Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Juges 5.27
Bible en Swahili de l’est


Cantique de Débora

1 Ndipo Debora, na Baraka mwana wa Abinoamu, wakaimba siku ile, wakisema;
Exode 15.1 Esaïe 25.1 Esaïe 12.1-12.6 1 Samuel 2.1 Job 38.7
2 Kwa sababu wakuu walitangulia katika Israeli, Kwa sababu watu walijitoa nafsi zao kwa hiari yao, Mhimidini Bwana.
Juges 5.9 2 Chroniques 17.16 Psaumes 110.3 Philémon 1.14 Psaumes 136.15
3 Sikieni, enyi wafalme; tegeni masikio, enyi wakuu; Mimi, naam mimi, nitamwimbia Bwana; Nitamhimidi Bwana, Mungu wa Israeli.
Psaumes 49.1-49.2 Psaumes 138.4-138.5 Esdras 7.21 Psaumes 119.46 Psaumes 2.10-2.12
4 Bwana, ulipotoka katika Seiri, Ulipokwenda vitani kutoka mashamba ya Edomu, Nchi ilitetema, mbingu nazo zikadondoza maji, Naam, mawingu yakadondoza maji.
Deutéronome 33.2 Psaumes 68.7-68.8 2 Samuel 22.8 Psaumes 77.17 Psaumes 18.7-18.15
5 Milima ikayeyuka mbele za uso wa Bwana, Naam hata Sinai ule mbele za uso wa Bwana, Mungu wa Israeli.
Exode 19.18 Psaumes 97.5 Nahum 1.5 Habakuk 3.10 Esaïe 64.1-64.3
6 Katika siku za Shamgari, mwana wa Anathi, Siku za Yaeli, njia kuu zilikuwa hazina watu; Nao wenye kusafiri walipita kwa njia za kando.
Juges 3.31 Esaïe 33.8 Lévitique 26.22 Lamentations 1.4 Michée 3.12
7 Maliwali walikoma katika Israeli, walikoma, Hata mimi Debora nilipoinuka, Nilipoinuka mimi, mama katika Israeli.
2 Samuel 20.19 Esther 9.19 Esaïe 49.23 Juges 4.4-4.6 Romains 16.13
8 Walichagua miungu mipya, Ndipo kulikuwa na vita malangoni; Je! Ilionekana ngao au mkuki Katika watu elfu arobaini wa Israeli?
Juges 2.17 Deutéronome 32.16-32.17 Juges 2.12 1 Samuel 13.19-13.22 Juges 4.3
9 Moyo wangu unawaelekea maliwali wa Israeli, Waliojitoa nafsi zao kwa hiari yao miongoni mwa watu; Mhimidini Bwana.
Juges 5.2 2 Corinthiens 8.17 2 Corinthiens 8.3-8.4 2 Corinthiens 8.12 2 Corinthiens 9.5
10 Itangazeni habari, ninyi mpandao punda weupe, Ninyi mketio juu ya mazulia ya thamani, Na ninyi mnaopita njiani kwa miguu.
Juges 12.14 Juges 10.4 Psaumes 145.11 Psaumes 145.5 Joël 3.12
11 Mbali na kelele za hao wapigao mishale, katika mahali pa kuteka maji, Hapo watatangaza matendo ya haki ya Bwana; Naam, matendo ya haki ya kutawala kwake katika Israeli. Ndipo watu wa Bwana waliposhuka malangoni.
1 Samuel 12.7 Michée 6.5 Job 29.7 Esaïe 28.6 Exode 2.17-2.19
12 Amka, amka, Debora; Amka, amka, imba wimbo. Inuka, Baraka, wachukue mateka wao Waliokuchukua mateka, Ee mwana wa Abinoamu.
Psaumes 57.8 Ephésiens 4.8 Psaumes 68.18 1 Corinthiens 15.34 Ephésiens 5.14
13 Ndipo walitelemka mabaki ya waungwana na ya watu; Bwana alishuka kwa ajili yangu apigane na mashujaa.
Psaumes 75.7 Apocalypse 3.9 Ezéchiel 17.24 Romains 8.37 Daniel 7.18-7.27
14 Kutoka Efraimu walitelemka wao ambao shina lao ni katika Amaleki, Nyuma yako, Benyamini, kati ya watu wako. Kutoka Makiri walishuka maliwali, Na kutoka Zabuloni wao washikao fimbo ya mwandishi.
Juges 3.13 Juges 3.27 Juges 12.15 Nombres 32.39-32.40 Juges 4.14
15 Na wakuu wa Isakari walikuwa pamoja na Debora. Kama alivyokuwa Isakari, ndivyo alivyokuwa Baraka. Waliingia bondeni kwa kasi miguuni pake. Kwenye vijito vya Reubeni Palikuwa na makusudi makuu mioyoni.
Juges 4.14 Actes 20.13 2 Corinthiens 11.2 Actes 15.39 1 Chroniques 12.32
16 Mbona ulikaa katika mazizi ya kondoo, Kusikiliza filimbi zipigwazo ili kuita makundi? Kwenye vijito vya Reubeni Palikuwa na makusudi makuu mioyoni.
Nombres 32.24 Lamentations 3.40-3.41 Philippiens 3.19 Nombres 32.1-32.5 Psaumes 77.6
17 Gileadi alikaa ng’ambo ya Yordani, Na Dani, mbona alikaa katika merikebu? Asheri alikaa kimya penye bandari ya bahari, Alikaa katika hori zake.
Josué 13.25 Josué 13.31 Josué 19.24-19.31
18 Zabuloni ndio watu waliohatirisha roho zao hata kufa; Nao Naftali mahali palipoinuka kondeni.
Juges 4.10 Juges 4.6 1 Jean 3.16 Actes 20.24 Juges 4.14
19 Wafalme walikuja wakafanya vita, Ndipo wafalme wa Kanaani walifanya vita. Katika Taanaki, karibu na maji ya Megido; Hawakupata faida yo yote ya fedha.
Juges 5.30 Juges 1.27 1 Rois 4.12 Genèse 4.16 Josué 10.22-10.27
20 Walipigana kutoka mbinguni, Nyota katika miendo yao zilipigana na Sisera.
Josué 10.11 1 Samuel 7.10 Psaumes 77.17-77.18 Juges 4.15
21 Mto ule wa Kishoni uliwachukua, Ule mto wa zamani, mto wa Kishoni. Ee roho yangu, endelea mbele kwa nguvu.
Juges 4.7 Psaumes 44.5 Michée 7.10 Juges 4.13 Genèse 49.18
22 Ndipo kwato za farasi zilikanyaga-kanyaga Kwa sababu ya kupara-para, Kupara-para kwao wenye nguvu.
Michée 4.13 Psaumes 33.17 Jérémie 47.4 Esaïe 5.28 Psaumes 20.7
23 Ulaanini Merozi, alisema malaika wa Bwana, Walaanini kwa uchungu wenyeji wake; Kwa maana hawakuja kumsaidia Bwana, Kumsaidia Bwana juu ya hao wenye nguvu.
Juges 21.9-21.10 Juges 4.6 Romains 15.18 Juges 6.11 1 Corinthiens 16.22
24 Atabarikiwa Yaeli kuliko wanawake wote; Mkewe Heberi, Mkeni, Atabarikiwa kuliko wanawake wote hemani.
Juges 4.17 Luc 1.42 Proverbes 31.31 Genèse 14.19 Luc 1.28
25 Aliomba maji, naye akampa maziwa. Akamletea siagi katika sahani ya heshima.
Juges 4.19-4.21
26 Akanyosha mkono wake akashika kigingi, Nao mkono wake wa kuume ukashika nyundo ya fundi; Akampiga Sisera kwa hiyo nyundo, akamtoboa kichwa chake. Naam, alimpiga akamtoboa kipaji chake.
1 Samuel 17.49-17.51 2 Samuel 20.22 Juges 4.21
27 Miguuni pake aliinama, akaanguka, akalala. Miguuni pake aliinama, akaanguka. Hapo alipoinama, ndipo alipoanguka amekufa.
Jacques 2.13 Matthieu 7.2 Psaumes 52.7
28 Alichungulia dirishani, akalia, Mama yake Sisera alilia dirishani; Mbona gari lake linakawia kufika? Mbona gurudumu za gari lake zinakawia?
Proverbes 7.6 Cantique 2.9 Cantique 8.14 Juges 4.15 Jacques 5.7
29 Mabibi yake wenye akili wakamjibu, Naam, alijipa nafsi yake jawabu.
30 Je! Hawakupata mateka na kuyagawanya, Kijakazi, vijakazi wawili, kwa kila mtu? Kwa Sisera nyara ya mavazi ya rangi mbali mbali, Nyara za mavazi ya rangi mbali mbali ya darizi; Ya rangi mbali mbali ya darizi, pande zote mbili, Juu ya shingo za hao mateka.
Exode 15.9 Psaumes 45.14 Genèse 37.3 2 Samuel 13.18 Job 20.5
31 Na waangamie vivyo hivyo adui zako wote, Ee Bwana.
Psaumes 19.4-19.5 2 Samuel 23.4 Psaumes 37.6 1 Corinthiens 8.3 1 Pierre 1.8

Cette Bible est dans le domaine public.