1 Uwakumbushe watu kunyenyekea kwa wenye uwezo na mamlaka, na kutii, na kuwa tayari kwa kila kazi njema;
Romains 13.1-13.7 Ecclésiaste 10.4 2 Timothée 2.21 1 Pierre 2.13-2.17 Ecclésiaste 8.2-8.5
2 wasimtukane mtu ye yote, wasiwe wagomvi, wawe wema, wakionyesha upole wote kwa watu wote.
2 Timothée 2.24-2.25 1 Timothée 3.3 Ephésiens 4.31 Ephésiens 4.2 Matthieu 11.29
3 Maana hapo zamani sisi nasi tulikuwa hatuna akili, tulikuwa waasi, tumedanganywa, huku tukitumikia tamaa na anasa za namna nyingi, tukiishi katika uovu na husuda, tukichukiza na kuchukiana.Colossiens 3.7 Ephésiens 2.1-2.3 Colossiens 1.21 Romains 1.29-1.31 Romains 3.9-3.20
4 Lakini wema wake Mwokozi wetu Mungu, na upendo wake kwa wanadamu, ulipofunuliwa, alituokoa;
Tite 2.10-2.11 Hébreux 9.26 Ephésiens 2.4-2.10 2 Timothée 1.10 Romains 2.4
5 si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyatenda sisi; bali kwa rehema yake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa pili na kufanywa upya na Roho Mtakatifu;
Ephésiens 2.8-2.9 1 Corinthiens 6.11 Romains 12.2 1 Pierre 3.21 Ephésiens 2.4
6 ambaye alitumwagia kwa wingi, kwa njia ya Yesu Kristo Mwokozi wetu;
Romains 5.5 Actes 10.45 Joël 2.28 Actes 2.33 Proverbes 1.23
7 ili tukihesabiwa haki kwa neema yake, tupate kufanywa warithi wa uzima wa milele, kama lilivyo tumaini letu.
Romains 8.17 Tite 1.2 Romains 3.24 Tite 2.11 1 Corinthiens 6.11
8 Ni neno la kuaminiwa; na mambo hayo nataka uyanene kwa nguvu, ili wale waliomwamini Mungu wakumbuke kudumu katika matendo mema. Hayo ni mazuri, tena yana faida kwa wanadamu.
1 Timothée 1.15 Tite 3.14 Tite 2.14 Romains 4.5 Psaumes 16.2-16.3
9 Lakini maswali ya upuzi ujiepushe nayo, na nasaba, na magomvi, na mashindano ya sheria. Kwa kuwa hayana faida, tena hayana maana.
2 Timothée 2.14 2 Timothée 2.23 Tite 1.14 1 Timothée 4.7 Job 15.3
10 Mtu aliye mzushi, baada ya kumwonya mara ya kwanza na mara ya pili, mkatae;
Romains 16.17 2 Jean 1.10 2 Timothée 3.5 2 Thessaloniciens 3.14 Matthieu 18.15-18.17
11 ukijua ya kuwa mtu kama huyo amepotoka, tena atenda dhambi, maana amejihukumu hatia yeye mwenyewe.
Luc 19.22 Matthieu 25.26-25.28 1 Timothée 1.19-1.20 2 Timothée 2.14 Luc 7.30
Dernières instructions et salutations
12 Wakati nitakapomtuma Artema kwako au Tikiko, jitahidi kuja kwangu huku Nikopoli; kwa maana huku nimekusudia kukaa wakati wa baridi.
Actes 20.4 2 Timothée 4.9 2 Timothée 4.21 2 Timothée 4.12 1 Corinthiens 16.8-16.9
13 Zena, yule mwana-sheria, na Apolo, uwasafirishe kwa bidii, wasipungukiwe na cho chote.
Actes 18.24 Matthieu 22.35 Luc 11.52 Romains 15.24 1 Corinthiens 16.11
14 Watu wetu nao wajifunze kudumu katika matendo mema, kwa matumizi yaliyo lazima, ili wasiwe hawana matunda.
Colossiens 1.10 Philippiens 1.11 Philippiens 4.17 Matthieu 7.19 2 Pierre 1.8
15 Watu wote walio pamoja nami wakusalimu. Tusalimie wale watupendao katika imani. Neema na iwe pamoja nanyi nyote.
Colossiens 4.18 Philémon 1.5 Ephésiens 6.23-6.24 Galates 5.6 2 Jean 1.1-1.2