Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 6.16
Bible en Swahili de l’est


Inauguration du temple

1 Ndipo Sulemani akanena, Bwana alisema ya kwamba atakaa katika giza nene.
Exode 20.21 1 Rois 8.12-8.50 Hébreux 12.18 Psaumes 97.2 Psaumes 18.8-18.11
2 Lakini nimekujengea nyumba ya kukaa, iwe mahali pa makao yako milele.
1 Chroniques 28.6 Apocalypse 21.3 2 Chroniques 2.4-2.6 1 Chroniques 28.20 Psaumes 132.13-132.14
3 Mfalme akageuza uso wake, akawabarikia mkutano wote wa Israeli; na mkutano wote wa Israeli wakasimama.
1 Rois 8.14 Luc 24.50-24.51 1 Chroniques 16.2 Néhémie 8.5-8.7 Josué 22.6
4 Akasema, Bwana, Mungu wa Israeli, ahimidiwe, aliyenena kwa kinywa chake na baba yangu Daudi, akalitimiza kwa mikono yake, akasema,
1 Chroniques 29.10 Psaumes 68.32-68.35 Luc 1.68-1.70 1 Chroniques 17.12 1 Rois 8.15
5 Tangu siku ile nilipowatoa watu wangu katika nchi ya Misri, sikuchagua mji wo wote wa kabila zote za Israeli ili kujenga nyumba, jina langu liwe humo; wala sikumchagua mtu ye yote awe mkuu juu ya watu wangu Israeli;
1 Samuel 13.13-13.14 1 Samuel 15.23 Exode 20.24 Deutéronome 12.5 Daniel 9.19
6 lakini nimeuchagua Yerusalemu, jina langu liwe humo; na Daudi nimemchagua awe juu ya watu wangu Israeli.
1 Chroniques 28.4 2 Chroniques 12.13 Psaumes 78.68-78.70 Psaumes 48.1 Psaumes 132.13
7 Basi ilikuwa moyoni mwake Daudi, baba yangu, kujenga nyumba kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
1 Chroniques 17.1 1 Rois 5.3 1 Chroniques 22.7 1 Rois 8.17 1 Chroniques 28.2-28.4
8 Lakini Bwana akamwambia Daudi baba yangu, Kwa kuwa ilikuwa moyoni mwako kujenga nyumba kwa jina langu, ulifanya vema kuwaza hivi moyoni mwako;
Marc 14.8 2 Corinthiens 8.12 1 Rois 8.18-8.21
9 lakini si wewe utakayeijenga nyumba hiyo; ila mwanao atakayetoka katika viuno vyako, yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa jina langu.
1 Chroniques 17.4 1 Chroniques 17.11-17.12 2 Samuel 7.12-7.13
10 Basi Bwana amelitimiza neno lile alilolinena; nami nimesimama mahali pa Daudi baba yangu, na kuketi katika kiti cha enzi cha Israeli, kama Bwana alivyoahidi, nami nimeijenga nyumba kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
Ecclésiaste 1.4 1 Rois 2.12 1 Chroniques 28.5 1 Chroniques 29.23 1 Rois 3.6-3.7
11 Ndimo nilimoliweka hilo sanduku, ambalo ndani yake mna agano la Bwana, alilolifanya na wana wa Israeli.
2 Chroniques 5.10 2 Chroniques 5.7 1 Rois 8.21 Exode 40.20 Hébreux 9.4
12 Akasimama mbele ya madhabahu ya Bwana, machoni pa mkutano wote wa Israeli, akainyosha mikono;
Exode 9.33 Psaumes 63.4 Job 11.13 Psaumes 143.6 Esaïe 50.10
13 (maana Sulemani alikuwa amefanya mimbari ya shaba, urefu wake mikono mitano, na upana wake mikono mitano, na kwenda juu kwake mikono mitatu, na kuisimamisha katikati ya ua; akasimama juu yake, akapiga magoti mbele ya mkutano wote wa Israeli, akaikunjua mikono yake kuelekea mbinguni);
1 Rois 8.54 Néhémie 8.4 Psaumes 95.6 Daniel 6.10 Luc 22.41
14 akasema, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe, mbinguni, wala duniani; ushikaye maagano na rehema kwa watumishi wako, waendao mbele zako kwa moyo wao wote;
Exode 15.11 Deutéronome 7.9 Jérémie 10.6 Psaumes 103.17-103.18 Psaumes 89.8
15 uliyemtimizia mtumishi wako Daudi, baba yangu, ahadi uliyomwahidi; naam, ulinena kwa kinywa chako, ukayatimiza kwa mkono wako, kama ilivyo leo.
1 Chroniques 22.9-22.10 1 Rois 8.24 2 Samuel 7.12
16 Sasa, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, umfikilizie mtumishi wako Daudi, baba yangu, ahadi uliyomwahidia, ukisema, Hutakosa kuwa na mtu machoni pangu, wa kuketi katika kiti cha enzi cha Israeli; wakiwa tu watoto wako wataiangalia njia yao, ili kuiendea torati yangu, kama wewe ulivyokwenda mbele zangu.
1 Rois 2.4 2 Chroniques 7.18 Psaumes 132.12 Jean 15.14-15.15 Psaumes 119.1
17 Basi sasa, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, ulithibitishe neno lako, ulilomwambia mtumishi wako Daudi.
2 Chroniques 6.14 2 Chroniques 6.4 Exode 24.10 Jérémie 11.5 Esaïe 41.17
18 Lakini Mungu je! Yamkini atakaa na watu duniani? Tazama, mbingu na mbingu za mbingu za mbingu hazikutoshi; siuze nyumba hii niliyoijenga!
Esaïe 66.1 2 Chroniques 2.6 Psaumes 113.5-113.6 Psaumes 68.18 Psaumes 139.7-139.10
19 Walakini umwangalie mtumwa wako anayoyaomba, na kusihi, Ee Bwana, Mungu wangu, usikie kilio na maombi anayoyaomba mtumwa wako mbele zako;
Jean 17.20 Psaumes 4.1 Psaumes 74.20 Daniel 9.17-9.19 Psaumes 20.1-20.3
20 ili macho yako yafumbuke kwa nyumba hii mchana na usiku, mahali uliponena, ndipo utakapoliweka jina lako; usikie maombi atakayoomba mtumwa wako, akikabili mahali hapa.
Psaumes 34.15 Daniel 6.10 Colossiens 2.9 2 Chroniques 6.6 Deutéronome 12.11
21 Uyasikie atakayosihi mtumwa wako, na watu wako Israeli, watakapoomba wakikabili mahali hapa; naam, usikie toka makaoni mwako, toka mbinguni, nawe usikiapo, samehe.
Esaïe 43.25 Michée 7.18 Daniel 9.19 Job 22.12-22.14 Esaïe 44.22
22 Ikiwa mtu amemkosea mwenzake, akitiwa kiapo, aapishwe, naye akija na kuapa hapa mbele ya madhabahu yako nyumbani humu;
Exode 22.11 Matthieu 23.18 Proverbes 30.9 Nombres 5.19-5.22 1 Rois 8.31-8.32
23 basi, usikie mbinguni, ukatende, ukawahukumu watumwa wako; ukimlipiza mwovu, kumpatilizia njia yake kichwani; ukamfanyie haki mwenye haki, ukimjalia kwa kadiri ya haki yake.
Esaïe 3.10-3.11 Jérémie 51.56 Ezéchiel 18.20 Proverbes 17.15 Romains 2.9-2.10
24 Ikiwa watu wako Israeli wamepigwa mbele ya adui zao, kwa sababu wamekukosa wewe; kama wakirejea kwako, na kulikiri jina lako, wakikuomba na kukusihi nyumbani humu;
Lévitique 26.17 2 Rois 17.7-17.18 Deutéronome 30.1-30.6 Juges 2.11 Deutéronome 28.48
25 basi usikie huko mbinguni, ukaisamehe dhambi ya watu wako Israeli, na kuwarejeza tena katika nchi uliyowapa wao na baba zao.
Genèse 13.15 Esdras 1.1-1.6 Exode 6.8 Josué 21.43 Psaumes 106.40-106.47
26 Ikiwa mbingu zimefungwa, hata hakuna mvua, kwa sababu wamekukosa wewe; kama wakiomba wakikabili mahali hapa, na kulikiri jina lako, na kuiacha dhambi yao, uwatesapo;
Deutéronome 11.17 Lévitique 26.19 Joël 2.15-2.17 Ezéchiel 18.27-18.32 Osée 5.15-6.1
27 basi usikie huko mbinguni, ukaisamehe dhambi ya watumwa wako, na ya watu wako Israeli; uwafundishapo njia njema iwapasayo waiendee; ukainyeshee mvua nchi yako, uliyowapa watu wako iwe urithi.
Psaumes 94.12 Jacques 5.17-5.18 Jean 6.45 Psaumes 25.4-25.5 Job 37.11-37.14
28 Ikiwa nchi imeingia njaa, au tauni, au ukosefu wa mvua, au ukungu, au nzige, au panzi; ikiwa adui wamewahusuru katika nchi ya miji yao, au ukiwapo msiba wo wote, au uele wo wote;
Apocalypse 9.3-9.11 Exode 10.12-10.15 2 Chroniques 12.2-12.5 1 Rois 8.37-8.40 Joël 1.11
29 yo yote atakayoyaomba na kusihi mtu awaye yote, au watu wako Israeli wote pamoja, watakaojua kila mtu pigo lake mwenyewe, na msiba wake mwenyewe, akiinyoshea mikono nyumba hii;
Psaumes 50.15 Psaumes 32.2-32.6 Psaumes 91.15 Psaumes 33.12-33.13 Psaumes 142.1-142.2
30 basi usikie huko mbinguni, ukaapo, ukasamehe, ukampatilize kila mtu kwa kadiri ya njia zake zote; wewe umjuaye moyo; (maana wewe peke yako ndiwe uijuaye mioyo ya wanadamu);
1 Chroniques 28.9 1 Samuel 16.7 Apocalypse 2.23 1 Chroniques 29.17 Matthieu 16.27
31 ili wakuche wewe, waziendee njia zako, siku zote watakazoishi katika nchi uliyowapa baba zetu.
Psaumes 128.1 Job 28.28 1 Samuel 12.24 Exode 20.20 Psaumes 130.4
32 Hata na mgeni naye, asiyekuwa mmoja wa watu wako Israeli, atakapokuja kutoka nchi iliyo mbali sana kwa ajili ya jina lako kuu, na mkono wako ulio hodari, na mkono wako ulionyoshwa; hao watakapokuja na kuomba wakiielekea nyumba hii;
Esaïe 56.3-56.7 Exode 3.19-3.20 Jean 12.20 1 Rois 8.41-8.43 Exode 18.8-18.12
33 basi usikie huko mbinguni, toka makaoni mwako, ukatende yote atakayokuomba huyo mgeni; ili watu wote wa dunia wapate kulijua jina lako, na kukucha wewe, kama watu wako Israeli, tena wajue ya kuwa nyumba hii niliyoijenga imeitwa kwa jina lako.
2 Chroniques 7.14 Psaumes 46.10 Nombres 6.27 1 Samuel 17.46 Esaïe 11.10
34 Ikiwa watu wako wametoka kupigana na adui zao, utakakowatuma ko kote, wakikuomba kuuelekea mji huu uliouchagua, na nyumba hii niliyoijenga kwa jina lako;
2 Chroniques 18.31 2 Chroniques 20.6-20.13 Juges 1.1-1.2 1 Samuel 15.18 Josué 1.2-1.5
35 basi uyasikie huko mbinguni wayaombayo, na kusihi, ukaitetee haki yao.
Daniel 9.17-9.19 Psaumes 9.3-9.4 Esaïe 37.21-37.36 Jérémie 5.28
36 Wakikukosa, (maana hakuna mtu asiyekosa), hata uwakasirikie, na kuwatia mikononi mwa adui zao, wawahamishe, na kuwachukua mateka mpaka nchi iliyo mbali au iliyo karibu;
Jacques 3.2 1 Jean 1.8-1.10 Ecclésiaste 7.20 Job 15.14-15.16 Psaumes 143.2
37 basi wakikumbuka katika nchi walikohamishwa, na kutubu, na kukusihi katika nchi ya uhamisho wao, wakisema, Tumekosa, tumetenda kwa ukaidi, tumefanya maovu;
Néhémie 9.26-9.30 Lévitique 26.40-26.45 Psaumes 106.6 Deutéronome 4.29-4.30 Jérémie 31.18-31.20
38 wakurudiapo kwa mioyo yao yote, na kwa nia zao zote, katika nchi ya uhamisho wao, adui walikowahamisha, wakiomba na kuielekea nchi uliyowapa baba zao, na mji huu uliouchagua, na nyumba hii niliyoijenga kwa jina lako;
Osée 14.1-14.4 2 Chroniques 6.34 Daniel 6.10 Daniel 9.3-9.4 Deutéronome 30.2-30.6
39 basi uyasikie toka mbinguni, toka makaoni mwako, wayaombayo, na kusihi, ukaitetee haki yao; ukawasamehe watu wako, waliokosa juu yako.
Psaumes 25.18 Michée 7.18-7.20 Zacharie 1.15-1.16 2 Chroniques 6.35
40 Na sasa, Ee Mungu wangu, macho yako yafumbuke, nakusihi, masikio yako yakasikilize maombi yaombwayo mahali hapa.
2 Chroniques 7.15 Psaumes 17.1 Néhémie 1.6 Néhémie 1.11 Psaumes 31.2
41 Sasa, Ee Bwana, Mungu, uondoke, uende kwenye raha yako, wewe na sanduku la nguvu zako; makuhani wako, Ee Bwana, Mungu, wavikwe wokovu, watakatifu wako na washangilie mema.
1 Chroniques 28.2 Esaïe 61.10 Psaumes 132.16 Néhémie 9.25 Esaïe 61.6
42 Ee Bwana, Mungu, usiurudishe nyuma uso wa masihi wako,uzikumbuke fadhili za Daudi mtumishi wako.
Esaïe 55.3 Psaumes 132.1 1 Rois 1.34 Psaumes 89.28 1 Rois 2.16

Cette Bible est dans le domaine public.