Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Samuel 19.34
Bible en Swahili de l’est


1 Kisha Yoabu akaambiwa, Angalia, mfalme anamlilia Absalomu na kumwombolezea.
2 Samuel 18.14 2 Samuel 18.5 Proverbes 17.25 2 Samuel 18.12 2 Samuel 18.20
2 Na kushinda kwao vitani siku ile kukageuzwa kuwa maombolezo kwa watu wote; maana watu walisikia siku ile ya kwamba, Mfalme anahuzunika kwa ajili ya mwanawe.
Proverbes 16.15 Proverbes 19.12
3 Watu wakajificha siku ile, wakaingia mjini kama vile watu waonao fedheha wajifichavyo, hapo wakimbiapo vitani.
2 Samuel 19.32 Genèse 31.27 2 Samuel 17.24
4 Mfalme akajifunika uso; na mfalme akalia kwa sauti kuu, Mwanangu Absalomu, Absalomu, mwanangu, mwanangu!
2 Samuel 15.30 2 Samuel 18.33
5 Basi Yoabu akaingia nyumbani kwa mfalme, akasema, Wewe leo umefedhehesha nyuso za watumishi wako wote, waliokuokoa leo roho yako, na roho za wanao, na za binti zako, na roho za wakezo, na roho za masuria wako;
Psaumes 18.47-18.48 Néhémie 9.27 Psaumes 3.8
6 kwa kuwa unawapenda wakuchukiao, na unawachukia wakupendao. Maana umetangaza leo ya kuwa wakuu na watumishi wako si kitu kwako; maana leo nimetambua hivi; kama Absalomu angaliishi, na sisi sote tungalikufa leo, ingalikuwa vyema machoni pako.
2 Samuel 3.24-3.25 Job 34.18 Actes 23.5 Proverbes 19.9-19.10
7 Basi sasa, ondoka, utoke nje, ukaseme na watumishi wako maneno ya kuwatuliza roho zao; maana mimi nakuapia kwa Bwana, usipotoka, hatabaki hata mtu mmoja pamoja nawe usiku huu; na mambo haya yatakuwa mabaya kwako kuliko mabaya yote yaliyokupata tokea ujana wako hata sasa.
Proverbes 14.28 Genèse 34.3 Osée 2.14 Esaïe 40.1 Psaumes 71.18-71.20
8 Ndipo mfalme akaondoka, akaketi langoni. Nao wote wakaambiwa ya kwamba, Angalieni, mfalme ameketi langoni; watu wote wakaenda huko mbele ya mfalme. Basi, Israeli wote walikuwa wamekimbia kila mtu hemani kwake.
2 Samuel 18.24 2 Samuel 18.4 2 Rois 14.12 2 Samuel 18.6-18.8 2 Samuel 18.17
9 Wakashindana watu wote katika kabila zote za Israeli, wakisema, Mfalme alitutoa mikononi mwa adui zetu, akatuokoa mikononi mwa Wafilisti; naye sasa amekimbia kutoka nchi hii mbele ya Absalomu.
2 Samuel 15.14 2 Samuel 8.1-8.14 1 Samuel 18.25 1 Samuel 19.5 Genèse 3.12-3.13

Retour de David sur le trône

10 Na huyo Absalomu, tuliyemtia mafuta ili awe juu yetu, amekufa vitani. Basi sasa mbona ninyi hamsemi neno lo lote juu ya kumrudisha tena mfalme?
2 Samuel 15.12-15.13 2 Samuel 18.14 Juges 18.9 Osée 8.4
11 Naye mfalme Daudi akatuma kwa Sadoki na Abiathari, makuhani, kusema, Neneni na wazee wa Yuda, mkisema, Kwa nini ninyi mmekuwa wa mwisho wa kumrudisha tena mfalme nyumbani kwake? Kwa maana maneno ya Israeli wote yamemjia mfalme, ili kumleta nyumbani kwake.
2 Samuel 15.29 2 Thessaloniciens 3.9 2 Corinthiens 5.20 2 Samuel 15.35-15.36 Matthieu 5.16
12 Ninyi ni ndugu zangu, ninyi ni mfupa wangu na nyama yangu; mbona basi ninyi mmekuwa wa mwisho wa kumrudisha tena mfalme.
2 Samuel 5.1 Ephésiens 5.30 Genèse 2.23 Juges 9.2
13 Kisha mkamwambie Amasa, Je! Si wewe uliye mfupa wangu, na nyama yangu? Mungu anifanyie hivyo, na kuzidi, usipokuwa wewe jemadari wa jeshi mbele yangu daima mahali pa Yoabu.
2 Samuel 17.25 2 Samuel 8.16 1 Rois 19.2 Ruth 1.17 2 Samuel 19.5-19.7
14 Akawainamisha mioyo watu wote wa Yuda, kama mtu mmoja; basi wakatuma kwa mfalme, Rudi wewe na watumishi wako wote.
Juges 20.1 Actes 4.32 Psaumes 110.2-110.3
15 Hivyo mfalme akarudi, akafika Yordani. Kisha Yuda wakaja Gilgali kwenda kumlaki mfalme, na kumvusha mfalme Yordani.
Josué 5.9 1 Samuel 11.14-11.15
16 Akafanya haraka Shimei, mwana wa Gera, Mbenyamini, wa Bahurimu akashuka pamoja na watu wa Yuda ili kumlaki mfalme Daudi.
1 Rois 2.8 2 Samuel 16.5-16.13 Job 2.4 Proverbes 6.4-6.5 1 Rois 2.36-2.46
17 Na Watu elfu wa Benyamini walikuwa pamoja naye, na huyo Siba mtumwa, nyumba ya Sauli, na hao wanawe kumi na watano, na watumwa wake ishirini pamoja naye; wakavuka Yordani mbele ya mfalme.
2 Samuel 9.2 2 Samuel 16.1-16.4 2 Samuel 9.10 2 Samuel 19.26-19.27
18 Tena ikavuka mashua ili kuwavusha jamaa ya mfalme, na kufanya aliyoyaona kuwa mema. Ndipo Shimei, mwana wa Gera, akamwangukia mfalme alipokuwa amevuka Yordani.
Psaumes 81.15 Apocalypse 3.9 Psaumes 66.3
19 Akamwambia mfalme, Bwana wangu asinihesabie uovu, wala usiyakumbuke yale niliyoyatenda mimi mtumwa wako kwa upotoe siku ile alipotoka Yerusalemu bwana wangu mfalme, hata mfalme ayatie moyoni mwake.
1 Samuel 22.15 1 Samuel 25.25 2 Corinthiens 5.19 2 Samuel 13.33 1 Samuel 26.21
20 Kwa kuwa mimi mtumwa wako najua ya kwamba nimekosa; kwa hiyo, tazama, nimekuja leo, wa kwanza wa nyumba yote ya Yusufu, kushuka ili nimlaki bwana wangu mfalme.
2 Samuel 19.9 Genèse 48.20 2 Samuel 16.5 Psaumes 78.34-78.37 1 Rois 12.20
21 Lakini Abishai, mwana wa Seruya, akajibu na kusema, Je! Shimei hatauawa kwa sababu hii, kwa kuwa amemlaani masihi wa BWANA?
Exode 22.28 1 Samuel 26.9 1 Samuel 24.6 2 Samuel 16.13 1 Rois 21.10-21.11
22 Lakini Daudi akasema, Mimi nina nini nanyi, enyi wana wa Seruya, hata mmekuwa adui zangu leo? Je! Atauawa mtu ye yote leo katika Israeli? Kwa maana sijui mimi leo ya kwamba ndimi mfalme juu ya Israeli?
1 Samuel 11.13 2 Samuel 16.10 2 Samuel 3.39 Luc 9.54-9.56 Esaïe 16.5
23 Kisha mfalme akamwambia Shimei, Hutakufa. Mfalme akamwapia.
1 Rois 2.37 1 Rois 2.46 1 Rois 2.8-2.9 Hébreux 6.16 1 Samuel 28.10
24 Kisha Mefiboshethi, mwana wa Sauli, akashuka ili amlaki mfalme; alikuwa hakukata kucha za miguu yake wala kukata ndevu zake, wala kufua nguo zake, tangu siku alipoondoka mfalme, hata siku hiyo aliporudi kwake kwa amani.
Matthieu 6.16 2 Samuel 16.3 Romains 12.15 2 Samuel 15.30 2 Samuel 9.6-9.10
25 Basi ikawa, alipofika Yerusalemu kumlaki mfalme, mfalme akamwambia, Mbona hukwenda pamoja nami, Mefiboshethi?
2 Samuel 16.17
26 Naye akajibu, Bwana wangu, Ee mfalme, mtumwa wangu alinidanganya; kwa kuwa mimi mtumwa wako nilisema, Nitajitandikia punda, nipate kumpanda, na kwenda pamoja na mfalme; kwa sababu mimi mtumwa wako ni kiwete.
2 Samuel 4.4 2 Samuel 9.3 2 Samuel 16.2-16.3
27 Naye amenisingizia mimi mtumwa wako kwa bwana wangu mfalme; lakini bwana wangu mfalme ni kama malaika wa Mungu; utende basi yaliyo mema machoni pako.
2 Samuel 14.20 2 Samuel 14.17 2 Samuel 16.3 1 Samuel 29.9 Psaumes 15.3
28 Kwa kuwa jamaa yote ya baba yangu walikuwa kama watu wa kufa tu mbele ya bwana wangu mfalme; ila uliniweka mimi mtumwa wako kati ya hao walao mezani pako. Basi ni haki gani sasa niliyo nayo, hata nimlilie mfalme zaidi?
2 Samuel 9.13 2 Samuel 9.10 2 Rois 8.3 1 Samuel 26.16 2 Samuel 9.7-9.8
29 Basi mfalme akamwambia, Kwa nini unazidi kuyanena mambo yako? Mimi naamua, Wewe na Siba mwigawanye hiyo nchi.
Job 19.16-19.17 Actes 18.15 Psaumes 101.5 Proverbes 18.13 Deutéronome 19.17-19.19
30 Naye Mefiboshethi akamwambia mfalme, Naam, hata yote na atwae yeye, kwa kuwa bwana wangu mfalme amekuja kwa amani nyumbani kwake.
Actes 20.24 Philippiens 1.20 2 Samuel 1.26
31 Tena Barzilai, Mgileadi, akashuka kutoka Rogelimu; akavuka Yordani pamoja na mfalme, amvushe Yordani.
1 Rois 2.7 Néhémie 7.63 2 Samuel 17.27-17.29 Esdras 2.61
32 Naye huyo Barzilai alikuwa mzee sana, amepata umri wa miaka themanini; naye amemlisha mfalme hapo alipokuwapo Mahanaimu; kwa kuwa alikuwa mtu mwenye cheo kikubwa.
1 Samuel 25.2 Proverbes 16.31 2 Samuel 17.27-17.29 Genèse 50.26 Job 1.3
33 Naye mfalme akamwambia Barzilai, Uvuke pamoja nami; nami nitakulisha kwangu huko Yerusalemu.
Luc 22.28-22.30 Matthieu 25.34-25.40 2 Thessaloniciens 1.7 2 Samuel 9.11
34 Lakini Barzilai akamjibu mfalme, Siku ni ngapi za miaka ya maisha yangu, hata mimi nipande pamoja na mfalme kwenda Yerusalemu?
1 Corinthiens 7.29 Job 14.14 Jacques 4.14 Genèse 47.8-47.9 Psaumes 39.5-39.6
35 Nimepata leo miaka themanini; nami je! Naweza kupambanua mema na mabaya? Mimi mtumwa wako, je! Naweza kuonja nilacho au ninywacho? Naweza kusikia tena sauti ya waimbaji waume na wake? Kwa nini basi mtumwa wako amlemee bado bwana wangu mfalme?
2 Samuel 15.33 Psaumes 90.10 Esdras 2.65 Job 6.30 Exode 2.8
36 Mtumwa wako ataka kuvuka Yordani tu pamoja na mfalme; tena mbona mfalme anilipie thawabu ya namna hii?
Luc 6.38
37 Niache nirudi basi, mimi mtumwa wako, ili nife katika mji wangu mwenyewe, karibu na kaburi la baba yangu na la mama yangu. Lakini tazama, mtumwa wako Kimhamu; na avuke yeye pamoja na bwana wangu mfalme; nawe ukamtendee yeye yaliyo mema machoni pako.
Jérémie 41.17 1 Rois 2.7 2 Samuel 19.40 Genèse 50.13 Genèse 48.21
38 Mfalme akajibu, Haya, Kimhamu na avuke pamoja nami, nami nitamtendea yaliyo mema machoni pako wewe; na kila utakalotaka kwangu, mimi nitalifanya kwa ajili yako.
39 Basi watu wote wakavuka Yordani, naye mfalme akavuka; kisha mfalme akambusu Barzilai, akambariki; naye akarejea mahali pake.
Genèse 31.55 Genèse 47.7 Ruth 1.14 Genèse 14.19 2 Samuel 6.20
40 Hivyo mfalme akavuka, akafika Gilgali; Kimhamu akavuka pamoja naye; na watu wote wa Yuda wakamvusha mfalme, na nusu ya watu wa Israeli.
2 Samuel 19.11-19.15 Genèse 49.10 Matthieu 21.9

Tensions entre Judéens et Israélites

41 Tena, angalia, watu wote wa Israeli wakamjia mfalme wakamwambia mfalme, Kwa nini ndugu zetu, watu wa Yuda wamekuiba, na kumvusha Yordani mfalme, na jamaa yake, na watu wote wa Daudi pamoja naye?
Juges 12.1 Juges 8.1 Jean 7.5-7.6 2 Samuel 19.3 Genèse 31.26-31.27
42 Ndipo watu wote wa Yuda wakawajibu hao watu wa Israeli, Ni kwa sababu mfalme ndiye wa jamaa yetu; mbona basi ninyi mmekasirika kwa ajili ya jambo hili? Je! Sisi tumekula kitu cha mfalme? Ama ametupa sisi zawadi yo yote?
2 Samuel 19.12 2 Samuel 5.1 1 Chroniques 2.3-2.17
43 Hao watu wa Israeli wakawajibu watu wa Yuda, wakasema, Sisi tunazo sehemu kumi katika mfalme, tena tunayo haki yetu katika Daudi zaidi kuliko ninyi; mbona basi ninyi mmetudharau sisi, lisitakwe kwanza shauri letu katika kumrudisha tena mfalme wetu? Na maneno ya watu wa Yuda yakawa makali kuliko maneno ya watu wa Israeli.
Galates 5.20 2 Samuel 5.1 1 Rois 11.30-11.31 Jacques 3.14-3.16 Galates 5.26

Cette Bible est dans le domaine public.