Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 2.16
Bible en Swahili de l’est


Les mages et Hérode

1 Yesu alipozaliwa katika Bethlehemu ya Uyahudi zamani za mfalme Herode, tazama, mamajusi wa mashariki walifika Yerusalemu, wakisema,
Luc 2.4-2.7 Michée 5.2 Genèse 49.10 Luc 1.5 Daniel 9.24-9.25
2 Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia.
Nombres 24.17 Jérémie 23.5 Zacharie 9.9 Esaïe 9.6-9.7 Jean 18.37
3 Basi mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, na Yerusalemu pia pamoja naye.
Matthieu 8.29 Matthieu 23.37 Actes 5.24-5.28 Actes 17.6-17.7 1 Rois 18.17-18.18
4 Akakusanya wakuu wa makuhani wote na waandishi wa watu, akatafuta habari kwao, Kristo azaliwa wapi?
Actes 23.9 Jérémie 8.8 Actes 6.12 Esdras 7.6 Matthieu 7.29
5 Nao wakamwambia, Katika Bethlehemu ya Uyahudi; kwa maana ndivyo ilivyoandikwa na nabii,
Genèse 35.19 Josué 19.15 Ruth 1.19 Jean 7.42 Ruth 4.11
6 Nawe Bethlehemu, katika nchi ya Yuda, Hu mdogo kamwe katika majumbe wa Yuda; Kwa kuwa kwako atatoka mtawala Atakayewachunga watu wangu Israeli.
Michée 5.2 Apocalypse 11.15 Jean 7.42 Esaïe 40.11 Apocalypse 2.27
7 Kisha Herode akawaita wale mamajusi faraghani, akapata kwao hakika ya muda tangu ilipoonekana ile nyota.
1 Samuel 18.21 Psaumes 83.3-83.4 Exode 1.10 Psaumes 64.4-64.6 Psaumes 10.9-10.10
8 Akawapeleka Bethlehemu, akasema, Shikeni njia, mkaulize sana mambo ya mtoto; na mkiisha kumwona, nileteeni habari, ili mimi nami niende nimsujudie.
Proverbes 21.30 Job 5.12-5.13 1 Rois 19.2 Matthieu 26.48-26.49 2 Samuel 15.7-15.12
9 Nao waliposikia maneno ya mfalme, walishika njia; na tazama, ile nyota waliyoiona mashariki ikawatangulia, hata ikaenda ikasimama juu ya mahali alipokuwapo mtoto.
Matthieu 2.2 Psaumes 25.12 Proverbes 2.1-2.6 2 Pierre 1.19 Proverbes 8.17
10 Nao walipoiona ile nyota, walifurahi furaha kubwa mno.
Luc 2.10 Psaumes 67.4 Luc 2.20 Romains 15.9-15.13 Psaumes 105.3
11 Wakaingia nyumbani, wakamwona mtoto pamoja na Mariamu mamaye, wakaanguka wakamsujudia; nao walipokwisha kufungua hazina zao, wakamtolea tunu; dhahabu na uvumba na manemane.
Psaumes 72.10 Esaïe 60.6 Matthieu 2.2 Apocalypse 22.8-22.10 Nombres 7.86
12 Nao wakiisha kuonywa na Mungu katika ndoto wasimrudie Herode, wakaenda zao kwao kwa njia nyingine.
Matthieu 2.22 Matthieu 27.19 Exode 1.17 Matthieu 2.13 Matthieu 1.20
13 Na hao walipokwisha kwenda zao, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto, akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mama yake, ukimbilie Misri, ukae huko hata nikuambie; kwa maana Herode anataka kumtafuta mtoto amwangamize.
Exode 1.22 Actes 12.11 Matthieu 2.16 Matthieu 1.20 Actes 10.7
14 Akaondoka akamchukua mtoto na mama yake usiku, akaenda zake Misri;
Matthieu 2.20-2.21 Actes 26.21 Matthieu 1.24
15 akakaa huko hata alipokufa Herode; ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii, akisema, Kutoka Misri nalimwita mwanangu.
Osée 11.1 Exode 4.22 Jean 19.28 Jean 19.36 Matthieu 1.22
16 Ndipo Herode, alipoona ya kuwa amedhihakiwa na wale mamajusi, alighadhabika sana, akatuma watu akawaua watoto wote wanaume waliokuwako huko Bethlehemu na viungani mwake mwote, tangu wenye miaka miwili na waliopungua, kwa muda ule aliouhakikisha kwa wale mamajusi.
Esaïe 59.7 Juges 16.10 Proverbes 28.17 2 Rois 8.12 Nombres 24.10
17 Ndipo lilipotimia neno lililonenwa na nabii Yeremia, akisema,
18 Sauti ilisikiwa Rama, Kilio, na maombolezo mengi, Raheli akiwalilia watoto wake, Asikubali kufarijiwa, kwa kuwa hawako.
Jérémie 31.15 Jérémie 9.17-9.21 Genèse 42.36 Ezéchiel 2.10 Jérémie 4.31
19 Hata alipofariki Herode, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto huko Misri,
Matthieu 1.20 Psaumes 76.10 Ezéchiel 11.16 Psaumes 139.7 Matthieu 2.22
20 akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mamaye, ushike njia kwenda nchi ya Israeli; kwa maana wamekufa walioitafuta roho ya mtoto.
Exode 4.19 Proverbes 3.5-3.6 1 Rois 11.40 1 Rois 11.21 Matthieu 2.13
21 Akaondoka akamchukua mtoto na mamaye, akafika nchi ya Israeli.
Hébreux 11.8 Genèse 6.22
22 Lakini aliposikia ya kwamba Arkelao anamiliki huko Uyahudi mahali pa Herode babaye, aliogopa kwenda huko; naye akiisha kuonywa katika ndoto, akasafiri pande za Galilaya,
Luc 2.39 Matthieu 1.20 Genèse 19.17-19.21 Psaumes 73.24 Psaumes 107.6-107.7
23 akaenda, akakaa katika mji ulioitwa Nazareti; ili litimie neno lililonenwa na manabii, Ataitwa Mnazorayo.
Juges 13.5 Jean 1.45-1.46 Jean 18.7 Luc 1.26 Jean 19.19

Cette Bible est dans le domaine public.