Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 25.16
Bible en Swahili de l’est


70 ans d’exil

1 Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, katika habari za watu wote wa Yuda; katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda mwaka ule ndio mwaka wa kwanza wa Nebukadreza, mfalme wa Babeli;
Jérémie 36.1 2 Rois 24.1-24.2 Daniel 1.1 Jérémie 46.2
2 ambalo Yeremia, nabii, aliwaambia watu wote wa Yuda, na wenyeji wote wa Yerusalemu, kusema,
Jérémie 18.11 Jérémie 38.1-38.2 Jérémie 35.13 Jérémie 19.14-19.15 Jérémie 26.2
3 Tangu mwaka wa kumi na tatu wa kutawala kwake Yosia, mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda, hata siku hii ya leo, miaka hii ishirini na mitatu, neno la Bwana limenijia, nami nimesema nanyi, nikiamka mapema na kusema; lakini ninyi hamkusikiliza.
Jérémie 11.7 Jérémie 1.2 Jérémie 7.13 Jérémie 29.19 Jérémie 26.5
4 Naye Bwana ametuma kwenu watumishi wake wote, hao manabii, akiamka mapema na kuwatuma, lakini ninyi hamkusikiliza, wala hamkutega masikio yenu, msikilize.
Jérémie 25.3 Jérémie 26.5 Jérémie 19.15 Jérémie 11.7-11.10 Jérémie 17.23
5 Akasema, Rudini sasa, kila mtu na aiache njia yake mbaya; uacheni uovu wa matendo yenu, mkae katika nchi ambayo Bwana aliwapa, ninyi na baba zenu, tangu zamani za kale na hata milele;
Jérémie 7.7 Genèse 17.8 Jérémie 35.15 Esaïe 55.6-55.7 Jonas 3.8-3.10
6 wala msiwafuate miungu mingine, ili kuwatumikia na kuwasujudia, wala msinikasirishe kwa kazi ya mikono yenu; basi, mimi sitawadhuru ninyi kwa dhara lo lote.
Deutéronome 8.19 Jérémie 35.15 Jérémie 7.6 2 Rois 17.35 Deutéronome 6.14
7 Lakini ninyi hamkunisikiliza, asema Bwana; ili mnikasirishe kwa kazi ya mikono yenu, na kujidhuru nafsi zenu.
2 Rois 21.15 Deutéronome 32.21 Jérémie 32.30-32.33 Néhémie 9.26 2 Rois 17.17
8 Basi Bwana wa majeshi asema hivi, Kwa kuwa hamkuyasikiliza maneno yangu,
9 angalieni, nitapeleka watu na kuzitwaa jamaa zote za upande wa kaskazini, asema Bwana, nami nitatuma ujumbe kwa Nebukadreza, mfalme wa Babeli, mtumishi wangu, nami nitawaleta juu ya nchi hii, na juu yao wakaao ndani yake, na juu ya mataifa haya yote yaliyopo pande zote; nami nitawaangamiza kabisa, na kuwafanya kitu cha kushangaza, na kitu cha kuzomewa, na ukiwa wa daima.
Jérémie 18.16 Jérémie 1.15 Esaïe 13.3 Jérémie 43.10 1 Rois 9.7-9.8
10 Tena, nitawaondolea sauti ya kicheko, na sauti ya furaha, sauti ya bwana arusi, na sauti ya bibi arusi, sauti ya mawe ya kusagia, na nuru ya mishumaa.
Jérémie 7.34 Apocalypse 18.22-18.23 Ezéchiel 26.13 Jérémie 16.9 Jérémie 33.10-33.11
11 Na nchi hii yote pia itakuwa ukiwa, na kitu cha kushangaza; nayo mataifa haya watamtumikia mfalme wa Babeli miaka sabini.
Daniel 9.2 Zacharie 7.5 Jérémie 12.11-12.12 Zacharie 1.12 Jérémie 4.27
12 Na itakuwa miaka hiyo sabini itakapotimia, nitamwadhibu mfalme wa Babeli, na taifa lile, asema Bwana, kwa sababu ya uovu wao, nayo nchi ya Wakaldayo pia; nami nitaifanya kuwa ukiwa wa milele.
Esaïe 13.19 Daniel 9.2 Jérémie 29.10 Jérémie 51.62-51.64 Esaïe 14.23
13 Nami nitaleta juu ya nchi ile maneno yangu yote niliyoyanena juu yake, naam, yote yaliyoandikwa ndani ya kitabu hiki, aliyotabiri Yeremia juu ya mataifa haya yote.
Jérémie 1.5 Jérémie 1.10 Apocalypse 10.11 Daniel 5.28 Daniel 5.31
14 Kwa maana mataifa mengi na wafalme wakuu watawatumikisha; naam, hao pia; nami nitawalipa kwa kadiri ya matendo yao, na kwa kadiri ya kazi ya mikono yao.
Jérémie 51.6 Jérémie 27.7 Jérémie 50.9 Jérémie 50.41 Esaïe 14.2
15 Maana Bwana, Mungu wa Israeli, aniambia hivi, Pokea kikombe cha divai ya ghadhabu hii mkononi mwangu, ukawanyweshe mataifa yote, ambao nitakupeleka kwao;
Esaïe 51.17 Psaumes 75.8 Apocalypse 14.10 Job 21.20 Esaïe 51.22
16 nao watakunywa, na kulewalewa, na kufanya wazimu, kwa sababu ya upanga nitakaoupeleka kati yao.
Nahum 3.11 Jérémie 51.7 Lamentations 4.21 Apocalypse 18.3 Apocalypse 14.8
17 Ndipo nikakipokea kikombe kile mkononi mwa Bwana, nikawanywesha mataifa yote, ambao Bwana alinipeleka kwao;
Jérémie 1.10 Jérémie 25.28 Jérémie 27.3 Ezéchiel 43.3 Jérémie 46.1-46.28
18 yaani, Yerusalemu, na miji ya Yuda, na wafalme wake, na wakuu wake, ili kuwafanya kuwa ukiwa, na ajabu, na mazomeo, na laana; vile vile kama ilivyo leo;
Psaumes 60.3 Jérémie 24.9 Jérémie 44.22 1 Pierre 4.17 Néhémie 9.36
19 Farao, mfalme wa Misri, na watumishi wake na wakuu wake na watu wake wote;
Nahum 3.8-3.10 Jérémie 46.2 Jérémie 46.13-46.26 Ezéchiel 29.1-29.21 Jérémie 43.9-43.11
20 na watu wote waliochanganyika pamoja, na wafalme wote wa nchi ya Uzi, na wafalme wote wa nchi ya Wafilisti, na Ashkeloni, na Gaza, na Ekroni, na mabaki ya Ashdodi;
Job 1.1 Lamentations 4.21 Esaïe 20.1 Jérémie 50.37 Ezéchiel 30.5
21 Edomu, na Moabu, na wana wa Amoni;
Jérémie 48.1-49.22 Jérémie 9.26 Psaumes 137.7 Abdias 1.1-1.16 Amos 1.11-2.3
22 na wafalme wote wa Tiro, na wafalme wote wa Sidoni, na wafalme wote wa kisiwa kilicho ng’ambo ya pili ya bahari;
Jérémie 47.4 Amos 1.3-1.5 Ezéchiel 32.30 Ezéchiel 26.1-26.21 Jérémie 27.3
23 Dedani, na Tema, na Buzi, na watu wote wakatao denge;
Jérémie 9.26 Jérémie 49.32 Jérémie 49.8 Genèse 22.21 Job 6.19
24 na wafalme wote wa Arabuni, na wafalme wote wa watu waliochanganyika wakaao jangwani;
2 Chroniques 9.14 Jérémie 25.20 Jérémie 50.37 Ezéchiel 30.5 Ezéchiel 27.21
25 na wafalme wote wa Zimri, na wafalme wote wa Elamu, na wafalme wote wa Wamedi;
Esaïe 11.11 Genèse 10.22 Jérémie 51.11 Jérémie 51.28 Esaïe 13.17
26 na wafalme wote wa kaskazini, walio mbali na walio karibu, wote pamoja; na wafalme wote wa dunia, wakaao juu ya uso wa dunia; na mfalme wa Sheshaki atakunywa baada yao.
Jérémie 51.41 Jérémie 25.9 Jérémie 50.1-50.46 Daniel 5.1-5.31 Esaïe 47.1-47.15
27 Nawe utawaambia hivi, Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nyweni, na kulewa, na kutapika, na kuanguka msiinuke tena, kwa sababu ya upanga nitakaoupeleka kati yenu.
Jérémie 25.16 Habakuk 2.16 Lamentations 4.21 Esaïe 51.21 Ezéchiel 21.4-21.5
28 Tena itakuwa, kama wakikataa kukipokea kikombe kile mkononi mwako, wanywe, ndipo utakapowaambia, Bwana wa majeshi asema hivi, Lazima mtakunywa.
Job 34.33 Esaïe 46.10-46.11 Jérémie 4.28 Jérémie 51.29 Daniel 4.35
29 Maana angalieni, ninaanza kutenda mabaya katika mji uitwao kwa jina langu, je! Mtaachiliwa ninyi msiadhibiwe? Hamtaachiliwa msiadhibiwe; kwa maana nitauita upanga ule uwapige wote wakaao katika dunia, asema Bwana wa majeshi.
Ezéchiel 38.21 Proverbes 11.31 1 Pierre 4.17 1 Rois 8.43 Ezéchiel 9.6
30 Basi, tabiri wewe maneno haya yote juu yao, na kuwaambia, Bwana atanguruma toka juu, Naye atatoa sauti yake toka patakatifu pake; Atanguruma sana juu ya zizi lake; Atapiga kelele kama mtu akanyagaye zabibu, Juu ya wenyeji wote wa dunia.
Joël 3.16 Amos 1.2 Esaïe 42.13 Esaïe 16.9 Jérémie 48.33
31 Mshindo utafika hata mwisho wa dunia; Maana Bwana ana mashindano na mataifa, Atateta na watu wote wenye mwili; Na waovu atawatoa wauawe kwa upanga; asema Bwana.
Osée 4.1 Joël 3.2 Esaïe 66.16 Michée 6.2 Ezéchiel 20.35-20.36
32 Bwana wa majeshi asema hivi, Tazama, uovu utatokea toka taifa hata taifa, na tufani kuu itainuliwa toka pande za mwisho wa dunia.
Jérémie 23.19 Esaïe 34.2 Esaïe 30.30 Jérémie 30.23 2 Chroniques 15.6
33 Na waliouawa na Bwana siku ile watakuwapo, toka upande mmoja wa dunia hata upande wa pili; hawataliliwa, wala kukusanywa, wala kuzikwa; watakuwa samadi juu ya uso wa nchi.
Esaïe 66.16 Psaumes 79.3 Jérémie 8.2 Esaïe 5.25 Ezéchiel 39.4-39.20
34 Pigeni yowe, enyi wachungaji, na kulia; na kugaagaa katika majivu, enyi mlio hodari katika kundi; maana siku za kuuawa kwenu zimetimia kabisa, nami nitawavunja vipande vipande, nanyi mtaanguka kama chombo cha anasa.
Jérémie 6.26 Jérémie 25.23 Jacques 5.1-5.2 Jérémie 3.19 Lamentations 4.21
35 Nao wachungaji watakuwa hawana njia ya kukimbia, wala walio hodari katika kundi hawataokoka.
Job 11.20 Amos 2.14 Esaïe 24.21-24.23 Jérémie 52.8-52.11 Daniel 5.30
36 Sauti ya kilio cha wachungaji, na sauti ya kupiga yowe kwao walio hodari katika kundi, kwa maana Bwana anayaharibu malisho yao.
Jérémie 4.8 Jérémie 25.34
37 Na mazizi yenye amani yamenyamazishwa, kwa sababu ya hasira kali ya Bwana.
Esaïe 27.10-27.11 Esaïe 32.14
38 Ameacha mahali pake pa kujificha, kama simba; maana nchi yao imekuwa kitu cha kushangaza, kwa sababu ya ukali wa upanga uoneao, na kwa sababu ya hasira yake kali.
Jérémie 4.7 Jérémie 5.6 Osée 13.7-13.8 Osée 5.14 Jérémie 50.44

Cette Bible est dans le domaine public.