Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Daniel 5.2
Bible en Swahili de l’est


Chute de Babylone

1 Belshaza, mfalme, aliwafanyia wakuu wake elfu karamu kubwa akanywa divai mbele ya elfu hao.
Esther 1.3 Esaïe 22.12 Esaïe 22.14 Esaïe 21.4-21.5 Marc 6.21-6.22
2 Belshaza, alipokuwa akionja ile divai, akaamuru wavilete vile vyombo vya dhahabu na fedha, ambavyo baba yake, Nebukadreza, alivitoa katika hekalu lililokuwako Yerusalemu; ili kwamba mfalme, na wakuu wake, na wake zake, na masuria wake, wapate kuvinywea.
Daniel 1.2 2 Rois 24.13 Jérémie 52.19 Esdras 1.7-1.11 2 Rois 25.15
3 Basi wakavileta vile vyombo vya dhahabu, vilivyotolewa katika hekalu la nyumba ya Mungu lililokuwako Yerusalemu; na mfalme na wakuu wake, na wake zake, na masuria wake, wakavinywea.
4 Wakanywa divai, wakaisifu miungu ya dhahabu, na ya fedha, na ya shaba, na ya chuma, na ya mti, na ya mawe.
Daniel 5.23 Habakuk 2.19 Esaïe 40.19-40.20 Psaumes 135.15-135.18 Esaïe 42.8
5 Saa iyo hiyo vikatokea vidole vya mkono wa mwanadamu, vikaandika katika chokaa ya ukuta wa nyumba ya enzi ya mfalme, mahali palipokikabili kinara; naye mfalme akakiona kitanga cha ule mkono ulioandika.
Daniel 4.31 Job 20.5 Daniel 5.24-5.28 Proverbes 29.1 Apocalypse 20.12-20.15
6 Ndipo uso wa mfalme ukambadilika; fikira zake zikamfadhaisha; viungo vya viuno vyake vikalegea; magoti yake yakagongana.
Daniel 7.28 Nahum 2.10 Ezéchiel 7.17 Daniel 4.5 Psaumes 69.23
7 Mfalme akalia kwa sauti kubwa, akaamuru waletwe wachawi, na Wakaldayo na wanajimu. Mfalme akanena, akawaambia wenye hekima wa Babeli, mtu awaye yote atakayesoma maandiko haya, na kunionyesha tafsiri yake, atavikwa mavazi ya rangi ya zambarau, na kuwa na mkufu wa dhahabu shingoni mwake, naye atakuwa mtu wa tatu katika ufalme.
Daniel 5.29 Daniel 5.16 Daniel 6.2-6.3 Daniel 2.48 Daniel 2.6
8 Basi wakaingia wenye hekima wote wa mfalme; lakini hawakuweza kuyasoma yale maandiko, wala kumjulisha mfalme tafsiri yake.
Daniel 2.27 Daniel 4.7 Genèse 41.8 Daniel 5.15 Esaïe 47.12-47.15
9 Ndipo mfalme Belshaza akahangaika sana, uso wake ukambadilika, na wakuu wake wakaona fadhaa.
Daniel 5.6 Daniel 2.1 Jérémie 6.24 Esaïe 13.6-13.8 Esaïe 21.2-21.4
10 Basi malkia, kwa sababu ya maneno ya mfalme na ya wakuu wake, akaingia katika nyumba ya karamu; malkia akanena, akasema, Ee mfalme, uishi milele; fikira zako zisikufadhaishe; wala uso wako usibadilike.
Daniel 3.9 Daniel 6.6 Daniel 2.4 Genèse 35.17-35.18 1 Samuel 4.20-4.22
11 Yuko mtu katika ufalme wako, ambaye roho ya miungu watakatifu inakaa ndani yake; na katika siku za baba yako nuru na ufahamu na hekima zilionekana ndani yake; na mfalme Nebukadreza, baba yako, naam, mfalme, baba yako, akamfanya kuwa mkuu wa waganga, na wachawi, na Wakaldayo, na wanajimu;
Daniel 4.8-4.9 Daniel 2.47-2.48 Daniel 4.18 Genèse 41.11-41.15 Actes 16.16
12 kwa kuwa roho njema kupita kiasi, na maarifa, na ufahamu, na uwezo wa kufasiri ndoto, na kufunua maneno ya fumbo, na kufungua mafundo, zilionekana katika Danielii huyo, ambaye mfalme alimwita Belteshaza. Basi na aitwe Danielii, naye ataionyesha tafsiri.
Daniel 5.16 Daniel 5.14 Daniel 1.7 Daniel 6.3 Daniel 4.8
13 Ndipo Danielii akaletwa mbele ya mfalme. Na Mfalme akanena, akamwambia Danielii, Je! Wewe ndiwe Danielii yule, aliye mmoja wa wana wa Yuda waliohamishwa, ambao mfalme, baba yangu, aliwaleta huku toka Yerusalemu?
Daniel 5.11 Daniel 6.13 Daniel 2.25 Esdras 6.19-6.20 Esdras 4.1
14 Nimesikia habari zako, kwamba roho ya miungu imo ndani yako, na kwamba nuru na ufahamu na akili bora zimeonekana kwako.
Daniel 5.11-5.12
15 Basi sasa, watu wenye hekima na wachawi wameletwa mbele yangu, wapate kulisoma andiko hili, na kunijulisha tafsiri yake; lakini hawakuweza kunijulisha tafsiri ya jambo hili.
Daniel 5.7-5.8 Esaïe 47.12 Esaïe 29.10-29.12 Daniel 2.3-2.11
16 Lakini nimesikia habari zako, kwamba waweza kuleta tafsiri, na kufumbua mafumbo; haya! Kama ukiweza kulisoma andiko hili, na kunijulisha tafsiri yake, utavikwa mavazi ya rangi ya zambarau, na kuwa na mkufu wa dhahabu shingoni mwako, nawe utakuwa mtu wa tatu katika ufalme.
Daniel 5.7 Daniel 5.29 Genèse 40.8 Actes 8.18
17 Ndipo Danielii akajibu, akasema mbele ya mfalme; Zawadi zako zishike wewe mwenyewe; na thawabu zako mpe mtu mwingine; walakini nitamsomea mfalme maandiko haya, na kumjulisha tafsiri yake.
2 Rois 5.16 Daniel 2.6 Genèse 14.23 Actes 8.20 Daniel 5.29
18 Kwa habari zako, Ee mfalme, Mungu Aliye juu alimpa Nebukadreza, baba yako, ufalme, na ukuu, na fahari, na utukufu;
Daniel 2.37-2.38 Daniel 4.17 Psaumes 47.2 Deutéronome 32.8 Actes 26.19
19 na kwa sababu ya ule ukuu aliompa, watu wa kabila zote, na mataifa, na lugha, wakatetemeka na kuogopa mbele yake; aliyetaka kumwua alimwua; na aliyetaka kumwacha hai, alimwacha hai; aliyetaka kumtukuza, alimtukuza; na aliyetaka kumshusha, alimshusha.
Daniel 3.6 Daniel 2.12-2.13 Daniel 3.4 Daniel 3.20-3.21 Daniel 4.22
20 Lakini moyo wake ulipoinuliwa, na roho yake ilipokuwa ngumu akatenda kwa kiburi, aliuzuliwa katika kiti chake cha enzi, nao wakamwondolea utukufu wake.
Jérémie 13.18 2 Chroniques 36.13 Exode 9.17 2 Rois 17.14 Job 40.11-40.12
21 Akafukuzwa mbali na wanadamu, moyo wake ukafanywa kuwa kama moyo wa mnyama, na makao yake yalikuwa pamoja na punda-mwitu; akalishwa majani kama ng’ombe, mwili wake ukalowa maji kwa umande wa mbinguni; hata alipojua ya kuwa Mungu Aliye juu ndiye anayetawala katika ufalme wa wanadamu, na ya kuwa humweka juu yake yeye amtakaye, awaye yote.
Daniel 4.25 Daniel 4.35 Ezéchiel 17.24 Daniel 4.17 Job 30.3-30.7
22 Na wewe, mwanawe, Ee Belshaza, hukujinyenyekeza moyo wako, ijapokuwa ulijua hayo yote.
2 Chroniques 33.23 Exode 10.3 2 Chroniques 36.12 1 Pierre 5.5-5.6 Jacques 4.6
23 Bali umejiinua juu ya Bwana wa mbingu; nao wamevileta vyombo vya nyumba yake mbele yako; na wewe, na wakuu wako, na wake zako, na masuria wako, mmevinywea; nawe umeisifu miungu ya fedha na ya dhahabu na ya shaba, na ya chuma, na ya mti, na ya mawe; wasioona, wala kusikia, wala kujua neno lo lote; na Mungu yule, ambaye pumzi yako i mkononi mwake, na njia zako zote ni zake, hukumtukuza.
Job 12.10 Jérémie 10.23 Job 31.4 Jérémie 50.29 Daniel 4.37
24 Ndipo kile kitanga cha ule mkono kikaletwa kutoka mbele zake, na maandiko haya yameandikwa.
Daniel 5.5
25 Na maandiko yaliyoandikwa ni haya; MENE, MENE, TEKELI, NA PERESI.
26 Na tafsiri ya maneno haya ni hii; MENE, Mungu ameuhesabu ufalme wako na kuukomesha.
Jérémie 27.7 Jérémie 25.11-25.12 Job 14.14 Esaïe 47.1-47.15 Daniel 9.2
27 TEKELI, umepimwa katika mizani nawe umeonekana kuwa umepunguka.
Psaumes 62.9 Job 31.6 Ezéchiel 22.18-22.20 Matthieu 22.11-22.12 Jérémie 6.30
28 PERESI, ufalme wako umegawanyika, nao wamepewa Wamedi na Waajemi.
Esaïe 13.17 Daniel 6.28 Esaïe 21.2 Daniel 5.31 Daniel 9.1
29 Ndipo Belshaza akatoa amri, nao wakamvika Danielii mavazi ya rangi ya zambarau, wakatia mkufu wa dhahabu shingoni mwake, wakapiga mbiu kutangaza habari zake, ya kwamba yeye ni mtu wa tatu katika ufalme.
Daniel 5.7 Daniel 5.16
30 Usiku uo huo Belshaza, mfalme wa Wakaldayo, akauawa.
Jérémie 51.31 Jérémie 51.57 Jérémie 51.39 Esaïe 21.4-21.9 Esaïe 47.9
31 Na Dario, Mmedi, akaupokea ufalme, naye umri wake alikuwa na miaka sitini na miwili.
Daniel 9.1 Daniel 6.1

Cette Bible est dans le domaine public.