Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 15.19
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 2 d’Éliphaz

1 Ndipo Elifazi, Mtemani, akajibu, na kusema,
Job 2.11 Job 42.9 Job 4.1 Job 42.7 Job 22.1
2 Je! Yapasa mtu mwenye hekima kujibu kwa ujuzi wa uvuvio, Na kujaza tumbo lake na upepo wa mashariki?
Job 6.26 Job 8.2 Osée 12.1 Job 13.2 Jacques 3.13
3 Je! Ahoji na mazungumzo yasiyo faida, Au kwa maneno ambayo hawezi kufanya mema kwayo?
Malachie 3.13-3.15 1 Timothée 6.4-6.5 Job 13.4-13.5 Colossiens 4.6 Matthieu 12.36-12.37
4 Naam, wewe waondoa kicho, Nawe wazuia ibada mbele za Mungu.
Romains 3.31 Job 4.5-4.6 Psaumes 36.1-36.3 Amos 6.10 Job 5.8
5 Kwani uovu wako unakufundisha kinywa chako, Nawe wachagua ulimi wake mwenye hila.
Luc 6.45 Job 12.6 Marc 7.21-7.22 Jérémie 9.8 Jérémie 9.3-9.5
6 Kinywa chako mwenyewe chakuhukumia makosa, wala si mimi; Naam, midomo yako mwenyewe hushuhudia juu yako.
Luc 19.22 Matthieu 12.37 Job 9.20 Job 35.2-35.3 Job 33.8-33.12
7 Je! Wewe u mtu wa kwanza aliyezaliwa? Au, ulizawa wewe kabla ya milima?
Psaumes 90.2 Job 38.4-38.41 Proverbes 8.22-8.25 Genèse 4.1 Job 12.12
8 Je! Umesikia mashauri ya siri ya Mungu? Nawe je! Wazuia hekima iwe yako tu?
Romains 11.34 Jérémie 23.18 Job 29.4 Jean 15.15 Psaumes 25.14
9 Je! Wewe wajua neno lipi, ambalo sisi hatulijui? Nawe wafahamu nini, ambalo halimo ndani yetu?
Job 13.2 Job 12.3 Job 26.3-26.4 2 Corinthiens 11.21-11.30 2 Corinthiens 11.5
10 Wenye mvi, na walio wazee sana, wote wapo pamoja nasi, Ambao ni wazee kuliko baba yako.
Job 32.6-32.7 Job 12.12 Job 8.8-8.10 Proverbes 16.31 Deutéronome 32.7
11 Je! Utulizi wa Mungu ni mdogo sana kwako, Na hilo neno la upole si kitu kwako?
Job 36.16 2 Corinthiens 7.6 Job 11.13-11.19 Job 15.8 Job 13.2
12 Mbona moyo wako unakutaharakisha! Na macho yako, je! Kwani kung’ariza?
Marc 7.21-7.22 Actes 8.22 Jacques 1.14-1.15 Ecclésiaste 11.9 Actes 5.3-5.4
13 Hata ukageuza roho yako iwe kinyume cha Mungu, Na kuyatoa maneno kama hayo kinywani mwako.
Romains 8.7-8.8 Job 15.25-15.27 Job 9.4 Job 12.6 Jacques 3.2-3.6
14 Je! Mwanadamu ni kitu gani, hata akawa safi? Huyo aliyezaliwa na mwanamke, hata awe na haki?
Ecclésiaste 7.20 Proverbes 20.9 Job 14.4 Job 25.4-25.6 Psaumes 14.3
15 Yeye hawategemei watakatifu wake; Naam, mbingu nazo si safi machoni pake.
Job 25.5 Job 4.18 Job 5.1 Esaïe 6.2-6.5
16 Sembuse mtu ambaye ni mwenye kuchukiza na uchafu, Mwanadamu anywaye uovu kama anywavyo maji!
Proverbes 19.28 Job 34.7 Tite 3.3 Job 20.12 Romains 3.9-3.19
17 Mimi nitakuonyesha, unisikilize; Na hayo yote niliyoyaona nitayanena;
Job 13.5-13.6 Job 36.2 Job 5.27 Job 33.1 Job 34.2
18 (Ambayo watu wenye hekima wameyatangaza Tokea baba zao, wala hawakuyaficha;
Job 8.8 Esaïe 38.19 Psaumes 78.3-78.6 Job 15.10 Psaumes 71.18
19 Waliopewa hiyo nchi peke yao, Wala mgeni hakupita kati yao);
Joël 3.17 Genèse 10.32 Genèse 10.25 Deutéronome 32.8
20 Mtu mwovu huwa na uchungu siku zake zote, Hata hesabu ya miaka aliyowekewa mwenye kuonea.
Job 27.13 Job 24.1 Jacques 5.1-5.6 Psaumes 90.3-90.4 Psaumes 90.12
21 Sauti za utisho zi masikioni mwake; Katika kufanikiwa kwake mtekaji nyara atamjia juu yake;
Job 18.11 1 Thessaloniciens 5.3 Lévitique 26.36 Job 20.5-20.7 Job 1.13-1.19
22 Yeye hasadiki kwamba atarudi kutoka gizani, Naye hungojewa na upanga;
Matthieu 27.5 Job 9.16 Job 6.11 Job 27.14 2 Rois 6.33
23 Hutanga-tanga ili apate chakula, akisema, Ki wapi? Ajua kwamba siku ya giza i tayari karibu yake;
Psaumes 109.10 Psaumes 59.15 Job 18.12 Job 18.5-18.6 Hébreux 10.27
24 Mateso na dhiki humtia hofu; Humshinda kama vile mfalme aliye tayari kwa vita;
Proverbes 1.27 Proverbes 6.11 Esaïe 13.3 Proverbes 24.34 Psaumes 119.143
25 Kwa kuwa amenyosha mkono wake juu ya Mungu, Na kuendelea kwa kiburi kinyume cha Mwenyezi;
Psaumes 73.9 Psaumes 52.7 Actes 9.5 Psaumes 73.11 Actes 12.23
26 Humshambulia na shingo ngumu, Kwa mafundo makubwa ya ngao zake;
Job 16.12 Psaumes 18.40 2 Chroniques 28.22 2 Chroniques 32.13-32.17 Genèse 49.8
27 Kwa kuwa amefunika uso wake na kunona kwake, Na kuwandisha mafuta kiunoni mwake; Naye amekaa katika miji iliyo ukiwa,
Psaumes 17.10 Psaumes 73.7 Esaïe 6.10 Jérémie 5.28 Job 17.10
28 Katika nyumba ambazo hapana mtu azikaaye, Zilizokuwa tayari kuwa magofu.
Job 3.14 Jérémie 26.18 Esaïe 5.8-5.10 Jérémie 51.37 Michée 7.18
29 Hatakuwa tajiri, wala mali zake hazitadumu, Wala maongeo yao hayatainama nchi.
Job 27.16-27.17 Psaumes 49.16-49.17 Job 22.15-22.20 Job 20.22-20.28 Jacques 5.1-5.3
30 Hataondoka gizani; Ndimi za moto zitayakausha matawi yake, Naye ataondoka kwa pumzi za kinywa chake.
Job 4.9 Job 15.22 Job 20.26 Esaïe 30.33 Job 18.5-18.6
31 Asiutumainie ubatili, na kujidanganya; Kwa kuwa huo ubatili ndio utakaokuwa ujira wake.
Esaïe 59.4 Osée 8.7 Job 4.8 Proverbes 22.8 Psaumes 62.10
32 Jambo hili litatendeka kabla ya wakati wake, Na tawi lake halitasitawi.
Ecclésiaste 7.17 Job 22.16 Psaumes 55.23 Jean 15.6 Job 18.16-18.17
33 Atayapukutisha mapooza yake kama mzabibu, Na kuyatupa maua yake kama mzeituni.
Deutéronome 28.39-28.40 Esaïe 33.9 Apocalypse 6.13
34 Kwa kuwa jamii ya hao wasiomcha Mungu watakuwa tasa, Na moto utateketeza mahema yenye rushwa.
Job 8.13 Job 8.22 Matthieu 24.51 Job 29.12-29.17 Job 36.13
35 Wao hutunga mimba ya madhara, na kuzaa uovu, Nalo tumbo lao hutengeza udanganyifu.
Psaumes 7.14 Osée 10.13 Esaïe 59.4-59.5 Jacques 1.15 Galates 6.7-6.8

Cette Bible est dans le domaine public.