Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Samuel 20.11
Bible en Swahili de l’est


1 Basi ilitukia ya kwamba kulikuwapo mtu asiyefaa, jina lake akiitwa Sheba, mwana wa Bikri, Mbenyamini; naye akapiga tarumbeta, akasema, Sisi hatuna sehemu katika Daudi, wala hatuna urithi katika mwana wa Yese; nendeni kila mtu hemani kwake, enyi Israeli.
1 Rois 12.16 Deutéronome 13.13 2 Chroniques 10.16 Juges 19.22 Proverbes 25.8
2 Basi wakapanda watu wote wa Israeli kutoka kumfuata Daudi, wakamfuata Sheba, mwana wa Bikri; lakini watu wa Yuda wakaambatana na mfalme wao, toka Yordani hata kufika Yerusalemu.
2 Samuel 19.40-19.41 Psaumes 62.9 2 Chroniques 10.17 Actes 11.23 Psaumes 118.8-118.10
3 Basi Daudi akaja Yerusalemu nyumbani kwake; kisha mfalme akawatwaa wale wanawake kumi, masuria, aliowaacha kuitunza nyumba, akawatia nyumbani mwa kulindwa, akawalisha, ila asiingie kwao. Basi wakafungwa hata siku ya kufa kwao, huku wakiishi hali ya ujane.
2 Samuel 16.21-16.22 2 Samuel 15.16 Genèse 40.3
4 Ndipo mfalme akamwambia Amasa, Uwakusanye pamoja kwangu kwa siku tatu watu wa Yuda, na uwepo wewe hapa.
2 Samuel 17.25 2 Samuel 19.13 1 Chroniques 2.17
5 Amasa akaenda kuwakusanya Yuda; lakini akakawia zaidi ya huo muda aliowekewa.
1 Samuel 13.8 2 Samuel 19.13
6 Basi Daudi akamwambia Abishai, Sasa Sheba, mwana wa Bikri, atatudhuru, kuliko Absalomu; twaa wewe watumishi wa bwana wako, ukamfuatie, asiingie katika miji yenye boma, na kujiponya machoni petu.
2 Samuel 21.17 2 Samuel 11.11 1 Rois 1.33 2 Samuel 23.18 1 Samuel 26.6
7 Ndipo wakatoka nyuma yake watu wa Yoabu, na Wakerethi na Wapelethi, na mashujaa wote; wakatoka Yerusalemu, ili kumfuatia Sheba, mwana wa Bikri.
2 Samuel 8.18 1 Rois 1.38 2 Samuel 15.18 2 Samuel 20.23 2 Samuel 8.16
8 Basi walipokuwako kwenye lile jiwe kubwa lililoko Gibeoni, Amasa akaja kuwalaki. Naye Yoabu alikuwa amefungwa mavazi yake ya vita aliyoyavaa, na juu yake alikuwa na mshipi, na upanga uliotiwa viunoni mwake ndani ya ala yake; naye alipokuwa akiendelea, ukaanguka.
2 Samuel 3.30 2 Samuel 2.13 2 Samuel 20.4-20.5
9 Naye Yoabu akamwambia Amasa, Amani kwako, ndugu yangu. Kisha Yoabu akamshika Amasa ndevu kwa mkono wake wa kuume ili ambusu.
Proverbes 26.24-26.26 Matthieu 26.48-26.49 Michée 7.2 Luc 22.47-22.48 Psaumes 55.21
10 Wala Amasa hakuangalia huo upanga uliomo mkononi mwa Yoabu; basi akampiga nao wa tumbo, akamwaga matumbo yake chini, asimpige mara ya pili; naye akafa. Kisha Yoabu na Abishai, nduguye, wakamfuata Sheba, mwana wa Bikri.
2 Samuel 2.23 2 Samuel 3.27 Juges 3.21 2 Samuel 20.9 1 Rois 2.31-2.34
11 Akasimama karibu naye mmojawapo wa vijana wa Yoabu, huyo akasema, Ampendaye Yoabu, na aliye wa Daudi, na amfuate Yoabu.
2 Samuel 20.13 2 Samuel 20.4 2 Samuel 20.6-20.7 2 Rois 9.32 2 Samuel 20.21
12 Lakini Amasa alikuwa anagaagaa katika damu yake katikati ya njia kuu. Basi yule mtu alipowaona watu wote wamesimama, akamwondoa Amasa toka njia kuu akamtia kondeni, akamfunika nguo, hapo alipoona ya kuwa kila mtu aliyefika kwake amesimama.
2 Samuel 17.25 Psaumes 55.23 Proverbes 24.21-24.22 Psaumes 9.16
13 Na alipoondolewa katika njia kuu, watu wote wakapita, wakamwandama Yoabu ili kumfuatia Sheba, mwana wa Bikri.
Esaïe 7.3 1 Samuel 6.12 Esaïe 62.10 Juges 21.19 Marc 10.46
14 Naye akapita kati ya kabila zote za Israeli mpaka Abeli, na kwa Bethmaaka na Wabikri wote; nao wakakusanyika, wakaenda pia kumwandama.
2 Rois 15.29 Nombres 21.16 Josué 18.25 2 Chroniques 16.4 1 Rois 15.20
15 Na hao wakaja wakamhusuru katika Abeli wa Bethmaaka, wakafanya chuguu mbele ya mji, nayo ikasimama kuielekea ngome; na watu wote waliokuwa pamoja na Yoabu wakavunja-vunja ukuta, wapate kuubomoa.
2 Rois 19.32 Jérémie 32.24 2 Rois 15.29 1 Rois 15.20 Jérémie 33.4
16 Ndipo akalia mwanamke mmoja mwenye akili toka mjini, Sikieni, sikieni; mwambieni na Yoabu, aje hapa karibu, niseme naye.
2 Samuel 14.2 1 Samuel 25.32-25.33 Ecclésiaste 9.14-9.18 1 Samuel 25.3
17 Basi akamkaribia; na yule mwanamke akasema, Ndiwe Yoabu? Akajibu, Ndimi. Ndipo akamwambia Sikia maneno ya mjakazi wako. Akajibu, Mimi nasikia.
2 Samuel 14.12 1 Samuel 25.24
18 Kisha akanena, akisema, Watu hunena zamani za kale, wakisema, Wasikose kuuliza huko Abeli; ndivyo walivyomaliza shauri.
Deutéronome 20.10-20.11
19 Mimi ni wa hao wenye amani, walio waaminifu katika Israeli; wewe unatafuta kuuharibu mji, na mama wa Israeli; mbona wataka kuumeza urithi wa Bwana?
1 Samuel 26.19 2 Samuel 21.3 2 Samuel 17.16 Nombres 26.10 Genèse 18.23
20 Yoabu akajibu, akasema, Isiwe, isiwe kwangu, niumeze wala kuuharibu.
Jérémie 17.9 2 Samuel 23.17 Job 22.18 2 Samuel 20.10 Proverbes 28.13
21 Neno hili silo hivyo; lakini mtu mmoja wa milima ya Efraimu, Sheba, mwana wa Bikri, jina lake, ameinua mkono wake juu ya mfalme, naam, Daudi, basi mtoeni yeye tu, nami nitaondoka katika mji huu. Basi yule mwanamke akamwambia Yoabu, Tazama, kichwa chake utatupiwa juu ya ukuta.
2 Rois 10.7 2 Samuel 20.1 Juges 18.4-18.8 2 Samuel 17.2-17.3 1 Samuel 26.9
22 Ndipo yule mwanamke akawaendea watu wote katika akili zake. Nao wakamkata kichwa Sheba, mwana wa Bikri, wakamtupia Yoabu huko nje. Ndipo akapiga tarumbeta, nao wakatawanyika kutoka mjini kila mtu hemani kwake. Naye Yoabu akarudi mpaka Yerusalemu kwa mfalme.
Ecclésiaste 7.19 2 Samuel 20.1 Ecclésiaste 9.13-9.18 2 Samuel 18.16 2 Samuel 20.16
23 Basi Yoabu alikuwa juu ya jeshi lote la Israeli; na Benaya, mwana wa Yehoyada, alikuwa juu ya Wakerethi, na juu ya Wapelethi;
2 Samuel 8.16-8.18 1 Rois 4.3-4.6 1 Chroniques 18.15-18.17
24 na Adoramu alikuwa juu ya shokoa; na Yehoshafati, mwana wa Ahiludi, alikuwa mkumbushi;
1 Rois 4.3 1 Rois 12.18 1 Rois 4.6
25 na Shausha mwandishi; na Sadoki na Abiathari walikuwa makuhani.
2 Samuel 8.17 1 Rois 4.4 1 Chroniques 18.16
26 Tena na Ira, Myairi, alikuwa kuhani kwa Daudi.
2 Samuel 23.38 Exode 2.14 Juges 10.4-10.5 2 Samuel 8.18 Exode 24.11

Cette Bible est dans le domaine public.