Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 31.26
Bible en Swahili de l’est


Proverbes de Lemuel

Conseils d’une mère

1 Maneno ya mfalme Lemueli; mausia aliyofundishwa na mama yake.
Proverbes 6.20 2 Timothée 1.5 2 Timothée 3.15 Proverbes 1.8 Proverbes 30.1
2 Ni nini, mwanangu? Tena ni nini, mwana wa tumbo langu? Tena, ni nini mwana wa nadhiri zangu?
Esaïe 49.15 1 Samuel 1.11 1 Samuel 1.28
3 Usiwape wanawake nguvu zako; Wala moyo wako usiwape wale wawaharibuo wafalme.
Néhémie 13.26 Deutéronome 17.17 Proverbes 5.9-5.11 1 Rois 11.1 Proverbes 7.26-7.27
4 Ee Lemueli, kunywa mvinyo hakuwafai wafalme, hakuwafai wafalme; Wala haifai wakuu waseme, Ki wapi kileo?
Ecclésiaste 10.17 Proverbes 20.1 Esaïe 5.22 Habakuk 2.5 Lévitique 10.9-10.10
5 Wasije wakanywa na kuisahau sheria, Na kuipotosha hukumu ya mtu aliye taabuni.
Habakuk 2.5
6 Mpe kileo yeye aliye karibu na kupotea; Kampe divai yeye aliye na uchungu nafsini.
1 Timothée 5.23 1 Samuel 30.6 Job 3.20 Psaumes 104.15 2 Rois 4.27
7 Anywe akausahau umaskini wake; Asiikumbuke tena taabu yake.
Ephésiens 5.18
8 Fumbua kinywa chako kwa ajili yake aliye bubu; Uwatetee watu wote walioachwa peke yao;
Psaumes 82.3-82.4 Jérémie 26.16-26.19 Jérémie 26.24 Jean 7.51 1 Samuel 22.14-22.15
9 Fumbua kinywa chako, uhukumu kwa haki; Uwapatie maskini na wahitaji haki yao.
Esaïe 1.17 Deutéronome 1.16 Lévitique 19.15 Job 29.15-29.16 Jérémie 22.15-22.16

Une femme de valeur

10 Mke mwema, ni nani awezaye kumwona? Maana kima chake chapita kima cha marijani.
Proverbes 19.14 Proverbes 12.4 Proverbes 18.22 Ruth 3.11 Proverbes 3.15
11 Moyo wa mumewe humwamini, Wala hatakosa kupata mapato.
2 Rois 4.9-4.10 1 Pierre 3.1-3.7 2 Rois 4.22-4.23
12 Humtendea mema wala si mabaya, Siku zote za maisha yake.
1 Samuel 25.26-25.27 1 Samuel 25.18-25.22
13 Hutafuta sufu na kitani; Hufanya kazi yake ya mikono kwa moyo.
1 Timothée 5.10 Genèse 24.13-24.14 Ruth 2.23 Esaïe 32.9-32.11 Esaïe 3.16-3.24
14 Afanana na merikebu za biashara; Huleta chakula chake kutoka mbali.
1 Rois 9.26-9.28 Proverbes 31.24 Ezéchiel 27.3-27.36 2 Chroniques 9.10
15 Tena huamka, kabla haujaisha usiku; Huwapa watu wa nyumbani mwake chakula; Na wajakazi wake sehemu zao.
Luc 12.42 Romains 12.11 Marc 1.35 Proverbes 20.13 Ecclésiaste 9.10
16 Huangalia shamba, akalinunua; Kwa mapato ya mikono yake hupanda mizabibu.
Matthieu 13.44 Josué 15.18 Cantique 8.12
17 Hujifunga nguvu viunoni kama mshipi; Hutia mikono yake nguvu.
1 Rois 18.46 Job 38.3 2 Rois 4.29 1 Pierre 1.13 Ephésiens 6.10
18 Huona kama bidhaa yake ina faida; Taa yake haizimiki usiku.
Psaumes 127.2 2 Thessaloniciens 3.7-3.9 Genèse 31.40 1 Thessaloniciens 2.9 Matthieu 25.3-25.10
19 Hutia mikono yake katika kusokota; Na mikono yake huishika pia.
Exode 35.25-35.26
20 Huwakunjulia maskini mikono yake; Naam, huwanyoshea wahitaji mikono yake.
Ephésiens 4.28 Proverbes 22.9 Hébreux 13.16 Job 31.16-31.20 Ecclésiaste 11.1-11.2
21 Hawahofii theluji watu wa nyumbani mwake; Maana wote wa nyumbani mwake huvikwa nguo nyekundu.
Proverbes 25.20 Genèse 45.22 2 Samuel 1.24
22 Hujifanyia mazulia ya urembo; Mavazi yake ni kitani safi na urujuani.
Proverbes 7.16 Genèse 41.42 Apocalypse 19.14 Psaumes 45.13-45.14 Esther 5.1
23 Mume wake hujulikana malangoni; Aketipo pamoja na wazee wa nchi.
Ruth 4.1 Proverbes 12.4 Deutéronome 16.18 Ruth 4.11 Deutéronome 21.19
24 Hufanya nguo za kitani na kuziuza; Huwapa wafanya biashara mishipi.
Ezéchiel 27.16 Proverbes 31.19 1 Rois 10.28 Proverbes 31.13 Luc 16.19
25 Nguvu na hadhi ndiyo mavazi yake; Anaucheka wakati ujao.
Esaïe 65.13-65.14 Esaïe 61.10 Job 29.14 Ephésiens 4.24 Romains 13.14
26 Hufumbua kinywa chake kwa hekima, Na sheria ya wema i katika ulimi wake.
Proverbes 10.31 Ephésiens 4.29 1 Pierre 3.4-3.5 Esther 7.3-7.6 Luc 1.38
27 Huangalia sana njia za watu wa nyumbani mwake; Wala hali chakula cha uvivu.
Proverbes 14.1 Tite 2.4 1 Timothée 5.10 1 Thessaloniciens 4.11 2 Thessaloniciens 3.6
28 Wanawe huondoka na kumwita heri; Mumewe naye humsifu, na kusema,
2 Timothée 3.15-3.17 Proverbes 31.1 1 Rois 2.19 Esaïe 62.4-62.5 Psaumes 116.16
29 Binti za watu wengi wamefanya mema, Lakini wewe umewapita wote.
Cantique 6.8-6.9 Ephésiens 5.27
30 Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili; Bali mwanamke amchaye Bwana, ndiye atakayesifiwa.
1 Pierre 3.4-3.5 Proverbes 11.22 Proverbes 6.25 Luc 1.6 Proverbes 8.13
31 Mpe mapato ya mikono yake, Na matendo yake yamsifu malangoni.
Romains 6.21-6.22 Hébreux 6.10 Romains 16.12 Proverbes 11.30 Romains 16.1-16.4

Cette Bible est dans le domaine public.