Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 9.20
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 3 de Job

1 Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2 Kweli najua kuwa ndivyo hivyo; Lakini mtu huwaje mwenye haki mbele za Mungu?
Job 4.17 Job 25.4 Romains 3.20 Psaumes 143.2 Psaumes 130.3
3 Kama akipenda kushindana naye, Hawezi kumjibu neno moja katika elfu.
Job 10.2 Job 40.2 Romains 9.20 1 Jean 1.8 Psaumes 40.12
4 Yeye ni mwenye hekima moyoni, na mwenye uwezo katika nguvu; Ni nani aliyejifanya kuwa mgumu juu yake, naye akafanikiwa?
Job 36.5 Job 9.19 Proverbes 29.1 Daniel 4.34-4.37 Daniel 2.20
5 Aiondoaye milima, nayo haina habari, Akiipindua katika hasira zake.
Habakuk 3.6 Psaumes 114.6 Apocalypse 11.13 Nombres 1.5-1.6 Habakuk 3.10
6 Aitikisaye dunia itoke mahali pake, Na nguzo zake hutetema.
Esaïe 2.21 Psaumes 75.3 Aggée 2.6 Hébreux 12.26 Job 26.11
7 Aliamuruye jua, nalo halichomozi; Nazo nyota huzipiga muhuri.
Esaïe 13.10 Luc 21.25-21.26 Amos 8.9 Daniel 4.35 Job 38.19-38.20
8 Ambaye peke yake ni mwenye kuzitandika mbingu, Na kuyakanyaga mawimbi ya bahari.
Esaïe 44.24 Esaïe 40.22 Psaumes 104.2-104.3 Jérémie 10.11 Zacharie 12.1
9 Yeye afanyaye hizo nyota za Dubu, na Orioni, na hicho Kilimia, Na makundi ya nyota ya kusini.
Amos 5.8 Genèse 1.16 Job 38.31-38.41 Psaumes 104.13 Actes 28.13
10 Atendaye mambo makuu yasiyotafutikana; Naam, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
Job 5.9 Psaumes 71.15 Psaumes 72.18 Romains 11.33 Ecclésiaste 3.11
11 Tazama, yuaenenda karibu nami, nisimwone; Tena yuapita kwenda mbele, nisimtambue.
Job 23.8-23.9 Job 35.14 1 Timothée 6.16 Psaumes 77.19
12 Tazama, yuakamata, ni nani awezaye kumzuia? Ni nani awezaye kumwuliza, Wafanya nini?
Esaïe 45.9 Job 11.10 Job 23.13 Matthieu 20.15 Job 34.29
13 Mungu haondoi hasira zake; Hao wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
Esaïe 30.7 Job 26.12 Psaumes 89.10 Esaïe 51.9 Jacques 4.6-4.7
14 Je! Mimi nitamjibuje, Na kuyachagua maneno yangu kuhojiana naye?
Job 4.19 Job 25.6 Job 23.4 Job 11.4-11.5 Job 23.7
15 Ambaye, nijapokuwa mimi ni mwenye haki, nisingemjibu; Ningemsihi-sihi mtesi wangu.
Job 10.15 Job 8.5 Job 22.27 Job 34.31-34.32 Job 5.8
16 Kama ningemwita, naye akaniitikia; Hata hivyo singeamini kuwa amesikiza sauti yangu.
Juges 6.13 Exode 6.9 Psaumes 66.18-66.20 Job 29.24 Actes 12.14-12.16
17 Yeye anipondaye kwa dhoruba, Na kuziongeza jeraha zangu pasipokuwa na sababu.
Job 2.3 Job 16.14 Job 34.6 Job 16.12 Matthieu 7.27
18 Haniachi nipate kuvuta pumzi, Lakini hunijaza uchungu.
Job 7.19 Lamentations 3.15 Psaumes 39.13 Job 27.2 Job 3.20
19 Kama tukitaja nguvu za mashujaa, tazama yupo hapo! Kama tukitaja hukumu, ni nani atakayeniwekea muhula?
Job 9.4 1 Corinthiens 1.25 Job 9.32-9.33 Matthieu 6.13 Psaumes 62.11
20 Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; Ingawa ni mkamilifu, kitanishuhudia kuwa ni mpotovu.
Job 15.5-15.6 Job 34.35 1 Timothée 6.5 Psaumes 130.3 Jacques 3.2
21 Mimi ni mkamilifu; siangalii nafsi yangu; Naudharau uhai wangu.
Job 1.1 Psaumes 139.23-139.24 Job 7.21 1 Jean 3.20 Proverbes 28.26
22 Hayo yote ni mamoja; kwa hiyo nasema, Yeye huangamiza wakamilifu na waovu pia.
Ecclésiaste 9.1-9.3 Ezéchiel 21.3-21.4 Job 10.8 Luc 13.2-13.4
23 Kama hilo pigo likiua ghafula, Atayadhihaki majaribu yake asiye na kosa.
Job 2.7 Job 1.13-1.19 2 Samuel 14.15 2 Samuel 14.17 Job 24.12
24 Dunia imetiwa mkononi mwa waovu; Yeye hufunika nyuso za waamuzi wake; Kama si yeye, ni nani basi?
Job 10.3 Job 24.25 2 Samuel 19.4 Psaumes 17.14 Daniel 7.7-7.28
25 Basi siku zangu zina mbio kuliko tarishi; Zakimbia, wala hazioni mema.
Job 7.6-7.7 Psaumes 90.9-90.10 Jacques 4.14 Psaumes 39.5 Psaumes 89.47
26 Zimepita kama merikebu ziendazo mbio; Mfano wa tai ayashukiaye mawindo.
Habakuk 1.8 Esaïe 18.2 Jérémie 4.13 2 Samuel 1.23 Proverbes 23.5
27 Nikisema, Mimi nitasahau kuugua kwangu, Nitaacha kununa uso nikachangamke moyo;
Job 7.13 Job 7.11 Jérémie 8.18 Psaumes 77.2-77.3
28 Mimi huziogopa huzuni zangu zote, Najua kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
Psaumes 119.120 Job 3.25 Exode 20.7 Job 14.16 Psaumes 88.15-88.16
29 Nitahukumiwa kuwa ni mkosa; Ya nini basi nitaabike bure?
Job 21.16-21.17 Psaumes 37.33 Job 10.2 Job 22.5-22.30 Job 9.22
30 Ingawaje najiosha kwa maji ya theluji, Na kuitakasa mikono yangu kwa sabuni;
Jérémie 2.22 1 Jean 1.8 Psaumes 26.6 Jérémie 4.14 Job 31.7
31 Lakini utanitupa shimoni, Nami hata nguo zangu zitanichukia.
Philippiens 3.8-3.9 Esaïe 64.6 Job 15.6 Job 9.20 Esaïe 59.6
32 Kwani yeye si mtu, kama mimi, hata nimjibu, Hata tukaribiane katika hukumu.
Romains 9.20 Ecclésiaste 6.10 Nombres 23.19 Psaumes 143.2 Jérémie 49.19
33 Hapana mwenye kuamua katikati yetu, Awezaye kutuwekea mkono sote wawili.
1 Samuel 2.25 Job 9.19 Psaumes 106.23 1 Rois 3.16-3.28 1 Jean 2.1-2.2
34 Na aniondolee fimbo yake, Na utisho wake usinitie hofu;
Psaumes 39.10 Job 33.7 Job 13.11 Job 37.1 Job 31.23
35 Ndipo hapo ningesema, nisimwogope; Kwani sivyo nilivyo nafsini mwangu.

Cette Bible est dans le domaine public.