Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 35.28
Bible en Swahili de l’est


Prière de David contre ses ennemis

1 Ee Bwana, utete nao wanaoteta nami, Upigane nao wanaopigana nami.
Exode 14.25 Actes 5.39 Psaumes 43.1 Proverbes 23.11 Esaïe 49.25
2 Uishike ngao na kigao, Usimame unisaidie.
Esaïe 42.13 Exode 15.3 Psaumes 7.12-7.13 Esaïe 13.5 Deutéronome 32.41-32.42
3 Uutoe na mkuki uwapinge wanaonifuatia, Uiambie nafsi yangu, Mimi ni wokovu wako.
1 Samuel 23.26-23.27 Esaïe 10.12 Job 1.10 Esaïe 8.9-8.10 Psaumes 27.2
4 Waaibishwe, wafedheheshwe, Wanaoitafuta nafsi yangu. Warudishwe nyuma, wafadhaishwe, Wanaonizulia mabaya.
Psaumes 129.5 1 Rois 19.10 Psaumes 70.2-70.3 Psaumes 31.17-31.18 Psaumes 38.12
5 Wawe kama makapi mbele ya upepo, Malaika wa Bwana akiwaangusha chini.
Job 21.18 Esaïe 29.5 Psaumes 1.4 Esaïe 37.36 Exode 14.19
6 Njia yao na iwe giza na utelezi, Malaika wa Bwana akiwafuatia.
Jérémie 23.12 Psaumes 73.18 Proverbes 4.19 Jérémie 13.16
7 Maana bila sababu wamenifichia wavu, Bila sababu wameichimbia shimo nafsi yangu.
Psaumes 140.5 Psaumes 9.15 Job 18.8 Psaumes 64.4 Psaumes 25.3
8 Uharibifu na umpate kwa ghafula, Na wavu aliouficha umnase yeye mwenyewe; Kwa uharibifu aanguke ndani yake.
1 Thessaloniciens 5.3 Psaumes 9.15 Psaumes 73.18-73.20 1 Samuel 18.17 Luc 21.34
9 Na nafsi yangu itamfurahia Bwana, Na kuushangilia wokovu wake.
Esaïe 61.10 Psaumes 13.5 Psaumes 68.1-68.3 Psaumes 48.11 Psaumes 58.10-58.11
10 Mifupa yangu yote itasema, Bwana, ni nani aliye kama Wewe? Umponyaye maskini na mtu aliye hodari kumshinda yeye, Naam, maskini na mhitaji na mtu amtekaye.
Exode 15.11 Psaumes 51.8 Psaumes 18.17 Psaumes 86.8 Psaumes 71.19
11 Mashahidi wa udhalimu wanasimama, Wananiuliza mambo nisiyoyajua.
Psaumes 27.12 Actes 24.12-24.13 Actes 6.13 Matthieu 26.59-26.60 1 Samuel 25.10
12 Wananilipa mabaya badala ya mema, Hata nafsi yangu ikaingia ukiwa.
Jean 10.32 Jérémie 18.20 Psaumes 38.20 Proverbes 17.13 Psaumes 109.3-109.5
13 Bali mimi, walipougua wao, Nguo yangu ilikuwa gunia. Nalijitesa nafsi yangu kwa kufunga; Maombi yangu yakarejea kifuani mwangu.
Job 30.25 Matthieu 10.13 Psaumes 69.10-69.11 Luc 10.6 Lévitique 16.29
14 Nalijifanya kama kwamba ni rafiki au ndugu yangu, Naliinama nikilia kama aliyefiwa na mamaye.
Genèse 24.67 Luc 19.41-19.42 2 Samuel 1.11-1.12 2 Samuel 1.17-1.27 Psaumes 38.6
15 Lakini nikijikwaa hufurahi na kukusanyana, Walinikusanyikia watu ovyo nisiowajua, Wananipapura wala hawakomi.
Psaumes 7.2 Marc 14.65 Psaumes 69.12 Proverbes 24.17-24.18 Psaumes 38.17
16 Kama wenye mzaha wakikufuru karamuni Wananisagia meno.
Lamentations 2.16 Job 16.9 Psaumes 37.12 1 Corinthiens 5.8 Esaïe 1.14-1.15
17 Bwana, hata lini utatazama? Uiokoe nafsi yangu na maharabu yao, Na mpenzi wangu na wana-simba.
Habakuk 1.13 Psaumes 22.20-22.21 Psaumes 10.14 Psaumes 74.9-74.10 Psaumes 89.46
18 Nitakushukuru katika kusanyiko kubwa; Nitakusifu kati ya watu wengi.
Psaumes 116.18 Romains 15.9 Psaumes 138.4-138.5 Psaumes 111.1 Psaumes 22.22-22.25
19 Walio adui zangu bure wasinisimange, Wanaonichukia bila sababu wasining’ong’e.
Psaumes 69.4 Psaumes 38.19 Jean 15.25 Psaumes 13.4 Proverbes 6.13
20 Maana hawasemi maneno ya amani, Na juu ya watulivu wa nchi huwaza hila.
Actes 23.15 Matthieu 12.19 Psaumes 52.2 Psaumes 36.3-36.4 Jérémie 11.19
21 Nao wananifumbulia vinywa vyao, Husema, Ewe! Ewe! Jicho letu limeona.
Psaumes 40.15 Psaumes 22.13 Psaumes 70.3 Esaïe 9.12 Psaumes 54.7
22 Wewe, Bwana, umeona, usinyamaze; Ee Bwana, usiwe mbali nami.
Psaumes 28.1 Psaumes 10.1 Exode 3.7 Psaumes 71.12 Psaumes 22.11
23 Uamke, uwe macho ili kunipatia hukumu Kwa ajili ya madai yangu, Mungu wangu na Bwana wangu.
Psaumes 44.23 Psaumes 80.2 Psaumes 7.6 Psaumes 59.4 Psaumes 89.26
24 Unihukumu kwa haki yako, Ee Bwana, Mungu wangu, Wala wasinisimangize.
Psaumes 7.8 Psaumes 43.1 Psaumes 35.19 Psaumes 26.1 Job 20.5
25 Wasiseme moyoni, Haya! Ndivyo tutakavyo; Wasiseme, Tumemmeza.
Lamentations 2.16 Psaumes 124.3 Exode 15.9 Matthieu 27.43 Marc 2.8
26 Waaibishwe, wafedheheshwe pamoja, Wanaoifurahia hali yangu mbaya. Wavikwe aibu na fedheha, Wanaojikuza juu yangu.
Psaumes 38.16 Psaumes 132.18 Job 19.5 Job 8.22 Esaïe 65.13-65.15
27 Washangilie na kufurahi, Wapendezwao na haki yangu. Naam, waseme daima, Atukuzwe Bwana, Apendezwaye na amani ya mtumishi wake.
Psaumes 149.4 Psaumes 40.16 Psaumes 70.4 Jérémie 32.40-32.41 Sophonie 3.17
28 Na ulimi wangu utanena haki yako, Na sifa zako mchana kutwa.
Psaumes 71.24 Psaumes 145.21 Psaumes 145.5 Psaumes 71.15 Psaumes 104.33-104.34

Cette Bible est dans le domaine public.