Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Marc 12.36
Bible en Swahili de l’est


Parabole des vignerons

1 Akaanza kusema nao kwa mifano; Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu, akazungusha ugo, akachimba shimo la shinikizo, akajenga mnara, akapangisha wakulima, akasafiri.
Esaïe 5.1-5.4 Cantique 8.11-8.12 Matthieu 25.14 Marc 4.33-4.34 Psaumes 80.8-80.16
2 Hata kwa wakati wake akatuma mtumwa kwa wale wakulima, ili apokee kwa wakulima katika matunda ya mizabibu.
Hébreux 1.1 Jean 15.1-15.8 Jérémie 44.4 Psaumes 1.3 Esdras 9.11
3 Wakamtwaa, wakampiga, wakamtoa nje, hana kitu.
Néhémie 9.26 Actes 7.52 2 Chroniques 36.16 1 Thessaloniciens 2.15 Hébreux 11.36-11.37
4 Akatuma tena kwao mtumwa mwingine, na huyo wakamtia jeraha za kichwa, wakamfanyia jeuri.
5 Akamtuma mwingine, huyo wakamwua; na wengine wengi, hawa wakiwapiga na hawa wakiwaua.
Matthieu 21.35-21.36 Jérémie 7.25-7.28 Matthieu 23.37 Luc 6.36 Luc 6.22-6.23
6 Basi alikuwa na mmoja bado, mwana mpendwa wake; huyu naye akamtuma kwao mwisho, akisema, Watamstahi mwanangu.
Matthieu 3.17 Hébreux 1.1-1.2 Genèse 44.20 Jean 1.34 Jean 5.23
7 Lakini wale wakulima wakasemezana, Huyu ni mrithi; haya, na tumwue, na urithi utakuwa wetu.
Genèse 37.20 Actes 7.52 Matthieu 2.3-2.13 Marc 12.12 Esaïe 53.7-53.8
8 Wakamkamata, wakamwua, wakamtupa nje ya shamba la mizabibu.
Hébreux 13.11-13.13 Matthieu 21.39 Luc 20.15 Matthieu 21.33
9 basi atafanyaje yule bwana wa shamba la mizabibu? Atakuja na kuwaangamiza wale wakulima, na lile shamba la mizabibu atawapa wengine.
Matthieu 21.43 Luc 19.27 Esaïe 5.5-5.7 Luc 19.41-19.44 Luc 20.15-20.16
10 Hata andiko hili hamjalisoma, Jiwe walilolikataa waashi, Hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni.
Psaumes 118.22-118.23 Matthieu 21.16 Esaïe 28.16 Ephésiens 2.20-2.22 1 Pierre 2.7-2.8
11 Neno hili limetoka kwa Bwana, Nalo ni ajabu machoni petu?
Actes 2.32-2.36 Actes 3.12-3.16 Ephésiens 3.8-3.11 Habakuk 1.5 Psaumes 118.23
12 Nao wakatafuta kumkamata, wakaogopa mkutano; maana walitambua ya kwamba ule mfano amewanenea wao. Wakamwacha wakaenda zao.
Marc 11.18 Jean 7.30 Matthieu 22.22 Marc 11.32 Jean 7.25

Tentatives de piéger Jésus

13 Wakatuma kwake baadhi ya Mafarisayo na Maherodi, ili wamnase kwa maneno.
Luc 11.54 Luc 20.20-20.26 Marc 3.6 Marc 8.15 Jérémie 18.18
14 Hata walipofika walimwambia, Mwalimu, twajua ya kuwa wewe u mtu wa kweli, wala hujali cheo cha mtu; kwa maana hutazami sura za watu; lakini katika kweli waifundisha njia ya Mungu. Je! Ni halali kumpa Kaisari kodi au siyo?
Deutéronome 33.9-33.10 Michée 3.8 Romains 13.6 Psaumes 120.2 2 Corinthiens 2.17
15 Tumpe, tusimpe? Naye, akijua unafiki wao, akawaambia, Mbona mmenijaribu? Nileteeni dinari niione.
Hébreux 4.13 Jean 21.17 Actes 5.9 1 Corinthiens 10.9 Ezéchiel 17.2
16 Wakaileta. Akawaambia, Ni ya nani sanamu hii na anwani hii? Wakamwambia, Ni ya Kaisari.
Apocalypse 3.12 Luc 20.24-20.26 2 Timothée 2.19 Matthieu 22.19-22.22
17 Yesu akajibu, akawaambia, Mpeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, na yaliyo ya Mungu mpeni Mungu. Wakamstaajabia sana.
Romains 13.7 Matthieu 17.25-17.27 Romains 6.13 Matthieu 22.33 Marc 12.30
18 Kisha Masadukayo, watu wasemao ya kwamba hakuna kiyama, wakamwendea, wakamwuliza na kusema,
Actes 4.1-4.2 Matthieu 22.23-22.33 1 Corinthiens 15.13-15.18 Actes 23.6-23.9 2 Timothée 2.18
19 Mwalimu, Musa alituandikia ya kwamba ndugu ya mtu akifa, akamwacha mkewe wala hana mtoto, ndugu yake amtwae yule mkewe akampatie ndugu yake mzao.
Ruth 4.5 Deutéronome 25.5-25.10 Ruth 1.11-1.13 Genèse 38.8
20 Basi kulikuwa na ndugu saba, wa kwanza akatwaa mke, akafa, asiache mzao.
Luc 20.29-20.33 Matthieu 22.25-22.28
21 Wa pili naye akamtwaa akafa, wala yeye hakuacha mzao. Na wa tatu kadhalika;
22 hata na wote saba, wasiache mzao. Mwisho wa wote yule mwanamke akafa naye.
23 Basi, katika kiyama atakuwa mke wa yupi katika hao? Maana wote saba walikuwa naye.
24 Yesu akajibu, akawaambia, Je! Hampotei kwa sababu hii, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu?
Jean 20.9 Matthieu 22.29 Osée 6.2 2 Timothée 3.15-3.17 Esaïe 25.8
25 Kwa maana watakapofufuka katika wafu, hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika walioko mbinguni.
Hébreux 12.22-12.23 1 Corinthiens 15.42-15.54 Matthieu 22.30 Luc 20.35-20.36 1 Jean 3.2
26 Na kwa habari ya wafu ya kwamba wafufuliwa, hamjasoma katika kitabu cha Musa, Sura ya Kijiti, jinsi Mungu alivyomwambia, akisema, Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo?
Luc 20.37 Genèse 17.7-17.8 Marc 12.10 Exode 3.2-3.6 Genèse 33.20
27 Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai. Hivyo mwapotea sana.
Romains 14.9 Romains 4.17 Proverbes 19.27 Hébreux 3.10 Marc 12.24
28 Na mmojawapo wa waandishi akafika, akawasikia wakisemezana naye, akatambua ya kuwa amewajibu vema, akamwuliza, Katika amri zote ni ipi iliyo ya kwanza?
Matthieu 22.34-22.40 Luc 20.39 Luc 10.25-10.28 Matthieu 19.18 Luc 11.42
29 Yesu akamjibu, Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja;
Deutéronome 6.4 Galates 3.20 Jacques 2.19 Jude 1.25 Romains 3.30
30 nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.
Deutéronome 6.5
31 Na ya pili ndiyo hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi.
Galates 5.14 Romains 13.8-13.9 Matthieu 19.18-19.19 Lévitique 19.18 1 Jean 4.21
32 Yule mwandishi akamwambia, Hakika, Mwalimu, umesema vema ya kwamba Mungu ni mmoja, wala hakuna mwingine ila yeye;
Esaïe 46.9 Esaïe 45.14 Deutéronome 4.39 Esaïe 44.8 Deutéronome 4.35
33 na kumpenda yeye kwa moyo wote, na kwa ufahamu wote, na kwa nguvu zote, na kumpenda jirani kama nafsi yako, kwafaa kuliko sadaka nzima za kuteketezwa na dhahibu zote pia.
Osée 6.6 1 Samuel 15.22 Michée 6.6-6.8 Matthieu 9.13 Matthieu 12.7
34 Naye Yesu, alipoona kwamba amejibu kwa busara, alimwambia, Wewe hu mbali na ufalme wa Mungu. Wala hakuthubutu mtu kumsaili neno tena tokea hapo.
Matthieu 22.46 Luc 20.40 Tite 1.9-1.11 Colossiens 4.6 Romains 3.19-3.20

Reproches de Jésus aux chefs religieux

35 Hata Yesu alipokuwa akifundisha katika hekalu, alijibu, akasema, Husemaje waandishi ya kwamba Kristo ni Mwana wa Daudi?
Luc 20.41-20.44 Matthieu 26.55 Jean 18.20 Matthieu 22.41-22.45 Jean 7.42
36 Daudi mwenyewe alisema, kwa uweza wa Roho Mtakatifu, Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwawekapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako.
Psaumes 110.1 1 Corinthiens 15.25 Hébreux 1.13 Matthieu 22.43-22.45 Hébreux 10.12-10.13
37 Daudi mwenyewe asema ni Bwana; basi amekuwaje mwanawe? Na mkutano mkubwa walikuwa wakimsikiliza kwa furaha.
Romains 1.3-1.4 Matthieu 11.25 Jean 7.46-7.49 Apocalypse 22.16 Matthieu 21.46
38 Akawaambia katika mafundisho yake, Jihadharini na waandishi, wapendao kutembea wamevaa mavazi marefu, na kusalimiwa masokoni,
Luc 11.43 Matthieu 23.1-23.7 Luc 20.45-20.47 3 Jean 1.9 Marc 4.2
39 na kuketi mbele katika masinagogi, na viti vya mbele katika karamu;
Jacques 2.2-2.3
40 ambao hula nyumba za wajane, na kwa unafiki husali sala ndefu; hawa watapata hukumu iliyo kubwa.
Matthieu 23.13 Luc 20.47 Matthieu 6.7 Matthieu 23.33 Michée 3.1-3.4
41 Naye akaketi kulielekea sanduku la hazina, akatazama jinsi mkutano watiavyo mapesa katika sanduku. Matajiri wengi wakatia mengi.
Jean 8.20 2 Rois 12.9 Luc 21.1-21.4 Matthieu 27.6
42 Akaja mwanamke mmoja, mjane, maskini, akatia senti mbili, kiasi cha nusu pesa.
43 Akawaita wanafunzi wake, akawaambia, Amin, nawaambia, Huyu mjane maskini ametia zaidi kuliko wote wanaotia katika sanduku la hazina;
2 Corinthiens 8.2 2 Corinthiens 9.6-9.8 2 Corinthiens 8.12 Exode 35.21-35.29 Actes 11.29
44 maana hao wote walitia baadhi ya mali iliyowazidi; bali huyu katika umaskini wake ametia vyote alivyokuwa navyo, ndiyo riziki yake yote pia.
Luc 8.43 1 Jean 3.17 Deutéronome 24.6 Esdras 2.68-2.69 Marc 14.8

Cette Bible est dans le domaine public.