Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 15.20
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 2 d’Éliphaz

1 Ndipo Elifazi, Mtemani, akajibu, na kusema,
Job 2.11 Job 42.7 Job 22.1 Job 42.9 Job 4.1
2 Je! Yapasa mtu mwenye hekima kujibu kwa ujuzi wa uvuvio, Na kujaza tumbo lake na upepo wa mashariki?
Job 6.26 Job 8.2 Osée 12.1 Job 13.2 Jacques 3.13
3 Je! Ahoji na mazungumzo yasiyo faida, Au kwa maneno ambayo hawezi kufanya mema kwayo?
Matthieu 12.36-12.37 Job 16.2-16.3 Job 26.1-26.3 Malachie 3.13-3.15 1 Timothée 6.4-6.5
4 Naam, wewe waondoa kicho, Nawe wazuia ibada mbele za Mungu.
Galates 2.21 Job 27.10 Luc 18.1 Romains 3.31 Job 4.5-4.6
5 Kwani uovu wako unakufundisha kinywa chako, Nawe wachagua ulimi wake mwenye hila.
Psaumes 120.2-120.3 Job 9.22-9.24 Psaumes 50.19-50.20 Luc 6.45 Job 12.6
6 Kinywa chako mwenyewe chakuhukumia makosa, wala si mimi; Naam, midomo yako mwenyewe hushuhudia juu yako.
Luc 19.22 Matthieu 12.37 Job 9.20 Job 34.5-34.9 Job 42.3
7 Je! Wewe u mtu wa kwanza aliyezaliwa? Au, ulizawa wewe kabla ya milima?
Psaumes 90.2 Proverbes 8.22-8.25 Job 38.4-38.41 Job 15.10 Genèse 4.1
8 Je! Umesikia mashauri ya siri ya Mungu? Nawe je! Wazuia hekima iwe yako tu?
Romains 11.34 Jérémie 23.18 Proverbes 3.32 Job 13.5-13.6 Deutéronome 29.29
9 Je! Wewe wajua neno lipi, ambalo sisi hatulijui? Nawe wafahamu nini, ambalo halimo ndani yetu?
Job 13.2 2 Corinthiens 11.21-11.30 2 Corinthiens 11.5 2 Corinthiens 10.7 Job 12.3
10 Wenye mvi, na walio wazee sana, wote wapo pamoja nasi, Ambao ni wazee kuliko baba yako.
Job 32.6-32.7 Deutéronome 32.7 Job 12.20 Job 12.12 Job 8.8-8.10
11 Je! Utulizi wa Mungu ni mdogo sana kwako, Na hilo neno la upole si kitu kwako?
2 Corinthiens 1.3-1.5 Job 5.8-5.26 1 Rois 22.24 Job 36.16 2 Corinthiens 7.6
12 Mbona moyo wako unakutaharakisha! Na macho yako, je! Kwani kung’ariza?
Proverbes 6.13 Psaumes 35.19 Job 17.2 Marc 7.21-7.22 Actes 8.22
13 Hata ukageuza roho yako iwe kinyume cha Mungu, Na kuyatoa maneno kama hayo kinywani mwako.
Malachie 3.13 Jacques 1.26 Psaumes 34.13 Romains 8.7-8.8 Job 15.25-15.27
14 Je! Mwanadamu ni kitu gani, hata akawa safi? Huyo aliyezaliwa na mwanamke, hata awe na haki?
Job 14.4 Ecclésiaste 7.20 Proverbes 20.9 Job 25.4-25.6 Psaumes 14.3
15 Yeye hawategemei watakatifu wake; Naam, mbingu nazo si safi machoni pake.
Job 25.5 Job 4.18 Job 5.1 Esaïe 6.2-6.5
16 Sembuse mtu ambaye ni mwenye kuchukiza na uchafu, Mwanadamu anywaye uovu kama anywavyo maji!
Job 34.7 Proverbes 19.28 Tite 3.3 Psaumes 53.3 Romains 1.28-1.30
17 Mimi nitakuonyesha, unisikilize; Na hayo yote niliyoyaona nitayanena;
Job 5.27 Job 33.1 Job 34.2 Job 13.5-13.6 Job 36.2
18 (Ambayo watu wenye hekima wameyatangaza Tokea baba zao, wala hawakuyaficha;
Job 8.8 Job 15.10 Psaumes 71.18 Esaïe 38.19 Psaumes 78.3-78.6
19 Waliopewa hiyo nchi peke yao, Wala mgeni hakupita kati yao);
Joël 3.17 Genèse 10.25 Deutéronome 32.8 Genèse 10.32
20 Mtu mwovu huwa na uchungu siku zake zote, Hata hesabu ya miaka aliyowekewa mwenye kuonea.
Job 24.1 Job 27.13 Romains 8.22 Ecclésiaste 9.3 Jacques 5.1-5.6
21 Sauti za utisho zi masikioni mwake; Katika kufanikiwa kwake mtekaji nyara atamjia juu yake;
Job 18.11 1 Thessaloniciens 5.3 Lévitique 26.36 1 Samuel 25.36-25.38 Psaumes 92.7
22 Yeye hasadiki kwamba atarudi kutoka gizani, Naye hungojewa na upanga;
Job 20.24-20.25 Esaïe 8.21-8.22 Job 19.29 Matthieu 27.5 Job 9.16
23 Hutanga-tanga ili apate chakula, akisema, Ki wapi? Ajua kwamba siku ya giza i tayari karibu yake;
Psaumes 59.15 Psaumes 109.10 Job 18.12 Job 18.18 Ecclésiaste 11.8
24 Mateso na dhiki humtia hofu; Humshinda kama vile mfalme aliye tayari kwa vita;
Romains 2.9 Job 6.2-6.4 Matthieu 26.37-26.38 Proverbes 1.27 Proverbes 6.11
25 Kwa kuwa amenyosha mkono wake juu ya Mungu, Na kuendelea kwa kiburi kinyume cha Mwenyezi;
Lévitique 26.23 Esaïe 10.12-10.14 Exode 5.2-5.3 Job 40.9-40.11 Job 9.4
26 Humshambulia na shingo ngumu, Kwa mafundo makubwa ya ngao zake;
2 Chroniques 28.22 2 Chroniques 32.13-32.17 Genèse 49.8 Job 16.12 Psaumes 18.40
27 Kwa kuwa amefunika uso wake na kunona kwake, Na kuwandisha mafuta kiunoni mwake; Naye amekaa katika miji iliyo ukiwa,
Psaumes 17.10 Esaïe 6.10 Psaumes 73.7 Deutéronome 32.15 Psaumes 78.31
28 Katika nyumba ambazo hapana mtu azikaaye, Zilizokuwa tayari kuwa magofu.
Job 3.14 Jérémie 9.11 Job 18.15 Michée 3.12 Jérémie 26.18
29 Hatakuwa tajiri, wala mali zake hazitadumu, Wala maongeo yao hayatainama nchi.
Job 27.16-27.17 Jacques 1.11 Luc 16.2 Luc 12.19-12.21 Psaumes 49.16-49.17
30 Hataondoka gizani; Ndimi za moto zitayakausha matawi yake, Naye ataondoka kwa pumzi za kinywa chake.
Job 4.9 Job 15.22 Job 20.26 Matthieu 8.12 Matthieu 25.41
31 Asiutumainie ubatili, na kujidanganya; Kwa kuwa huo ubatili ndio utakaokuwa ujira wake.
Esaïe 59.4 Esaïe 44.20 Jonas 2.8 Galates 6.3 Osée 8.7
32 Jambo hili litatendeka kabla ya wakati wake, Na tawi lake halitasitawi.
Ecclésiaste 7.17 Job 22.16 Psaumes 55.23 Esaïe 27.11 Psaumes 52.5-52.8
33 Atayapukutisha mapooza yake kama mzabibu, Na kuyatupa maua yake kama mzeituni.
Esaïe 33.9 Apocalypse 6.13 Deutéronome 28.39-28.40
34 Kwa kuwa jamii ya hao wasiomcha Mungu watakuwa tasa, Na moto utateketeza mahema yenye rushwa.
Job 8.13 Esaïe 33.14-33.15 Michée 7.2 1 Samuel 12.3 Job 8.22
35 Wao hutunga mimba ya madhara, na kuzaa uovu, Nalo tumbo lao hutengeza udanganyifu.
Psaumes 7.14 Osée 10.13 Esaïe 59.4-59.5 Galates 6.7-6.8 Jacques 1.15

Cette Bible est dans le domaine public.