Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 46
Bible en Swahili de l’est


Prescriptions pour le service du temple

1 Bwana MUNGU asema hivi; Lango la ua wa ndani, lielekealo upande wa mashariki litafungwa siku sita za kazi; lakini siku ya sabato litafunguliwa, na siku ya mwezi mpya litafunguliwa.
Esaïe 66.23 Ezéchiel 44.1-44.2 Exode 20.9 Luc 13.14 Ezéchiel 8.16
2 Naye mkuu ataingia kwa njia ya ukumbi wa lango lile, upande wa nje, naye atasimama karibu na mwimo wa lango, nao makuhani wataitengeneza sadaka yake ya kuteketezwa, na sadaka zake za amani, naye ataabudu penye kizingiti cha lango; kisha atatoka; lakini lango lile halitafungwa hata wakati wa jioni.
Ezéchiel 44.3 Ezéchiel 46.8 Matthieu 26.39 2 Chroniques 23.13 2 Chroniques 34.31
3 Watu wa nchi nao wataabudu mbele ya mlango wa lile lango mbele za Bwana, siku za sabato, na siku za mwezi mpya.
Luc 1.10 Jean 10.9 Hébreux 10.19-10.22
4 Nayo sadaka ya kuteketezwa, ambayo mkuu atamtolea Bwana siku ya sabato, itakuwa wana-kondoo sita wakamilifu, na kondoo mume mkamilifu.
Ezéchiel 45.17 Nombres 28.9-28.10
5 Na sadaka ya unga itakuwa efa moja kwa kondoo mume, na sadaka ya unga kwa wale wana-kondoo, kiasi awezacho kutoa, na hini moja ya mafuta kwa efa moja.
Ezéchiel 45.24 Ezéchiel 46.7 Nombres 28.12 Deutéronome 16.17 Nombres 6.21
6 Na siku ya mwezi mpya itakuwa ni ng’ombe mume mchanga mkamilifu; na wana-kondoo sita, na kondoo mume; nao watakuwa wakamilifu.
Ezéchiel 46.1
7 Naye atatengeneza sadaka ya unga, efa moja kwa ng’ombe mume, na efa moja kwa kondoo mume, na kwa wale wana-kondoo, kwa kiasi awezacho kutoa, na hini moja ya mafuta kwa efa moja.
Ezéchiel 46.5
8 Naye mkuu atakapoingia, ataingia kwa njia ya ukumbi wa lango lile, naye atatoka kwa njia iyo hiyo.
Ezéchiel 46.2 Colossiens 1.18 Ezéchiel 44.1-44.3
9 Lakini watu wa nchi watakapokuja mbele za Bwana katika sikukuu zilizoamriwa, yeye aingiaye kwa njia ya lango la upande wa kaskazini ili kuabudu, atatoka kwa njia ya lango la upande wa kusini; na yeye aingiaye kwa njia ya lango la upande wa kusini, atatoka kwa njia ya lango la upande wa kaskazini; hatarudi kwa njia ya lango aliloingia kwalo, lakini atatoka kwa kwenda mbele moja kwa moja.
Deutéronome 16.16 Psaumes 84.7 Exode 34.23 Exode 23.14-23.17 Ezéchiel 1.17
10 Naye mkuu atakapoingia, ataingia katikati yao, nao, watakapotoka, watatoka wote pamoja.
Psaumes 42.4 1 Chroniques 29.20 1 Chroniques 29.22 Matthieu 28.20 Apocalypse 2.1
11 Na katika sikukuu hizo, na sikukuu nyingine zilizoamriwa, sadaka ya unga itakuwa efa moja kwa ng’ombe mmoja, na efa moja kwa kondoo mume mmoja, na kwa wale wana-kondoo kiasi awezacho kutoa, na hini moja ya mafuta kwa efa moja.
Ezéchiel 46.5 Ezéchiel 46.7 Lévitique 23.1-23.44 Nombres 15.1-15.41 Nombres 28.1-28.29
12 Naye mkuu atakapotengeneza sadaka atoayo kwa hiari yake mwenyewe, sadaka ya kuteketezwa, au sadaka za amani, ziwe sadaka amtoleazo Bwana kwa hiari yake mwenyewe, mtu mmoja atamfungulia lango lile lielekealo upande wa mashariki, naye ataitengeneza sadaka yake ya kuteketezwa, na sadaka zake za amani, kama afanyavyo siku ya sabato; kisha atatoka; na baada ya kutoka kwake mtu mmoja atalifunga lango.
Ezéchiel 46.1-46.2 Ezéchiel 45.17 Ezéchiel 46.8 2 Chroniques 29.31 Lévitique 23.38
13 Nawe utatengeneza mwana-kondoo wa mwaka wa kwanza, mkamilifu, kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana kila siku; kila siku asubuhi utamtengeneza.
Esaïe 50.4 Nombres 28.10 Psaumes 92.2 Lévitique 12.6 Nombres 28.3-28.8
14 Nawe utatengeneza sadaka ya unga pamoja nayo kila siku asubuhi, sehemu ya sita ya efa moja, na sehemu ya tatu ya hini moja ya mafuta; kuchanganya na unga ule mzuri; sadaka ya unga kwa Bwana daima, kwa amri ya milele.
Nombres 28.5
15 Hivyo ndivyo watakavyomtengeneza mwana-kondoo, na sadaka ya unga, na mafuta, kila siku asubuhi, kuwa sadaka ya kuteketezwa ya daima.
Exode 29.42 Nombres 28.6 Hébreux 9.26 Hébreux 10.1-10.10 Hébreux 7.27
16 Bwana MUNGU asema hivi; Mkuu akimpa mwanawe awaye yote zawadi, ni urithi wake, itakuwa mali ya wanawe; ni milki yao kwa kurithiwa.
2 Chroniques 21.3 Luc 10.42 Galates 4.7 Genèse 25.5-25.6 Jean 8.35-8.36
17 Bali akimpa mmoja wa watumishi wake baadhi ya urithi wake, itakuwa mali yake mpaka mwaka wa kuacha huru; ndipo itakapomrudia mkuu; lakini urithi wake, huo utakuwa wa wanawe.
Lévitique 25.10 Matthieu 25.14-25.29 Luc 19.25-19.26 Galates 4.30-4.31
18 Tena mkuu hatawaondolea watu urithi wao, hata kuwatoa kwa nguvu katika milki yao; atawapa wanawe urithi katika mali yake mwenyewe, watu wangu wasije wakatawanyika, kila mtu mbali na milki yake.
Ezéchiel 45.8 1 Rois 21.19 Ezéchiel 22.27 Psaumes 78.72 Ephésiens 4.8
19 Ndipo akanileta kati ya maingilio, yaliyokuwa kando ya lango, mpaka vyumba vitakatifu vya makuhani, vilivyoelekea upande wa kaskazini; na tazama, palikuwa na mahali, upande wa nyuma ulioelekea magharibi.
Ezéchiel 42.9 Ezéchiel 44.4-44.5 Ezéchiel 40.44-40.46
20 Akaniambia, Hapa ndipo mahali pa makuhani, watakapoitokosa sadaka ya hatia, na sadaka ya dhambi, watakapoioka sadaka ya unga; kusudi wasizilete nje katika ua wa nje, na kuwatakasa watu.
2 Chroniques 35.13 Ezéchiel 44.19 Ezéchiel 44.29 Lévitique 2.4-2.7 Lévitique 7.1-7.38
21 Kisha akanileta mpaka ua wa nje, akanipitisha karibu na pembe nne za ua huo; na tazama, katika kila pembe ya ua huo palikuwa na kiwanja.
22 Katika pembe nne za ua huo palikuwa na viwanja vilivyoungana, urefu wake dhiraa arobaini, na upana wake thelathini; viwanja hivyo vinne vya pembeni vilikuwa vya kipimo kimoja.
23 Tena palikuwa na safu ndani yake pande zote, kuvizunguka vile viwanja vinne; tena palifanywa meko ya kutokosea, chini ya safu pande zote.
24 Ndipo akaniambia, Hizi ni nyumba za kutokosea, ambamo wahudumu wa nyumba watatokosa sadaka za watu.
Ezéchiel 46.20 Matthieu 24.45 Jean 21.15-21.17 1 Pierre 5.2

Cette Bible est dans le domaine public.