Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 9.13
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 3 de Job

1 Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2 Kweli najua kuwa ndivyo hivyo; Lakini mtu huwaje mwenye haki mbele za Mungu?
Job 4.17 Romains 3.20 Job 25.4 Psaumes 143.2 Job 32.2
3 Kama akipenda kushindana naye, Hawezi kumjibu neno moja katika elfu.
Job 10.2 Job 40.2 Job 31.35-31.37 Esaïe 57.15-57.16 Job 9.32-9.33
4 Yeye ni mwenye hekima moyoni, na mwenye uwezo katika nguvu; Ni nani aliyejifanya kuwa mgumu juu yake, naye akafanikiwa?
Job 36.5 Job 9.19 Proverbes 29.1 1 Corinthiens 10.22 Exode 9.14-9.17
5 Aiondoaye milima, nayo haina habari, Akiipindua katika hasira zake.
Matthieu 21.21 Zacharie 4.7 Job 28.9 Matthieu 27.51 Luc 21.11
6 Aitikisaye dunia itoke mahali pake, Na nguzo zake hutetema.
Aggée 2.6 Hébreux 12.26 Esaïe 2.21 Psaumes 75.3 Esaïe 2.19
7 Aliamuruye jua, nalo halichomozi; Nazo nyota huzipiga muhuri.
Esaïe 13.10 Amos 8.9 Luc 21.25-21.26 Ezéchiel 32.7-32.8 Job 38.12-38.15
8 Ambaye peke yake ni mwenye kuzitandika mbingu, Na kuyakanyaga mawimbi ya bahari.
Esaïe 40.22 Psaumes 104.2-104.3 Esaïe 44.24 Zacharie 12.1 Job 37.18
9 Yeye afanyaye hizo nyota za Dubu, na Orioni, na hicho Kilimia, Na makundi ya nyota ya kusini.
Amos 5.8 Job 38.31-38.41 Genèse 1.16 Psaumes 147.4 Psaumes 104.13
10 Atendaye mambo makuu yasiyotafutikana; Naam, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
Job 5.9 Psaumes 71.15 Psaumes 72.18 Daniel 4.2-4.3 Job 26.12-26.14
11 Tazama, yuaenenda karibu nami, nisimwone; Tena yuapita kwenda mbele, nisimtambue.
Job 23.8-23.9 Job 35.14 1 Timothée 6.16 Psaumes 77.19
12 Tazama, yuakamata, ni nani awezaye kumzuia? Ni nani awezaye kumwuliza, Wafanya nini?
Job 11.10 Esaïe 45.9 Job 23.13 Romains 11.34 Daniel 4.35
13 Mungu haondoi hasira zake; Hao wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
Esaïe 30.7 Job 26.12 Psaumes 89.10 Esaïe 51.9 Jacques 4.6-4.7
14 Je! Mimi nitamjibuje, Na kuyachagua maneno yangu kuhojiana naye?
Job 9.3 Job 33.5 Job 4.19 Job 25.6 Job 23.4
15 Ambaye, nijapokuwa mimi ni mwenye haki, nisingemjibu; Ningemsihi-sihi mtesi wangu.
Job 8.5 Job 10.15 Jérémie 31.9 1 Pierre 2.23 2 Chroniques 33.13
16 Kama ningemwita, naye akaniitikia; Hata hivyo singeamini kuwa amesikiza sauti yangu.
Psaumes 126.1 Psaumes 18.6 Luc 24.41 Juges 6.13 Exode 6.9
17 Yeye anipondaye kwa dhoruba, Na kuziongeza jeraha zangu pasipokuwa na sababu.
Job 2.3 Job 16.14 Job 34.6 Ezéchiel 13.13 Job 2.13
18 Haniachi nipate kuvuta pumzi, Lakini hunijaza uchungu.
Job 7.19 Lamentations 3.15 Lamentations 3.3 Lamentations 3.18-3.19 Psaumes 39.13
19 Kama tukitaja nguvu za mashujaa, tazama yupo hapo! Kama tukitaja hukumu, ni nani atakayeniwekea muhula?
Job 9.4 Job 9.32-9.33 1 Corinthiens 1.25 Job 36.17-36.19 1 Corinthiens 10.22
20 Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; Ingawa ni mkamilifu, kitanishuhudia kuwa ni mpotovu.
Job 34.35 Job 15.5-15.6 Luc 10.29 Esaïe 6.5 Proverbes 10.19
21 Mimi ni mkamilifu; siangalii nafsi yangu; Naudharau uhai wangu.
Job 1.1 Job 7.15-7.16 1 Corinthiens 4.4 Psaumes 139.23-139.24 Job 7.21
22 Hayo yote ni mamoja; kwa hiyo nasema, Yeye huangamiza wakamilifu na waovu pia.
Ecclésiaste 9.1-9.3 Ezéchiel 21.3-21.4 Job 10.8 Luc 13.2-13.4
23 Kama hilo pigo likiua ghafula, Atayadhihaki majaribu yake asiye na kosa.
Ezéchiel 21.13 Hébreux 11.36-11.37 Psaumes 44.22 Ezéchiel 14.19-14.21 Job 4.7
24 Dunia imetiwa mkononi mwa waovu; Yeye hufunika nyuso za waamuzi wake; Kama si yeye, ni nani basi?
Job 24.25 Job 10.3 Job 21.7-21.15 Job 12.6-12.10 Jérémie 14.4
25 Basi siku zangu zina mbio kuliko tarishi; Zakimbia, wala hazioni mema.
Job 7.6-7.7 Psaumes 90.9-90.10 Jacques 4.14 Psaumes 39.11 Psaumes 39.5
26 Zimepita kama merikebu ziendazo mbio; Mfano wa tai ayashukiaye mawindo.
Habakuk 1.8 Esaïe 18.2 Job 39.27-39.30 Jérémie 4.13 2 Samuel 1.23
27 Nikisema, Mimi nitasahau kuugua kwangu, Nitaacha kununa uso nikachangamke moyo;
Job 7.13 Job 7.11 Jérémie 8.18 Psaumes 77.2-77.3
28 Mimi huziogopa huzuni zangu zote, Najua kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
Psaumes 119.120 Job 9.2 Job 7.21 Job 9.20-9.21 Job 21.6
29 Nitahukumiwa kuwa ni mkosa; Ya nini basi nitaabike bure?
Job 21.27 Psaumes 73.13 Jérémie 2.35 Job 10.14-10.17 Job 21.16-21.17
30 Ingawaje najiosha kwa maji ya theluji, Na kuitakasa mikono yangu kwa sabuni;
Jérémie 2.22 1 Jean 1.8 Romains 10.3 Psaumes 26.6 Jérémie 4.14
31 Lakini utanitupa shimoni, Nami hata nguo zangu zitanichukia.
Philippiens 3.8-3.9 Esaïe 64.6 Job 15.6 Job 9.20 Esaïe 59.6
32 Kwani yeye si mtu, kama mimi, hata nimjibu, Hata tukaribiane katika hukumu.
Ecclésiaste 6.10 Romains 9.20 Psaumes 143.2 Nombres 23.19 Esaïe 45.9
33 Hapana mwenye kuamua katikati yetu, Awezaye kutuwekea mkono sote wawili.
1 Samuel 2.25 Job 9.19 Psaumes 106.23 1 Rois 3.16-3.28 1 Jean 2.1-2.2
34 Na aniondolee fimbo yake, Na utisho wake usinitie hofu;
Psaumes 39.10 Job 13.11 Job 33.7 Job 23.15 Job 37.1
35 Ndipo hapo ningesema, nisimwogope; Kwani sivyo nilivyo nafsini mwangu.

Cette Bible est dans le domaine public.