Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 22.16
Bible en Swahili de l’est


Les souffrances et la gloire du Sauveur

1 Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha? Mbona U mbali na wokovu wangu, Na maneno ya kuugua kwangu?
Marc 15.34 Matthieu 27.46 Hébreux 5.7 Psaumes 22.16 Job 3.24
2 Ee Mungu wangu, nalia mchana lakini hujibu Na wakati wa usiku lakini sipati raha.
Luc 18.7 Psaumes 88.1 Psaumes 42.3 1 Thessaloniciens 3.10 Lamentations 3.44
3 Na Wewe U Mtakatifu, Uketiye juu ya sifa za Israeli.
Deutéronome 10.21 Esaïe 6.3 Apocalypse 4.8 Psaumes 65.1 Psaumes 50.23
4 Baba zetu walikutumaini Wewe, Walitumaini, na Wewe ukawaokoa.
Exode 14.13-14.14 Psaumes 44.1-44.7 Genèse 15.6 Genèse 32.28 Romains 4.18-4.22
5 Walikulilia Wewe wakaokoka, Walikutumaini wasiaibike.
Esaïe 49.23 Psaumes 31.1 Psaumes 71.1 Romains 9.33 Juges 4.3
6 Lakini mimi ni mdudu wala si mtu, Laumu ya wanadamu na mzaha wa watu.
Job 25.6 Esaïe 41.14 Esaïe 49.7 Esaïe 53.3 Matthieu 11.19
7 Wote wanionao hunicheka sana, Hunifyonya, wakitikisa vichwa vyao;
Marc 15.29 Psaumes 109.25 Matthieu 27.39-27.40 Psaumes 44.14 Marc 15.20
8 Husema, Umtegemee Bwana; na amponye; Na amwokoe sasa, maana apendezwa naye.
Psaumes 91.14 Matthieu 27.42-27.43 Marc 15.30-15.32 Matthieu 17.5 Proverbes 16.3
9 Naam, Wewe ndiwe uliyenitoa tumboni, Ulinitumainisha matitini mwa mama yangu.
Psaumes 71.6 Matthieu 2.13-2.15 Esaïe 9.6 Esaïe 49.1-49.2 Apocalypse 12.4-12.5
10 Kwako nalitupwa tangu tumboni, Toka tumboni mwa mamangu ndiwe Mungu wangu.
Galates 1.15 Esaïe 49.1 Esaïe 46.3-46.4 Jérémie 1.5 Jean 20.17
11 Usiwe mbali nami maana taabu i karibu, Kwa maana hakuna msaidizi.
Psaumes 72.12 Psaumes 10.1 Psaumes 71.12 Esaïe 63.5 Psaumes 142.4-142.6
12 Mafahali wengi wamenizunguka, Walio hodari wa Bashani wamenisonga;
Psaumes 68.30 Amos 4.1-4.3 Deutéronome 32.14-32.15 Ezéchiel 39.18 Jérémie 50.11
13 Wananifumbulia vinywa vyao, Kama simba apapuraye na kunguruma.
Psaumes 35.21 Lamentations 3.46 Job 16.10 Psaumes 17.12 Lamentations 2.16
14 Nimemwagika kama maji, Mifupa yangu yote imeteguka, Moyo wangu umekuwa kama nta, Na kuyeyuka ndani ya mtima wangu.
Daniel 5.6 Josué 7.5 Job 23.16 Psaumes 22.17 Jean 12.27
15 Nguvu zangu zimekauka kama gae, Ulimi wangu waambatana na taya zangu; Unaniweka katika mavumbi ya mauti
Jean 19.28 Psaumes 104.29 Psaumes 69.21 Proverbes 17.22 Esaïe 53.12
16 Kwa maana mbwa wamenizunguka; Kusanyiko la waovu wamenisonga; Wamenizua mikono na miguu.
Zacharie 12.10 Matthieu 27.35 Jean 19.23 Luc 23.33 Jean 19.37
17 Naweza kuihesabu mifupa yangu yote; Wao wananitazama na kunikodolea macho.
Luc 23.35 Luc 23.27 Matthieu 27.39-27.41 Esaïe 52.14 Matthieu 27.36
18 Wanagawanya nguo zangu, Na vazi langu wanalipigia kura.
Luc 23.34 Matthieu 27.35 Jean 19.23-19.24 Marc 15.24
19 Nawe, Bwana, usiwe mbali, Ee Nguvu zangu, fanya haraka kunisaidia.
Psaumes 22.11 Psaumes 10.1 Psaumes 40.13 Psaumes 69.13-69.18 Psaumes 70.5
20 Uniponye nafsi yangu na upanga, Mpenzi wangu na nguvu za mbwa.
Psaumes 35.17 Zacharie 13.7 Psaumes 17.13
21 Kinywani mwa simba uniokoe; Naam, toka pembe za nyati umenijibu.
2 Timothée 4.17 Nombres 23.22 Jean 14.30 Actes 4.27 Esaïe 34.7
22 Nitalihubiri jina lako kwa ndugu zangu, Katikati ya kusanyiko nitakusifu.
Romains 8.29 Psaumes 40.9-40.10 Matthieu 28.10 Jean 20.17 Matthieu 12.48-12.49
23 Ninyi mnaomcha Bwana, msifuni, Enyi nyote mlio wazao wa Yakobo, mtukuzeni, Mcheni, enyi nyote mlio wazao wa Israeli.
Psaumes 135.19-135.20 Psaumes 50.23 Apocalypse 15.4 Psaumes 145.19 Psaumes 115.11
24 Maana hakulidharau teso la mteswa, Wala hakuchukizwa nalo; Wala hakumficha uso wake, Bali alipomlilia akamsikia.
Hébreux 5.7 Psaumes 34.6 Psaumes 118.5 Esaïe 50.6-50.9 Psaumes 116.3-116.6
25 Kwako zinatoka sifa zangu Katika kusanyiko kubwa. Nitaziondoa nadhiri zangu Mbele yao wamchao.
Psaumes 40.9-40.10 Psaumes 35.18 Psaumes 111.1 Psaumes 66.13 Psaumes 56.12
26 Wapole watakula na kushiba, Wamtafutao Bwana watamsifu; Mioyo yenu na iishi milele.
Psaumes 69.32 Esaïe 65.13 Esaïe 25.6 Psaumes 107.9 Psaumes 40.16
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka, Na watu watamrejea Bwana; Jamaa zote za mataifa watamsujudia.
Psaumes 2.8 Psaumes 86.9 Psaumes 96.7 Esaïe 45.22 Esaïe 49.6
28 Maana ufalme una Bwana, Naye ndiye awatawalaye mataifa.
Zacharie 14.9 Psaumes 47.7-47.8 Abdias 1.21 Matthieu 6.13 Daniel 7.14
29 Wakwasi wote wa dunia watakula na kusujudu, Humwinamia wote washukao mavumbini; Naam, yeye asiyeweza kujihuisha nafsi yake,
Psaumes 45.12 Philippiens 2.10 Esaïe 26.19 Romains 14.10-14.12 Esaïe 45.23
30 Wazao wake watamtumikia. Zitasimuliwa habari za Bwana, Kwa kizazi kitakachokuja,
Galates 3.26-3.29 Psaumes 73.15 1 Pierre 2.9 Esaïe 53.10 Psaumes 14.5
31 Nao watawahubiri watakaozaliwa haki yake, Ya kwamba ndiye aliyeyafanya.
Psaumes 78.6 Psaumes 86.9 Psaumes 102.18 Romains 3.21-3.25 Esaïe 54.1

Cette Bible est dans le domaine public.