Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 7.58
Bible en Swahili de l’est


1 Kuhani Mkuu akasema, Je! Mambo hayo ndivyo yalivyo?
Actes 6.13-6.14 Matthieu 26.61-26.62 Jean 18.19-18.21 Marc 14.58-14.60 Jean 18.33-18.35
2 Naye akasema, Ndugu zangu na baba zangu, sikilizeni: Mungu wa utukufu alimtokea baba yetu Ibrahimu, alipokuwa katika Mesopotamia, kabla hajakaa Harani,
Genèse 11.31 Actes 22.1 Psaumes 29.3 Genèse 15.7 Hébreux 1.3
3 akamwambia, Toka katika nchi yako na katika jamaa zako, ukaende hata nchi nitakayokuonyesha.
Genèse 12.1 Hébreux 11.8 Néhémie 9.8 Matthieu 10.37 2 Corinthiens 6.17
4 Ndipo alipotoka katika nchi ya Wakaldayo, akakaa Harani, akatoka huko baada ya kufa babaye, Mungu akamhamisha mpaka nchi hii mnayokaa ninyi sasa.
Genèse 12.4-12.5 Genèse 11.31-11.32 Esaïe 41.9 Esaïe 41.2
5 Wala hakumpa urithi humu hata kiasi cha kuweka mguu; akaahidi kwamba atampa, iwe milki yake, na ya uzao wake baadaye alipokuwa hana mtoto.
Genèse 17.8 Genèse 12.7 Genèse 15.18 Genèse 13.15 Genèse 26.3
6 Mungu akanena hivi, ya kwamba wazao wake watakuwa wageni katika nchi ya watu wengine, nao watawafanya kuwa watumwa wao, na kuwatenda mabaya kwa muda wa miaka mia nne.
Genèse 15.13 Galates 3.17 Genèse 15.16 Exode 12.40-12.41
7 Na lile taifa watakaowafanya watumwa nitawahukumu mimi, alisema Mungu; na baada ya hayo watatoka, nao wataniabudu mahali hapa.
Exode 3.12 Psaumes 105.27-105.36 Néhémie 9.9-9.11 Psaumes 74.12-74.14 Psaumes 135.8-135.9
8 Akampa agano la tohara; basi Ibrahimu akamzaa Isaka, akamtahiri siku ya nane. Isaka akamzaa Yakobo. Yakobo akawazaa wale kumi na wawili, wazee wetu.
Genèse 35.23-35.26 Genèse 17.9-17.14 Genèse 35.16 Actes 2.29 Exode 1.1-1.4
9 Wale wazee wetu wakimwonea wivu Yusufu, wakamwuza aende Misri. Mungu akawa pamoja naye,
Genèse 39.2 Genèse 45.4 Psaumes 105.17 Esaïe 43.2 Genèse 49.23-49.24
10 akamtoa katika dhiki zake zote, akampa fadhili na hekima mbele ya Farao, mfalme wa Misri; naye akamfanya awe mtawala juu ya Misri na nyumba yake yote.
Genèse 42.6 Proverbes 3.4 Proverbes 2.6 Psaumes 22.24 Proverbes 16.7
11 Basi kukawa njaa katika nchi yote ya Misri na Kanaani, na dhiki nyingi, wala baba zetu hawakupata chakula cha kuwatosha.
Psaumes 105.16 Genèse 45.11 Genèse 47.13-47.15 Genèse 42.5 Genèse 41.54-41.57
12 Hata Yakobo aliposikia ya kwamba huko Misri kuna nafaka, akawatuma baba zetu mara ya kwanza.
Genèse 42.1-42.24 Genèse 43.2
13 Hata safari ya pili Yusufu akajitambulisha kwa ndugu zake, jamaa ya Yusufu ikawa dhahiri kwa Farao.
Genèse 46.31-47.10 Genèse 45.1-45.18
14 Yusufu akatuma watu akamwita Yakobo babaye na jamaa zake wote pia, watu sabini na watano.
Deutéronome 10.22 Genèse 46.26-46.27 Exode 1.5 1 Chroniques 2.5-2.6 Genèse 45.9-45.11
15 Basi Yakobo akashuka mpaka Misri; akafa yeye na baba zetu;
Exode 1.6 Genèse 49.33 Genèse 46.3-46.7 Hébreux 11.21-11.22 Nombres 20.15
16 wakachukuliwa mpaka Shekemu wakazikwa katika kaburi lile, ambalo Ibrahimu alilinunua kwa kima cha fedha kwa wana wa Hamori, huko Shekemu.
Josué 24.32 Exode 13.19 Genèse 23.16 Genèse 49.29-49.32 Genèse 34.2-34.31
17 Basi wakati wa ile ahadi ambayo Mungu alimpa Ibrahimu ulipokuwa unakaribia, wale watu wakazidi na kuongezeka sana huko Misri,
Actes 13.17 Actes 7.6 Exode 1.7-1.12 Exode 1.20 Genèse 15.13-15.16
18 hata mfalme mwingine akainuka juu ya Misri, asiyemfahamu Yusufu.
Exode 1.8
19 Huyo akawafanyia hila kabila yetu, na kuwatenda mabaya baba zetu, akiwaamuru wawatupe watoto wao wachanga, ili wasiishi.
Exode 1.9-1.22 Psaumes 105.25 Psaumes 129.1-129.3 Psaumes 83.4-83.5 Apocalypse 12.4-12.5
20 Wakati huo akazaliwa Musa, naye alikuwa mzuri sana, akalelewa muda wa miezi mitatu katika nyumba ya babaye.
Hébreux 11.23 1 Samuel 16.12 Exode 2.2-2.10
21 Hata alipotupwa, binti Farao akamtwaa, akamlea awe kama mwanawe.
Hébreux 11.24 Exode 2.2-2.10 Deutéronome 32.26
22 Musa akafundishwa hekima yote ya Wamisri, akawa hodari wa maneno na matendo.
Esaïe 19.11 Daniel 1.4 Luc 24.19 1 Rois 4.29-4.30 Daniel 1.17-1.20
23 Umri wake ulipopata kama miaka arobaini akaazimu moyoni mwake kwenda kuwatazama ndugu zake Waisraeli.
Hébreux 11.24-11.26 Exode 2.11-2.12 Jacques 1.17 2 Corinthiens 8.16 Esdras 1.1
24 Akamwona mmoja akidhulumiwa, akamtetea, akamlipia kisasi yule aliyekuwa akionewa, akampiga huyo Mmisri.
Jean 18.25-18.27 Jean 18.10-18.11 Actes 7.28
25 Alidhani kwamba ndugu zake watafahamu ya kuwa Mungu anawapa wokovu kwa mkono wake, lakini hawakufahamu.
Actes 15.7 1 Samuel 19.5 Romains 15.18 Actes 15.4 Actes 14.27
26 Siku ya pili yake akawatokea walipokuwa wakishindana, akataka kuwapatanisha, akisema, Enyi bwana zangu, ninyi ni ndugu. Mbona mnadhulumiana?
Exode 2.13-2.15 Proverbes 18.19 1 Corinthiens 6.6-6.8 Philippiens 2.3 Psaumes 133.1
27 Lakini yeye aliyemdhulumu mwenziwe akamsukumia mbali, akisema, Ni nani aliyekuweka wewe kuwa mkuu na mwamuzi juu yetu?
Actes 7.35 Luc 12.14 1 Samuel 25.14-25.15 Actes 5.33 Actes 3.13-3.15
28 Je! Wataka kuniua mimi kama ulivyomwua yule Mmisri jana?
29 Musa akakimbia kwa neno hilo, akakaa hali ya ugeni katika nchi ya Midiani, akazaa wana wawili huko.
Exode 4.19-4.20 Exode 2.14-2.22 Exode 18.2-18.4
30 Hata miaka arobaini ilipotimia, malaika wa Bwana akamtokea katika jangwa la mlima wa Sinai katika mwali wa moto, kijitini.
Actes 7.35 Exode 3.1-3.2 Esaïe 63.9 Esaïe 43.2 Daniel 3.27
31 Musa alipouona, akastaajabia maono yale, na alipokaribia ili atazame, sauti ya Bwana ikamjia,
Exode 3.3-3.4
32 Mimi ni Mungu wa baba zako, Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akatetemeka, asithubutu kutazama.
Exode 3.6 Matthieu 22.32 Exode 3.15 Job 37.1-37.2 Apocalypse 1.17
33 Bwana akamwambia, Vua viatu miguuni mwako, kwa maana mahali hapa unaposimama ni nchi takatifu.
Josué 5.15 Exode 3.5 2 Pierre 1.18 Ecclésiaste 5.1
34 Yakini nimeona mateso ya watu wangu waliomo Misri, nimesikia kuugua kwao, nami nimeshuka niwatoe. Basi sasa, nitakutuma mpaka Misri.
Exode 3.7-3.10 Jean 6.38 Esaïe 64.1 Psaumes 144.5 Exode 3.14
35 Musa huyo waliyemkataa, wakisema, Ni nani aliyekuweka kuwa mkuu na mwamuzi? Ndiye aliyetumwa na Mungu kuwa mkuu na mkombozi, kwa mkono wa yule malaika aliyemtokea katika kile kijiti.
Nombres 20.16 Psaumes 75.7 Luc 19.14 Psaumes 113.7-113.8 Exode 14.19
36 Huyo ndiye aliyewatoa, akifanya ajabu na ishara katika nchi ya Misri, na katika bahari ya Shamu, na katika jangwa muda wa miaka arobaini.
Exode 12.41 Exode 14.21 Exode 33.1 Exode 14.27-14.29 Exode 7.1-7.14
37 Musa huyo ndiye aliyewaambia Waisraeli, Bwana Mungu wenu atawainulieni nabii, katika ndugu zenu, kama mimi; msikieni yeye.
Deutéronome 18.15-18.19 Matthieu 17.3-17.5 Luc 9.30-9.31 Jean 18.37 Actes 3.22-3.23
38 Yeye ndiye aliyekuwa katika kanisa jangwani pamoja na yule malaika aliyesema naye katika mlima wa Sinai, tena pamoja na baba zetu; ndiye aliyepokea maneno ya uzima atupe sisi.
Romains 3.2 Hébreux 5.12 Actes 7.53 1 Pierre 4.11 Esaïe 63.9
39 Mtu huyo baba zetu hawakutaka kumtii, bali wakamsukumia mbali, na kwa mioyo yao wakarejea Misri,
Nombres 14.3-14.4 Nombres 11.5 Exode 16.3 Nombres 21.5 Néhémie 9.16-9.17
40 wakamwambia Haruni, Tufanyie miungu, watakaotutangulia; maana huyo Musa, aliyetutoa katika nchi ya Misri, hatujui lililompata.
Exode 32.1 Exode 32.23
41 Wakafanya ndama siku zile, wakaleta dhabihu kwa sanamu ile, wakafurahia kazi za mikono yao.
Esaïe 2.8-2.9 Esaïe 44.9-44.20 Néhémie 9.18 Exode 32.2-32.8 Habakuk 2.18-2.20
42 Basi Mungu akaghairi, akawaacha ili waliabudu jeshi la mbinguni, kama ilivyoandikwa katika chuo cha manabii, Je! Mlinitolea mimi dhabihu na sadaka Miaka arobaini katika jangwa, enyi nyumba ya Israeli?
Jérémie 19.13 Ezéchiel 20.39 2 Rois 17.16 Deutéronome 4.19 Esaïe 63.10
43 Nanyi mlichukua hema ya Moleki, Na nyota za mungu wenu Refani, Sanamu mlizozifanya ili kuziabudu; Nami nitawafahamisha mwende mbali kupita Babeli.
Amos 5.26-5.27 2 Rois 21.6 Lévitique 18.21 Lévitique 20.2-20.5 Deutéronome 4.16-4.18
44 Ile hema ya ushahidi ilikuwa pamoja na baba zetu jangwani, kama alivyoagiza yeye aliyesema na Musa, ya kwamba aifanye sawasawa na mfano ule aliouona;
Exode 25.40 Exode 38.21 1 Chroniques 28.11 Nombres 10.11 2 Chroniques 24.6
45 ambayo baba zetu, kwa kupokezana, wakaiingiza pamoja na Yoshua katika milki ya Mataifa wale, ambao Mungu aliwafukuza mbele ya baba zetu, mpaka siku za Daudi;
Psaumes 44.2 Josué 18.1 Actes 13.19 1 Samuel 4.4 1 Rois 8.4
46 aliyepata fadhili mbele za Mungu, naye aliomba ampatie Mungu wa Yakobo maskani.
Actes 13.22 Psaumes 132.1-132.5 1 Samuel 16.1 1 Chroniques 17.1-17.4 2 Samuel 7.1-7.5
47 Lakini Sulemani alimjengea nyumba.
1 Rois 8.20 1 Rois 6.37-6.38 2 Samuel 7.13 1 Rois 5.1-6.2 Zacharie 6.12-6.13
48 Ila Yeye aliye juu hakai katika nyumba zilizofanywa kwa mikono, kama vile asemavyo nabii,
1 Rois 8.27 2 Chroniques 2.5-2.6 Esaïe 66.1-66.2 Actes 17.24-17.25 Psaumes 91.1
49 Mbingu ni kiti changu cha enzi, Na nchi ni pa kuwekea miguu yangu; Ni nyumba gani mtakayonijengea? Asema Bwana,
Psaumes 11.4 Apocalypse 3.21 Jérémie 23.24 Esaïe 66.1 Matthieu 5.34-5.35
50 Au ni mahali gani nitakapostarehe? Si mkono wangu uliofanya haya yote?
Esaïe 44.24 Jérémie 10.11 Esaïe 45.12 Actes 14.15 Psaumes 146.5-146.6
51 Enyi wenye shingo gumu, msiotahiriwa mioyo wala masikio, siku zote mnampinga Roho Mtakatifu; kama baba zenu walivyofanya, na ninyi ni vivyo hivyo.
Lévitique 26.41 Deutéronome 10.16 Exode 33.5 Exode 32.9 Jérémie 6.10
52 Ni yupi katika manabii ambaye baba zenu hawakumwudhi? Nao waliwaua wale waliotabiri habari za kuja kwake yule Mwenye Haki; ambaye ninyi sasa mmekuwa wasaliti wake, mkamwua;
Matthieu 5.12 2 Chroniques 36.16 1 Rois 19.10 1 Thessaloniciens 2.15 Luc 11.47-11.51
53 ninyi mlioipokea torati kwa agizo la malaika msiishike.
Galates 3.19 Hébreux 2.2 Deutéronome 33.2 Jean 7.19 Actes 7.38
54 Basi waliposikia maneno haya, wakachomwa mioyo, wakamsagia meno.
Actes 5.33 Psaumes 35.16 Job 16.9 Luc 13.28 Matthieu 13.42
55 Lakini yeye akijaa Roho Mtakatifu, akakaza macho yake, akitazama mbinguni, akauona utukufu wa Mungu, na Yesu akisimama upande wa mkono wa kuume wa Mungu.
Actes 6.5 Michée 3.8 Jean 12.41 Hébreux 1.3 Marc 16.19
56 Akasema, Tazama! Naona mbingu zimefunguka, na Mwana wa Adamu amesimama mkono wa kuume wa Mungu.
Matthieu 3.16 Apocalypse 11.19 Matthieu 25.31 Jean 5.22-5.27 Jean 1.51
57 Wakapiga kelele kwa sauti kuu, wakaziba masikio yao, wakamrukia kwa nia moja,
Actes 21.27-21.31 Zacharie 7.11 Actes 7.54 Actes 23.27 Psaumes 58.4
58 wakamtoa nje ya mji, wakampiga kwa mawe. Nao mashahidi wakaweka nguo zao miguuni pa kijana mmoja aliyeitwa Sauli.
Actes 8.1 Actes 22.20 Luc 4.29 Actes 6.13 Lévitique 24.14-24.16
59 Wakampiga kwa mawe Stefano, naye akiomba, akisema, Bwana Yesu, pokea roho yangu.
Actes 9.14 Psaumes 31.5 Luc 23.46 Actes 9.21 1 Corinthiens 1.2
60 Akapiga magoti, akalia kwa sauti kuu, Bwana, usiwahesabie dhambi hii. Akiisha kusema haya akalala. Na Sauli alikuwa akiona vema kwa kuuawa kwake.
Matthieu 5.44 Actes 20.36 Luc 23.34 Actes 9.40 Actes 21.5

Cette Bible est dans le domaine public.