Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 22.20
Bible en Swahili de l’est


Les souffrances et la gloire du Sauveur

1 Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha? Mbona U mbali na wokovu wangu, Na maneno ya kuugua kwangu?
Marc 15.34 Matthieu 27.46 Hébreux 5.7 Psaumes 38.8 Psaumes 22.16
2 Ee Mungu wangu, nalia mchana lakini hujibu Na wakati wa usiku lakini sipati raha.
Luc 18.7 Psaumes 88.1 Psaumes 42.3 Luc 22.41-22.46 Luc 6.12
3 Na Wewe U Mtakatifu, Uketiye juu ya sifa za Israeli.
Deutéronome 10.21 Esaïe 6.3 Apocalypse 4.8 Psaumes 65.1 Psaumes 50.23
4 Baba zetu walikutumaini Wewe, Walitumaini, na Wewe ukawaokoa.
Exode 14.13-14.14 Romains 4.18-4.22 Exode 14.31 Hébreux 11.8-11.32 Genèse 32.9-32.12
5 Walikulilia Wewe wakaokoka, Walikutumaini wasiaibike.
Esaïe 49.23 Romains 9.33 Psaumes 31.1 Psaumes 71.1 Psaumes 25.2-25.3
6 Lakini mimi ni mdudu wala si mtu, Laumu ya wanadamu na mzaha wa watu.
Job 25.6 Esaïe 41.14 Esaïe 49.7 Esaïe 53.3 Matthieu 11.19
7 Wote wanionao hunicheka sana, Hunifyonya, wakitikisa vichwa vyao;
Marc 15.29 Psaumes 109.25 Psaumes 44.14 Matthieu 27.39-27.40 Luc 23.11
8 Husema, Umtegemee Bwana; na amponye; Na amwokoe sasa, maana apendezwa naye.
Matthieu 27.42-27.43 Psaumes 91.14 Marc 15.30-15.32 Psaumes 18.19 Matthieu 3.17
9 Naam, Wewe ndiwe uliyenitoa tumboni, Ulinitumainisha matitini mwa mama yangu.
Psaumes 71.6 Esaïe 9.6 Matthieu 2.13-2.15 Psaumes 71.17 Esaïe 7.14-7.15
10 Kwako nalitupwa tangu tumboni, Toka tumboni mwa mamangu ndiwe Mungu wangu.
Esaïe 49.1 Galates 1.15 Jérémie 1.5 Jean 20.17 Luc 2.52
11 Usiwe mbali nami maana taabu i karibu, Kwa maana hakuna msaidizi.
Psaumes 72.12 Psaumes 71.12 Psaumes 10.1 Psaumes 35.22 2 Rois 14.26
12 Mafahali wengi wamenizunguka, Walio hodari wa Bashani wamenisonga;
Psaumes 68.30 Amos 4.1-4.3 Matthieu 27.1 Actes 4.27 Esaïe 34.7
13 Wananifumbulia vinywa vyao, Kama simba apapuraye na kunguruma.
Psaumes 35.21 Psaumes 17.12 Lamentations 2.16 Lamentations 3.46 Job 16.10
14 Nimemwagika kama maji, Mifupa yangu yote imeteguka, Moyo wangu umekuwa kama nta, Na kuyeyuka ndani ya mtima wangu.
Daniel 5.6 Job 23.16 Josué 7.5 Psaumes 31.10 Psaumes 68.2
15 Nguvu zangu zimekauka kama gae, Ulimi wangu waambatana na taya zangu; Unaniweka katika mavumbi ya mauti
Jean 19.28 Psaumes 104.29 Proverbes 17.22 Esaïe 53.12 Job 29.10
16 Kwa maana mbwa wamenizunguka; Kusanyiko la waovu wamenisonga; Wamenizua mikono na miguu.
Zacharie 12.10 Matthieu 27.35 Jean 19.23 Luc 23.33 Jean 19.37
17 Naweza kuihesabu mifupa yangu yote; Wao wananitazama na kunikodolea macho.
Luc 23.35 Luc 23.27 Matthieu 27.39-27.41 Matthieu 27.36 Marc 15.29-15.32
18 Wanagawanya nguo zangu, Na vazi langu wanalipigia kura.
Luc 23.34 Matthieu 27.35 Jean 19.23-19.24 Marc 15.24
19 Nawe, Bwana, usiwe mbali, Ee Nguvu zangu, fanya haraka kunisaidia.
Psaumes 22.11 Psaumes 70.5 Psaumes 40.17 Psaumes 21.1 Psaumes 18.1
20 Uniponye nafsi yangu na upanga, Mpenzi wangu na nguvu za mbwa.
Psaumes 35.17 Zacharie 13.7 Psaumes 17.13
21 Kinywani mwa simba uniokoe; Naam, toka pembe za nyati umenijibu.
2 Timothée 4.17 Nombres 23.22 Luc 22.53 Job 39.9-39.10 Jean 8.59
22 Nitalihubiri jina lako kwa ndugu zangu, Katikati ya kusanyiko nitakusifu.
Psaumes 40.9-40.10 Matthieu 28.10 Jean 20.17 Romains 8.29 Matthieu 25.40
23 Ninyi mnaomcha Bwana, msifuni, Enyi nyote mlio wazao wa Yakobo, mtukuzeni, Mcheni, enyi nyote mlio wazao wa Israeli.
Psaumes 135.19-135.20 Psaumes 50.23 Psaumes 22.30 1 Corinthiens 10.31 Psaumes 33.8
24 Maana hakulidharau teso la mteswa, Wala hakuchukizwa nalo; Wala hakumficha uso wake, Bali alipomlilia akamsikia.
Hébreux 5.7 Esaïe 50.6-50.9 Psaumes 34.6 Psaumes 118.5 Psaumes 22.6
25 Kwako zinatoka sifa zangu Katika kusanyiko kubwa. Nitaziondoa nadhiri zangu Mbele yao wamchao.
Psaumes 35.18 Psaumes 40.9-40.10 Psaumes 66.13 Psaumes 111.1 Psaumes 118.19-118.20
26 Wapole watakula na kushiba, Wamtafutao Bwana watamsifu; Mioyo yenu na iishi milele.
Psaumes 69.32 Esaïe 25.6 Esaïe 65.13 Lévitique 7.11-7.17 Jean 6.48-6.58
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka, Na watu watamrejea Bwana; Jamaa zote za mataifa watamsujudia.
Psaumes 2.8 Psaumes 86.9 Psaumes 96.7 Esaïe 45.22 Esaïe 49.6
28 Maana ufalme una Bwana, Naye ndiye awatawalaye mataifa.
Zacharie 14.9 Psaumes 47.7-47.8 Abdias 1.21 Matthieu 6.13 Apocalypse 11.15
29 Wakwasi wote wa dunia watakula na kusujudu, Humwinamia wote washukao mavumbini; Naam, yeye asiyeweza kujihuisha nafsi yake,
Psaumes 45.12 Esaïe 26.19 Philippiens 2.10 Romains 14.10-14.12 Esaïe 45.23
30 Wazao wake watamtumikia. Zitasimuliwa habari za Bwana, Kwa kizazi kitakachokuja,
Psaumes 87.6 Matthieu 3.9 Psaumes 102.28 Psaumes 24.6 Hébreux 2.13
31 Nao watawahubiri watakaozaliwa haki yake, Ya kwamba ndiye aliyeyafanya.
Psaumes 78.6 Psaumes 86.9 Psaumes 102.18 Psaumes 145.4-145.7 Psaumes 40.9

Cette Bible est dans le domaine public.