Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 19.17
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 6 de Job

1 Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2 Je! Mtanichukiza nafsi yangu hata lini, Na kunivunja-vunja kwa maneno?
Proverbes 18.21 Psaumes 42.10 Job 27.2 Job 18.2 Apocalypse 6.10
3 Mara kumi hizi mmenishutumu; Hamwoni haya kunifanyia mambo magumu.
Genèse 31.7 Daniel 1.20 Job 19.17 Job 18.4-18.21 Néhémie 4.12
4 Ingawaje nimekosa, Kosa langu hukaa kwangu mwenyewe.
Proverbes 9.12 Ezéchiel 18.4 Galates 6.5 2 Samuel 24.17 Job 11.3-11.6
5 Kwamba mtajitukuza juu yangu, Na kunena juu yangu shutumu langu;
Psaumes 35.26 Psaumes 38.16 Psaumes 55.12 Sophonie 2.10 1 Samuel 1.6
6 Jueni basi kuwa Mungu amenipotosha, Na kunizingira kwa wavu wake.
Job 18.8-18.10 Job 7.20 Ezéchiel 32.3 Job 16.11-16.14 Psaumes 66.10-66.12
7 Tazama, nalia, Udhalimu, lakini sisikiwi; Naulilia msaada, wala hapana hukumu.
Habakuk 1.2-1.3 Lamentations 3.8 Job 30.20 Job 40.8 Job 10.15-10.17
8 Yeye ameiziba njia yangu nisipate kupita, Na kutia giza katika mapito yangu.
Job 3.23 Lamentations 3.7 Lamentations 3.9 Osée 2.6 Jérémie 13.16
9 Amenivua utukufu wangu, Na kuiondoa taji kichwani mwangu.
Psaumes 89.44 Job 29.7-29.14 Lamentations 5.16 Psaumes 89.39 Psaumes 49.16-49.17
10 Amenibomoa pande zote, nami nimetoweka; Na tumaini langu ameling’oa kama mti.
Job 24.20 Psaumes 37.35-37.36 Job 12.14 Psaumes 102.11 Job 7.6
11 Tena ameziwasha ghadhabu zake juu yangu, Akanihesabia kuwa mmoja katika watesi wake.
Job 13.24 Job 33.10 Job 16.9 Lamentations 2.5 Deutéronome 32.22
12 Majeshi yake husongea pamoja, na kunipandishia njia yao, Na kupiga marago kuizunguka hema yangu.
Job 30.12 Job 16.13 Esaïe 10.5-10.6 Job 16.11 Esaïe 51.23
13 Amewaweka ndugu zangu mbali nami, Na wanijuao wametengwa nami kabisa.
Psaumes 88.8 Psaumes 69.8 Psaumes 88.18 Psaumes 31.11 Psaumes 69.20
14 Watu wa mbari yangu wamekoma, Na rafiki zangu niwapendao wamenisahau.
Psaumes 38.11 Michée 7.5-7.6 Psaumes 55.12-55.14 Jean 13.18 Proverbes 18.24
15 Wakaao nyumbani mwangu, na vijakazi vyangu, wanihesabu kuwa mgeni; Mimi ni mgeni machoni pao.
Job 31.31-31.32 Psaumes 123.3
16 Namwita mtumishi wangu, wala haniitikii, Ingawa namsihi kwa kinywa changu.
Job 1.15-1.17 Job 1.19
17 Pumzi zangu ni kama za mgeni kwa mke wangu, Nami ni machukizo kwa ndugu zangu.
Job 17.1 Job 2.9-2.10
18 Hata watoto wadogo hunidharau; Nikiondoka, huninena.
2 Rois 2.23 Job 30.1 Job 30.12 Esaïe 3.5
19 Wasiri wangu wote wanichukia; Na hao niliowapenda wamenigeukia.
Psaumes 41.9 Psaumes 55.12-55.14 Luc 22.48 Job 6.14-6.15 Psaumes 109.4-109.5
20 Mfupa wangu unagandamana na ngozi yangu na nyama yangu, Nami nimeokoka na ngozi ya meno yangu tu.
Psaumes 102.5 Lamentations 4.8 Job 33.19-33.22 Lamentations 5.10 Psaumes 22.14-22.17
21 Nihurumieni, nihurumieni, enyi rafiki zangu, Kwa maana mkono wa Mungu umenigusa.
Job 1.11 Psaumes 38.2 Job 6.14 Hébreux 13.3 Job 2.5
22 Mbona ninyi mnaniudhi kama Mungu, Wala hamkutosheka na nyama yangu?
Psaumes 69.26 Job 10.16 Job 31.31 Job 2.5 Michée 3.3
23 Laiti maneno yangu yangeandikwa sasa! Laiti yangeandikwa kitabuni!
Esaïe 30.8 Esaïe 8.1 Job 31.35
24 Yakachorwa katika mwamba milele, Kwa kalamu ya chuma na risasi.
Jérémie 17.1 Exode 28.21 Deutéronome 27.2-27.3 Deutéronome 27.8 Exode 28.11-28.12
25 Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai, Na ya kuwa hatimaye atasimama juu ya nchi.
Esaïe 43.14 Proverbes 23.11 Psaumes 19.14 Psaumes 78.35 Esaïe 54.5
26 Na baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi, Lakini, pasipokuwa na mwili wangu nitamwona Mungu;
Psaumes 17.15 1 Jean 3.2 1 Corinthiens 13.12 Matthieu 5.8 Psaumes 16.9
27 Nami nitamwona mimi nafsi yangu, Na macho yangu yatamtazama, wala si mwingine. Mtima wangu unazimia ndani yangu.
Psaumes 73.26 Esaïe 26.19 Nombres 24.17
28 Kama mkisema, Jinsi tutakavyomwudhi! Kwa kuwa shina la jambo hili limeonekana kwake;
Job 19.22 Psaumes 69.26 1 Rois 14.13
29 Uogopeni upanga; Kwa maana adhabu za upanga zina ghadhabu, Mpate kujua ya kwamba hukumu iko.
Ecclésiaste 11.9 Jacques 4.11-4.12 Ecclésiaste 12.14 Job 13.7-13.11 Psaumes 58.10-58.11

Cette Bible est dans le domaine public.