Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 16.17
Bible en Swahili de l’est


Annonce de l’exil et de la restauration

1 Tena neno la Bwana likanijia, kusema,
Jérémie 1.2 Jérémie 1.4 Jérémie 2.1
2 Wewe hutaoa mke, wala hutakuwa na wana wala binti mahali hapa.
1 Corinthiens 7.26-7.27 Luc 21.23 Luc 23.29 Genèse 19.14 Matthieu 24.19
3 Maana Bwana asema hivi, katika habari za wana, na katika habari za binti, wazaliwao mahali hapa, na katika habari za mama zao waliowazaa, na katika habari za baba zao waliowazaa, katika nchi hii;
Jérémie 16.9 Jérémie 16.5 Jérémie 6.21
4 watakufa kwa maradhi mabaya; hawataliliwa, wala hawatazikwa; watakuwa kama samadi juu ya uso wa nchi; nao wataangamizwa kwa upanga, na kwa njaa; na mizoga yao itakuwa chakula cha ndege wa angani, na cha wanyama wa nchi.
Jérémie 25.33 Psaumes 83.10 Jérémie 34.20 Jérémie 9.22 Sophonie 1.17
5 Maana Bwana asema hivi, Usiingie ndani ya nyumba yenye matanga, wala usiende kuwaombolezea, wala kuwalilia; maana nimewaondolea watu hawa amani yangu, asema Bwana, hata fadhili zangu na rehema zangu.
Esaïe 27.11 Ezéchiel 24.16-24.23 Deutéronome 31.17 Jérémie 15.1-15.4 2 Chroniques 15.5-15.6
6 Wakubwa kwa wadogo wote pia watakufa katika nchi hii; hawatazikwa, wala watu hawatawalilia, wala kujikata-kata kwa ajili yao, wala kujinyoa kwa ajili yao;
Jérémie 41.5 Deutéronome 14.1 Lévitique 19.28 Jérémie 47.5 Jérémie 16.4
7 wala watu hawatamega mkate kwa ajili yao, wakati wa kuomboleza, ili kuwafariji kwa ajili yao waliokufa; wala watu hawatawapa kikombe cha faraja, wanywe kwa ajili ya baba yao au mama yao.
Osée 9.4 Ezéchiel 24.17 Deutéronome 26.14 Proverbes 31.6-31.7 Job 42.11
8 Wala usiingie ndani katika nyumba yenye karamu, kuketi pamoja nao, na kula na kunywa.
Ecclésiaste 7.2-7.4 Jérémie 15.17 Esaïe 22.12-22.14 Amos 6.4-6.6 Matthieu 24.38
9 Maana Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Mimi, mbele ya macho yenu, na katika siku zenu, nitaikomesha sauti ya furaha, na sauti ya kicheko, mahali hapa; sauti ya bwana arusi, na sauti ya bibi arusi.
Ezéchiel 26.13 Osée 2.11 Jérémie 7.34 Jérémie 25.10 Esaïe 24.7-24.12
10 Tena itakuwa, utakapowaonyesha watu hawa maneno haya yote, nao wakakuambia, Mbona Bwana amenena juu yetu mabaya haya makuu? Uovu wetu ni uovu gani? Na dhambi yetu, tuliyomtenda Bwana, Mungu wetu, ni nini?
Jérémie 5.19 1 Rois 9.8-9.9 Jérémie 13.22 Deutéronome 29.24-29.25 Osée 12.8
11 Ndipo utakapowaambia, Ni kwa sababu baba zenu wameniacha mimi, asema Bwana, na kuwafuata miungu mingine, na kuwatumikia, na kuwaabudu, wakaniacha mimi, wasiishike torati yangu;
Psaumes 106.35-106.41 1 Rois 9.9 1 Pierre 4.3 Jérémie 22.9 Deutéronome 29.25-29.26
12 na ninyi mmetenda mabaya kupita baba zenu; maana angalieni, mnaenenda kila mmoja wenu kwa ushupavu wa moyo wake mbaya, msinisikilize mimi;
Jérémie 7.26 Jérémie 13.10 Jérémie 9.14 Ecclésiaste 9.3 Marc 7.21
13 basi, kwa sababu hiyo, nitawatoeni katika nchi hii, na kuwaingiza katika nchi ambayo hamkuijua, wala ninyi wala baba zenu; na huko mtawatumikia miungu mingine mchana na usiku; kwa maana mimi sitawapa fadhili zangu hata kidogo.
Deutéronome 28.36 Jérémie 17.4 Deutéronome 4.26-4.28 Jérémie 15.14 2 Chroniques 7.20
14 Kwa hiyo, angalia, siku zinakuja, asema Bwana, ambapo hawatasema tena, Aishivyo Bwana, aliyewaleta wana wa Israeli toka nchi ya Misri;
Deutéronome 15.15 Jérémie 23.7-23.8 Exode 20.2 Esaïe 43.18-43.19 Osée 3.4-3.5
15 lakini, Aishivyo Bwana, aliyewaleta wana wa Israeli toka nchi ya kaskazini, na toka nchi zote alikowafukuza; nami nitawarudisha katika nchi yao wenyewe niliyowapa baba zao.
Jérémie 3.18 Jérémie 24.6 Psaumes 106.47 Esaïe 11.11-11.16 Jérémie 32.37
16 Tazama, asema Bwana, Nitatuma watu kuwaita wavuvi wengi, nao watawavua; na baada ya hayo nitatuma watu kuwaita wawindaji wengi, nao watawawinda, watoke katika kila mlima, na kila kilima, na pango za majabali.
Amos 4.2 Habakuk 1.14-1.15 Michée 7.2 1 Samuel 26.20 Amos 9.1-9.3
17 Maana macho yangu yaziangalia njia zao zote, hawakufichwa uso wangu usiwaone, wala haukusitirika uovu wao macho yangu yasiuone.
Proverbes 15.3 2 Chroniques 16.9 Jérémie 32.19 Psaumes 90.8 Hébreux 4.13
18 Nami kwanza nitawalipa uovu wao na dhambi zao maradufu, kwa kuwa wameitia unajisi nchi yangu, kwa mizoga ya vitu vyao vichukizavyo, na kuujaza urithi wangu kwa machukizo yao.
Esaïe 40.2 Ezéchiel 11.21 Apocalypse 18.6 Nombres 35.33-35.34 Jérémie 17.18
19 Ee Bwana, nguvu zangu, ngome yangu, na kimbilio langu siku ya taabu, kwako wewe watakuja mataifa yote toka ncha za dunia, wakisema, Baba zenu hawakurithi kitu ila uongo, naam, ubatili na vitu visivyofaa.
Jérémie 10.14-10.15 Esaïe 25.4 Nahum 1.7 Esaïe 49.6 Psaumes 18.1-18.2
20 Je! Mwanadamu ajifanyie miungu, wasio miungu?
Psaumes 115.4-115.8 Esaïe 37.19 Osée 8.4-8.6 Galates 4.8 Jérémie 2.11
21 Basi, tazama, nitawajulisha, mara moja hii nitawajulisha, mkono wangu, na nguvu zangu; nao watajua ya kuwa, jina langu ni YEHOVA.
Jérémie 33.2 Esaïe 43.3 Psaumes 9.16 Amos 5.8 Psaumes 83.18

Cette Bible est dans le domaine public.