Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 20.29
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 2 de Tsophar

1 Ndipo Sofari, Mnaamathi, akajibu, na kusema,
Job 2.11 Job 11.1 Job 42.9
2 Kwa hiyo mawazo yangu hunipa jawabu, Kwa ajili ya haraka niliyo nayo ndani yangu.
Psaumes 39.2-39.3 Marc 6.25 Jacques 1.19 Job 20.3 Job 4.2
3 Nimesikia maonyo yanayonitahayarisha, Nayo roho ya ufahamu wangu hunijibu.
Job 27.11 Job 20.2 Psaumes 78.2-78.5 Job 19.3 Job 19.29
4 Je! Hujui neno hili tangu zamani za kale, Tangu wanadamu kuwekwa juu ya nchi,
Psaumes 115.16 Job 15.10 Job 8.8-8.9 Genèse 1.28 Genèse 9.1-9.3
5 Ya kuwa shangwe ya waovu ni kwa muda kidogo, Na furaha ya wapotovu ni ya dakika moja tu?
Psaumes 37.35-37.36 Job 15.29-15.34 Galates 6.4 Esther 7.10 Job 27.8
6 Ujapopanda ukuu wake mpaka mbinguni, Na kichwa chake kufikilia mawinguni;
Esaïe 14.13-14.14 Abdias 1.3-1.4 Genèse 11.4 Daniel 4.22 Matthieu 11.23
7 Hata hivyo ataangamia milele kama mavi yake mwenyewe; Hao waliomwona watasema, Yuko wapi?
Job 14.10 1 Rois 14.10 Psaumes 83.10 2 Rois 9.37 Job 8.18
8 Ataruka mfano wa ndoto, asionekane; Naam, atafukuzwa kama maono ya usiku,
Psaumes 73.20 Psaumes 90.5 Esaïe 29.7-29.8 Job 18.18 Job 27.21-27.23
9 Jicho lililomwona halitamwona tena; Wala mahali pake hapatamtazama tena.
Job 7.8 Job 7.10 Job 8.18 Psaumes 37.36 Psaumes 37.10
10 Watoto wake watataka fadhili kwa maskini, Na mikono yake itarudisha mali yake.
Job 20.18 Job 27.16-27.17 Psaumes 109.10 Proverbes 6.31 2 Samuel 12.6
11 Mifupa yake imejaa ujana wake, Lakini utalala nchi naye mavumbini.
Job 21.26 Job 13.26 Psaumes 25.7 Proverbes 5.22-5.23 Actes 1.25
12 Ingawa uovu una tamu kinywani mwake, Ingawa auficha chini ya ulimi wake;
Job 15.16 Psaumes 10.7 Psaumes 109.17-109.18 Genèse 3.6 Ecclésiaste 11.9
13 Ingawa auhurumia, asikubali kuuacha uende zake. Lakini akaushika vivyo kinywani mwake;
Marc 9.43-9.49 Matthieu 5.29-5.30 Nombres 11.18-11.20 Romains 8.13
14 Hata hivyo chakula chake matumboni mwake kinabadilika, Kimekuwa ni nyongo za majoka ndani yake.
Proverbes 23.29-23.35 Deutéronome 32.24 Proverbes 1.31 2 Samuel 11.2-11.5 Psaumes 32.3-32.4
15 Amemeza mali, naye atayatapika tena; Mungu atayatoa tumboni mwake.
Proverbes 23.8 Matthieu 27.3-27.4
16 Ataamwa sumu ya majoka; Na ulimi wa fira utamwua.
Romains 3.13 Actes 28.3-28.6 Matthieu 3.7 Deutéronome 32.24 Esaïe 30.6
17 Hataiangalia hiyo mito ya maji, Vile vijito vilivyojaa asali na siagi.
Deutéronome 32.13-32.14 Job 29.6 Esaïe 41.17 Esaïe 7.22 Esaïe 7.15
18 Aliyoyataabikia kazi atayarudisha, asiyameze; Kwa mali aliyoyapata, hatafurahi.
Job 20.10 Job 20.15 Job 31.29 Jérémie 22.17 Matthieu 23.24
19 Kwa maana amewaonea na kuwaacha maskini; Amenyang’anya nyumba kwa jeuri, wala hataijenga.
Job 35.9 Proverbes 14.31 Jacques 2.13 1 Samuel 12.3-12.4 Psaumes 10.18
20 Kwa sababu hakujua utulivu ndani yake, Hataponya cho chote katika hicho alichokifurahia.
Ecclésiaste 5.13-5.14 Esaïe 57.20-57.21
21 Hakikusalia kitu asichokula; Kwa hiyo kufanikiwa kwake hakutadumu.
Job 18.19 Luc 16.24-16.25 Job 15.29 Jérémie 17.11
22 Katika kujaa kwa wingi wake atakuwa katika dhiki; Mkono wa kila anayesumbuliwa utamjia.
Job 18.7 2 Rois 24.2 Job 1.17 Job 16.11 Job 15.29
23 Hapo atakapo kulijaza tumbo lake, Mungu atamtupia ukali wa ghadhabu zake, Na kuunyesha juu yake akiwa anakula.
Psaumes 78.30-78.31 Nombres 11.33 Genèse 19.24 Malachie 2.2 Psaumes 11.6
24 Ataikimbia silaha ya chuma, Na uta wa shaba utamchoma kwa pili.
Amos 5.19 Esaïe 24.18 2 Samuel 22.35 1 Rois 20.30 Amos 9.1-9.3
25 Yeye autoa, nao watoka mwilini mwake; Naam, ncha ing’aayo yatoka katika nyongo yake; Vitisho viko juu yake.
Job 16.13 Job 18.11 Deutéronome 32.41 Psaumes 7.12 2 Samuel 18.14
26 Giza lote linawekwa kwa ajili ya hazina zake; Moto ambao haukuvuviwa na mtu utamla; Utayateketeza yaliyosalia hemani mwake.
Psaumes 21.9 Psaumes 120.4 Psaumes 109.9-109.15 Jude 1.13 Esaïe 14.20-14.22
27 Mbingu zitafunua wazi uovu wake, Nayo nchi itainuka kinyume chake.
Esaïe 26.21 Job 16.18 Romains 2.16 Malachie 3.5 Jérémie 29.23
28 Maongeo ya nyumba yake yataondoka, Yatamwagika mbali katika siku ya ghadhabu zake.
Proverbes 11.4 Apocalypse 18.17 Job 27.14-27.19 Sophonie 1.18 Job 5.5
29 Hii ndiyo sehemu ya mtu mwovu itokayo kwa Mungu, Na urithi aliowekewa na Mungu.
Job 27.13 Job 31.2-31.3 Job 18.21 Deutéronome 29.20-29.28 Matthieu 24.51

Cette Bible est dans le domaine public.