Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 3.20
Bible en Swahili de l’est


Dialogue entre Job et ses amis

Intervention n° 1 de Job

1 Baada ya hayo Ayubu akafunua kinywa chake, na kuilaani siku yake.
Jérémie 20.14-20.15 Psaumes 106.33 Psaumes 39.2-39.3 Job 2.5 Job 1.22
2 Ayubu akajibu, na kusema;
Juges 18.14
3 Na ipotelee mbali ile siku niliyozaliwa mimi, Na ule usiku uliosema, Mtoto mume ametungishwa mimba.
Jérémie 20.14-20.18 Job 10.18-10.19 Jérémie 15.10
4 Siku hiyo na iwe giza; Mungu asiiangalie toka juu, Wala mwanga usiiangazie.
Exode 10.22-10.23 Amos 5.18 Matthieu 27.45 Joël 2.2 Deutéronome 11.12
5 Ishikwe na giza, giza tupu, kuwa yake; Wingu na likae juu yake; Chote kiifanyacho siku kuwa giza na kiitishe.
Psaumes 23.4 Job 10.21-10.22 Jérémie 13.16 Job 28.3 Esaïe 9.2
6 Tena usiku huo, na ushikwe na giza kuu; Usihesabiwe katika siku za mwaka; Wala kutiwa katika hesabu ya miezi.
7 Tazama, usiku huo na uwe tasa; Wala isiwe ndani yake sauti ya shangwe.
Apocalypse 18.22-18.23 Jérémie 7.34 Esaïe 24.8 Esaïe 13.20-13.22
8 Na waulaani hao waulaanio mchana, Hao walio tayari kumwamsha huyo lewiathani.
Job 41.1 Job 41.10 Marc 5.38 Matthieu 11.17 Jérémie 9.17-9.18
9 Nyota za mapambazuko yake na ziwe giza; Na utafute mwanga lakini usiupate; Wala usiyaone makope ya asubuhi;
Job 41.18 Job 30.26 Jérémie 13.16 Jérémie 8.15
10 Kwa sababu haukuifunga milango ya tumbo la mamangu. Wala kunifichia taabu machoni.
Ecclésiaste 11.10 Jérémie 20.17 Job 10.18-10.19 1 Samuel 1.5 Job 6.2-6.3
11 Mbona si kufa mimi tokea mimbani? Mbona nisitoe roho hapo nilipotoka tumboni?
Job 10.18-10.19 Psaumes 58.8 Esaïe 46.3 Osée 9.14 Psaumes 71.6
12 Mbona hayo magoti kunipokea? Au hayo maziwa, hata nikanyonya?
Esaïe 66.12 Genèse 30.3 Genèse 50.23 Ezéchiel 16.4-16.5
13 Maana hapo ningelala na kutulia; Ningelala usingizi; na kupata kupumzika;
Job 21.23 Ecclésiaste 6.3-6.5 Job 17.13 Job 21.13 Job 10.22
14 Pamoja na wafalme na washauri wa dunia, Hao waliojijengea maganjoni;
Job 15.28 Esaïe 14.10-14.16 Ezéchiel 26.20 1 Rois 2.10 Psaumes 49.6-49.10
15 Au pamoja na wakuu wenye dhahabu, Waliozijaza fedha nyumba zao;
Job 12.21 Esaïe 2.7 Job 22.25 Nombres 22.18 1 Rois 10.27
16 Au, kama kuzikwa mimba iliyoharibika, nisingekuwako; Kama wachanga wasiouona mwanga kabisa.
Psaumes 58.8 1 Corinthiens 15.8 Ecclésiaste 6.3
17 Huko waovu huacha kusumbua; Huko nako hao waliochoka wapumzika
Apocalypse 14.13 Job 17.16 Esaïe 57.1-57.2 Hébreux 4.11 Hébreux 4.9
18 Huko wafungwa waona raha pamoja; Hawaisikii sauti yake msimamizi.
Job 39.7 Esaïe 14.3-14.4 Juges 4.3 Exode 5.15-5.19 Exode 5.6-5.8
19 Wakuu na wadogo wako huko; Mtumishi yu huru kwa bwana wake.
Ecclésiaste 8.8 Hébreux 9.27 Psaumes 49.2 Ecclésiaste 12.7 Job 30.23
20 Mbona yeye aliye mashakani kupewa mwanga, Na hao wenye uchungu rohoni kupewa uhai;
Job 7.15-7.16 Jérémie 20.18 Proverbes 31.6 1 Samuel 1.10 2 Rois 4.27
21 Ambao wangojea mauti, lakini hawayapati; Na kuyachimbulia zaidi ya kutafuta hazina iliyostirika;
Apocalypse 9.6 Proverbes 2.4 Jonas 4.8 Jonas 4.3 Nombres 11.15
22 Ambao wafurahi mno, Na kushangilia watakapoliona kaburi?
23 Kwa nini mtu aliyezibiwa njia kupewa mwanga, Ambaye Mungu amemzingira kwa ukingo?
Job 19.8 Lamentations 3.7 Esaïe 40.27 Psaumes 31.8 Lamentations 3.9
24 Kwani kuugua kwangu kwaja kana kwamba ni chakula, Na kunguruma kwangu kumemiminika kama maji.
Psaumes 102.9 Psaumes 38.8 Psaumes 42.3-42.4 Psaumes 80.5 Job 6.7
25 Maana jambo hilo nichalo hunipata, Nalo linitialo hofu hunijilia.
Job 1.5 Job 30.15 Job 31.23
26 Mimi sioni raha, wala situlii, wala kupumzika; Lakini huja taabu.
Job 7.14 Psaumes 143.11 Job 27.9

Cette Bible est dans le domaine public.