Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 6.39
Bible en Swahili de l’est


Inauguration du temple

1 Ndipo Sulemani akanena, Bwana alisema ya kwamba atakaa katika giza nene.
1 Rois 8.12-8.50 Hébreux 12.18 Exode 20.21 Psaumes 18.8-18.11 Lévitique 16.2
2 Lakini nimekujengea nyumba ya kukaa, iwe mahali pa makao yako milele.
1 Chroniques 17.12 1 Chroniques 22.10-22.11 2 Samuel 7.13 Psaumes 132.5 1 Rois 8.13
3 Mfalme akageuza uso wake, akawabarikia mkutano wote wa Israeli; na mkutano wote wa Israeli wakasimama.
1 Rois 8.14 Néhémie 8.5-8.7 Josué 22.6 1 Rois 8.55-8.61 2 Chroniques 29.29
4 Akasema, Bwana, Mungu wa Israeli, ahimidiwe, aliyenena kwa kinywa chake na baba yangu Daudi, akalitimiza kwa mikono yake, akasema,
Psaumes 138.1-138.2 1 Chroniques 29.20 Psaumes 68.4 Psaumes 41.13 Matthieu 24.35
5 Tangu siku ile nilipowatoa watu wangu katika nchi ya Misri, sikuchagua mji wo wote wa kabila zote za Israeli ili kujenga nyumba, jina langu liwe humo; wala sikumchagua mtu ye yote awe mkuu juu ya watu wangu Israeli;
Daniel 9.19 1 Rois 8.16 2 Samuel 7.6-7.7 Deutéronome 12.11 Exode 23.21
6 lakini nimeuchagua Yerusalemu, jina langu liwe humo; na Daudi nimemchagua awe juu ya watu wangu Israeli.
2 Chroniques 12.13 1 Chroniques 28.4 Psaumes 78.68-78.70 Psaumes 48.1 Psaumes 132.13
7 Basi ilikuwa moyoni mwake Daudi, baba yangu, kujenga nyumba kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
1 Rois 5.3 1 Chroniques 17.1 1 Rois 8.17 1 Chroniques 28.2-28.4 2 Samuel 7.2-7.3
8 Lakini Bwana akamwambia Daudi baba yangu, Kwa kuwa ilikuwa moyoni mwako kujenga nyumba kwa jina langu, ulifanya vema kuwaza hivi moyoni mwako;
1 Rois 8.18-8.21 Marc 14.8 2 Corinthiens 8.12
9 lakini si wewe utakayeijenga nyumba hiyo; ila mwanao atakayetoka katika viuno vyako, yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa jina langu.
2 Samuel 7.12-7.13 1 Chroniques 17.4 1 Chroniques 17.11-17.12
10 Basi Bwana amelitimiza neno lile alilolinena; nami nimesimama mahali pa Daudi baba yangu, na kuketi katika kiti cha enzi cha Israeli, kama Bwana alivyoahidi, nami nimeijenga nyumba kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
1 Chroniques 28.5 1 Chroniques 29.23 1 Rois 3.6-3.7 Ecclésiaste 2.18-2.19 1 Chroniques 17.11
11 Ndimo nilimoliweka hilo sanduku, ambalo ndani yake mna agano la Bwana, alilolifanya na wana wa Israeli.
2 Chroniques 5.10 2 Chroniques 5.7 Exode 40.20 Hébreux 9.4 1 Rois 8.9
12 Akasimama mbele ya madhabahu ya Bwana, machoni pa mkutano wote wa Israeli, akainyosha mikono;
Esaïe 50.10 Exode 9.33 Psaumes 63.4 Job 11.13 Psaumes 143.6
13 (maana Sulemani alikuwa amefanya mimbari ya shaba, urefu wake mikono mitano, na upana wake mikono mitano, na kwenda juu kwake mikono mitatu, na kuisimamisha katikati ya ua; akasimama juu yake, akapiga magoti mbele ya mkutano wote wa Israeli, akaikunjua mikono yake kuelekea mbinguni);
1 Rois 8.54 Néhémie 8.4 Psaumes 95.6 2 Chroniques 4.9 1 Rois 6.36
14 akasema, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe, mbinguni, wala duniani; ushikaye maagano na rehema kwa watumishi wako, waendao mbele zako kwa moyo wao wote;
Exode 15.11 Deutéronome 7.9 Néhémie 1.5 1 Rois 18.36 Genèse 35.10
15 uliyemtimizia mtumishi wako Daudi, baba yangu, ahadi uliyomwahidi; naam, ulinena kwa kinywa chako, ukayatimiza kwa mkono wako, kama ilivyo leo.
1 Chroniques 22.9-22.10 2 Samuel 7.12 1 Rois 8.24
16 Sasa, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, umfikilizie mtumishi wako Daudi, baba yangu, ahadi uliyomwahidia, ukisema, Hutakosa kuwa na mtu machoni pangu, wa kuketi katika kiti cha enzi cha Israeli; wakiwa tu watoto wako wataiangalia njia yao, ili kuiendea torati yangu, kama wewe ulivyokwenda mbele zangu.
2 Chroniques 7.18 1 Rois 2.4 Psaumes 132.12 Psaumes 119.1 Ezéchiel 36.37
17 Basi sasa, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, ulithibitishe neno lako, ulilomwambia mtumishi wako Daudi.
Exode 24.10 Jérémie 11.5 Esaïe 41.17 Esaïe 45.3 2 Samuel 7.25-7.29
18 Lakini Mungu je! Yamkini atakaa na watu duniani? Tazama, mbingu na mbingu za mbingu za mbingu hazikutoshi; siuze nyumba hii niliyoijenga!
Esaïe 66.1 2 Chroniques 2.6 Psaumes 113.5-113.6 Job 25.4-25.6 2 Chroniques 32.15
19 Walakini umwangalie mtumwa wako anayoyaomba, na kusihi, Ee Bwana, Mungu wangu, usikie kilio na maombi anayoyaomba mtumwa wako mbele zako;
Psaumes 74.20 Daniel 9.17-9.19 Psaumes 20.1-20.3 Psaumes 130.2 Luc 18.1-18.7
20 ili macho yako yafumbuke kwa nyumba hii mchana na usiku, mahali uliponena, ndipo utakapoliweka jina lako; usikie maombi atakayoomba mtumwa wako, akikabili mahali hapa.
Psaumes 34.15 1 Rois 8.29-8.30 2 Chroniques 16.9 2 Rois 19.16 Psaumes 121.5
21 Uyasikie atakayosihi mtumwa wako, na watu wako Israeli, watakapoomba wakikabili mahali hapa; naam, usikie toka makaoni mwako, toka mbinguni, nawe usikiapo, samehe.
Esaïe 43.25 Michée 7.18 Daniel 9.19 2 Chroniques 6.39 Psaumes 130.3-130.4
22 Ikiwa mtu amemkosea mwenzake, akitiwa kiapo, aapishwe, naye akija na kuapa hapa mbele ya madhabahu yako nyumbani humu;
Exode 22.11 Nombres 5.19-5.22 1 Rois 8.31-8.32 Lévitique 5.1 Matthieu 23.18
23 basi, usikie mbinguni, ukatende, ukawahukumu watumwa wako; ukimlipiza mwovu, kumpatilizia njia yake kichwani; ukamfanyie haki mwenye haki, ukimjalia kwa kadiri ya haki yake.
Ezéchiel 18.20 Proverbes 17.15 Romains 2.9-2.10 Esaïe 3.10-3.11 Jérémie 51.56
24 Ikiwa watu wako Israeli wamepigwa mbele ya adui zao, kwa sababu wamekukosa wewe; kama wakirejea kwako, na kulikiri jina lako, wakikuomba na kukusihi nyumbani humu;
Lévitique 26.17 Deutéronome 4.29-4.31 Jérémie 3.12-3.13 Deutéronome 28.25 Juges 2.14-2.15
25 basi usikie huko mbinguni, ukaisamehe dhambi ya watu wako Israeli, na kuwarejeza tena katika nchi uliyowapa wao na baba zao.
Exode 6.8 Josué 21.43 Psaumes 106.40-106.47 Jérémie 33.6-33.13 Genèse 13.15
26 Ikiwa mbingu zimefungwa, hata hakuna mvua, kwa sababu wamekukosa wewe; kama wakiomba wakikabili mahali hapa, na kulikiri jina lako, na kuiacha dhambi yao, uwatesapo;
Lévitique 26.19 Deutéronome 11.17 Luc 4.25 2 Chroniques 33.12-33.13 Esaïe 50.1-50.2
27 basi usikie huko mbinguni, ukaisamehe dhambi ya watumwa wako, na ya watu wako Israeli; uwafundishapo njia njema iwapasayo waiendee; ukainyeshee mvua nchi yako, uliyowapa watu wako iwe urithi.
Psaumes 94.12 1 Rois 18.40-18.45 Psaumes 68.9 Osée 2.21-2.22 Jérémie 42.3
28 Ikiwa nchi imeingia njaa, au tauni, au ukosefu wa mvua, au ukungu, au nzige, au panzi; ikiwa adui wamewahusuru katika nchi ya miji yao, au ukiwapo msiba wo wote, au uele wo wote;
2 Rois 6.25-6.29 2 Chroniques 32.24 Lévitique 26.16 2 Chroniques 32.1 Deutéronome 28.21-28.61
29 yo yote atakayoyaomba na kusihi mtu awaye yote, au watu wako Israeli wote pamoja, watakaojua kila mtu pigo lake mwenyewe, na msiba wake mwenyewe, akiinyoshea mikono nyumba hii;
Psaumes 32.2-32.6 Psaumes 91.15 Psaumes 33.12-33.13 Psaumes 142.1-142.2 2 Chroniques 6.12-6.13
30 basi usikie huko mbinguni, ukaapo, ukasamehe, ukampatilize kila mtu kwa kadiri ya njia zake zote; wewe umjuaye moyo; (maana wewe peke yako ndiwe uijuaye mioyo ya wanadamu);
1 Chroniques 28.9 1 Samuel 16.7 Psaumes 11.4-11.5 Jean 2.25 Hébreux 4.13
31 ili wakuche wewe, waziendee njia zako, siku zote watakazoishi katika nchi uliyowapa baba zetu.
1 Samuel 12.24 Exode 20.20 Psaumes 130.4 Actes 9.31 Psaumes 128.1
32 Hata na mgeni naye, asiyekuwa mmoja wa watu wako Israeli, atakapokuja kutoka nchi iliyo mbali sana kwa ajili ya jina lako kuu, na mkono wako ulio hodari, na mkono wako ulionyoshwa; hao watakapokuja na kuomba wakiielekea nyumba hii;
Exode 3.19-3.20 Jean 12.20 Esaïe 56.3-56.7 Actes 10.1-10.4 Esaïe 66.20
33 basi usikie huko mbinguni, toka makaoni mwako, ukatende yote atakayokuomba huyo mgeni; ili watu wote wa dunia wapate kulijua jina lako, na kukucha wewe, kama watu wako Israeli, tena wajue ya kuwa nyumba hii niliyoijenga imeitwa kwa jina lako.
2 Chroniques 7.14 Psaumes 138.4-138.5 Esaïe 49.6 Esaïe 54.1-54.3 2 Rois 19.19
34 Ikiwa watu wako wametoka kupigana na adui zao, utakakowatuma ko kote, wakikuomba kuuelekea mji huu uliouchagua, na nyumba hii niliyoijenga kwa jina lako;
Daniel 6.10 1 Rois 8.13 1 Samuel 15.3 2 Chroniques 14.9-14.12 2 Chroniques 20.4
35 basi uyasikie huko mbinguni wayaombayo, na kusihi, ukaitetee haki yao.
Esaïe 37.21-37.36 Jérémie 5.28 Daniel 9.17-9.19 Psaumes 9.3-9.4
36 Wakikukosa, (maana hakuna mtu asiyekosa), hata uwakasirikie, na kuwatia mikononi mwa adui zao, wawahamishe, na kuwachukua mateka mpaka nchi iliyo mbali au iliyo karibu;
Jacques 3.2 1 Jean 1.8-1.10 Ecclésiaste 7.20 Job 15.14-15.16 Psaumes 143.2
37 basi wakikumbuka katika nchi walikohamishwa, na kutubu, na kukusihi katika nchi ya uhamisho wao, wakisema, Tumekosa, tumetenda kwa ukaidi, tumefanya maovu;
Jérémie 3.12-3.14 Daniel 9.5-9.11 Esdras 9.6-9.7 Job 33.27-33.28 Luc 15.17-15.19
38 wakurudiapo kwa mioyo yao yote, na kwa nia zao zote, katika nchi ya uhamisho wao, adui walikowahamisha, wakiomba na kuielekea nchi uliyowapa baba zao, na mji huu uliouchagua, na nyumba hii niliyoijenga kwa jina lako;
Daniel 6.10 Daniel 9.3-9.4 Deutéronome 30.2-30.6 Jérémie 29.12-29.14 2 Chroniques 33.11-33.13
39 basi uyasikie toka mbinguni, toka makaoni mwako, wayaombayo, na kusihi, ukaitetee haki yao; ukawasamehe watu wako, waliokosa juu yako.
Zacharie 1.15-1.16 2 Chroniques 6.35 Psaumes 25.18 Michée 7.18-7.20
40 Na sasa, Ee Mungu wangu, macho yako yafumbuke, nakusihi, masikio yako yakasikilize maombi yaombwayo mahali hapa.
2 Chroniques 7.15 Psaumes 17.1 Néhémie 1.11 Néhémie 1.6 Psaumes 88.1
41 Sasa, Ee Bwana, Mungu, uondoke, uende kwenye raha yako, wewe na sanduku la nguvu zako; makuhani wako, Ee Bwana, Mungu, wavikwe wokovu, watakatifu wako na washangilie mema.
1 Chroniques 28.2 Néhémie 9.25 Esaïe 61.10 Psaumes 132.16 Apocalypse 19.14
42 Ee Bwana, Mungu, usiurudishe nyuma uso wa masihi wako,uzikumbuke fadhili za Daudi mtumishi wako.
Esaïe 55.3 Psaumes 132.1 1 Rois 2.16 Actes 13.34 Psaumes 2.2

Cette Bible est dans le domaine public.