawafuatia, wakaingia ndani kati ya bahari, farasi zote za Farao, na magari yake, na wapanda farasi wake.
Exode 14.17 Ecclésiaste 9.3 Exode 15.9 Esaïe 14.24-14.27 Exode 15.19
24 Ikawa katika zamu ya alfajiri, Bwana akalichungulia jeshi la Wamisri katika ile nguzo ya moto na ya wingu, akalifadhaisha jeshi la Wamisri.
Exode 13.21 1 Samuel 11.11 Job 22.13 Job 40.12 Job 34.20
25 Akayaondoa magurudumu ya magari yao, hata yakaenda kwa uzito; na Wamisri wakasema, Na tukimbie mbele ya Israeli; kwa kuwa Bwana anawapigania, kinyume cha Wamisri.
Exode 14.14 Amos 9.1 Psaumes 68.12 Psaumes 76.6 Job 11.20
26 Bwana akamwambia Musa, Nyosha mkono wako juu ya bahari, ili maji yarudi tena juu ya Wamisri, juu ya magari yao, na juu ya farasi zao.
Exode 14.16 Apocalypse 16.6 Jacques 2.13 Juges 1.6-1.7 Exode 7.19
27 Musa akaunyosha mkono wake juu ya bahari, na kulipopambazuka, bahari ikarudi kwa nguvu zake; Wamisri wakakimbia mbele yake; na Bwana akawakukutia mbali hao Wamisri kati ya bahari.
Josué 4.18 Psaumes 78.53 Deutéronome 11.4 Exode 14.21-14.22 Hébreux 11.29
28 Yale maji yakarudi yakafunikiza magari na wapanda farasi, hata jeshi lote la Farao lililoingia katika bahari nyuma yao; hakusalia hata mtu mmoja.
Habakuk 3.13 Habakuk 3.8-3.10 Psaumes 78.53 Psaumes 136.15 Hébreux 11.29
29 Lakini wana wa Israeli wakaenda katika nchi kavu katikati ya bahari; na hayo maji yalikuwa ni kuta upande wao wa kuume, na upande wao wa kushoto.
Exode 14.22 Psaumes 66.6-66.7 Esaïe 63.12-63.13 Esaïe 51.10 Esaïe 51.13
30 Ndivyo Bwana alivyowaokoa Israeli siku ile mikononi mwa Wamisri; Waisraeli wakawaona Wamisri ufuoni kwa bahari, wamekufa.
Psaumes 106.10 Psaumes 106.8 Psaumes 59.10 Psaumes 58.10 Exode 14.13
31 Israeli akaiona ile kazi kubwa aliyoifanya Bwana juu ya Wamisri, ndipo hao watu wakamcha Bwana, wakamwamini Bwana, na Musa mtumishi wake.
Jean 2.11 Jean 11.45 Exode 19.9 Exode 4.31 Luc 8.13

Cette Bible est dans le domaine public.