Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 15.7
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 2 d’Éliphaz

1 Ndipo Elifazi, Mtemani, akajibu, na kusema,
Job 2.11 Job 4.1 Job 42.7 Job 22.1 Job 42.9
2 Je! Yapasa mtu mwenye hekima kujibu kwa ujuzi wa uvuvio, Na kujaza tumbo lake na upepo wa mashariki?
Job 6.26 Job 8.2 Osée 12.1 Job 11.2-11.3 Job 13.2
3 Je! Ahoji na mazungumzo yasiyo faida, Au kwa maneno ambayo hawezi kufanya mema kwayo?
Colossiens 4.6 Matthieu 12.36-12.37 Job 16.2-16.3 Job 26.1-26.3 Malachie 3.13-3.15
4 Naam, wewe waondoa kicho, Nawe wazuia ibada mbele za Mungu.
Osée 7.14 Psaumes 119.126 Galates 2.21 Job 27.10 Luc 18.1
5 Kwani uovu wako unakufundisha kinywa chako, Nawe wachagua ulimi wake mwenye hila.
Psaumes 52.2-52.4 Job 5.13 Psaumes 120.2-120.3 Job 9.22-9.24 Psaumes 50.19-50.20
6 Kinywa chako mwenyewe chakuhukumia makosa, wala si mimi; Naam, midomo yako mwenyewe hushuhudia juu yako.
Luc 19.22 Job 9.20 Matthieu 12.37 Job 34.5-34.9 Job 42.3
7 Je! Wewe u mtu wa kwanza aliyezaliwa? Au, ulizawa wewe kabla ya milima?
Psaumes 90.2 Proverbes 8.22-8.25 Job 38.4-38.41 Job 12.12 Job 15.10
8 Je! Umesikia mashauri ya siri ya Mungu? Nawe je! Wazuia hekima iwe yako tu?
Romains 11.34 Jérémie 23.18 Matthieu 13.11 1 Corinthiens 2.16 Matthieu 13.35
9 Je! Wewe wajua neno lipi, ambalo sisi hatulijui? Nawe wafahamu nini, ambalo halimo ndani yetu?
Job 13.2 2 Corinthiens 11.21-11.30 2 Corinthiens 11.5 2 Corinthiens 10.7 Job 12.3
10 Wenye mvi, na walio wazee sana, wote wapo pamoja nasi, Ambao ni wazee kuliko baba yako.
Job 32.6-32.7 Proverbes 16.31 Deutéronome 32.7 Job 12.20 Job 12.12
11 Je! Utulizi wa Mungu ni mdogo sana kwako, Na hilo neno la upole si kitu kwako?
Job 13.2 2 Corinthiens 1.3-1.5 Job 5.8-5.26 1 Rois 22.24 Job 36.16
12 Mbona moyo wako unakutaharakisha! Na macho yako, je! Kwani kung’ariza?
Job 11.13 Proverbes 6.13 Psaumes 35.19 Job 17.2 Marc 7.21-7.22
13 Hata ukageuza roho yako iwe kinyume cha Mungu, Na kuyatoa maneno kama hayo kinywani mwako.
Job 10.3 Malachie 3.13 Jacques 1.26 Psaumes 34.13 Romains 8.7-8.8
14 Je! Mwanadamu ni kitu gani, hata akawa safi? Huyo aliyezaliwa na mwanamke, hata awe na haki?
Job 14.4 Ecclésiaste 7.20 Proverbes 20.9 Job 25.4-25.6 Psaumes 14.3
15 Yeye hawategemei watakatifu wake; Naam, mbingu nazo si safi machoni pake.
Job 25.5 Job 4.18 Job 5.1 Esaïe 6.2-6.5
16 Sembuse mtu ambaye ni mwenye kuchukiza na uchafu, Mwanadamu anywaye uovu kama anywavyo maji!
Job 34.7 Proverbes 19.28 Tite 3.3 Psaumes 14.1-14.3 Psaumes 53.3
17 Mimi nitakuonyesha, unisikilize; Na hayo yote niliyoyaona nitayanena;
Job 36.2 Job 5.27 Job 33.1 Job 34.2 Job 13.5-13.6
18 (Ambayo watu wenye hekima wameyatangaza Tokea baba zao, wala hawakuyaficha;
Job 8.8 Psaumes 78.3-78.6 Job 15.10 Psaumes 71.18 Esaïe 38.19
19 Waliopewa hiyo nchi peke yao, Wala mgeni hakupita kati yao);
Joël 3.17 Genèse 10.32 Genèse 10.25 Deutéronome 32.8
20 Mtu mwovu huwa na uchungu siku zake zote, Hata hesabu ya miaka aliyowekewa mwenye kuonea.
Job 24.1 Job 27.13 Luc 12.19-12.21 Romains 8.22 Ecclésiaste 9.3
21 Sauti za utisho zi masikioni mwake; Katika kufanikiwa kwake mtekaji nyara atamjia juu yake;
Job 18.11 1 Thessaloniciens 5.3 Lévitique 26.36 2 Rois 7.6 Actes 12.21-12.23
22 Yeye hasadiki kwamba atarudi kutoka gizani, Naye hungojewa na upanga;
2 Rois 6.33 Job 20.24-20.25 Esaïe 8.21-8.22 Job 19.29 Matthieu 27.5
23 Hutanga-tanga ili apate chakula, akisema, Ki wapi? Ajua kwamba siku ya giza i tayari karibu yake;
Psaumes 109.10 Psaumes 59.15 Job 18.12 Lamentations 5.6 Lamentations 5.9
24 Mateso na dhiki humtia hofu; Humshinda kama vile mfalme aliye tayari kwa vita;
Psaumes 119.143 Romains 2.9 Job 6.2-6.4 Matthieu 26.37-26.38 Proverbes 1.27
25 Kwa kuwa amenyosha mkono wake juu ya Mungu, Na kuendelea kwa kiburi kinyume cha Mwenyezi;
Malachie 3.13 Esaïe 27.4 1 Samuel 6.6 Actes 12.1 Job 36.9
26 Humshambulia na shingo ngumu, Kwa mafundo makubwa ya ngao zake;
Psaumes 18.40 2 Chroniques 28.22 2 Chroniques 32.13-32.17 Genèse 49.8 Job 16.12
27 Kwa kuwa amefunika uso wake na kunona kwake, Na kuwandisha mafuta kiunoni mwake; Naye amekaa katika miji iliyo ukiwa,
Psaumes 17.10 Esaïe 6.10 Psaumes 73.7 Job 17.10 Deutéronome 32.15
28 Katika nyumba ambazo hapana mtu azikaaye, Zilizokuwa tayari kuwa magofu.
Job 3.14 Michée 7.18 Jérémie 9.11 Job 18.15 Michée 3.12
29 Hatakuwa tajiri, wala mali zake hazitadumu, Wala maongeo yao hayatainama nchi.
Job 27.16-27.17 Luc 16.19-16.22 Jacques 1.11 Luc 16.2 Luc 12.19-12.21
30 Hataondoka gizani; Ndimi za moto zitayakausha matawi yake, Naye ataondoka kwa pumzi za kinywa chake.
Job 4.9 Job 15.22 Job 20.26 Job 5.14 Jude 1.13
31 Asiutumainie ubatili, na kujidanganya; Kwa kuwa huo ubatili ndio utakaokuwa ujira wake.
Esaïe 59.4 Galates 6.7-6.8 Esaïe 44.20 Jonas 2.8 Galates 6.3
32 Jambo hili litatendeka kabla ya wakati wake, Na tawi lake halitasitawi.
Ecclésiaste 7.17 Job 22.16 Psaumes 55.23 Osée 9.16 Esaïe 27.11
33 Atayapukutisha mapooza yake kama mzabibu, Na kuyatupa maua yake kama mzeituni.
Deutéronome 28.39-28.40 Esaïe 33.9 Apocalypse 6.13
34 Kwa kuwa jamii ya hao wasiomcha Mungu watakuwa tasa, Na moto utateketeza mahema yenye rushwa.
Job 8.13 Job 20.1 Job 12.6 Job 27.8 Esaïe 33.14-33.15
35 Wao hutunga mimba ya madhara, na kuzaa uovu, Nalo tumbo lao hutengeza udanganyifu.
Psaumes 7.14 Osée 10.13 Esaïe 59.4-59.5 Galates 6.7-6.8 Jacques 1.15

Cette Bible est dans le domaine public.