Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Romains 2.15
Bible en Swahili de l’est


1 Kwa hiyo, wewe mtu uwaye yote uhukumuye, huna udhuru; kwa maana katika hayo umhukumuyo mwingine wajihukumu mwenyewe kuwa na hatia; kwa maana wewe uhukumuye unafanya yale yale.
Romains 2.3 Luc 6.37 2 Samuel 12.5-12.7 Matthieu 7.1-7.5 Jean 8.7-8.9
2 Nasi twajua ya kuwa hukumu ya Mungu ni ya kweli juu yao wafanyao hayo.
Psaumes 9.7-9.8 Sophonie 3.5 Jérémie 12.1 Apocalypse 19.2 Psaumes 9.4
3 Wewe binadamu, uwahukumuye wale wafanyao hayo na kutenda yayo hayo mwenyewe, je! Wadhani ya kwamba utajiepusha na hukumu ya Mungu?
Romains 1.32-2.1 Luc 12.14 Proverbes 16.5 Ezéchiel 17.15 1 Thessaloniciens 5.3
4 Au waudharau wingi wa wema wake na ustahimili wake na uvumilivu wake, usijue ya kuwa wema wa Mungu wakuvuta upate kutubu?
2 Pierre 3.9 Esaïe 30.18 Romains 3.25 Exode 34.6 Ephésiens 2.7
5 Bali kwa kadiri ya ugumu wako, na kwa moyo wako usio na toba, wajiwekea akiba ya hasira kwa siku ile ya hasira na ufunuo wa hukumu ya haki ya Mungu,
Deutéronome 32.34 Ecclésiaste 12.14 Hébreux 3.13 Hébreux 3.15 Jacques 5.3
6 atakayemlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake;
Psaumes 62.12 Job 34.11 Matthieu 16.27 Jérémie 17.10 Jérémie 32.19
7 wale ambao kwa saburi katika kutenda mema wanatafuta utukufu na heshima na kutokuharibika, watapewa uzima wa milele;
Luc 8.15 2 Timothée 1.10 Romains 6.23 1 Corinthiens 15.53-15.54 Colossiens 1.27
8 na wale wenye fitina, wasioitii kweli, bali wakubalio dhuluma, watapata hasira na ghadhabu;
1 Corinthiens 11.16 Psaumes 90.11 Hébreux 10.27 Romains 1.18 Apocalypse 14.10
9 dhiki na shida juu ya kila nafsi ya mwanadamu atendaye uovu, Myahudi kwanza na Myunani pia;
1 Pierre 4.17 Romains 15.8-15.9 Romains 2.10 Actes 13.46-13.47 Actes 18.5-18.6
10 bali utukufu na heshima na amani kwa kila mtu atendaye mema, Myahudi kwanza na Myunani pia;
Esaïe 32.17 Esaïe 57.19 1 Pierre 1.7 Romains 2.7 Job 22.21
11 kwa maana hakuna upendeleo kwa Mungu.
Actes 10.34 Deutéronome 10.17 Colossiens 3.25 Galates 2.6 Galates 6.7-6.8
12 Kwa kuwa wote waliokosa pasipo sheria watapotea pasipo sheria, na wote waliokosa, wenye sheria, watahukumiwa kwa sheria.
Galates 2.16-2.19 1 Corinthiens 9.21 Galates 3.10 Deutéronome 27.26 Ezéchiel 16.49-16.50
13 Kwa sababu sio wale waisikiao sheria walio wenye haki mbele za Mungu, bali ni wale waitendao sheria watakaohesabiwa haki.
Jacques 1.22-1.25 1 Jean 3.7 Romains 2.25 1 Jean 2.29 Galates 2.16
14 Kwa maana watu wa Mataifa wasio na sheria wafanyapo kwa tabia zao yaliyo ndani ya torati, hao wasio na sheria wamekuwa sheria kwa nafsi zao wenyewe.
Romains 2.12 Psaumes 147.19-147.20 Actes 17.30 Ephésiens 2.12 Romains 1.19-1.20
15 Hao waionyesha kazi ya torati iliyoandikwa mioyoni mwao, dhamiri yao ikiwashuhudia, na mawazo yao, yenyewe kwa yenyewe, yakiwashitaki au kuwatetea;
Romains 1.18-1.19 2 Corinthiens 5.11 1 Jean 3.19-3.21 Tite 1.15 Romains 9.1
16 katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, sawasawa na injili yangu, kwa Kristo Yesu.
Ecclésiaste 12.14 Actes 10.42 Romains 16.25 1 Corinthiens 4.5 2 Timothée 2.8

Culpabilité des Juifs

17 Lakini wewe, ukiwa unaitwa Myahudi na kuitegemea torati, na kujisifu katika Mungu,
Romains 2.23 Michée 3.11 Jean 5.45 Jean 8.41 Psaumes 135.4
18 na kuyajua mapenzi yake, na kuyakubali mambo yaliyo bora, nawe umeelimishwa katika torati,
Deutéronome 4.8 1 Thessaloniciens 5.21 Jacques 4.17 Philippiens 1.10 Luc 12.47
19 na kujua hakika ya kuwa wewe mwenyewe u kiongozi wa vipofu, mwanga wao walio gizani,
1 Corinthiens 4.10 Jean 9.40-9.41 Matthieu 15.14 Apocalypse 3.17-3.18 Philippiens 2.15
20 mkufunzi wa wajinga, mwalimu wa watoto wachanga, mwenye namna ya maarifa na ya kweli katika torati;
2 Timothée 3.5 Tite 1.16 2 Timothée 1.13 Romains 6.17 1 Corinthiens 3.1
21 basi wewe umfundishaye mwingine, je! Hujifundishi mwenyewe? Wewe uhubiriye kwamba mtu asiibe, waiba mwenyewe?
Matthieu 23.3-23.28 Michée 3.11 Luc 12.47 Psaumes 50.16-50.21 Amos 8.4-8.6
22 Wewe usemaye kwamba mtu asizini, wazini mwenyewe? Wewe uchukiaye sanamu, wateka mahekalu?
Actes 19.37 Malachie 3.8 Jérémie 5.7 Ezéchiel 22.11 Matthieu 12.39
23 Wewe ujisifuye katika torati, wamvunjia Mungu heshima kwa kuiasi torati?
Romains 2.17 Romains 9.4 Jean 5.45 Romains 3.2 Luc 18.11
24 Kwa maana jina la Mungu latukanwa katika Mataifa kwa ajili yenu, kama ilivyoandikwa.
Esaïe 52.5 Ezéchiel 36.20-36.23 Lamentations 2.15-2.16 Tite 2.8 2 Samuel 12.14
25 Kwa maana kutahiriwa kwafaa kama ukiwa mtendaji wa sheria, lakini ukiwa mvunjaji wa sheria kutahiriwa kwako kumekuwa kutokutahiriwa.
Jérémie 4.4 Jérémie 9.25-9.26 Romains 2.28-3.2 Actes 7.51 Galates 5.3-5.6
26 Basi ikiwa yeye asiyetahiriwa huyashika maagizo ya torati, je! Kutokutahiriwa kwake hakutahesabiwa kuwa kutahiriwa?
Romains 8.4 1 Corinthiens 7.18-7.19 Colossiens 2.11 Esaïe 56.6-56.7 Actes 10.2-10.4
27 Na yeye asiyetahiriwa kwa asili, aishikaye torati, je! Hatakuhukumu wewe, uliye na kutahiriwa, ukaihalifu torati?
Romains 2.29 Matthieu 12.41-12.42 2 Corinthiens 3.6 Ezéchiel 16.48-16.52 Hébreux 11.3
28 Maana yeye si Myahudi aliye Myahudi kwa nje tu, wala tohara siyo ile ya nje tu katika mwili;
Galates 6.15 Matthieu 3.9 Romains 9.6-9.8 Apocalypse 2.9 Esaïe 48.1-48.2
29 bali yeye ni Myahudi aliye Myahudi kwa ndani, na tohara ni ya moyo, katika roho, si katika andiko; ambaye sifa yake haitoki kwa wanadamu bali kwa Mungu.
1 Pierre 3.4 Philippiens 3.3 Deutéronome 30.6 1 Thessaloniciens 2.4 2 Corinthiens 10.18

Cette Bible est dans le domaine public.