Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 19.10
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 6 de Job

1 Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2 Je! Mtanichukiza nafsi yangu hata lini, Na kunivunja-vunja kwa maneno?
Psaumes 59.7 2 Pierre 2.7-2.8 Psaumes 6.2-6.3 Psaumes 13.1 Proverbes 18.21
3 Mara kumi hizi mmenishutumu; Hamwoni haya kunifanyia mambo magumu.
Genèse 31.7 Job 15.11-15.12 Daniel 1.20 Job 19.17 Job 18.4-18.21
4 Ingawaje nimekosa, Kosa langu hukaa kwangu mwenyewe.
Proverbes 9.12 2 Samuel 24.17 Job 11.3-11.6 2 Corinthiens 5.10 Ezéchiel 18.4
5 Kwamba mtajitukuza juu yangu, Na kunena juu yangu shutumu langu;
Psaumes 55.12 Psaumes 35.26 Psaumes 38.16 Michée 7.8 Psaumes 41.11
6 Jueni basi kuwa Mungu amenipotosha, Na kunizingira kwa wavu wake.
Job 18.8-18.10 Job 27.2 Osée 7.12 Ezéchiel 12.13 Job 7.20
7 Tazama, nalia, Udhalimu, lakini sisikiwi; Naulilia msaada, wala hapana hukumu.
Habakuk 1.2-1.3 Lamentations 3.8 Job 30.20 Job 34.5 Job 10.3
8 Yeye ameiziba njia yangu nisipate kupita, Na kutia giza katika mapito yangu.
Lamentations 3.7 Job 3.23 Lamentations 3.9 Osée 2.6 Jérémie 23.12
9 Amenivua utukufu wangu, Na kuiondoa taji kichwani mwangu.
Psaumes 89.44 Job 29.7-29.14 Lamentations 5.16 Psaumes 89.39 Job 29.20-29.21
10 Amenibomoa pande zote, nami nimetoweka; Na tumaini langu ameling’oa kama mti.
Job 24.20 Psaumes 37.35-37.36 Job 12.14 Job 2.7 Job 17.15
11 Tena ameziwasha ghadhabu zake juu yangu, Akanihesabia kuwa mmoja katika watesi wake.
Job 13.24 Job 16.9 Job 33.10 Deutéronome 32.22 Psaumes 89.46
12 Majeshi yake husongea pamoja, na kunipandishia njia yao, Na kupiga marago kuizunguka hema yangu.
Job 30.12 Esaïe 10.5-10.6 Job 16.11 Esaïe 51.23 Job 16.13
13 Amewaweka ndugu zangu mbali nami, Na wanijuao wametengwa nami kabisa.
Psaumes 88.8 Psaumes 88.18 Psaumes 69.8 Psaumes 31.11 Matthieu 26.56
14 Watu wa mbari yangu wamekoma, Na rafiki zangu niwapendao wamenisahau.
Psaumes 38.11 Matthieu 10.21 2 Samuel 16.23 Jérémie 20.10 Michée 7.5-7.6
15 Wakaao nyumbani mwangu, na vijakazi vyangu, wanihesabu kuwa mgeni; Mimi ni mgeni machoni pao.
Job 31.31-31.32 Psaumes 123.3
16 Namwita mtumishi wangu, wala haniitikii, Ingawa namsihi kwa kinywa changu.
Job 1.15-1.17 Job 1.19
17 Pumzi zangu ni kama za mgeni kwa mke wangu, Nami ni machukizo kwa ndugu zangu.
Job 17.1 Job 2.9-2.10
18 Hata watoto wadogo hunidharau; Nikiondoka, huninena.
2 Rois 2.23 Job 30.12 Job 30.1 Esaïe 3.5
19 Wasiri wangu wote wanichukia; Na hao niliowapenda wamenigeukia.
Psaumes 41.9 Luc 22.48 Psaumes 55.12-55.14 Psaumes 38.11 Psaumes 55.20
20 Mfupa wangu unagandamana na ngozi yangu na nyama yangu, Nami nimeokoka na ngozi ya meno yangu tu.
Psaumes 102.5 Lamentations 4.8 Job 33.19-33.22 Job 7.5 Lamentations 3.4
21 Nihurumieni, nihurumieni, enyi rafiki zangu, Kwa maana mkono wa Mungu umenigusa.
Job 1.11 Psaumes 38.2 Romains 12.15 Job 2.10 Job 6.14
22 Mbona ninyi mnaniudhi kama Mungu, Wala hamkutosheka na nyama yangu?
Psaumes 69.26 Job 16.13-16.14 Esaïe 51.23 Job 16.11 Job 10.16
23 Laiti maneno yangu yangeandikwa sasa! Laiti yangeandikwa kitabuni!
Esaïe 30.8 Esaïe 8.1 Job 31.35
24 Yakachorwa katika mwamba milele, Kwa kalamu ya chuma na risasi.
Jérémie 17.1 Deutéronome 27.8 Exode 28.11-28.12 Exode 32.16 Exode 28.21
25 Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai, Na ya kuwa hatimaye atasimama juu ya nchi.
Esaïe 43.14 Psaumes 78.35 Esaïe 54.5 Proverbes 23.11 Psaumes 19.14
26 Na baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi, Lakini, pasipokuwa na mwili wangu nitamwona Mungu;
Psaumes 17.15 1 Jean 3.2 1 Corinthiens 13.12 Matthieu 5.8 Psaumes 16.9
27 Nami nitamwona mimi nafsi yangu, Na macho yangu yatamtazama, wala si mwingine. Mtima wangu unazimia ndani yangu.
Psaumes 73.26 Nombres 24.17 Esaïe 26.19
28 Kama mkisema, Jinsi tutakavyomwudhi! Kwa kuwa shina la jambo hili limeonekana kwake;
Job 19.22 1 Rois 14.13 Psaumes 69.26
29 Uogopeni upanga; Kwa maana adhabu za upanga zina ghadhabu, Mpate kujua ya kwamba hukumu iko.
Job 15.22 Psaumes 1.5 Job 22.4 Romains 13.1-13.4 Ecclésiaste 11.9

Cette Bible est dans le domaine public.