Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Hébreux 9.26
Bible en Swahili de l’est


Le sanctuaire de la nouvelle alliance

1 Basi hata agano la kwanza lilikuwa na kawaida za ibada, na patakatifu pake, pa kidunia.
Exode 25.8 Hébreux 8.2 Hébreux 9.10-9.11 Lévitique 18.30 Luc 1.6
2 Maana hema ilitengenezwa, ile ya kwanza, mlimokuwa na kinara cha taa, na meza, na mikate ya Wonyesho; ndipo palipoitwa, Patakatifu.
Exode 40.4 Exode 26.35 Lévitique 24.5-24.8 Exode 39.36-39.38 Exode 40.2
3 Na nyuma ya pazia la pili, ile hema iitwayo Patakatifu pa patakatifu,
Exode 26.31-26.33 Exode 40.3 Exode 40.21 Hébreux 10.19-10.20 Esaïe 25.7
4 yenye chetezo cha dhahabu, na sanduku la agano lililofunikwa kwa dhahabu pande zote, mlimokuwa na kopo la dhahabu lenye ile mana, na ile fimbo ya Haruni iliyochipuka, na vile vibao vya agano;
Exode 26.33 Nombres 17.10 Exode 40.3 2 Chroniques 5.10 1 Rois 8.21
5 na juu yake makerubi ya utukufu, yakikitia kivuli kiti cha rehema; basi hatuna nafasi sasa ya kueleza habari za vitu hivi kimoja kimoja.
Lévitique 16.2 Exode 25.17-25.22 1 Rois 8.6-8.7 1 Chroniques 28.11 1 Samuel 4.4
6 Basi, vitu hivi vikiisha kutengenezwa hivyo, makuhani huingia katika hema hiyo ya kwanza daima, wakiyatimiza mambo ya ibada.
Nombres 28.3 Daniel 8.11 Luc 1.8-1.11 Exode 30.7-30.8 Exode 27.21
7 Lakini katika hema hiyo ya pili kuhani mkuu huingia peke yake, mara moja kila mwaka; wala si pasipo damu, atoayo kwa ajili ya nafsi yake na kwa dhambi za kutokujua za hao watu.
Lévitique 16.34 Exode 30.10 Lévitique 5.18 Hébreux 7.27 Hébreux 10.3
8 Roho Mtakatifu akionyesha neno hili, ya kwamba njia ya kupaingia patakatifu ilikuwa haijadhihirishwa bado, hapo hema ya kwanza ilipokuwa ingali ikisimama;
Jean 14.6 Hébreux 3.7 Hébreux 10.15 Esaïe 63.11 Actes 7.51-7.52
9 ambayo ndiyo mfano wa wakati huu uliopo sasa; wakati huo sadaka na dhabihu zinatolewa, zisizoweza kwa jinsi ya dhambi kumkamilisha mtu aabuduye,
Hébreux 5.1 Hébreux 11.19 Hébreux 10.11 Hébreux 11.39-11.40 1 Pierre 3.21
10 kwa kuwa ni sheria za jinsi ya mwili tu, vyakula na vinywaji na kutawadha kwingine kwingine, zilizoamriwa hata wakati wa matengenezo mapya.
Hébreux 7.16 Colossiens 2.16 Lévitique 11.2-11.47 Exode 30.19-30.21 Ezéchiel 4.14
11 Lakini Kristo akiisha kuja, aliye kuhani mkuu wa mambo mema yatakayokuwapo, kwa hema iliyo kubwa na kamilifu zaidi, isiyofanyika kwa mikono, maana yake, isiyo ya ulimwengu huu,
Hébreux 10.1 2 Corinthiens 5.1 Hébreux 2.17 Hébreux 9.23-9.24 Actes 7.48
12 wala si kwa damu ya mbuzi na ndama, bali kwa damu yake mwenyewe aliingia mara moja tu katika Patakatifu, akiisha kupata ukombozi wa milele.
Hébreux 10.4 Hébreux 7.27 1 Thessaloniciens 1.10 Hébreux 10.9-10.14 Actes 20.28
13 Kwa maana, ikiwa damu ya mbuzi na mafahali na majivu ya ndama ya ng’ombe waliyonyunyiziwa wenye uchafu hutakasa hata kuusafisha mwili;
Lévitique 16.14-16.16 Psaumes 51.7 Nombres 19.2-19.21 1 Pierre 1.22 Nombres 8.7
14 basi si zaidi damu yake Kristo, ambaye kwamba kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na mawaa, itawasafisha dhamiri zenu na matendo mafu, mpate kumwabudu Mungu aliye hai?
1 Pierre 3.18 Hébreux 1.3 Hébreux 6.1 Tite 2.14 Hébreux 10.22
15 Na kwa sababu hii ni mjumbe wa agano jipya, ili, mauti ikiisha kufanyika kwa kukomboa makosa yaliyokuwa chini ya agano la kwanza, hao walioitwa waipokee ahadi ya urithi wa milele.
1 Timothée 2.5 Hébreux 12.24 Hébreux 11.39-11.40 Hébreux 9.28 Hébreux 3.1
16 Maana agano la urithi lilipo, lazima iwepo mauti yake aliyelifanya.
17 Kwa maana agano la urithi lina nguvu palipotukia kufa kwa mtu; kwa kuwa halina nguvu kabisa, akiwa yu hai yeye aliyelifanya.
Galates 3.15 Jean 14.27 Genèse 48.21
18 Kwa hiyo hata lile la kwanza halikuanzwa pasipo damu.
Exode 24.3-24.8 Exode 12.22 Hébreux 8.7-8.9 Hébreux 9.22 Hébreux 9.14
19 Maana kila amri ilipokwisha kunenwa na Musa kwa hao watu wote, kama ilivyoamuru sheria, aliitwaa damu ya ndama na ya mbuzi, pamoja na maji na sufu nyekundu na hisopo, akakinyunyizia kitabu chenyewe, na watu wote,
Hébreux 9.12 Nombres 19.6 1 Pierre 1.2 Nombres 19.18 Lévitique 1.2-1.3
20 akisema, Hii ni damu ya agano mliloamriwa na Mungu.
Matthieu 26.28 Exode 24.8 Hébreux 13.20 Deutéronome 29.12 Zacharie 9.11
21 Na ile hema nayo na vyombo vyote vya ibada alivinyunyizia damu vivyo hivyo.
Lévitique 8.15 Lévitique 8.19 Exode 29.36 Exode 29.12 Ezéchiel 43.18-43.26
22 Na katika Torati karibu vitu vyote husafishwa kwa damu, na pasipo kumwaga damu hakuna ondoleo.
Lévitique 17.11 Lévitique 6.7 Lévitique 14.25 Lévitique 4.35 Lévitique 5.10
23 Basi ilikuwa sharti nakala za mambo yaliyo mbinguni zisafishwe kwa hizo, lakini mambo ya mbinguni yenyewe yasafishwe kwa dhabihu zilizo bora kuliko hizo.
Hébreux 8.5 Hébreux 9.24 1 Pierre 1.19-1.21 Jean 14.3 Hébreux 10.10-10.17
24 Kwa sababu Kristo hakuingia katika patakatifu palipofanyika kwa mikono, ndio mfano wa patakatifu halisi; bali aliingia mbinguni hasa, aonekane sasa usoni pa Mungu kwa ajili yetu;
Hébreux 8.2 Jean 16.28 Marc 16.19 Ephésiens 1.20-1.22 Actes 3.21
25 wala si kwamba ajitoe mara nyingi, kama vile kuhani mkuu aingiavyo katika patakatifu kila mwaka kwa damu isiyo yake;
Hébreux 9.7 Hébreux 10.19 Hébreux 9.14 Lévitique 16.2-16.34 Hébreux 9.26
26 kama ni hivyo, ingalimpasa kuteswa mara nyingi tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu; lakini sasa, mara moja tu, katika utimilifu wa nyakati, amefunuliwa, azitangue dhambi kwa dhabihu ya nafsi yake.
Hébreux 1.2 Hébreux 9.12 Matthieu 25.34 1 Pierre 1.20 Hébreux 7.27
27 Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu;
2 Corinthiens 5.10 Ecclésiaste 12.14 Jude 1.15 Matthieu 25.31-25.46 2 Samuel 14.14
28 kadhalika Kristo naye, akiisha kutolewa sadaka mara moja azichukue dhambi za watu wengi; atatokea mara ya pili, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu.
1 Pierre 2.24 Romains 6.10 Tite 2.13 Actes 1.11 1 Pierre 3.18

Cette Bible est dans le domaine public.