Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Rois 20.7
Bible en Swahili de l’est


Attaques syriennes contre Samarie

1 Basi, Ben-hadadi mfalme wa Shamu akakusanya jeshi lake lote; nao walikuwapo wafalme thelathini na wawili pamoja naye, na farasi, na magari: akakwea akauhusuru Samaria, akaupiga vita.
1 Rois 15.18 1 Rois 15.20 1 Rois 22.31 Daniel 2.37 1 Rois 20.24
2 Akatuma wajumbe kwa Ahabu mfalme wa Israeli, mjini, akamwambia, Ndivyo asemavyo Ben-hadadi.
Esaïe 37.9-37.10 2 Rois 19.9 Esaïe 36.2-36.22
3 Fedha yako na dhahabu yako ni zangu mimi; na wakezo na wanao, walio wema, ni wangu.
Esaïe 10.13-10.14 Exode 15.9
4 Mfalme wa Israeli akajibu, akasema, Ni kama ulivyosema, bwana wangu, mfalme; mimi ni wako, na vyote nilivyo navyo.
Deutéronome 28.48 1 Samuel 13.6-13.7 Juges 15.11-15.13 Lévitique 26.36 2 Rois 18.14-18.16
5 Wajumbe wakarudi tena, wakasema, Ndivyo asemavyo Ben-hadadi, Hakika nimetuma kwako kusema, Fedha yako, na dhahabu yako, na wake zako, na wanao, utanitolea mimi;
6 lakini kesho kama wakati huu nitatuma kwako watumwa wangu, ili watazame-tazame nyumba yako na nyumba za watumwa wako; na itakuwa kila kipendezacho machoni pako watakitia mikononi mwao,na kukichukua.
Genèse 27.15 Lamentations 1.7 Esdras 8.27 2 Rois 18.31-18.32 Esaïe 44.9
7 Ndipo mfalme wa Israeli, akawaita wazee wote wa nchi, akasema, Angalieni, nawaomba, mwone, kwamba huyu ataka madhara; maana ametuma kwangu kutaka wake zangu na watoto wangu; na fedha yangu na dhahabu yangu, sikumkatalia.
2 Rois 5.7 Daniel 11.27 Psaumes 62.3 Proverbes 11.27 1 Chroniques 13.1
8 Wakamwambia wazee wote na watu wote, Usisikie, wala usikubali.
9 Kwa hiyo akawaambia wale wajumbe wa Ben-hadadi, Mwambieni bwana wangu mfalme, Kila uliyotuma kumtakia mtumwa wako kwanza, nitafanya, ila neno hili siwezi kulifanya. Basi wajumbe wakaenda zao, wakamrudishia maneno hayo.
10 Ndipo Ben-hadadi akatuma kwake, akasema, Miungu wanifanyie hivi na kuzidi, yakiwa mavumbi ya Samaria yatatosha makonzi ya watu wote walio miguuni pangu.
1 Rois 19.2 Exode 11.8 2 Rois 19.23-19.24 Actes 23.12 Juges 4.10
11 Mfalme wa Israeli akajibu, akasema, Mwambieni, Avaaye asijisifu kama avuaye.
Proverbes 27.1 Esaïe 10.15-10.16 Matthieu 26.33-26.35 1 Samuel 14.6 Ecclésiaste 9.11
12 Ikawa, Ben-hadadi alipolisikia neno hilo, naye alikuwa akinywa, yeye na wafalme, mabandani, aliwaambia watumwa wake, Jipangeni. Wakajipanga juu ya mji.
1 Rois 16.9 1 Rois 20.16 Proverbes 31.4-31.5 1 Samuel 25.36 Luc 21.34
13 Na tazama, nabii akamjia Ahabu mfalme wa Israeli, akasema, Bwana asema hivi, Je! Umeona makutano haya yote walio wengi? Angalia, nitawatia leo mkononi mwako; nawe utajua ya kuwa ndimi Bwana.
1 Rois 20.28 Esaïe 7.1-7.9 Esaïe 37.20 Joël 3.17 Ezéchiel 20.14
14 Ahabu akanena, Kwa nani? Akasema, Bwana asema hivi, Kwa vijana wa maliwali wa majimbo. Ndipo akanena, Ni nani atakayepanga vita? Naye akajibu, Ni wewe.
Genèse 14.14-14.16 1 Rois 18.44 1 Samuel 17.50 Juges 7.16-7.20 1 Corinthiens 1.27-1.29
15 Ndipo akawaandika vijana wa maliwali wa majimbo, nao walikuwa mia mbili thelathini na wawili; kisha baada ya hao akawaandika watu wote, wana wa Israeli wote, nao walikuwa elfu saba.
1 Samuel 14.6 Juges 7.16 Juges 7.7 1 Rois 19.18 2 Rois 13.7
16 Wakatoka wakati wa adhuhuri. Lakini Ben-hadadi alikuwa akinywa hata kulewa mabandani, yeye na wale wafalme thelathini na wawili waliomsaidia.
Ecclésiaste 10.16-10.17 Proverbes 23.29-23.32 1 Rois 16.9 Esaïe 54.15 Osée 4.11
17 Wakatoka wale vijana wa maliwali wa majimbo wakitangulia; na Ben-hadadi akatuma watu, nao wakamwambia, Wako watu wametoka katika Samaria.
1 Rois 20.14-20.15 1 Rois 20.19
18 Akasema, Kwamba wametoka kwa amani, wakamateni wa hai; au kwamba wametoka kwa vita, wakamateni wa hai.
2 Rois 14.8-14.12 Proverbes 18.12 1 Samuel 2.3-2.4 1 Samuel 17.44 1 Samuel 14.11-14.12
19 Basi wakatoka mjini hao vijana wa maliwali wa majimbo, na jeshi nyuma yao.
20 Wakapiga kila mmoja mtu wake; Washami wakakimbia, na Israeli wakawafuatia; Ben-hadadi mfalme wa Shamu akaokoka amepanda farasi, pamoja na wapandao farasi.
2 Rois 7.6-7.7 Ecclésiaste 9.11 Lévitique 26.8 Psaumes 46.6 2 Rois 19.36
21 Mfalme wa Israeli akatoka, akawapiga farasi na magari, akawapiga Washami pigo kubwa.
1 Samuel 14.20-14.22 2 Rois 3.24 1 Samuel 17.52 Juges 3.28 Juges 7.23-7.25
22 Naye yule nabii akamjia mfalme wa Israeli, akamwambia, Enenda, kusanya nguvu zako, ujue, na kuangalia ufanyavyo; kwa maana mwakani mfalme wa Shamu atakuja juu yako.
1 Rois 20.13 2 Samuel 11.1 1 Rois 20.26 1 Chroniques 20.1 2 Chroniques 25.8
23 Basi watumwa wake mfalme wa Shamu wakamwambia, Mungu wao ni mungu wa milima; ndiyo sababu ya kutushinda sisi; lakini na tupigane nao katika nchi tambarare, na hakika tutawashinda wao.
1 Rois 14.23 Romains 1.21-1.23 2 Rois 19.12 Psaumes 50.21-50.22 Psaumes 121.1-121.2
24 Ufanye neno hili; uwaondoe hao wafalme, kila mtu atoke mahali pake, ukaweke majemadari mahali pao.
1 Rois 22.31 Proverbes 21.30 1 Rois 20.1 1 Rois 20.16
25 Kisha ujihesabie jeshi, kama jeshi lililokupotea, farasi kwa farasi na gari kwa gari; nasi tutapigana nao katika nchi tambarare, na bila shaka tutawashinda. Akaisikiliza sauti yao, akafanya kama hivyo.
Psaumes 10.3
26 Basi ikawa mwakani, Ben-hadadi akawahesabu Washami, akakwea mpaka Afeki ili apigane na Israeli.
2 Rois 13.17 1 Rois 20.22 1 Rois 20.30 Josué 19.30 1 Samuel 29.1
27 Wana wa Israeli nao wakahesabiwa, wakapewa vyakula, wakaenda kupigana nao; wakatua wana wa Israeli mbele yao kama vikundi viwili vya wana-mbuzi; bali Washami wakaijaza nchi.
1 Samuel 13.5-13.8 Juges 6.5 Deutéronome 32.30 1 Samuel 14.2 Juges 7.8
28 Akaja yule mtu wa Mungu, akamwambia mfalme wa Israeli, akasema, Bwana asema hivi, Kwa sababu Washami wamesema, Bwana ni Mungu wa milima wala si Mungu wa nchi tambarare; basi nitawatia makutano haya yote walio wengi mkononi mwako, nanyi mtajua ya kuwa ndimi Bwana.
1 Rois 20.13 1 Rois 17.18 1 Rois 13.1 Deutéronome 32.27 1 Rois 20.22-20.23
29 Wakatua kuelekeana muda wa siku saba. Ikawa siku ya saba vikapangwa vita; wana wa Israeli wakawapiga miongoni mwa Washami siku moja watu mia elfu waendao kwa miguu.
Josué 6.15 2 Samuel 10.18 1 Samuel 17.16 Esaïe 37.36 2 Chroniques 28.6
30 Lakini waliosalia wakakimbia mpaka Afeki, mjini; na ukuta ukaanguka juu ya watu ishirini na saba elfu waliosalia. Ben-hadadi naye akakimbia, akaingia mjini, katika chumba cha ndani.
1 Rois 22.25 2 Chroniques 18.24 1 Rois 20.26 Psaumes 18.25 Amos 5.19
31 Watumwa wake wakamwambia, Angalia sasa, tumesikia ya kuwa wafalme wa nyumba ya Israeli ni wafalme wenye rehema; tafadhali, tuvae magunia viunoni, na kamba vichwani, tumtokee mfalme wa Israeli; labda atakuokoa roho yako.
Genèse 37.34 2 Samuel 3.31 1 Rois 20.23 Jonas 3.5-3.6 Esther 4.1-4.3
32 Basi wakajifungia magunia viunoni, na kamba vichwani, wakamjia mfalme wa Israeli, wakasema, Mtumwa wako Ben-hadadi asema Roho yangu, nakusihi, iishi. Akasema, Je! Yu hai bado? Ni ndugu yangu yeye.
1 Rois 20.3-20.6 Job 40.11-40.12 1 Rois 20.31 Abdias 1.3-1.4 1 Rois 20.42
33 Wale watu wakaangalia sana, wakafanya haraka kulishika neno hilo kama ni nia yake, wakasema, Ndugu yako, Ben-hadadi. Akasema, Haya! Nendeni mkamlete. Ndipo Ben-hadadi akamtokea, naye akampandisha garini.
2 Rois 10.15 Proverbes 25.13 Luc 16.8 Actes 8.31
34 Na Ben-hadadi akamwambia, Miji ile baba yangu aliyomnyang’anya baba yako nitairudisha; nawe utajifanyia njia huko Dameski, kama baba yangu aliyoifanya huko Samaria. Ahabu akasema, Nami nitakuacha kwa mapatano haya. Akafanya mapatano naye, akamwacha.
1 Rois 15.20 1 Rois 22.31 2 Chroniques 18.30 2 Chroniques 16.4 1 Rois 20.42
35 Basi, mtu mmoja wa wana wa manabii akamwambia mwenzake kwa neno la Bwana, Nipige, nakusihi. Akakataa yule kumpiga.
2 Rois 2.15 1 Rois 13.17-13.18 Jérémie 27.2-27.3 Ezéchiel 4.3 1 Rois 20.37-20.38
36 Akamwambia, Kwa sababu hukuisikiliza sauti ya Bwana, angalia, mara ukitoka kwangu simba atakuua. Na mara alipotoka kwake, simba alimwona, akamwua.
1 Rois 13.26 1 Rois 13.21-13.24 1 Samuel 15.22-15.23
37 Ndipo akaona mtu mwingine, akasema, Nipige, nakusihi. Yule mtu akampiga, hata kumpiga na kumtia jeraha.
Exode 21.12 1 Rois 20.35
38 Basi yule nabii akaenda akamngoja mfalme njiani, amejibadilisha kwa kilemba juu ya macho yake.
1 Rois 14.2 1 Rois 22.30 2 Samuel 14.2 Matthieu 6.16
39 Ikawa mfalme alipopita, alimwita mfalme; akasema, Mtumwa wako aliingia katikati ya pigano; na tazama, mtu mmoja akanigeukia akaniletea mtu, akaniambia, Umlinde mtu huyu; akipotea kwa njia yo yote, roho yako itakuwa mahali pa roho yake, au utatoa talanta ya fedha.
2 Rois 10.24 1 Rois 20.42 Proverbes 13.8 Psaumes 49.7 Exode 21.30
40 Ikawa mtumishi wako alipokuwa akitenda haya na haya, yule akaenda zake. Mfalme wa Israeli akamwambia, Ndivyo itakavyokuwa hukumu yako; umejihukumu mwenyewe.
2 Samuel 12.5-12.7 Job 15.6 Matthieu 25.24-25.27 Luc 19.22 Matthieu 21.41-21.43
41 Akafanya haraka akakiondoa kilemba machoni mwake, mfalme wa Israeli akamtambua kuwa ni mmoja wao manabii.
Job 2.8 1 Rois 20.38 Jérémie 6.26 2 Samuel 13.19
42 Akamwambia, Bwana asema hivi, Kwa sababu umemwachilia atoke mkononi mwako mtu niliyemweka ili aangamizwe kabisa, roho yako itakuwa mahali pa roho yake, na watu wako mahali pa watu wake.
1 Rois 22.31-22.37 1 Rois 20.39 1 Rois 20.34 2 Rois 8.12 2 Rois 6.24
43 Mfalme wa Israeli akaenda nyumbani kwake na moyo mzito, mwenye hasira, akaja Samaria.
1 Rois 21.4 Esther 6.12-6.13 Esther 5.13 1 Rois 22.8 Proverbes 19.3

Cette Bible est dans le domaine public.