1 Maneno ya mfalme Lemueli; mausia aliyofundishwa na mama yake.
Proverbes 6.20  2 Timothée 1.5  2 Timothée 3.15  Proverbes 1.8  Proverbes 30.1  
 2 Ni nini, mwanangu? Tena ni nini, mwana wa tumbo langu? Tena, ni nini mwana wa nadhiri zangu?
Esaïe 49.15  1 Samuel 1.11  1 Samuel 1.28  
 3 Usiwape wanawake nguvu zako; Wala moyo wako usiwape wale wawaharibuo wafalme.
Néhémie 13.26  Deutéronome 17.17  Proverbes 5.9-5.11  1 Rois 11.1  Proverbes 7.26-7.27  
 4 Ee Lemueli, kunywa mvinyo hakuwafai wafalme, hakuwafai wafalme; Wala haifai wakuu waseme, Ki wapi kileo?
Ecclésiaste 10.17  Proverbes 20.1  Esaïe 5.22  Esaïe 28.7-28.8  Habakuk 2.5  
 5 Wasije wakanywa na kuisahau sheria, Na kuipotosha hukumu ya mtu aliye taabuni.
Habakuk 2.5  
 6 Mpe kileo yeye aliye karibu na kupotea; Kampe divai yeye aliye na uchungu nafsini.
1 Timothée 5.23  1 Samuel 30.6  Job 3.20  Psaumes 104.15  2 Rois 4.27  
 7 Anywe akausahau umaskini wake; Asiikumbuke tena taabu yake.
Ephésiens 5.18  
 8 Fumbua kinywa chako kwa ajili yake aliye bubu; Uwatetee watu wote walioachwa peke yao;
Psaumes 82.3-82.4  Proverbes 24.11-24.12  Jérémie 26.16-26.19  Jérémie 26.24  Jean 7.51  
 9 Fumbua kinywa chako, uhukumu kwa haki; Uwapatie maskini na wahitaji haki yao.
Esaïe 1.17  Deutéronome 1.16  Lévitique 19.15  Job 29.15-29.16  Jérémie 22.15-22.16  
 10 Mke mwema, ni nani awezaye kumwona? Maana kima chake chapita kima cha marijani.
Proverbes 19.14  Proverbes 12.4  Proverbes 18.22  Ruth 3.11  Ephésiens 5.25-5.33  
 11 Moyo wa mumewe humwamini, Wala hatakosa kupata mapato.
2 Rois 4.9-4.10  1 Pierre 3.1-3.7  2 Rois 4.22-4.23  
 12 Humtendea mema wala si mabaya, Siku zote za maisha yake.
1 Samuel 25.26-25.27  1 Samuel 25.18-25.22  
 13 Hutafuta sufu na kitani; Hufanya kazi yake ya mikono kwa moyo.
1 Timothée 5.10  Genèse 29.9-29.10  Genèse 24.13-24.14  Ruth 2.23  Esaïe 32.9-32.11  
 14 Afanana na merikebu za biashara; Huleta chakula chake kutoka mbali.
1 Rois 9.26-9.28  Proverbes 31.24  Ezéchiel 27.3-27.36  2 Chroniques 9.10  
 15 Tena huamka, kabla haujaisha usiku; Huwapa watu wa nyumbani mwake chakula; Na wajakazi wake sehemu zao.
Luc 12.42  Romains 12.11  Marc 1.35  Proverbes 20.13  Ecclésiaste 9.10  
 16 Huangalia shamba, akalinunua; Kwa mapato ya mikono yake hupanda mizabibu.
Matthieu 13.44  Josué 15.18  Cantique 8.12  
 17 Hujifunga nguvu viunoni kama mshipi; Hutia mikono yake nguvu.
1 Rois 18.46  Job 38.3  2 Rois 4.29  1 Pierre 1.13  Genèse 49.24  
 18 Huona kama bidhaa yake ina faida; Taa yake haizimiki usiku.
Psaumes 127.2  2 Thessaloniciens 3.7-3.9  Genèse 31.40  1 Thessaloniciens 2.9  Matthieu 25.3-25.10  
 19 Hutia mikono yake katika kusokota; Na mikono yake huishika pia.
Exode 35.25-35.26  
 20 Huwakunjulia maskini mikono yake; Naam, huwanyoshea wahitaji mikono yake.
Ephésiens 4.28  Proverbes 22.9  Hébreux 13.16  Job 31.16-31.20  Marc 14.7  
 21 Hawahofii theluji watu wa nyumbani mwake; Maana wote wa nyumbani mwake huvikwa nguo nyekundu.
Proverbes 25.20  Genèse 45.22  2 Samuel 1.24  
 22 Hujifanyia mazulia ya urembo; Mavazi yake ni kitani safi na urujuani.Genèse 41.42  Proverbes 7.16  Apocalypse 19.14  Psaumes 45.13-45.14  Esther 5.1  
 23 Mume wake hujulikana malangoni; Aketipo pamoja na wazee wa nchi.
Ruth 4.1  Proverbes 12.4  Deutéronome 16.18  Ruth 4.11  Deutéronome 21.19  
 24 Hufanya nguo za kitani na kuziuza; Huwapa wafanya biashara mishipi.
Ezéchiel 27.16  Proverbes 31.19  1 Rois 10.28  Proverbes 31.13  Luc 16.19  
 25 Nguvu na hadhi ndiyo mavazi yake; Anaucheka wakati ujao.
Job 40.10  Psaumes 132.16  Esaïe 65.13-65.14  Esaïe 61.10  Job 29.14  
 26 Hufumbua kinywa chake kwa hekima, Na sheria ya wema i katika ulimi wake.
Proverbes 10.31  Ephésiens 4.29  Cantique 2.14  Juges 13.23  Luc 1.42-1.56  
 27 Huangalia sana njia za watu wa nyumbani mwake; Wala hali chakula cha uvivu.
Proverbes 14.1  Tite 2.4  1 Timothée 5.10  1 Thessaloniciens 4.11  2 Thessaloniciens 3.6  
 28 Wanawe huondoka na kumwita heri; Mumewe naye humsifu, na kusema,
2 Timothée 3.15-3.17  Proverbes 31.1  1 Rois 2.19  Esaïe 62.4-62.5  Psaumes 116.16  
 29 Binti za watu wengi wamefanya mema, Lakini wewe umewapita wote.
Cantique 6.8-6.9  Ephésiens 5.27  
 30 Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili; Bali mwanamke amchaye Bwana, ndiye atakayesifiwa.
1 Pierre 3.4-3.5  Proverbes 11.22  Proverbes 6.25  Psaumes 147.11  Luc 1.6  
 31 Mpe mapato ya mikono yake, Na matendo yake yamsifu malangoni.
Matthieu 7.16  Matthieu 7.20  Romains 6.21-6.22  Hébreux 6.10  Romains 16.12